Sunday, 28 December 2014

Indonesia yasitisha utafutaji wa Airasia.


Indonesia imesitisha utafutaji wa ndege ya AirAsia hadi kesho iliopotea na takriban abiria 160 waliokuwa wakielekea Singapore kutoka mji wa Surabaya nchini Indonesia.
Ndege za kijeshi kutoka indonesia na singapore zilikuwa zikiisaka ndege hiyo kusini magharibi mwa pwani ya Borneo ambapo ndege hiyo ilitoweka.
Takriban abiria 162 walikuwa wakiabiri ndege hiyo aina ya Airbus 320 wengi wao wakiwa raia wa Indonesia.

Rubani wa chombo hicho anadaiwa kutaka kubadilisha njia ili kuepuka kimbunga lakini hakuomba usaidizi wowote.
Baadhi ya meli katika eneo hilo zinaendelea kuitafuta ndege hiyo,licha ya hali mbaya ya hali ya anga
Familia na marafiki wa waathiriwa wamekongamana nchini Singapore na uwanje wa ndege wa surabaya wakingojea habari kuhusu ndege hiyo.
Share:

Saturday, 27 December 2014

Tibaijuka:Nitatetea kiti changu.


Siku kadhaa tu baada ya rais Kikwete kumfuta kazi Anne Tibaijuka kama waziri wa ardhi,nyumba na makao ,kiongozi huyo amewaambia wakaazi wa bunge lake kwamba hawakumchagua kama waziri bali kama mwakilishi wao wa bunge, kulingana na gazeti la The citizen nchini Tanzania.
Tibaijuka alipigwa kalamu kutokana na maadili yake kufuatia kashfa ya akaunti ya tageta escrow ambapo alipokea sh.billioni 1.6.'' Mungu anayetoa ndiye aliyechukua jina la mungu libarikiwe alisema tibaijuka akimaanisha kuwa yule aliyempa kiti hicho cha uwaziri ndiye aliyekichukua.
Katika kile alichoelezea kama harakati za kukitetea kiti chake katika uchaguzi wa 2015,Tibaijuka aliwaonya wapinzani wake wa kisiasa kwamba yeye ndiyo chagua bora la wapiga kura.
Kulingana na The Citizen kiongozi huyo aliwashukuru wapiga kura wa eneo bunge lake kwa kumchagua kuwa mbunge,wadhfa aliodai kumfungulia milango ya kupewa uwaziri.
''Lazima muelewe kwamba ninyi mulinipigia kura mimi ili niwahudumie bungeni na sio kama waziri,kwa hivyo yaliotokea si ndwele tugange yajayo kwa kuwa tayari kashfa ya escrow imezikwa'',aliwaambia wakaazi wa Muleba.
Hatahivyo bi Tibaijuka amesema kuwa yuko tayari kufanya kazi na viongozi wa upinzani waliochaguliwa katika uchaguzi wa madiwani wa hivi karibuni.
Share:

Korea Kazkazini yamtusi Obama.


Tume ya taifa ya ulinzi nchini Korea Kaskazini inasema kuwa Marekani inavuruga mifumo ya mitandao ya nchi hiyo huku ikimfananisha rais wa marekani Barack obama na tumbili wa misitu ya tropiki mbali na kumshutumu kwa kuhusika katika kuonyeshwa kwa filamu yenye utata inayojulikana kama The Interview.

Filamu hiyo iliyotengenezwa na kampuni ya Sony ambayo ni ya ucheshi inayoonyesha kuuawa kwa kiongozi wa korea kaskazini Kim Jong Un.
Korea kaskazini imekana kuhusika kwenye uhalifu wa mtandao dhidi ya kampuni ya Sony uliosababisha kampuni hiyo kusitisha maonyesho ya filamu hiyo.
Share:

Wanaume waliooana wapunguziwa hukumu.


