Wednesday, 10 December 2014

Soko la Nguo lashambuliwa Nigeria....

Bomu limelipuka karibu na soko katika mji wa Kaskazini mjini mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa maafisa wakuu wanasema bomu hilo lilipuka katika eneo ambako mizigo hupakiwa, katika soko la nguo la Kantini Kwari.

Taarifa za majeruhi bado hazijatolewa. Takriban watu 2,000 wameuawa katika mashambulizi yaliyofanywa na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram mwaka huu.
Mwezi jana zaidi ya watu 100 walifariki katika shambulizi lengine lililofanywa na kundi hilo wakati wa maombi katika msikiti mkubwa mjini Kano.

Mwandishi wa BBC Habiba Adamu anasema Kantin Kwari ni soko kubwa zaidi la nguo mjini Kano ambako watu kutoka nchi jirani na maeneo mengine ya nchi kuendeshea biashara zao.
Soko hilo daima huwa limejaa watu.
Share:

Ukatili wa majasusi Marekani wafichuliwa......

Ripoti ya Seneti Marekani imekosoa vikali zinazotumiwa na CIA, kuwahoji washukiwa wa uhalifu, kwamba ni za kikatili na zisizofaa.
Ripoti ya kamati ya bunge la Seneti nchini Marekani imekosoa vikali mbinu zinazotumiwa na Shirika la Ujasusi la nchi hiyo za kuwahoji washukiwa wa uhalifu na kuelezea kwamba ni za kikatili na zisizofaa.
Mwenyekiti wa kamati ya usalama ya bunge la seneti Dianne Feinstein amesema katika baadhi ya matukio wanavyotendewa washukiwa hao ni sawa na mateso.
''Watu waliowekwa kizuizini walipaswa kutii mbinu zilizokuwa zikitumiwa, kuvuliwa nguo na kuachwa watupu, walikuwa wakiwekwa katika hali ya mateso ya muda mrefu.


Walikuwa wakizuiwa kulala kwa siku kadhaa, hadi saa 180- ikiwa ni sawa na siku saba na nusu, zaidi ya wiki bila ya kulala, kawaida wakiwa wamwesimama au katika hali ya kuwachosha na wakati huohuo mikono yao ikiwa imefungwa pamoja juuya vichwa.
Mbonu hizo za utesaji zilianzishwa baada ya shambulio la kigaidi la Septemba 11, mwaka 2001
nchini Marekani...''
Mbinu hizo zinazotumiwa na shirika hilo la ujasusi zimeelezwa na wabunge hao wa seneti kuwa zinamapungufu na kwamba CIA imekuwa ikitoa taarifa zisizo sahihi kwa umma.
Share:

Kilio cha Albino Tanzania...


