Tuesday, 16 December 2014

Tahadhari:'Hatari za urembo bandia'.

Kilio cha uchungu baada ya upasuaji wa pua ili kunyooshwa
Huwezi kuepuka matangazo ya mauzo kila utembeapo katika Mji wa Seoul,utapata wito wa kukutaka ubadilishe umbo kwa njia ya upasuaji wa kuongeza urembo bandia.
Katika mtaa wa ukwasi wa Gangnam,kila ukuta una ishara ya kukuelekeza sehemu ya upasuaji wa aina hii
Kwenye treni na mitaani,unaelezewa kuwa ''unaweza kurudisha uchanga usoni mwako.''kuweka ama kuondoa mikunjo usoni'' inapendekezwa kufanyiwa-''upasuaji wa matiti'',''kuzuia kuzeeka'' ''kubadili kope za macho''''kupunguza nyama na ngozi inayolegea mwilini''..........>>>INGIA HAPA<<<
Share:

Mtoto amuibia nyanyake na kuwashangaza wengi.


Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 11 aliiba maelfu ya dola kutoka kwa nyanyake na kisha kukodi taxi kumpeleka eneo la mbali kukutana na kijana mwenye umri wa miaka 16 ambaye walikuwa wakiongea naye tu kupitia mtandao wa Internet.
Wawili hao hawajawahi kuonana hata siku moja.
Msichana huyo Alexis Waller yuko salama na bukheri wa afya na hatakabiliwa na kesi yoyote baada ya kitendo chake ambacho kimewashangaza wengi.
Maafisa wanasema Waller aliiba dola elfu kumi kutoka kwa chumba cha nyanyake katika mji wa Bryant, jimbo la Arkansas.
Baada ya kitendo chake cha wizi, msichana huyo alikodisha taxi na kumtaka dereva kumpeleka kwa kijana huyo katika jimbo la Florida.
"nilisema nitaka kwenda mjini Jacksonville, Florida," Waller aliambia shirika la habari la KARK. "kijana huyo aliniuliza kama nina pesa na nikamwambia ndio. ''
Gharama ya safari yake ilikuwa dola 1,300.
Jarida la Arkansas Democrat-Gazette linasema kuwa Waller alikuwa tayari amesafiri umbali wa maili 500 kuelekea kwa kijana huyo lakini polisi waliweza kuwasiliana na dereva wa taxi hio na kuwafuata.
Wazazi wake walisema Waller aliwakasirisha sana lakini ni afunei kwao kwani mtoto wao aliweza kurejea nyumbani
Share:

Alipanda kreni kumposa mpenzi.Yalomkuta?


Mwanamume mmoja raia wa udachi amejikuta akikimbilia usalama wake baada ya jaribio la kutaka kumposa mpenzi wake kwa mbwembwe kwenda mrama.
Mtu huyo ambaye hakutajwa kwa jina anayeishi mjini Ijsselstein alikodisha 'kreni' au Crane na kuipanda akipanga kwamba kreni hilo imtoe chini na kumpanidhs hadi dirishani mwa mpenzi wake ambapo angemchezea wimbo na kisha kumposa.
Badala yake yaliyomkuta hakuyatarajia kabisa.Kreni hiyo ilianguka chini na kupita dirishani kwa mpenzi wake huku ikiangukia nyumba za majirani.
Mwanamume huyo alilazimika kukimbilia usalama wake na hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo lililowaacha wengi wakiangua kicheko.
Kwa mujibu wa jarida la Algemeen Dagblad, mpenzi wake mwanamume huyo alimkubali na kusema yuko radhi kuolewa naye licha ya tukio hilo.
Baada ya kuongea na polisi, wawili hao walisafiri kwenda mjini Paris Ufaransa kusherehekea.
Kreni hio ilianguka tena kwa mara ya pili ilipokuwa inainuliwa na hata kuharibu zaidi nyumba za majirani. Meya wa mji huo, amezomewa na wengi baada ya eneo hilo kusemekana kutokuwa salama.
Share:

Roboti zapata ajira mgahawani China


Hadimu hivi karibuni huenda wakakosa ajira maana roboti zimezinduka
Mgahawa mmoja nchini China umeanza kutumia Roboti badala ya kuwaajiri hadimu au wafanyakazi wa hotelini kuwapakulia chakula na vinywaji wageni.
Share:

Wafungwa Philippines waponda raha.