Mahakama moja ya Misri imepunguza hukumu ya watu wanane waliodaiwa kushiriki katika ndoa ya watu wa jinsia moja kutoka miaka mitatu hadi mwaka mmoja.
Mwezi Uliopita ,wanane hao walipatikana na hatia ya kuchochea uasherati.
Walishtakiwa baada ya kanda moja ya video kusambaa katika mitandao ikiwaonyesha wakisherehekea katika boti moja lililokuwa mto Nile huku wanaume wawili wakionekana wakivalishana pete na kukumbatiana.

Watu hao baadaye walikataa kwamba ilikuwa harusi ya watu wa jinsia moja.
Ushoga ni kinyume na utamaduni wa Misri ,ijapokuwa si kinyume na sheria.
Wanaharakati wa kupigania haki za kibinaadamu wanasema kuwa kampeni dhidi ya mashoga imeimarishwa katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni nchini Misri.
Share:

Kiongozi wa Al-Shabaab akamatwa.


Maafisa nchini Somali wanasema kuwa kiongozi mkuu wa kundi la wapiganaji wa Alshabaab amekamatwa karibu na mji mmoja karibu na mpaka wa Kenya na Somali.
Kamishna wa Wilaya ya El Wak mjini Gedo ameiambia BBC Somalia kwamba vikosi vya usalama vilimkamata Zakariya Ismail Ahmed Hersi katika maficho yake ndani ya nyumba moja baada ya kupashwa habari.
Mwaka 2012 Marekani ilitoa zawadi ya dola millioni 3 kwa yeyote yule ambaye angeweza kutoa habari za Hersi.
Kundi la Al Shabaab limejiondoa kutoka miji kadhaa nchini Somalia tangu uzinduzi wa mashambulizi makali dhidi ya kundi hilo yanayotekelezwa na vikosi vya AMISOM vikishirikiana na wanajeshi wa serikali ya Somalia.
Bwana Hersi alikuwa kiongozi wa kundi la Alshabaab upande wa Amniyat.
Mapema mwaka huu alikosana na kiongozi wa kundi hilo Ahmed Abdi Godane ambaye aliuawa katika mashambulizi ya Marekani mnamo mwezi Septemba.
Share:

Monday, 22 December 2014

Ndoto ya mjasiriamali


Hii ni Makala ya mwisho katika mfululizo wa ndoto ya Africa Makala ambayo ilikuwa ikiwaangazia wajasiriamali wa bara hili kwa muda wa wiki nane sasa.kila Makala ilikuwa na changamoto zake mwanzoni mwa biashara,hivyo muda wote wa mfululizo huu,ulikuwa na fursa ya kujifunza namna ya kuifikia ndoto yako, ama ndoto zao,na kama walifaulu,na inawezekanaje kwa wengine pia.
Binti huyu alionja ladha ya tasnia ya vyombo vya habari akiwa na umri mdogo wakati huo akimsindikiza babake.hata hivyo binti huyo amehitimu masomo ya sheria Kemi Adetiba baada ya muda mfupi alijitosa katika burudani na kuwika nchini mwake Nigeria nan chi zote za ukanda wa Jangwa la Sahara.
Leo hii tunapomzungumzi Adea Kemi, amekwaa tuzo ya uongozaji,mzalishaji na upigaji picha bora mjini Lagos, Nigeria Kemi anamiliki kampuni ya masuala ya filamu iitwayo K-Alpha Innovations. Na hapa anatumegea kidogo siri ya mafanikio katika biashara ya tasnia ya burudani.
Tuanze na suala ambalo liko katika vichwa vya watu wengi.ni kawaida kusikia katika tasnia ya burudani kinachogomba ni UNAMJUA NANI , wengine wana dhana kuwa ukimjua mtu ndio umefanikiwa na kumjua mtu hii inafanya kazi hata kama huna muingiliano na watu wengi.sio kweli.kama biashara zingine zote,inategemea juhudi zako binafsi changanya na uvumilivu.
Tuanze kuzitazama njia za mafanikio na kuitendea haki ndoto yako.