Mtobi Namigambo, ni mvuvi anayeuza samaki, amekaa kwa utulivi nje ya nyumba yake ya matope katika kisiwa cha ukerewa mahali ambapo zamani palikuwa makao ya albino lakini kwa sasa si hivyo. Mtoto wake wa miaka nne May Mosi ameketi kwenye paja lake akionyesha umarufu wake wa hisabati kwa kuhesabau moja hadi kumi kwa ujasiri.
Mara kwa mara Mtobi anamtazama mke wake, Sabina, ambaye ameketi kwa mkeka kando yake akitayarisha chakula cha jioni. Watoto wake wengine wawili wanachezea hapa karibu na pia wamejaliwa na mtoto mchanga amabye yuko chumbani analala.
May alipokuwa na umri wa miezi mitatu, aliponea jaribio la kutekwa nyara.
" nilikuwa nimeenda ziwani kuvua samaki. walikuwa pekee yao nyumbani wavamizi walipokuja, mke wangu alitorokea kwa dirisha na kukimbillia usalama akiwa na May, na akawawacha watoto hawa wawili nyumabani ambao hawakuwadhuru kabisa", Mtobi ananiarifu.
"Wavamazi hao walikuwa wakimtaka May," Sabina anaongezea, "mume wangu alikuwa ameenda safari ya uvuvi na wavamizi hao walijua na hio ndio sababu walikujia mtoto wangu, baada ya kutorokea kwa dirisha, bado waliniandama huku nikipiga mayoye ya usaidizi, waliwacha kuniandama wakati tu niliwaamsha majirani"
May ni mojawapo wa Albino sabini wanaoishi katika kisiwa hiki cha Ukerewa ambacho ni masaa matatu tu kutoka mwanza, mji wa pili mkubwa zaidi Tanzania.
Elimu kwa jamii
Mtobi anasema "tunaiomba serikali kufanya juhudu zaidi za kuelimisha jamii hapa, serikali ishawahi kuandaa majadiliano kuhusu Albino na kulikuwa na mabadiliko makuwa, akini si hivyo tena"
Shirika lisilo la kiserekali chini ya mrengo wa 'The Same Sun' linalowashughulikia jamii ya Albino hapa Ukerewa, linasema kuwa kisiwa hiki hakina usalama kando na vile watu wangependa kuamini.
Mwenye kiti wa chama cha maalbino tawi la Mwanza, (TAS) Alfred Kapole, mzaliwa wa Ukerewe, alilazimika kutorokea mji wa Mwanza akiwa mmoja wa albino wa kwanza kufika kortini baada ya kiognozi mmoja wa kijiji akitaka kumuua kwa ajili ya nywele zake.
Mwaka uliopita boma lake lilivamiwa, kwa bahati nzuri alikuwa ameenda mwanza. Kulikuwa na jairibio lEngine la kumuua mwaka huu.
Kampeni kabambe
Serikali ya Tanzania imeanzisha kampeni ili kuchangisha fedha za kuelimisha jamii.
Kampeni nyingi za uhamasishaji hufanyika mijini kwani ni rahisi kufikia watu,lakini ni vijiji ndivyo vinahitaji msaada zaidi.
Ramadhan Khalfan, ambaye ni mwenyekiti wa chama cha albino Ukerewa,anasema kuwa wanataka kufikia maeneo ya vijiji na kuzungumza na watu,lakini ni vigumu kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha.''Hatuna uwezo ama njia za kufikia jamii zilizoko vijijini.Aliongezea kusema,''tunategemea pakubwa redio na televisheni,lakini hatuwezi kufika mashinani kwa sababu ya gharama.''
Sehemu ya Serengema inapatikana kilomita 60 (maili 33.5) kutoka Mwanza.Ili kusisitiza shida hii,umejengwa mnara katika mzunguko katikati ya mji.
Ni sanamu ya chuma kimo cha binadamu,inayoonyesha baba mwenye rangi akimbeba begani mto wake albino huku mama yake mwenye rangi akitundika kofia yenye ukingo mpana kwenye kichwa cha mwana huyo kumkinga kutokana na miale ya jua.Pia kuna majina ya watu 139 ya waathiriwa waliouawa,kuvamiwa ama miili yao kuibiwa kutoka kwenye makaburi.
Serengema ndio sehemu iliyoathirika vibaya zaidi.
Kuna mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi pamoja na chama cha Tanzania Albino katika kuhamasisha na pia kujenga makaazi.
Mashirika yasiyo ya kiserikali yanaamini kuwa uhamasisho na kuacha imani potovu zinaweza kusimamisha mauaji haya.
Mwakilishi wa chama cha Serengema Mashaka Benedict anasema kuwa watu bado wanaamini kuwa sehemu za mwili wa albino zinaweza kuleta utajiri.''Kama hiyo ndiyo hali,mbona sisi si matajiri?''anauliza.
Anadai kuwa watu mashuhuri wanahusika katika ''biashara ya mauaji'' na ndio maanake watu wachache sana wamekamatwa,kushitakiwa,kupatikana na hatia ama kufungwa.''Itakuwa vipi masikini kutoa dola 10,000 kwa kipande cha mwili?,ni wanabiashara na wanasiasa ndio wanaohusika.''
Hata hivyo polisi wanasema kuwa wanachungunza kila moja ya visa lakini wanakosa ushahidi wa kuthibitisha madai yanayotolewa.Kamanda wa polisi wa Mwanza,Valentino Mlolowa anasema,''Kesi hizi ni ngumu kwa kuwa visa hufanyika mashinani sana katika sehemu ambazo hazina stima kwa mfano,na hiyo inafanya kuwajua wahalifu usiku kuwa vigumu.Tunachunguza kila moja ya kesi na madai,lakini kama uonavyo,si rahisi.''
Yaweza onekana kama kuwa tumepoteza kila kitu lakini hii haiwazuilii watu wanaoishi na hali ya Uhalbino kama May Mosi,kutokuwa na tumaini kuwa fedha zinazochangishwa kutoka kwenye kampeni iliyoanzishwa na serikali zitasaidia kusikizwa zaidi kwa Albino nchini Tanzania.





