Basi la kwanza nchini Uingereza linalotumia kinyesi na uchafu unaotokana na chakula limeanza safari yake ya kwanza>>>>>INGIA HAPA<<<<<
Friday, 21 November 2014
Basi linalotumia kinyesi lazinduliwa.......
Basi la kwanza nchini Uingereza linalotumia kinyesi na uchafu unaotokana na chakula limeanza safari yake ya kwanza>>>>>INGIA HAPA<<<<<
wanawake
wakiandamana huku wakiomboleza nchini Uganda
shughuli
za mazishi ya mtoto wa miaka miwili zimefanyika nchini Uganda, mtoto
ambaye kifo chake kimezua ghadhabu baada ya mtoto huyo kugongwa na
gari la halmashauri ya jiji la Kampala ,baada ya mama yake kukamatwa
akiuza matunda kinyume cha sheria.
Familia
ya Ryan Ssemaganda na wanasiasa wa upinzani walitishia kutomzika
mtoto huyo mpaka maofisa hao watakapo wajibika kwa kitendo
hicho.Mwili wake ulichukuliwa wakati wakiandamana kuelekea bungeni
siku ya alhamisi.
Raia
wa Uganda wanaona kuwa halmashauri hiyo inatumia nguvu nyingi
kupambana na wachuuzi wa mitaani.
Mama
wa mtoto Ryan alikamatwa siku ya jumatatu baada ya kukutwa akiuza
matunda huku akiwa hana leseni.
Siku
iliyofuata, Bibi wa mtoto huyo alimpeleka katika Ofisi za Mamlaka ya
mji wa Kampala ambako mama mtoto alikuwa akishiliwa , nia ilikua
kumpa mama mtoto ili amnyonyeshe.
Maafisa
wa Ofisi hiyo walikataa na wakati wakijadiliana kuhusu hilo, mtoto
alichoropoka kutoka kwa mama yake na kugongwa na gari linalomilikiwa
na Mamlaka hiyo.
Siku
ya Alhamisi polisi ilizuia kupelekwa kwa mwili katika Bunge,
wakisisitiza mwili huo uzikwe ili marehemu apumzike kwa amani, na
kuwataka waepuka jambo hilo kushughulikiwa kisiasa.
Mkanyagano hatari wawaua 11 Zimbabwe.......
Watu
11 wamefariki katika mkanyagano nchini Zimbabwe baada ya ibada ya
kidini kufnayika katika uwanja wa soka.
Polisi
wanasema kuwa watu wanne walifariki katika uwanja huo ulio mjini
Kwekwe wakati wengine saba wakifariki hospitalini.
Mkanyagano
huo ulitokea wakati maelfu ya waumini wakikimbilia kuondoka uwanjani
humo baada ya ibada iliyoongozwa na mhubiri wa kipentekoste Walter
Magaya.
Mhubiri
huyo anadai kuwaponya watu kwa kufanya miujiza.
Baadhi
ya walioshuhudia mkanyagano huo wanatuhumu polisi kwa kufunga baadhi
ya milngo ya kuondokea uwanjani humo, huku watu wakiondoka kupitia
mlango mmoja tu.
Hata
hivyo polisi wanakana kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya.
Bwana
Mugaya ambaye ni mkuu wa kanisa la 'Prophetic Healing and
Deliverance' aliambia vyombo vya habari kuwa alipopata habari ya
kutokea vifo hivyo alihuzunika sana.
Shambulio laua tena Mombasa Kenya.....source BBC
Mtu
mmoja ameripotiwa kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mapigano
katika mji wa Mombasa pwani ya Kenya. Polisi walipambana na vijana
walioingia katika Msikiti wa Swafaa eneo la Kisauni na mpaka sasa
zaidi ya vijana 400 wanashikiliwa tangu kuanza kwa msako huo, mapema
wiki hii.
Mwandishi wa BBC, Emmanuel Igunza anasema Msikiti huo
ulifungwa jana baada ya polisi kuuvamia Jumatano, ambamo walipata
magruneti, mabomu ya petroli na silaha nyingine. Hali ya wasi wasi
bado imetanda katika mji huo wa pwani. Serikali imekwishafunga
misikiti minne ambayo wanasema ina uhusiano wa watu wenye misimamo
mikali ya imani ya kidini.
