Sunday, 19 April 2015

Jacob Zuma aapa kukabiliana na ghasia

Rais Jacob Zuma amewatembelea watu walioathirika na ghasia hizo, mauwaji pamoja na kuibwa kwa mali zao huku akiahidi kukabiliana vilivyo na wimbi la mashambulio hayo.

Bwana Zuma alifutilia mbali ziara yake nchini Indonesia, ili kukabiliana na vurumai hizo zilizoanza majuma mawili yaliyopita.Amesema kuwa ghasia hizo ni kinyume na maadili ya taifa la Afrika kusini.

Maafisa zaidi wa polisi wametumwa katika maeneo yenye mashambulio dhidi ya raia wa kigeni nchini Afrika Kusini.

Yamkini watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini.

Nchini Harare Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, alilaani ghasia hizo.

Ghasia hizo zilianza baada ya mfalme mmoja wa Kizulu, Goodwill Zwelethini, kusema kuwa raia wa kigeni sharti waondoke Afrika Kusini.

Akiongea katika kambi hiyo iliyoko mjini Durban kiongozi mkuu wa jimbo la Gauteng, David Makhura, anasema kuwa uhasama na ghasia hizo zinazoshuhudiwa, haundamani na uhuru wa miaka mingi ambayo Afrika Kusini ilipigania.





Share:

Vita vya kikabila:Watu 45 wauawa Nigeria


Takriban watu 45 wameuawa kwenye mapambano ya kikabila katika jimbo la Benue, katikati mwa Nigeria.

Polisi wanasema ghasia hizo baina ya jamii za Ologba na Egba, zilizuka kutokana na umiliki wa bwawa la samaki.

Watu zaidi waliuawa pale kundi moja liliposhambulia mazishi ya mtu aliyekufa katika ghasia za awali.

Watu wengi wamelitoroka eneo hilo.

Kumetokea mapambano mengi katika jimbo la Benue katika miaka ya karibuni, lakini mara nyingi ni mizozo baina ya wafugaji na wakulima.
Share:

Dawa ya magugu yauwa watu Nigeria


Shirika la Afya Duniani, WHO, linasema inavoelekea dawa ya kuuwa magugu ndio chanzo cha vifo vya watu 18 vilivyotokea kusini-magharibi mwa Nigeria, bila ya sababu kujulikana.

Katika siku chache zilizopita wakaazi katika jimbo la Ondo wamekufa saa chache baada ya kuhisi macho hayaoni sawasawa na kuumwa na vichwa, Baadae wakazimia.

Msemaji wa WHO alieleza kuwa ukaguzi uliofanywa hadi sasa kutafuta virusi au bacteria haukugundua kitu
Alisema kwa sasa mawazo yao ni kuwa vifo hivyo vilisa-babishwa na dawa ya kuuwa magugu.
Share:

IS watoa tena video ya mauaji


Kundi la wapiganaji wadola ya Kiislam IS limetoa video inayo onyesha mauaji ya zaidi ya watu 30 raia Ethiopia ambao ni Wakristo wakiuawa wengine kwa kuchinjwa katika ufukwe wa bahari na wengine kwa kupigwa risasi kichwani jangwani. Hata hivyo video hiyo inabainisha wazi kwamba kundi hilo la IS linawaua watu hao kwa sababu ni wakristo. Serikali ya Ethipia imesema kuwa inajaribu kufuatilia utambulisho wa utaifa wa watu hao kupitia ubalozi wa Cairo nchini Misri. Hali ya usalama nchini Libya imetetereka tangu kuangushwa kwa utawala wa Kanal Muamar Gadaf, ambapo pia ustawi wa kundi la kigaidi wa wapiganaji wa dola ya Kiislam umekuwa mkubwa.
Share:

Saturday, 18 April 2015

Balotelli ndiye aliyebaguliwa zaidi EPL


Mario Balotelli ndiye mchezaji aliyebaguliwa sana katika ligi ya Uingereza ,huku mchezaji huyo akipokea zaidi ya ujumbe 8000 ,asilimia 50 zikiwa ni za kibaguzi.
Takwimu hizo za kushtua zimeripotiwa na Kick it Out ,ambao walibaini kwamba raia huyo wa Itali alilengwa sana katika mitandao ya Twitter huku mshambuliaji wa Arsenal Danny Welbeck akipokea ujumbe 1700 asilimia hamsini zikiwa za kibaguzi.
Mshambuliaji mwenza wa Balotelli katika kilabu ya Liverpool Daniel Sturridge pia alionekana kulengwa katika mitandao ya kijamii baada ya kupokea ujumbe wa 1600 asilimia 60 ikiwa ni ujumbe wenye mwelekeo wa kijinsia.
Utafiti huo pia umebaini kwamba kilabu ya Chelsea ndio kilabu iliobaguliwa zaidi kwa ujumbe 20,000 huku liverpool ikiwa ya pili na ujumbe 19,000 Arsenal ikiwa ya tatu kwa ujumbe 12,000 huku Manchester City na Manchester United zikipokea ujumbe 11,000.
Share:

Obama: mabadiliko ya hewa hayakanushiki

Mwanamme mbele ya moto Colorado, Marekani,  Juni 2013,
Rais Obama ameonya kuwa mabadiliko ya hali ya hewa hayawezi tena kukanushwa au kudharauliwa, na amesema ndio tishio kubwa kabisa linalokabili dunia.
Katika hotuba yake ya kila juma, Rais Obama alisema anataka aweze kuwatazama watoto na wajuukuu wake machoni na kusema kuwa kila liwezalo limefanywa kupambana na msukosuko huo.
Bwana Obama hivi karibuni aliahidi kupunguza sana kiwango cha gesi inayozidisha joto inayotolewa na Marekani - kiwango cha pili kikubwa kabisa duniani - kabla ya mkutano wa viongozi wa dunia mwezi wa Disemba.
Mipango yake inapingwa vikali na wanasiasa wengi wa chama cha Republican ambao wanadai kuwa itaumiza makampuni ya Marekani.
Share:

Saudia kutoa msaada unaohitajika Yemen


Saudi Arabia, inayoongoza mashambulio ya ndege dhidi ya wapiganaji nchini Yemen, imeahidi kutoa idadi ya fedha ambayo Umoja wa Mataifa imesema inahitajika nchini Yemen.
Umoja wa Mataifa uliomba msaada huo wa kimataifa hapo jana, kwa shughuli za dharura za usaidizi nchini Yemen.
Shirika la habari la taifa la Saudi Arabia, linasema kuwa nchi hiyo itatoa dola laki mbili na 74 milioni, kama msaada wa kiutu kwa Wayemeni walioathirika na vita.

Taarifa rasmi ilisema Saudi Arabia inasimama pamoja na ndugu zake wa Yemen.
Oparesheni inayoongozwa na Saudi Arabia, dhidi ya wapiganaji wa Houthi (na askari wanaopigana kwa niaba ya rais wa zamani, Ali Abdullah Saleh, ilianza wiki tatu zilizopita.
(Umoja wa Mataifa unasema mamia ya watu wamekufa, na maelfu ya familia zimekimbia makwao wakati vita vikizidi.)
Share:

Ghasia zasababisha mauaji ya watu Libya


Zaid ya watu kumi wameuawa katika msururu wa ghasia viungani mwa mji mkuu wa Libya Tripoli.
Ghasia hizo kutoka maeneo mawili zilikuwa kati ya wanamgambo walio watiifu kwa serikali ya tripoli na wale walio watiifu kwa serikali inayatombuliwa na jamii ya kimataifa iliopo mashariki mwa taifa hilo.
Milipuko ya mabomu ya mara kwa mara pamoja na milio ya risasi imesika katika eneo la Fashloum ambapo baadhi ya watu wamekamatwa na wapiganaji walio watiifu kwa serikali ya Tripoli.
Share:

Jacob Zuma aahirisha ziara ya Indonesia


Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ameahirisha ziara yake ya ughaibuni kutokana na hali ya ghasia za kibaguzi dhidi ya wageni katika taifa lake.
Alitarajiwa kuhudhuria mkutano nchini Indonesia. Rais Zuma ambaye amekosolewa kwa kushindwa kuonyesha uongozi anatarajiwa kuitembelea kambi ya wakimbizi ya Chatsworth mjini Durban.
Polisi nchini Afrika Kusini wamewaagiza raia kutotuma ujumbe usiothibitishwa kuhusu mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni kwa sababu hatua hiyo inazua hofu.
Polisi wanesema kuwa kuna wasiwasi kuwa uvumi huo unachochea ghasia dhdi ya wahamiaji.Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ameahirisha ziara yake ya ughaibuni kutokana na hali ya ghasia za kibaguzi dhidi ya wageni katika taifa lake.
Alitarajiwa kuhudhuria mkutano nchini Indonesia. Rais Zuma ambaye amekosolewa kwa kushindwa kuonyesha uongozi anatarajiwa kuitembelea kambi ya wakimbizi ya Chatsworth mjini Durban.
Polisi nchini Afrika Kusini wamewaagiza raia kutotuma ujumbe usiothibitishwa kuhusu mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni kwa sababu hatua hiyo inazua hofu.
Polisi wanesema kuwa kuna wasiwasi kuwa uvumi huo unachochea ghasia dhdi ya wahamiaji.

Watu 30 waliakamatwa wakati wa ghasia za usiku kucha mjini Johannesburg.
Biashara kadha zinazomilikiwa na raia wa kigeni ziliharibiwa.
Takriban watu watano wameuawa kwenye mashambulizi yaliyaonza baada mfalme wa kizulu Goodwill Zwelethini kusema kuwa wageni wanahitajka kuondoka Afrika Kusini.
Share:

Watu zaidi ya 30 wauawa Afghanistan


Shambulizi la kujitoa mhanga kwenye mji ulio mashariki mwa Afghanistan wa Jalalabad limewaua watu 33 na kuwajeruhiwa karibu wengine 100.
Ripoti zinasema kuwa shambulizi hilo lilitokea karibu na benki ambapo wafanyikazi wa serikali wanalipwa misharaha yao.
Maafisa wanasema kuwa mtu aliyeendesha shambulizi hilo alikuwa na pikipiki.
Kulitokea shambulizi la pili karibu na madhabahu mjini Jalalabad lakini haijulikani kama kulikuwa na madhara yoyote.
Hakuna kundi lililokiri kuhusika, lakini mji wa Jalalabad umekuwa ukilengwa kila mara na kundi la Taliban.
Share:

Friday, 17 April 2015

Somalia yalenga kushiriki mechi za CAF


Rais wa shirikisho la soka nchini Somalia Adbi Qani anatumai kwamba taifa lake litashiriki katika michuano ya kombe la Afrika mwaka 2019 na kumaliza kiu ya taifa hilo tangu mwaka 1974.
Walishiriki katika kombe la mataifa ya Afrika mara moja kutokana na ghasia za kisiasa,ukosefu wa fedha na miundo msingi mibovu.
Pamoja na Eritrea nchi hizo mbili hazitashiriki katika mechi za kufuzu za mwaka 2017.
Ni mataifa hayo mawili katika shirikisho la soka barani afrika CAF yatakayokosa kushiriki.
Lakini Qani anaamini kwamba huu uwanja mpya ukitarajiwa kumalizwa kujengwa baadaye mwaka huu ,taifa hilo hilo linajiandaa kurudi katika michuano hiyo kabla ya kukamilika kwa muongo huu.
Share:

Waasi Ukrain: makubaliano yatashindwa


Kiongozi wa cheo cha juu zaidi anayeiunga mkono Urusi katika eneo linalothibitiwa na waasi mashariki mwa Ukrain amesema kuwa usitishwaji wa mapigano ulioafikiwa mapema mwaka huu na serikali hautadumu.
Alexander Zakharchenko aliiambia BBC kuwa maafikiano ya Minsk yangefanikiwa tu ikiwa serikali ya Ukrain ingetambua jamhuri iliyojitenga anayoiongoza eneo la Donetsk.
Bwana Zakharchenko aliongeza kuwa kile angependa kuona ni kupanuka zaidi kwa eneo hilo.
Chini ya makubaliano ya Minsk ambayo yaliungwa mkono na Urusi , Ujerumani na Ufaransa , serikali ya Ukrain ungerejesha mipaka chini ya udhibiti wake.
Mapigano yameendelea licha ya kuwepo kwa makubaliano hayo.
Share:

Washukiwa wa ugaidi wakamatwa Australia


Polisi katika jimbo la Victoria nchini Australia wanasema kuwa wamewakamata wanaume watano kufuatia oparesheni kubwa ya kupambana na ugaidi kwenye mji wa Melbourne.
Wawili kati ya wanaume hao walio na umri wa miaka 18 walikamatwa baada ya kushukiwa kupanga mashambulizi ya kigaidi yaikiwemo ya kuwalenga polisi.
Mshukiwa mwingine naye alikamatwa kufuatia sababu zinazohusiana na silaha. Shughuli za kuwatafuta washukiwa wengine zinaendelea sehemu zingine za mji wa Melbourne.
Share:

Hussein Machozi asema bado yupo hai


Mwimbaji wa wimbo ''Kafia Ghetto'' na 'Jela' Hussein machozi ameshtumu uvumi unaondelea kwamba amefariki baada ya ajali mbaya ya barabarani iliotokea katika mji wa Dodoma nchini Tanzania siku ya jumatano.
Kulingana na gazeti la Daily Nation nchini Kenya habari za kifo chake zilianza kuenea katika mitandao ya kijamii baada ya ajali hiyo ambapo mtu mmoja aliyeonekana kufanana na msanii huyo alifariki kutokana na majeraha.
Hussein amesema kuwa yuko hai na buheri wa afya kupitia mtandao wake wa facebook ambapo alisema kuwa habari hizo zilimwacha mamaake na dadaake wagonjwa baada ya kuzirai waliposikia habari hizo.
Huu ndio ujumbe alioandika katika mtandao wake wa facebook.
{Nilijiandaa hapa nimekwenda mazoezini kucheza mpira, niliacha simu yangu kwenye charge na niliporudi baada ya mazoezi nakuta missed calls nyingi sana, msg na simu za mama yangu pamoja na dada, wakati najiandaa kuanza kupiga simu ghafla naanza kupata simu za watu mbalimbali kwamba nimepata ajali na kufariki, mimi nikawaambia sio kweli mimi ni mzima na nipo}
Share:

Ashtakiwa kwa kumtia mimba mwanawe


Mahakama moja mjini Bungoma nchini Kenya imemshtaki afisa mmoja wa wadi ya Bukembe kwa kulala na mwanawe wa kike mwenye umri wa miaka 14 kwa zaidi ya miaka miwili baada ya mkewe kufariki mwaka 2013.
Kulingana na gazeti la The Standard nchini Kenya,mwathiriwa ambaye ni mjamzito wa miezi minne amesema kuwa mshukiwa huyo ambaye ni babaake amekuwa akimlazimisha kufanya mapenzi naye kila usiku na kumuonya kwamba angemdhuru iwapo angemwambia mtu yeyote.
''Babaangu pia ameninyima fursa ya kwenda katika shule ya upili licha ya mimi kufanya vyema katika mtihani wa KCPE. Mwaka 2013,nilifanya vyema lakini akanilazimisha kurudia darasa. Mwaka jana nilifanya vizuri zaidi lakini anadhani kwamba iwapo nitajiunga na shule ya upili ya bweni,nitamkosesha fursa ya kufanya tendo la ngono nami'',.Mwathiriwa aliiambia mahakama.
Hakimu mwandamizi Peter Ireri alimwachilia mtuhumiwa kwa dhamana ya shilingi laki moja ama pesa taslimu shilingi elfu ishirini.
Share:

Kanye West azindua biblia yake


Kanye West Hujulikana sana kwa maringo yake,lakini kwa kweli Kanye West asingekufuru na kujitambulisha kama mungu katika biblia hiyo.
Kitabu hicho kitukufu kimebadilishwa na kuwa Biblia ya sasa kwa jina ''Yeezus'' na amini usiamini kila neno la Mungu katika kitabu hicho limeondolewa na badala yake msanii huyo wa muziki wa kufoka foka ameweka jina lake.
Kulingana na gazeti la The Independence nchini Uingereza,kitabu hicho kinasema kuwa katika kizazi hiki ,Kanye West ndio mkubwa na vilevile kiongozi wa kidini
Kitabu hicho kinaongezea kwamba ''katika utangulizi wetu tunamsherehekea Kanye West na vile alivyotufanyia katika maisha yetu''

Ijapokuwa Kanye hajatoa tamko lolote kuhusu wadhfa huo aliojipatia,amekuwa akijifananisha na Mungu hapo mbeleni.
''Mungu alinichagua mie,alinitengezea njia.Mimi ni chombo cha mungu'',alisema mwaka 2009.
''Lakini kinachoniudhi maishani mwangu ni kwamba sitawahi kujiona nikicheza muziki moja kwa moja''.,aliongezea.