Polisi mjini Manila wamevamia gereza moja na kuushangaza umma wa Philippines baada ya kung'amua maisha ya anasa yanayoendelea ndani ya gereza hilo kwa kikundi cha baadhi ywa wafungwa wenye upendeleo wa kipekee.
Uvamizi huo umefanywa katika gereza hilo la Bilibid lenye wafungwa wengi nchini humo kufuatia taarifa kwamba mtandao wa dawa za kulevya nchini humo unafanya kazi katika gereza hilo kwa njia za panya.

Baada ya uvamizi huo maafisa wa polisi walikuta wafungwa hao wakiwa wamefunga viyoyozi,mabafu ya kuogea ya kisasa yenye marumaru na kupambwa kwa mawe ya thamani,makasha ya kuhifadhia fedha,saa za gharama na fedha lukuki.
Wafungwa hao walifanikiwa pia kununua pombe kali za gharama kubwa ,komputa na hata simu za kisasa za gharama kubwa.kufuatia tukio hilo serikali ya Philippine imeahidi kufanya uchunguzi wa kina.
Share:

''Niliokoa Kenya 2013'' asema Moreno Ocampo.


Kiongozi wa zamani wa mashitaka katika mahakama ya jinai ya ICC, ameteta uamuzi wake wa kumshitaki Rais Uhuru Kenyatta licha ya kesi hiyo kutupiliwa mbali.
Bwana Luis Moreno Ocampo anasema kua mashitaka hayo dhidi ya Uhuru yalizuia ghasia kutokea tena katika uchaguzi wa mwaka 2013.
Kenyatta alishinda uchaguzi huo baada ya kugombea kwa tiketi ya chama cha TNA, huku akiituhumu mahakama hiyo kwa kuingilia maswala ya ndani ya Kenya.
Alishtakiwa kwa kosa la kuchochea ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007.
Wiki jana mrithi wa Ocampo, Fatou Bensouda, alitupilia mbali kesi hio dhidi ya Kenyatta akisema amekosa kupata ushahidi wa kutosha kuthibitisha mashitaka dhidi ya Uhuru.
Kenyatta hata hivyo tangu mwanzoni alikanusha madai ya kutenda uhalifu dhidi ya Binadamu.
Alikuwa Rais wa kwanza aliye mamlakani kuwahi kufikishwa katika mahakama hio ambayo wengi wanasema ni ya kisiasa.
Watu 1,200 walifariki na wengine 600,000 kutoroka makwao katika ghasia hizo ambazo ndio mbaya zaidi kuwahi kushuhdiwa nchini humo tangu ijinyakulie uhuru.
Ocampo aliambia BBC kwamba kushitakiwa kwa Uhuru kulizuia ghasia kutokea tena nchini Kenya, wakati wa uchaguzi mwaka 2013. ''Mahakama ya ICC ilibadilisha siasa za Kenya, '' alisema Ocampo.
Wiki jana Rais was Uganda Yoweri Museveni alirejelea wito wake kwa mataifa ya Afrika kujiondoa ICC akisema kuwa mahakama hio inakandamiza mataifa ya Afrika.
Hata hivyo Ocampo amesema mahakama ya ICC ilikuwa kizingiti kwa viongozi kumi ambao walitegemea na kutumia sana ghasia ili kusalia mamlakani.
Share:

Idadi ya waliouawa Pakistan yafika 130.