HATUA YA 1
Andaa mpango kazi amba unaainisha misingi ya awali kampuni ya kampuni ya kuandaa picha za video,ujuzi ulionao kama mzalishaji (producer) na pia mgango wa mauzo.Ambatanisha na orodha ya vitendea kazi unavyomiliki ambavyo unajua kuvitumia pia na bajeti ya kununua mifumo ya utendaji kazi kama ya uhariri wa picha za video,mashine za kurudufu kazi zako na taa.

HATUA YA 2
Andaa vyanzo vya mapato.pata orodha ya makato ya kodi mapema.

HATUA YA 3
Nunua vifaa vya kazi. Mzalishaji wa picha za video anapaswa kuwa na camera mbili hadi tatu ,microphone isotumia waya ,taa,komputa ya uhariri ambayo imewekewa mfumo wa final cut , ama adobe primier na lenzi tofauti tofauti kwa muujibu wa kamera ulizonazo.pia itategemea na vifaa ulivyonavyo kampuni ya uzalishaji picha za video inakadiriwa kuanza na mtaji wa dola za kimarekani 15,000 kwa kuwa na vyombo hitajika kwa ujumla wake .

HATUA YA 4
Tayarisha alama ya utambulisho ya kampuni yako,businesscard na mtandao ambao utakuwa ukionesha kazi zako ulizozifanya za video.

HATUA YA 5
Andaa kazi yako ya video yenye urefu wa dakika tatu hadi tano.tumia kamera nzuri lakini pia kuwa mbunifu katika namna ya upigaji picha zako kwa jicho la tofauti,nenda kapige picha nje ya eneo lako la kazi ili uongeze uhifadhi maktaba.

HATUA YA 6
Buni bei za bidhaa zako.hii ina maana utaanza kutoza bei kwa huduma kuanzi saa moja ama kwa bidhaa.toa huduma ya kazi iliyokamilika,ikiwezekana fanya video ya familia ya mteja na kuzirudufu.

HATUA YA SABA
Weka mfumo wa utembezaji kazi zako za video gurudumu litakalo muwezesha mteja kupitia kazi zako bila usumbufu ,lazima uwe na mtandao na wateja wako, na uwasambazie kadi zenye maelezo ya kazi zako na watakavyokufikia yakiwemo mawasiliano.picha,michezo ya kuigiza,kwa wapenzi wa huduma zako kwa mtindo wa DVD.

Share:

Kwa wivu,Mume amjeruhi mkewe kwa shoka.






















Mama mwenye watoto watatu anapata matibabu hospitalini nchini Malaysia baada ya mumewe kuvamia mikono yake na miguu nakumcharanga kwa shoka la kucharangia nyama,na baadaye mwanamume huyo kujinyonga .
Mama huyo anatajwa kama K Menaga,amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Kluang upande wa kusini mwa jimbo la Johor baada ya shambulio hilo hatari lililotokea mapema mwezi huu.
Ingawa taarifa kutoka hospitalini hapo zinaarifu kuwa mama huyo ameshatolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi baada ya hali yake kuendelea vyema,na amelazwa katika wodi ya wagonjwa wa kawaida.
Inasemekana mume wa mwanamke huyo ana umri wa miaka 47 na asiye na kazi maalumu baada ya kumcharanga mkewe na kuona damu tele imtokayo mkewe, aliamua kunywa sumu na baadaye kujinyonga .Mke wa bwana huyo alikuwa akifanya kazi ya kuosha vyombo huko Singapore kwa muda wa miaka 15 sasa .
Majirani wanaeleza kuwa familia ya mwanamke huyo ilikuwa inaishi kwa kutegemea mshahara wa mwanamke huyo, wakati mumewe alikuwa hana chanzo cha mapato.Na mwanamke huyo alikuwa na utaratibu wa kurejea nyumbani kwake mara moja kwa mwezi kuwaona watoto wake akiwemo mama mkwe wake.
Mashuhuda hao wanasema kwamba,kila mwanamke huyo arejeapo kutoka kibaruani, mumewe alikuwa akimshutumu kwa kukosa uaminifu na kumshutumu kuwa ana bwana ambaye humrejesha kutoka Singapore,nao polisi wameeleza kuwa matokeo ya tukio hilo ni wivu wa mwanamume huyo,na baada ya tukio hilo kaka wa mwanamke huyo anaeleza kuwa watoto wa mwanamke huyo wamechukuliwa na jamaa zao kwa matunzo.
Share:

Rais Kikwete azungumza na wazee.