Pamoja na kukamata silaha
mbalimbali, polisi pia walikamata bendera nyeusi, alama ya kuunga
mkono kundi la kigaidi la Al-Shabab la nchini Somalia
Awali polisi mjini Mombasa pwani ya Kenya walisema
wamepata silaha nyingine zaidi yakiwemo mabomu katika msikiti wa tatu
ambao ulifanyiwa upekuzi Msako huo katika msikiti wa Swafaa mtaani Kisauni
unakuja baada ya msako mwingine wa Jumatatu ambapo polisi pia
walipata silaha ndani ya msikiti ambao wanasema hutumika kutoa
mafunzo yenye itikadi kali.
Mtaa wa Kisauni ndiko vijana waliokuwa wamejihami
kuwadunga visu watu wanne na kuwaua. Pia waliwashambulia kwa silaha
nyingine.
Waziri wa usalama wa ndani, Joseph Ole Lenku anasema
kuwa msako huo ulifanywa katika misikiti ambayo hutumiwa na watu
wanaoeneza itikadi kali za kiisilamu kwa vijana ambao inadaiwa
wanajiunga na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab nchini
Somalia.
Viongozi wa kiisilamu wamelaani misako hiyo katika
Misikiti wakisema kuwa itachochea zaidi vijana kuendeleza itikadi
kali za kidini.
Rais Obama awatangazia neema wahamiaji.....source BBC
Rais
Barack Obama amelihotubia taifa kueleza mageuzi makubwa katika mfumo
wa uhamiaji wa Marekani. Amesema atachukua hatua za kikatiba kutoa
ruhusa ya muda kisheria kwa takriban wahamiaji haramu milioni tano.
Obama amesema nchi hiyo ilijengwa kwa uhamiaji na ameshutumu
wanachama wa Republican kwa kuzuia mageuzi hayo. Wanachama hao
wametishia kuchukua hatua.
Amesema
watakaohalalishwa watalazimika kulipa kodi na wasiwe na rekodi ya
uhalifu. Hata hivyo amesema urejeshwaji makwao kwa watu wenye makosa
utaharakishwa.
Bwana
Obama ametangaza mpango wake, ambao anaupitisha bila baraza la
Congress, katika hotuba aliyoitoa kupitia televisheni.
Kwa
upande wao wajumbe wa Republican wamesema hatua ya Rais Obama inavuka
mipaka yake na uhusiano na rais utaingia dosari
Kuna
wahamiaji wasio halali wapatao milioni 11 nchini Marekani na mwaka
huu watoto wanaovuka mpaka wamesababisha tatizo.
Rais
Obama ameliambia taifa kuwa kile anachopendekeza sio msamaha
"Ninachokieleza
ni uwajibikaji - akili ya kawaida, mtazamo wa kawaida," amesema.
"Kama
unatimiza vigezo, unaweza kujitokeza na kuishi maisha ya kawaida
ukiendana na sheria."
"Iwapo
ni mhalifu utarejeshwa ulikotoka.Kama unapanga kuingia Marekani
kinyume cha sheria, nafasi ya kukamatwa na kurejeshwa ulikotoka ni
kubwa." anasema Rais Obama.
Rais
Obama amesema mfumo mpya wa uhamiaji utawawezesha watu wanaoishi
nchini Marekani kinyume cha sheria, kujulikana na kuchangia katika
uchumi wa taifa kwa kuwa watakuwa huru kufanyakazi.
Kuamuru
kufanyika kwa mageuzi hayo kumesababisha malalamiko ya hasira kwa
wanachama wa Republicans ambao wanasema hatua hiyo ni
kutolishirikisha baraza la Congress na kuendesha mambo kwa mfumo wa
Kifalme. Baadhi wanasema hawatatoa ushirikiano katika maeneo mengine
ya kisera, na wengine wamemtaka Bwana Obama ashitakiwe.
Rais
Obama anasema anachukua hatua hiyo kwa sababu baraza la Congress mara
kadha kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu limeshindwa kurekebisha mfumo
wa uhamiaji ambao umeharibika.
Msichana kutoka Syria ashitakiwa.....