Vikosi vya usalama nchini Pakistan vinakabiliwa na hali ngumu kuweza kudhibiti shule iliyovamiwa na wapiganaji wa Taliban katika jimbo la Peshawar Kaskazini Magharibi mwa Pakistan
Takriban watu miamoja na thelathini wamefariki , wengi wao wakiwa watoto.
Msemaji wa jeshi anasema washukiwa sita wameuawa huku operesheni hio ikiendelea.
Shule hio inasimamiwa na jeshi na wanafunzi wengi ni watoto wa wanajeshi.
Wakuu wa Hospitali wanasema kuwa zaidi ya watu 40 wanasemekana kujeruhiwa japo idadi hiyo inatarajiwa kupanda zaidi.
Maafisa mjini Peshawar wanasema kuwa wanaume watano ama sita waliokuwa na silaha waliingia shuleni humo wakiwa wamevalia magwanda ya kijeshi .


Wanafunzi mia tano na waalimu walikuwa katika shule hiyo ya umma ya kijeshi wakati sham,bulizi hilo lilipotokea .
Wakazi wa eneo hilop wanasema kuwa walisikia milio ya bunduki iliyodumu kwa dakika kadhaa .
Wanasema pia kuwa walisikia sauti za kelele za wanafunzi na waalimu .


Haijabainika wazi ni kwa namna gani wanamgambo wa Talebain waliweza kupenya hadi kuingia ndani ya majengo hayo yanayomilikiwa na jeshi.
Jeshi la Pakistan limesema operesheni ya uokozi ilikuwa ikiendelea na kwamba wengi wa wanafunzi na waalim wameokolewa toka eneo la hatari.
Shambulio hilo limetokea wakati operesheni kubwa ya kijeshi ikiendelea dhidi ya wapiganaji wa Taleban wa Pakistan na wanamgambo wengine wanaoendesha harakati zao kaskazini mwa jimbo la Waziristan.
Share:

Sunday, 14 December 2014

Vikosi vya Libya vyatibua shambulizi.


Wapiganaji wazidi kushambuliana nchini Libya tangu kuanguka kwa utawala wa Muamar Gadaff....

Shambulizi lililolenga kituo muhimu cha mafuta mashariki mwa Libya halikufua dafu kutokana na mashambulizi ya angani yaliotekelezwa na vikosi vya serikali vinavyotambuliwa kimataifa.
Kamanda mmoja wa jeshi la wanahewa anasema kuwa mashambulizi ya angani yaliwalenga watu wenye silaha waliokuwa wakisonga mbele katika kituo cha mafuta cha Al-Sidra ambapo watu wengi waliuawa.

Zaidi ya miaka mitatu tangu kuanguka kwa utawala wa kanali Muamar Gadaffi serikali hasimu bado zinapigania madaraka nchini Libya.
Share:

Jenerali aliyempinga Museveni arudi UG........























Jenerali Sejusa aliyeitoroka uagnda baada ya kutofautiana na rais Musevenei hadharani

Mwanajeshi wa Uganda ambaye alitofautiana hadharani na rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni mwaka uliopita amerejea nchini Uganda bila kutarajiwa kutoka nchini Uingereza ambapo alikuwa amekimbilia uhamishoni.
Jenerali David Sejusa aliitoroka Uganda baada ya kumshutumu rais Museveni kwa kujaribu kubuni familia ya kifalme akitaka kumkabidhi uongozi mwanawe wa kiume.
Sejusa pia alidai kuwa kulikuwa na njama ya kuwaua watu fulani katika serikali na jeshini ambao walikuwa wakipinga mpango huo.





















Rais Museveni anayedaiwa kumtayarisha mwanawe ili kuchukua utawala wa Uganda

Alipowasili mjini kampala Jenerali Sejuse alikutana na mkuu wa ujajusi ambapo pia aliwaambia waandishi wa habari kuwa rais Museveni alifahamu kuhusu kurejea kwake.
Share:

Zaidi ya abiria 100 wazama DRC.....