Rais Jakaya Kikwete ametengua nafasi ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka kupitia hotuba aliyotoa kuzungumzia kashfa ya upotevu wa fedha kutoka akaunti ya Tegeta Escrow.
Hatua hiyo imechukuliwa na Rais Kikwete mbele ya wazee wa Dar Es Salaam aliokuwa akiongea nao na matangazo kurushwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa na vyombo vingine.
Uchunguzi uliofanywa na kamati ya hesabu za umma ya Tanzania (PAC), ilidai kuwa Profesa Tibaijuka ni mmoja wa watu walionufaika kinyume cha sheria kwa kupata fedha zilizotoka katika akauti hiyo iliyofunguliwa kutunza fedha kusubiri ufumbuzi wa mgogoro wa kibiashara kati ya kampuni ya kusambaza umeme TANESCO na kampuni binafsi ya kuzalisha umeme ya IPTL.
Siku chache zilizopita Profesa Tibaijuja aliitisha mkutano na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam kubainisha kuwa hakuwa akikusudia kujiuzulu kutokana na tuhuma zilizokuwa zikimkabili.
Hata hivyo Rais Kikwete hakutangaza kuwachukulia hatua watumishi wengine waliodaiwa kuhusika na tuhuma hiyo kwa maelezo kuwa uchunguzi zaidi unatakiwa kwa kila mtuhumiwa.
Kumekuwa na ubishi mkubwa kujadili endapo fedha ambazo ni mabilioni zilizochukuliwa zilikuwa za umma au la. Na hata Rais Kikwete amesema maelezo aliyopewa na wataalam yanaonyesha hazikuwa mali ya TANESCO.
Share:

Sunday, 21 December 2014

Korea kazkazini sasa yaionya Marekani.


Korea Kazkazini sasa inataka uchunguzi wa pamoja na Marekani kufanywa kuhusu wizi wa mtandaoni uliosababisha kampuni ya Sony Pictures kuahirisha maonyesho ya filamu ya ucheshi inayomdhihaki raia wa Korea kazkazini Kim Jong-un.
Imesema kuwa shtuma hizo za shirika la ujasusi nchini marekani FBI kwamba Pyongyang ndio iliotekeleza uovu huo inaliharibia jina taiafa hilo.
Chombo rasmi cha habari nchini humo kilimnukuu waziri wa maswala ya kigeni ambaye jina lake halikutajwa akisema kuwa taifa lake litachukua hatua kali iwapo Marekani itakataa ombi hilo.
Taifa la Korea Kazkazini hapo awali lilikuwa limeunga mkono uvamizi huo wa kampuni ya Sony likisema kuwa ni kitendo cha haki.
Rais Obama amesema kuwa Marekani itajibu shambulizi hilo la mtandaoni wakati utakapowadia.
Share:

Wanaume 28 washtakiwa kwa uasherati..


Watu 28 wamefikishwa mahakamani mjini Cairo Misri kutokana na mashtaka ya uasherati katika kile kinachoonekana kama ishara za kampeni dhidi ya ushoga.
Baadhi ya washtakiwa walikuwa wakilia baada ya kufikishwa mahakamani wakiwa wamefungwa pingu.
Mmoja alilalama kwamba yeye na wafungwa wenzake walipigwa na polisi.
Wanaume hao walikamatwa mapema mwezi huu katika kidimbwi cha kuoga kwa jina hammam mjini Cairo.
Wanahabari wa chombo kimoja cha habari walichukua filamu ya uvamizi huo wa polisi.
Miezi miwili iliopita,watu wanane walifungwa miaka 3 jela baada ya kunaswa katika kanda ya video ambayo wakuu wa mashtaka wanasema ilionyesha wakifanya harusi ya watu wa jinsia moja mjini Cairo.
Share:

Kura zaanza kuhesabiwa Liberia.