Share:

Tuesday, 9 December 2014

Al Jazeera yaihusisha Kenya na mauaji.....source BBC


Shirika la habari la Al Jazeera limepeperusha ripoti ambayo imehusisha maafisa wa usalama wa Kenya na mauaji ya viongozi wa dini ya kiisilamu pamoja na washukiwa wa ugaidi.
Taarifa hiyo ya ufichuzi iliyopeperushwa Jumatatu, ilionyesha baadhi ya maafisa wa polisi wanaofanya kazi yao kwa usiri mkubwa wakikiri kuwaua baadhi ya viongozi wa kiisilamu wanaosemekana kufunza mafunzo yenye itikadi kali ya kiisilamu pwani ya Kenya.

Ripoti hio http://goo.gl/wYV91g ambayo ilikuwa ni kanda ya video yenye polisi hao wakikiri kuwaua waisilamu mjini Mombasa, iliwekwa kwenye mtandao wa YouTube na shirika hilo.
Inaonyesha sura za polisi hao zikiwa zimefichwa huku wakisimulia ambavyo wamekuwa wakiwaua watu wanaonekana kua wenye kutoa mafunzo ya itikadi kali na wanaotatiza usalama wa nchi.
Wengi ambao wameuawa na maafisa hao ni washukiwa wa ugaidi waliodaiwa kutoa mafunzo ya itikadi kali za kidini.

Walisema kuwa wampokea mafunzo yao kutoka kwa mashirika ya kijasusi ya kimataifa ikiwemo MI5 la Uingereza na Mossad la Israel.
Mmoja wa maafisa anasema wamewaua washukiwa wengi sana wa ugaidi akiwemo Sheikh Abubakar Shariff Makaburi mnamo mwezi April.
Taarifa hizo zilichapishwa kwenye vyombo vingine vya habari vikizungumzia mauaji ya kisiri ya washukiwa wa Ugaidi yanayofanywa na maafisa wa polisi waliopata mafunzo ya hali ya juu nchini Kenya.

Baadhi ya maafisa hawa wanatoka kitengo cha polisi wa kupambana na ghasia au GSU na shirika la kitaifa la ujasusi.
Mmoja wao alinukuliwa akisema katika kanda hio ....''sisi hupewa taarifa tu na kisha kutekeleza matakwa ya wakuu wetu. Huwa tunamuua yule mshukiwa tuliyetumwa kumuu na kazi hii huwa tunaifanya kwa usiri mkubwa sana,''

wote waliohojiwa wanasema wao hupokea mafunzo ya hali ya juu mno kabla ya kufanya kazi yao kwa umakini mkubwa.
Ripoti hiyo ya Al Jazeera inasema kuwa washukiwa wa ugaidi huuawa badala ya kupelekwa mahakamani.

Sio mara ya kwanza kwa mashirika ya usalama nchini Kenya kutuhumiwa kwa mauaji ya washukiwa wa ugaidi kwa siri.
Hata hivyo, Serikali ya Kenya imetoa taarifa kupinga ripoti hio inayodai kuwa polisi nchini humo walihusika na mauaji ya washukiwa wa ugaidi.