Ripoti kutoka Jamhuri ya Demokrasi ya Congo zinaeleza kuwa watu zaidi ya 100 wanafikiriwa kuwa wamekufa katika ajali ya feri.
Jahazi iliyojaa abiria imezama katika Ziwa Tanganyika kusini-mashariki mwa nchi siku ya Alkhamisi.
Waziri wa usafiri wa jimbo hilo la Katanga, Laurent Sumba Kahozi), aliliambia shirika la habari la Ufaransa kuwa miili kama 129 imepatikana.
Inaarifiwa watu 232 walinusurika.
Ajali hiyo ilitokea Alhamisi usiku kaskazini mwa jimbo la Katanga baina ya miji ya Moba na Kalemie.
Waandishi wa habari wanasema ajali kama hizo zinatokea kawaida kwa sababu feri mara nyingi zinakuwa zimejaa mno.
Share:

Saturday, 13 December 2014

Maelfu waandamana Washington na New York........
















Maelfu ya watu wanatarajiwa kuandamana katika bara-bara za miji ya Washington na New York kupinga mauaji ya wanaume weusi wasiokuwa na silaha yaliyofanywa na polisi wa Marekani, ili kulitaka bunge lilinde wananchi.

Taarifa iliyotolewa na kiongozi wa kutetea haki za raia, Al Sharpton, ilieleza kuwa bunge linahitaji kuchukua hatua kubadilisha sheria na hali bara-barani.
Kati ya wataohudhuria maandamano hayo ni familia za Michael Brown, kijana aliyeuwawa katika jimbo la Missouri, na Eric Garner, ambaye alikufa wakati anakamatwa mjini New York.
Kesi za askari polisi waliohusika na vifo hivyo zilifutwa na kuzusha maandamano kote Marekani.
Share:

Al-Bashir asema ameishinda ICC........















Rais Omar al-Bashir wa Sudan amedai ushindi katika mvutano wake na Mahakama ya Jinai ya Kimataifa, ICC, baada ya mkuu wa mashtaka wa ICC, Fatou Bensouda, kusimamisha uchunguzi kuhusu madai ya uhalifu wa vitani katika jimbo la Darfur.
Rais Bashir, ambaye alishtakiwa kwa mauaji ya kikabila mwaka wa 2009, alisema ICC imeshindwa katika kile alichoeleza kuwa juhudi za ICC za kuiaibisha Sudan.
Alisema wananchi wameamua kuwa afisa yoyote wa Sudan asisallim amri kwa mahakama ya kikoloni.
Fatou Bensouda alisema Ijumaa kwamba kwa vile Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa halikuchukua hatua basi wanaofanya uhalifu wa vitani Darfur wamepata nguvu kuendelea na ukatili wao hasa dhidi ya wanawake na wasichana.
Share:

Watu 3 wauawa katika vita Somalia......


Mapigano kati ya vikosi vya serikali na wanamgambo katikati ya Somali yamesababisha vifo vya watu watatu.
Pande hizo mbili zinapigania udhibiti wa jimbo la Galgadud ambalo linatarajiwa kuwa miongoni mwa majimbo ya serikali ya Somali.
Pande zote zinadai kudhibiti mji mkuu wa jimbo hilo Dusa Mareb na kuna mapigano mengine kusini magharibi kutoka kwa kundi la Ahlu Sunna,ambalo ndio kundi la kwanza lililowafukuza wapiganaji wa Alshabaab katika eneo hilo mwaka 2011 wakisaidiwa na wanajeshi wa Ethiopia.
Kundi la Ahlu Sunna limekuwa likiunga mkono Serikali ya Mogadishu lakini sasa viongozi wake wanasema kuwa wametengwa katika mpangilio mpya wa utawala.
Share:

Mahujaji milioni 17 wakusanyika Karbala...........