Wasanii wengine waliofananishwa na Yeezy ni Marilyn Monroe na Michael Jackson.
Share:

18 waaga katika ajali Tanzania


Watu wasiopungua 18 wameuawa katika ajali ya gari mkoa wa Mbeya Kusini Magharibi mwa Tanzania baada ya basi dogo la abiria kuanguka na kutumbukia kwenye bonde lenye maji.
Mwandishi mmoja wa habari aliyefika eneo la ajali ameeleza kuwa basi hilo dogo limetumbukia bondeni katika eneo lenye mteremko mkali na kona.
Polisi wanachunguza chanzo cha ajali, lakini walioshuhudia wanadai dereva wa gari hilo alikuwa akiwakimbia madereva wengine
waliotaka kumlazimisha aunge mkono mgomo wa utoaji huduma unaoendelea kwa safari za kati ya Mbeya na Kyela.
Imeelezwa kuwa madereva wa mabasi ambayo kwa kawaida hutoa huduma kati ya eneo la Kyela na Mbeya mjini walikuwa katika mgomo,
na kwamba hawakufurahishwa na basi hilo dogo kuendelea kutoa huduma ndipo wakawa wanamfukuza hatimaye akashindwa kulidhibiti
Ajali hiyo ni mwendelezo wa ajali mbaya za barabarani kuhusisha magari ya abiria ambazo zimetokea Tanzania kwa kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
Share:

Wageni waendelea kushambuliwa A Kusini


Kumekuwa na mashambulizi zaidi usiku dhidi ya biashara zinazomilikiwa na raia wa kigeni nchini Afrika Kusini.
Polisi walitumia gesi ya kutoa machozi na risasi za mipira kutawanya umati kusini mwa mji wa Johannesburg ambapo gari na nyumba vilichomwa moto.
Msemaji wa polisi aliiambia BBC kuwa karibu raia mia mbili wa kigeni walikimbilia usalama kwenye kituo cha polisi lakini wakaondoka muda baadaye.

Usalama umedumishwa kufuatia mashambulizi yaliyowalenga raia wa kigeni ambapo watu watano wameuawa.
Rais Jacob Zua amelaani ghasia hizo na maandamano ya amani mjini Durban siku ya Alhamisi yalihudhuriwa na zaidi ya watu elfu kumi.
Share:

Mwanzilishi wa IS auawa nchini Iraq


Runinga nchini Iraq imeripoti kuwa Izzat Ibrahim al-Douri, ambaye wakati mmoja alikuwa makamu wa Rais Saddam Hussein na mmoja wawaanzilishi wa kundi la Islamic State nchini Iraq, ameuawa.
BBC bado haijapata taarifa rasmi ya kuthibitisha kifo chake, lakini picha na maelezo kuhusu kifo cha Bwana Al Douri imeripotiwa pakubwa.
Iwapo taarifa hiyo ni kweli, kifo chake kitakuwa hatua kubwa kwa serikali ya Iraq dhidi ya makundi ya Jihadi.
Al Douri ambaye daima ana masharubu mekundu, alikuwa mfalme katika kilabu kwenye kadi zilizotolewa ili kusaidia majeshi ya Marekani kutawambua wanachama katika utawala wa Saddam Hussein, mnamo mwaka 2003.
Share:

Raia wa Burundi waandamana dhidi ya rais


Polisi nchini Burundi wamerusha mabomu ya kutoa machozi na maji, ili kuwatawanya mamia ya waandamanaji katika mji mkuu Bujumbura.
Maandamano hayo ni ya kumpinga Rais Pierre Nkurunziza, kutowania tena kiti cha Urais katika uchaguzi mkuu ujao, unaopangiwa kufanyika mwezi Juni.
Mwaandishi wa BBC mjini Bujumbura, anasema kuwa malori makubwa yanayobeba vitoa machozi yamewekwa tayari kukabiliana na waandamanaji hao kote katika mji huo.
Anasema kuwa wazazi wamekimbia shuleni ili kuwaondosha watoto wao na kuwapeleka nyumbani.
Bwana Nkurunziza hajasema hadharani iwapo atawania kiti cha urais kwa muhula mwingine, lakini kuna tetesi kuwa ana mpango wa kufanya hivyo.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.