Ripoti hiyo iliyoonyeshwa na runinga ya al jazeera ilidai kuwa maafisa kadhaa wa polisi walikiri kuwa kikosi maalum cha usakama kilihusika na kutoweka na hatimaye mauaji wa washukiwa wa ugaidi, hasa viongozi wa dini ya kiislamu waliokiswa kuwa na siasa za misimamo mikali.
Lakini katibu wa wizara ya habari nchini Kenya amesema ripoti hiyo haina msingi wowote na kutaka shirika hilo la habari kuiomba msamaha.
Share:

Watoto wa kiume Culcutta sio dili.........

Polisi Mashariki mwa mji wa Calcutta nchini India, wanachunguza tukio la mwanamke ambaye jamii yake ilimtelekeza katika bwawa,kwa kushindwa kuzaa mtoto wa kike ambaye baadaye walimtegemea kuwa kahaba.

Mwanamke huyo aliokolewa na chama cha kujitolea kuwahudumia makahaba kabla hajalazimika kujitosa kwenye ukahaba kamili.
Mwanamke huyo aliiambia BBC kwamba familia ya wakwe zake walianza kumdhihaki baada ya kuzaa watoto wa kiume watatu mfululizo, na kufahamishwa kwamba familia hiyo kwa kawaida huwapeleka watoto wa kike wa ukoo wao kufanya kazi ya ukahaba, iweje yeye azae watoto wakiume watupu?.
Share:

Rais Mugabe amfuta kazi makamu wake....


Taarifa kutoka nchini Zimbabwe zinasema kuwa Rais Robert Mugabe amemfuta kazi makamu wake Joice Mujuru, kufuatia ushindani wa uongozi katika chama tawala cha ZANU-PF.
Awali Bi Joyce Mujuru, alikanusha madai kuwa yeye ni mfisadi na alihusika na njama ya kutaka kumuua rais Robert Mugabe.

Bi Mujuru alilaaniwa na Rais Mugabe wiki iliyopita na kuondolewa kutoka wadhifa wake wa makamu wa rais wa chama tawala cha ZANU-PF wakati wa kongamano la chama hicho mjini Harare.

Amesema ameendelea kupokea vitisho na kuwa shirika la habari la serikali limeendelea kuchapisha habari za uongo za zisizo na msingi dhidi yake.
Ilikuwa wiki nzima ya tuhuma dhidi ya Bi Mujuru kutoka kwa vyombo vya habari vya serikali kwa ushirikiano na mkewe Mugabe, Grace Mugabe, ambaye kwa sasa ameteuliwa kama afisaa mkuu wa chama cha ZANU-PF.

Wengi walimuona Mujuru mwenye umri wa miaka 59, kama mrithi wa Mugabe.
Katika hatua yake ya kwanza kujibu tuhuma hizo tangu kuondolewa katika chama, Mujuru alisema amekuwa akitishiwa sana na watu asio wajua.
Aliongeza kuwa vyombo vya habari nchini humo vimeendelea kumchafulia jina lake kwa kuchapisha porojo na taarifa za uongo, dhidi yake.
Alisema hakuna hjata tone moja la ushahidi limetolewa dhidi yake kuthibitisha madai anayasingiziwa na kutajwa kuwa msaliti mkubwa.

Madai kuwa alipanga njama ya kumuondoa mamlakani Mugabe, ni ya kipuzi sana.
Rais Mugabe, mwnye umri wa miaka 90, amekua mamlakani tangu Zimbabwe kujipatia uhuru mwaka 1980.
Bi Mujuru alipambana bega kwa bega na Mugabe mapema miaka ya 1970, dhidi ya utawala wa kibaguzi na kwa wengi alionekana kama mrithi mtarajiwa wa Mugabe.
Share:

Askofu Desmond Tutu ana tezi dume....


Askofu mkuu mstaafu wa Cape Town,Desmond Tutu,ameahirisha mipango ya ziara zake kwa mwaka mzima ujao kutokana na sababu za kiafya.

Taarifa iliyotolewa na taasisi yake imeeleza kuwa Askofu huyo ataanza matibabu hivi karibuni ili kukabiliana na tezi dume ambayo amedumu nayo miaka kumi na mitano iliyopita.
Binti wa Askofu huyo amemuelezea baba yake mwenye umri wa miaka themanini na miwili,kwamba hatahudhuria tuzo za Nobel zitakazo fanyika baadaye wiki hii huko Rome, Italia.
Share:

Daktari feki akamatwa Tanzania.......












Hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam, Tanzania


Sekta ya afya nchini Tanzania bado inakabiliwa na tatizo la madaktari feki ambapo jana Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu, MOI ilimkamata daktari feki aliyefahamika kwa jina la Dismas John Macha mwenye umri wa miaka 35.

Taasisi hiyo ipo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili, MNH jijini Dar es Salaam, ambapo daktari huyo anadaiwa kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa wagonjwa na ndugu wa wagonjwa kwa madai kwamba angemhudumia mgonjwa wao.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo, Mkurugenzi wa MOI, Athumani Kiloloma, alisema mara ya kwanza alikamatwa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili, MUHAS, akijifanya mwanafunzi wa shahada ya uzamili katika shule ya tiba.
Dk. Kiloloma alisema alipokamatwa mara ya kwanza, walitoa matangazo katika hospitali nzima na kutoa taarifa kwa wananchi, lakini wanashangaa tukio hilo limejirudia tena.
Akizungumzia tukio hilo, mkurugenzi huyo alisema wanakabiliwa na tatizo kubwa la madaktari feki, ambao wamekuwa wakiomba michango mbalimbali ya fedha.

Mtuhumiwa Dismas Macha anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayomkabili.
Awali, Dismas akizungumza na waandishi wa habari, alisema yeye si daktari bali ni mgonjwa wa akili. Matukio ya madaktari feki yamekuwa yakiripotiwa katika hospitali mbalimbali nchini Tanzania katika siku za karibuni, ambapo inadaiwa madaktari hao kazi kubwa ni kuwatapeli wagonjwa na ndugu wa wagonjwa.
Share:

Watanzania waadhimisha miaka 53 ya uhuru..........


Tanzania bara leo inaadhimisha miaka 53 toka ilipojipatia uhuru toka kwa Muingereza Desemba 9, mwaka 1961.
Maadhimisho haya ya 53 ni muhimu kwa Watanzania, kutokana na kwamba nchi ipo katika kipindi cha uchaguzi, ambapo Watanzania siku ya Jumapili Desemba 14, watapiga kura, katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji.
Uchaguzi huo ni muhimu, kutokana na viongozi katika ngazi hiyo kuwa karibu kabisa na jamii.
Tanzania pia inaadhimisha miaka 53 ya uhuru wake ikiwa katika harakati za uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Ni miaka 53 tangu Tanzania ijipatie uhuru wake, lakini hali za Watanzania wengi bado ni duni, kiuchumi na kijamii.
Share:

Monday, 8 December 2014

Maelfu wahitaji msaada Somalia......


Umoja wa Mataifa unasema kua zaidi ya watu milioni tatu wanahitaji msaada wa dhahura kwa sababu ya tatizo kubwa la utapia mlo na mgogoro.
Tahadhari hio imetolewa miaka mitatu baada ya zaidi ya robo ya watu milioni moja kufariki kutokana na ukosefu wa chakula.
Katika taarifa yake ofisi ya mratibu wa misaada ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa inasma kuwa wasomali wanaendelea kukabiliwa na hali ngumu ya kibindamau.

Maelfu ya watu wameathirika kutokana na vita vinavyosababishwa na wanamgambo wa Al Shabaab.
Kikosi cha wanjeshi wa Muungano wa Afrika kiko nchini humo kuoambana na wanamgambo hao.
Wadadisi wanasema hali hiyo imechocewa zaidi na ukame pamoja na mafuriko katika baadhi ya sehemu za nchi hio.
Share:

Amezwa na Nyoka aina ya Anaconda....