Mamilioni ya mahujaji wa Kishia wamemiminika katika mji wa Karbala, Iraq, kwa ibada ya kila mwaka ya Arbaeen ingawa kuna tishio la mashambulio ya wapiganaji wa madhehebu ya Sunni wa Islamic State.
Wakuu wa Iraq wanasema mahujaji zaidi ya milioni 17 wamekusanyika Karbala kuhudhuria Arbaeen.
Picha zilizopigwa kutoka angani zinaonesha barabara zinazoelekea Karbala kama mito ya watu waliovaa nguo nyeusi, hadi upeo wa macho.
Na kuna wasiwasi kuwa mji wa Karbala hautaweza kuwapatia malazi waumini wote.
Ulinzi mkubwa umewekwa kuzuwia mashambulio ya wapiganaji wa Islamic State.
Arbaeen ni siku ya mwisho ya maombolezi baada ya kifo cha Imam Hussain cha karne ya 7 katika Vita vya Karbala - tukio muhimu ambapo Wasunni waligawanyika na Washia.
Share:

Thursday, 11 December 2014

Ebola bado tishio Sierra Leone......















Maafisa wa Afya nchini Sierra Leone wamegundua miili kadhaa katika maeneo ya mgodi wa Almasi, na kusababisha hofu kuwa pengine ugonjwa wa Ebola haujaripotiwa ipasavyo.
Shirika la afya duniani,WHO limesema limebaini kisa hiki kipya mashariki mwa mji wa Kono, timu ya Wataalamu imepelekwa Kono kufanya uchunguzi kuhusu uwepo wa ugonjwa wa Ebola.
Watu 6,346 wamepoteza maish akutokana na ugonjwa huo na zaidi ya 17,800 wameathirika na Ebola.

Sierra Leone ina idadi kubwa zaidi ya Watu wenye Ebola Afrika Magharibi, ikiwa na Watu walioathirika 7,897 tangu kuanza kwa ugonjwa huo.
WHO imesema katika kipindi cha takriban siku 11 mjini Kono, Miili 87 ilizikwa.
Miili ya Watu waliokufa kutokana na maradhi ya Ebola ni hatari kwa maambukizi hivyo huzikwa kwa uangalifu mkubwa ili kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo.
Share:

Mwanawe Rais Zuma hatiani Afrika Kusin....


Jopokazi moja nchini Afrika Kusini limesema kua mwanawe Jacob Zuma hakua makini alipokuwa anaendesha gari hadi kusababisha ajali ya barabarani ambapo mwanamke mmoja alifariki.
Awali kiongozi wa mashitaka hakuwa tayari kumchukulia hatua zozote za kisheria mwanawe Zuma. Sasa atakabiliwa na shinikizo za kumfungulia mashitaka.

Gari la Duduzane Zuma aina ya Porsche iligonga gari dogo la abiria mjini Johannesburg mwezi Februari, na kumuua mwanamke huyo papo hapo.
Mwandishi wa BBC Pumza Fihlani mjini Johannesburg anasema uamuzi huo unaonyesha uhuru wa vyombo vya sheria nchini humo.

Katika nchi ambapo swala la usawa bado ni tete, mahakama ndio mojawpao ya sehemu chache ambapo usawa unapatikana kwa wananchi na mwanawe Rais hajasazwa kwa hilo.
Rais Zuma ana watoto 21 na ameoa mara sita.

Duduzane mwenye umri wa miaka 30 aliambia jopokazi hilo kwa alipoteza mwelekeo wa barabaraalipokuwa anaendesha gari na kuingia ndani ya maji taka.
Hata hivyo hakimu alimwambia kwamba hakua na tabia njema hasa baada ya tukio hilo.
Mwezi Julai mamlaka ya mashitaka ilikataa kufungulia mashitaka kijana huyo ambaye pia ni mfanyabiashara na kosa la mauaji bila ya kukusudia ikisema hakuna ushahidi wa kutosha.
Share:

Punda watumiwa kutoa ujumbe Kenya......