Kura zimeanza kuhesabiwa nchini Liberia ambapo uchaguzi wa Useneta umefanyika licha ya mlipuko wa ebola.
Idadi ya watu waliojitokeza kupiga kura ilikuwa chini huku watu wengi wakisalia majumbani mwao kwa hofu ya maambukizi ya ugonjwa huo.
Viwango vya joto vya wapiga kura vilichukuliwa ,huku wakiambiwa kusimama kwa umbali wa mita moja mmoja baada ya mwengine na kuosha mikono yao kabla ya kupiga kura na hata baada ya kushiriki katika shughuli hiyo.
Matokeo ya mapema yanatarajiwa baadaye siku ya jumapili.
katika mji mkuu wa Monrovia ,mwana wa rais Ellen Johnson Sirleaf anakabiliana na mwanasoka mkongwe George Weah ambaye aliwania urais mwaka 2005.
Share:

Somalia yawakataa wanajeshi wa S.Leone.


Wanajeshi wa kulinda amani kutoka Sierra Leone wameondoka nchini Somali na hakuna wanajeshi wengine wa taifa hilo watakaochukua mahala pao kufuatia wasiwasi wa ugonjwa wa Ebola.
Umoja wa Afrika una mpango wa kutafuta wanajeshi wengine kutoka mataifa yenye wanajeshi wake nchini humo.
Zaidi ya wanajeshi 800 wa Sierra Leone walio kusini mwa bandari ya Kismayu wameondoka kuelekea nyumbani.
Walitarajiwa kuondoka mapema lakini safari yao ikacheleweshwa kwa zaidi ya miezi sita baada ya mmoja wa wanajeshi wa Sierra Leone waliotarajiwa kuchukua mahala pao kupatikana na ebola
Share:

Thursday, 18 December 2014

Gari linaloweza kujiegesha kwa kutumia saa.
























>>>> SOMA ZAIDI HAPA<<<<
Share:

Purukushani bungeni nchini Kenya.


Wabunge wa Kenya wametofautiana vikali bungeni na kuvuana mashati huku wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswada tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.
Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani walipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.

Mwenyekiti wa kamati ya usalama wa bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyaja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo wakisema 'bado mapambano.'
Spika wa bunge Justin Muturi wakati mmoja aliamuru walinzi wa bunge kuwaondoa baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.
Mswada huo ambao umewasilishwa bunge kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.


Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.
Pia ikiwa mswada huo utapistihwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa faini ya hadili shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.
Mswada huu umetolewa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab wakilalamika na kutaka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia
Rais Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikzo kuimarisha usalama wa tangui mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Share:

JK:Akatiza ziara ya Mizengo Pinda.... Source BBC


Waziri Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli maalumu.
Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu, ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji, amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow.
Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.
Katika barua yake ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa.

Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya B2B pamoja na kutembelea maeneo mengine lakini ziara hiyo imefutwa na badala yake anaondoka asubuhi kurudi nyumbani.
Baadaye leo Pinda alitakiwa kwenda Doha, Qatar kwa ziara kama hiyo hadi Desemba 23.
Baada ya kukamilisha jukumu aliloitiwa, Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea Falme za Kiarabu Jumamosi kuendelea na ziara yake.
Share:

M'marekani ahusishwa na fedha bandia UG.


Mamlaka ya Marekani imemkamata raia mmoja wa taifa hilo kwa kuongoza kashfa ya kimataifa ya fedha bandia,BBC imebaini.
Ryan Gustafson mwenye umri wa miaka 27 alishtakiwa kwa njama ya kuwa na fedha bandia nje ya Marekani baada ya fedha hizo kutumika katika biashara tofauti za Marekani.
Shirika la kijasusi la Marekani lilifuatilia fedha hizo hadi Kampala ,ambapo walibaini kuna njama ya fedha hizo bandia inayotengeza yuro,rupee pamoja na fedha tofauti za nchi za Afrika.
Mshukiwa huyo anakabiliwa na kifungo cha miaka 25 gerezani.