Watu nchini Marekani wameelezea ghadhabu na hasira zao kwenye mitandao ya kijamii kufuatia utafiti wa mtaalamu wa wanyamapori Paul Roslie kumezwa na Nyoka aina ya Anaconda ili ku chunguza maumbile ya ndani ya Nyoka huyo.
Lengo la utafiti huo ambao ulikuwa wa kwanza wa aina yake duniani, ilikuwa ni kuchunguza maumbulie ya ndani ya Nyoka huyo anayepatikana katika msitu wa Amazon.
Hata hivyo inaarifiwa bwana Paul alilazimika kusitisha utafiti wake ambao umezua utata muda mfupi tu baada ya kuuanzisha.
Watu nchini Marekani walijionea kwenye televisheni zao kipindi kilichokuwa kinapeperushwa cha mtaalamu huyo kuingia ndani ya tumbo la Anaconda akiwa amevalia vazi maalum ambalo yangesaidia kuchunguza kiwango cha joto mwilini mwake na pia kupima mipigo ya Moyo wake wakati akiwa ndani ya tumbo la Nyoka huyo.















Rosolie na kikundi cha wasaidizi wake walipata Nyoka ya Anaconda mwenye uzito wa kilo 180, walipokuwa katika msitu huo. Alipanga kuwa ataonyeshwa kwenye stesheni hio akiwa anamezwa mzima mzima na Nyoka huyo.
Rosolie alionekana akiingia ndani ya mdomo wa Anaconda kwa kichwa chake huku wenzake wakimtazama.
Alikuwa amevalia vazi maalum lenye Carbon na likiwa limepakwa damu ya Nguruwe, kabla ya kujielkeza kwa Nyoka huyo kama mlo wake.
"sikutana kumhangaisha mno mnyama na pia mimi mwenyewe sikutaka kujiumiza. ''
Share:

Watoto wauawa kikatili DRC......


Inaarifiwa kuwa watu kama 30 waliuwawa katika mashambulio kwenye vijiji mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Taarifa zinasema kuwa mashambulio hayo yalifanywa Jumamosi usiku kwenye vijiji karibu na mji wa Beni ambako watu zaidi ya 250 wameuawa tangu mwezi Oktoba.
Wakuu na mashirika ya raia yanawalaumu wapiganaji kutoka Uganda wa kundi la ADF, lakini baadhi ya wadadisi wanasema hakuna ushahidi wa kutosha wa kuhusisha kundi hilo.
Mwandishi mmoja wa habari katika eneo hilo aliambia BBC kuwa waliofariki ni pamoja na wanawake na watoto ambao walibururwa kutoka kwa nyumba zao na kukatwa katwa kwa mapanga.
Alisema haijulikani nani aliyefanmya mashambulizi hayo, ingawa maafisa wakuu wamelaumu kundi la waasi la Uganda la ADF.
Alisema maelfu ya watu wameachwa bila makao kutokana na vurugu zinazoendelea na kwamba wanahofia sana kurejea makwao.
Share:

Yaya aliyemtesa mtoto UG aomba msamaha..

Mfanyakazi wa nyumbani aliyenaswa kwenye kanda ya video akimchapa na kumkanyaga mtoto nchini Uganda, amefikishwa mahakamani leo.
Mfanyakazi huyo Jolly Tumuhirwe aliambia mahakama kuwa anajulia kile alichokifanya na hata kuomba msamaha. Ameshitakiwa kwa kosa la kumtesa mtoto Arnella.
Licha ya taarifa ya polisi kusema Jolly atashitakiwa kwa kosa la jaribio la ,mauaji, kiogozi wa mashitaka alimshitaki Jolly kwa kosa la kumtesa mtoto mdogo

Bi Tumuhirwe alikiri makosa yake na kuomba msamaha. Hakuna wakili yeyote aliyemwakilisha Jolly mahakamani licha ya mmoja wa mawakili mashuhuri kusema angemwakilisha Jolly bila malipo.
Kesi hio imeakhirishwa hadi Jumatano, wakati ambapo hakimu anatarajiwa kutoa hukumu yake dhidi ya Jolly.
Huenda akafungwa jela miaka 15 au kutozwa faini ya dola mianne au adhabu zote mbili.
Share:

Sunday, 7 December 2014

Wahamiaji 70 wafa maji Yemen.....