Hii leo kulikuwa na taharuki katikati mwa mji wa Nairobi baada ya Punda waliokuwa wamepakwa rangi kupatikana wakizurura mjini humo.
Walikuwa na maandiko katika mwili wao yakisema: 'Tumechoka'
Neno 'Tumechoka' ni kauli mbiu ambayo ilitumiwa na mashirika ya kijamii kuelezea wasiwasi kuhusu hali ya utovu wa usalama nchini kote.

Kauli mbiu hio ilitumiwa mashambulizi yalipofanywa dhidi ya wakenya mjini Mandera Kaskazini mwa Kenya ambapo wanaharakati walipiga kambi katika ofisi ya Rais wiki kadhaa zilizopita kulalamikia ukosefu wa usalama.
Kwa kutumia Punda, kupitisha ujumbe wao, ni dhahiri kuwa ujumbe wao umefika kwa wengi.
Wanaharakati hao, wamewahi kutumia Nguruwe kuonyesha walivyo walafi na wafisadi wanasiasa wa Kenya.
Punda hao walikuwa 22 na walifikishwa kati kati ya mji kwa Lori. Dereva wa lori hilo alisema kuwa alilipwa na mtu flani kupeleka wanyama hao mjini.
Lori hilo lilipofikishwa mjini, mwanamume aliyekuwa amekodisha lori hilo aliamua kutoka kwenye Lori na wanyama hao.


Wanyama hao walinuiwa kutuma ujumbe kwamba wakenya wamechoshwa na hali mbaya ya usalama, alisema mwanaharakti mmoja aliyekuwa kwenye Lori hilo.
''Tumechoshwa na uongozi mbaya, '' alisikika akisema mwanaharakati mmoja huku akiwaskuma Punda hao kutoka kwa Lori.
Polisi wanasema wanawasaka wale waliohusika na kitendo hicho.
Share:

Baiskeli iliyotengezwa kwa dhahabu...........


Ni rahisi sana kwa watu kulalamikia gharama ya kununua baiskeli wengi wakitaka bei nafuu. Nyingi ya baiskeli nchini Uingereza huuzwa kwa pauni 1,000 shilingi lakini moja na arobaini pesa za Kenya.
Kwa wengi nchini humo hizo ni pesa nyingi sana.
Hata hivyo baikeli mpya iliyotengezwa kwa dhahabu imezinduliwa nchini humo. Bei yake? Pauni laki mbili na hamsini au milioni 36,250,000 pesa za kenya. Bei hii ni ghali hata kuliko bei ya gari jipya la Ferari, kukufahamisha tu.















Baiskeli hio ambayo ilitengezwa na kampuni ambayo hutengeza vitu vya kifahari, Goldgenie imetengezwa kwa dhahabu kutoka kwa mikono na vyuma vyake vyote. Kiwango cha dhahabu iliyotumiwa ni karati 24.
Wataalamu wa kampuni hio ya Goldgenie, wameweka dhahabu katika vyuma vya baiskeli hio vyote , mnyororo na mfumo unaofanya baiskeli kwenda na kubadilisha gia vyote vimewekwa dhahabu.
















Na wakati baiskeli hio inavutia macho, inapowekwa nyuma ya kabati ya glasi na kulindwa na walinzi. Mkrugenzi wa kampuni hio anasema baiskeli hio inaweza kuendeshwa kwenye barabara.
"baiskeli hii sio tu ya kuvutia macho, bali pia ni nzuri ya kuendesha ikiwa mwenye kuiendesha atsatahimili kuangaliwa sana.''
Muundo wa baiskeli hii ni wa hali ya juu,'' aliongeza kusema mkurugenzi huyo.
Kwa sasa haijulikani idadi ya baiskeli hizo zitakazotengezwa, lakini ikiwa utakuwa na bahati sana unweza kupata moja kama hio. Lakini itakubidi ununue kufuli kuifungia baiskeli yako ikiwa hautakuwepo ambako umeiwacha.
Share:

Wednesday, 10 December 2014

Matatani kwa kumvua nguo mwanamke Kenya.......