Maajenti wa FBI waligundua fedha hizo zinatumwa kutoka Uganda.
Alama ya kidole kutoka kwa kifurushi cha fedha hizo ilitoa maelezo ya fedha hizo kutoka kwa bwana Gustafson,raia wa Marekani.
Shirika hilo la maafisa wa ujasusi lilishirikiana na mamlaka ya Uganda ili kuanzisha uchunguzi wa siri kwa lengo la kununua fedha hizo kutoka kwa mshukiwa huyo.
Alikamatwa ,na msako kufanywa katika nyumba yake ambapo fedha bandia za Uganda,Francs za Congo,Cedis za Ghana,Rupees za India na Yuros pamoja na vifaa vya kutengeza fedha bandia.
Mamlaka ya Marekani inakisia kwamba washukiwa hao waliingiza takriban dola millioni 2 fedha bandia katika soko.
Share:

Wednesday, 17 December 2014

Kijana mzungu abadilika kuwa m'masai..


Aliposafiri nchini Kenya mwaka 2011 kama mtu aliyejitolea katika shirika moja lisilo la kiserikali ,uamuzi wa kuwa kijana wa kimasai wa Ilchamus lilikuwa wazo la mwisho katika akili ya Max Roing,ambaye ni raia wa Sweden.
Lakini miaka mitatu baadaye ,Max mwenye umri wa miaka 25 amependa sana utamaduni wa watu hao walio wachache katika fukwe za ziwa Baringo.
Max pia alikuwa miongoni mwa vijana 5,000 wa Ilchamus katika kaunti ya Baringo waliotawazwa kuwa wanaume kamili baada ya kupashwa tohara.

''Nilikuja nchini Kenya kama mtalii na pia kusaidia kuhifadhi mazingira kupitia upandaji wa miti katika kaunti ya kajiado''bwana Roing aliliambia gazeti la Nation nchini Kenya baada ya kuhitimu.
Kwa sasa anafuata mila yake mpya inayoshirikisha mavazi yanayovaliwa pamoja na shuka nyeusi,simi iliofungwa katika ukanda wake wa rangi ya hudhurungi,viatu vyeusi na nguo iliorembeshwa kwa shanga.
Hafla hiyo ya kuhitimu imemfanya kuingia katika umri wa Ilmeng'ati.
''Mimi ni Max Lemeyan Le Kachuma kutoka kabila la Ilchamus na ukoo unaojiita Iltoimai''alisema jina lake huku akinywa maziwa yalio chungu katika kikombe.
Share:

Ebola:Msako wa wagonjwa kufanywa S.Leone


Rais wa Sierra Leone Ernest Bai Koroma ametaka kufanyika kwa msako wa nyumba hadi nyumba kwa waathiriwa wa ugonjwa wa ebola nchini humo

Rais Ernest Bai Koroma wa Sierra Leone amesema kuwa msako wa nyumba kwa nyumba unaanza kote nchini humo kuwatambua watu walio na ugonjwa hatari wa ebola.
Aidha, Rais huyo amepiga marufuku biashara siku ya Jumapili.....  >>>>INGIA HAPA<<<<


Share:

Mwanasheria Mkuu wa Tanzania ajiuzulu.



Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Jaji Frederick Werema amejiuzulu nafasi yake hiyo kuanzia jana, Jumanne, kufuatia sakata.......  >>>>INGIA HAPA<<<<
Share:

Pakistan yaomboleza mauaji ya watoto



Raia nchini Pakistan wanaadhimisha siku tatu za maombolezo kuwakumbuka zaidi ya watu 140 waliouwawa,karibia wote wakiwa...>>>>INGIA HAPA<<<<
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.