Watu 70 wamekufa baada ya boti iliyokuwa imejaza wahamiaji haramu kupinduka baharini, magharibi mwa Yemen.
Maafisa nchini Yemen wamesema wengi ya watu waliokuwa katika boti hiyo ni raia wa Ethiopia.
Hali mbaya ya hewa inaelezwa kwamba ndio chanzo cha kuzama kwa boti hiyo.
Mamia kwa maelfu ya wahamiaji wamekuwa wakihatarisha maisha yao kwa safari zisizo na usalama katika nchi zilizo katika pembe ya Afrika na Yemen kila mwaka.
Umoja wa Mataifa unamini kwamba kiasi cha watu watu mia mbili wamezama maji katika kipindi cha miezi kumi na mbili iliyopita.
Share:

Ndege iliyobeba silaha yakamatwa Nigeria...........

Ndege ya mizigo iliyosheheni silaha za kivita imekamatwa katika uwanja wa ndege wa Kano nchini Nigeria. Licha ya kukanusha awali, Urusi imesema inamiliki ndege ya mizigo iliyozuiwa katika uwanja wa ndege wa Kano kaskazini mwa Nigeria baada ya kugunduliwa imebeba silaha ambazo hazikuwa zimearifiwa. Hata hivyo, Msemaji wa Ubalozi wa Urusi nchini Nigeria, ambaye aliliambia Shirika la Habari la Urusi TASS kwamba wanamiliki ndege hiyo, amesema silaha hizo ni za kikosi cha kulinda amani cha Ufaransa.

Kwa mujibu wa Mwandishi wa habari wa BBC ndege hiyo bado inashikiliwa uwanjani hapo.
Awali, msemaji wa kikosi cha kulinda amani cha Ufaransa katika Jamhuri ya Afrika ya kati aliiambia BBC kwamba hawafahamu chochote kuhusu helikopta mbili, magari ya kijeshi na silaha nyingine zilizokuwa katika ndege hiyo.
Hata hivyo baadaye alipiga simu kufuta usemo wake kwa kusema kuwa ndege hiyo ilikuwa imebeba silaha kwa ajili ya wanajeshi wao, walioko katika kambi ya N’damena, ambazo zitapelekwa baadaye Ufaransa.

Msemaji wa Ubalozi wa Urusi mjini Abuja alisema pia ndege hiyo ni yao. Akitatanisha taarifa aliyoitoa awali kwamba ndege hiyo si yao. Kwa nini Ufaransa inatumia ndege ya Urusi kubeba silaha zake? na kwa nini ilisimama katika uwanja wa Kano, wakati ikiwa inaelekea nchi jirani ya Chad na hata Cameroun ikitokea Afrika ya kati? Kwanini baadhi ya silaha hazikuorodheshwa katika ndege hiyo kama zimebebwa?.
Hayo ni maswali yalioulizwa pande zote.

Seriakli ya Nigeria ambayo ndio muhusika mkuu wa tukio hilo, haijasema chochote.
Baadhi ya wachambuzi wanasema Nigeria inamiliki silaha hizo ilizonunua katika soko haramu. Wengine wanasema silaha hizo zilinunuliwa kutoka kwa waasi wa Seleka katika Jamhuri ya Afrika ya kati, wakielezea kwanini ndege hiyo imeingia nchini humo kutoka mji mkuu wa nchi hiyo, Bangui.
Nigeria imewekewa vikwazo vya silaha kutoka Marekani na nchi hiyo imekuwa ikiarifiwa kutumia njia zisizo halali kupata silaha kwa ajili ya kupambana na wapiganaji wa Boko haram.
Share:

MAANDALIZI YA SIKU YA UHURU YALIVYOPAMBA MOTO!........

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)MAANDALIZI ya siku ya uhuru wa Tanganyika (Tanzania Bara) Desemba 9, kutimiza miaka 53, yanaendelea Uwanja wa Uhuru ambapo kutakuwa na gwaride la kijeshi vikundi vya sanaa, kwaya, halaiki ya vijana, ‘brass band’ na matarumbeta.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Saidi Meck Sadiki, amesema milango katika Uwanja wa Uhuru itakuwa wazi kuanzia saa 12:00 asubuhi ambapo wananchi watakaofika katika hafla hiyo watatumia mlango wa kusini upande wa Barabara ya Mandela kuingia uwanjani, na waalikwa wenye kadi watatumoa mlango wa geti namba mbili 2 na viongozi watatumia geti namba tatu 3.


