Wafanyakazi wa basi moja waliotuhumiwa kwa kumnyanyasa kimapenzi mwanamke wanakabiliwa na hukumu ya kifo baada ya kushitakiwa kwa kosa la wizi wa mabavu.
Watu watatu wakiwemo wafanyakazi wanaofanya kazi katika basi hilo walikamatwa mwezi jana baada ya mwanamke huyo kujitoza na kusidia polisi kwuatambua watu waliomvamia.
Kanda ya video iliosambaa kwenye mitandao ya kijamii nchini Kenya na kusababisha maandamano ya wanawake nchini Kenya akiwasihi kutombaka na kuingiza chupa katika sehemu zake za siri.
Hata aliwasihi awape pesa wakati walipokuwa wanamtisha lakini wakakataa.
Mamia ya waandamanaji waliandamana mjini Nairobi baada ya tukio hilo na kulaani kitendo cha wanaume kuwavua wanawake nguo kwa kisingizio kuwa wamevalia nguo fupi sana au vimini hasa katika vituo vya basi.

Maandamano hayo yalipangwa kupitia kwa mtandao wa kijamii. Kauli mbiu ya maandamano hayo ilikuwa #MyDressMychoice yaani nitavalia kama nipendavyo.
Polisi walilazimika kubuni kikosi cha kuchunguza wale wanaowavua wanawake nguo zao kwa madai kuwa wamevalia nguo fupi sana.
Takriban wanawake watano wamevuliwa nguo zao mjini Nairobi na katika mji wa Mombasa pwani ya Kenya.

Polisi mmoja wa utawala alikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la kumvua nguo mwanamke mjini Nairobi.
Serikali ya Kenya imesema itafuta leseni za kampuni za basi ambazo wafanyakazi wake wanapatikana na hatia ya kuwavua nguo wanawake.
Share:

Ashindwa kujizuia kula 'Tissue'.....

 Mama mwenye watoto watano, ameelezea kuwa yeye hula roli moja ya karatasi ya msalani au Tissue kila siku.
Jade Sylvester,mwenye umri wa miaka 25, alianza kutamani kula karatasi hio alipokuwa mjamzito lakini hata baada ya kujifungua yeye hujipata akila roli moja ya tissue kila siku.
Kwa mujibu wa jarida la Mirror, Uingereza, kwa mara ya kwanza alipata hamu ya kula karatasi hio ni pale alipokua na mimba ya mtoto wake mdogo Jaxon.

Jade, anayetoka mtaa wa Gainsborough, Lincolnshire, alinukuliwa akisema, "miezi mwili tangu kushika mimba hio, nilianza kutamani kula karatasi ya chooni. Hadi sasa sijui kwa nini mimi bado huila. ''
"ninapenda tu ninavyojisikia nikiiweka mdomoni mwangu, lakini sipendi ladha yake. Familia yangu huniambia sio visuri kwangu kuila , lakini siwezi kujizuia. ''

Licha yakujifungua mwanawe miezi 15 iliyopita, Jade hawezi kabisa kujizuia kutokula karatasi hio.
Mama huyo ambaye hafanyi kazi, anasema yeye husubiri anapopata haja kwenda chooni na hapo ndipo haunza kuila karatasi ile. Yeye huitafuna na kuimeza yote kila siku.
Amepata wakati mgumu kujaribu kukomesha uraibu wake tangu alipojifungua lakini anasema ameshindwa kabisa.

''Najua kwamba sio vyema kwa afya yangu, lakini hadi sasa sijapata matatizo yoyote ya kiafya kama wanavyohofia watu wengi.''
Jade ana watoto watano , wavulana wanne na msichana mmoja.
Anasema yeye hujaribu kujificha kutoka kwa wanawe kwa sababu anahofia wakimpata akila karatasi hio watamkanya sana.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.