Share:

Wafungwa wengi watoroshwa Nigeria..........















Watu waliokuwa na silaha wamevamia gereza katika mji wa Minna, katikati mwa Nigeria, na kuwaachilia huru wafungwa 200.
Walingia kwa nguvu kwenye jela Jumamosi katika jimbo la Niger.
Polisi wanasema haijulikani ikiwa uvamizi huo ulifanywa na kundi la wapiganaji Waislamu, Boko Haram, au gengi la wahalifu.
Boko Haram wamevamia magereza kadha katika miaka ya karibuni.
Share:

Ebola yauwa daktari mwengine S-Leone........


Wakuu wa Sierra Leone wanasema daktari mwengine amefariki kutokana na Ebola - ni daktari wa 10 kufa na ugonjwa huo.
Aiah Solomon Konoyima alifariki Jumamosi kwenye kituo cha matibabu karibu na mji mkuu, Freetown, siku moja tu baada ya wenzake wawili kufa na ugonjwa huo huo.
Mwezi wa Julai daktari maarufu kabisa kutibu wagonjwa wa Ebola nchini Sierra Leone, Sheik Umar Khan, piya mwisho aliuliwa na virusi vya Ebola. Vifo 1,600 vya Ebola vimesajiliwa nchini humo.

Sierra Leone imekuwa ikijaribu kukarabati huduma za afya baada ya vita vikali vya wenyewe kwa wenyewe katika miaka ya 1990s. Na daktari kutoka Cuba ambaye alipona Ebola, ameahidi kuwa atarudi Sierra Leone kumaliza kupambana na ugonjwa huo nchini humo.

Dakta Felix Baez, ambaye alipata Ebola nchini Sierra Leone, alisema hayo aliporudi Havana baada ya kujaribiwa matibabu aina mpya nchini Uswiswi ambayo yalimponesha.
Dakta Baez alikuwa kati ya madkatari na wauguzi wa kwanza 250 walioambukizwa Ebola Afrika magharibi.

Cuba ndio nchi iliyotuma huko wafanyakazi wa utabibu wengi kabisa kwenda kupambana na Ebola.
Mchango huo wa Cuba umesifiwa kimataifa hata na Marekani, adui yake wa kisiasa.
Share:

Mutharika ajinyima nyongeza ya mshahara.......















Rais Peter Mutharika wa Malawi na naibu wake wameakhirisha kujipa nyongeza ya mishahara baada ya kuzuka malalamiko.
Nyongeza kutoka mshahara wa dola 3,000 na kufikia dola 5,000 kila mwezi, imezusha malalamiko nchini Malawi ambako pato la nusu ya wananchi halitimii dola moja kwa siku.
Bwana Mutharika na makamo wake, Saulos Chilima wamesema hawatojipa nyongeza ya mishahara hadi uchumi wa nchi utengenee.
Kabla ya viongozi hao kushika madaraka wafadhili walisimamisha msaada wa dola 150-milioni kwa sababu ya wasiwasi kuhusu rushwa.
Mishahara ya wabunge itazidishwa asili-mia-mia-tatu (300%)
Share:

Watu kadha wauwawa karibu na Beni DRC......















Inaarifiwa kuwa watu kama 30 waliuwawa katika mashambulio kwenye vijiji mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Inaarifiwa kuwa mashambulio hayo yalifanywa Jumamosi usiku kwenye vijiji karibu na mji wa Beni ambako watu zaidi ya 250 wameuwawa tangu mwezi Oktoba.
Wakuu na mashirika ya raia yanawalaumu wapiganaji kutoka Uganda wa kundi la ADF, lakini baadhi ya wadadisi wanasema hakuna ushahidi wa kutosha wa kuhusisha kundi hilo.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.