Monique
akiwa mbele ya TV akiomba binti yake kurejea nyumbani Uholanzi miezi
miwili iliyopita
Msichana wa kiholanzi aliyerejea kutoka Syria ambako
alikwenda huko kujiunga na wapiganaji wa jihadi lakini baadaye
alirudishwa nyumbani na mamake anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa
kushukiwa kutishia usalama wa taifa.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 19, akijulikana kama
Aicha, alikamatwa aliporejea nyumbani kwao katika mji wa Maastricht.
Aicha, aliyebadili dini hivi karibuni kuwa Mwislam,
anaaminika kusafiri kwenda kujiunga na wapiganaji wa Islamic State
(IS) katika ngome ya Raqqa nchini Syria kuoana na mpiganaji mmoja.
Mama yake Monique alisaidia kumrejesha nyumbani Uholanzi
na si mtuhumiwa.
Aicha ni mmoja wa idadi ndogo ya wasichana na wanawake
kutoka Ulaya ambao wamekwenda Syria na Iraq katika miezi ya karibuni.
Baadhi wanaaminika kusafiri kwenda hukokupata mafunzo ya
kiitikadi, wakati wengine wanasemekana kuoana na wapiganaji, wakiwemo
wanaopigana bega kwa bega na wapiganaji wa IS.
Mahakama nchini Uholanzi Ijumaa itasikiliza kesi hiyo
bila wasikilizaji na itaamliwa Aicha anaweza kushikiliwa kwa muda
gani.
Upande wa mashitaka unatarajiwa kumwomba jaji kuongeza
muda wa kumshikilia Aicha wakati wakichunguza ushahidi.
Thursday, 20 November 2014
Obama kutangaza mabadiliko ya uhamiaji......source BBC
Ikulu
ya Marekani imesema Rais Obama atatumia muda ambao watazamaji wa
televisheni nchini humo wanaangalia zaidi matangazo siku ya Alhamisi
kutangaza mabadiliko makubwa ya mfumo wa uhamiaji wa nchi hiyo.
Inatarajiwa
kuwa Rais Obama atasema kuwa atatumia madaraka yake aliyopewa
kikatiba kuzuia wahamiaji wapatao milioni tano kurejeshwa makwao na
badala yake wapatiwe vibali vya kufanya kazi nchini humo.
Rais
Obama amesema hayo katika video iliyotumwa katika ukurasa wa facebook
kabla ya hotuba yake.Tangu kuingia madaraka Obama amekuwa akipigania
baadhi ya mabadiliko ikiwemo huduma ya utoaji wa huduma za afya kwa
mfumo wa bima ya afya.
Bill Cosby ashutumiwa kuwa mdhalilishaji......source BBC
Televisheni ya NBC imesitisha mradi wa kurusha kipindi
cha mchekeshaji maarufu duniani, Bill Cosby baada ya kukabiliwa na
shutuma zaunyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake .
Katika taarifa hiyo, kampuni imethibitisha kusimamishwa
kwa kipindi hicho.
Siku ya jumanne kamouni inayotoa huduma ya vipindi vya
video kwa njia ya internet, Netflix iliahirisha kipindi kilichomuhusu
Cosby baada ya mwanamitindo mmoja kudai kuwa alidhalilishwa kijinsia
mwaka 1982.
Mtandao wa Netflix ulikataa kutoa sababu ya kusitisha
uzalishaji wa kipindi, lakini umesema kuwa maandalizi ya uzalishaji
ulikua haujaanza. Cosby amekana kuhusika na vitendo hivyo.
Hatua hii imekuja baada ya mwanamitindo na mtangazaji
kipindi cha Televisheni Janice Dickinson kusema kuwa alidhalilishwa
na Cosby walipokutana kwa ajili ya chakula cha usiku huko California
mwaka 1982.
Janice amesema aliandika katika kitabu kinachohusu
maisha yake kuhusu tukio hilo lakini alipata shinikizo kutoka kwa
Mwanasheria wa Cosby na mchapaji wa kitabu chake kuondoa sehemu hiyo.
Mwanasheria wa Cosby Martin Singer amesema madai ya
Dickinson ni ya uongo na hayana msingi.
Dickinson ni miongoni mwa wanawake kadhaa waliomshutumu
kuwadhalilisha kijinsia miaka takriban 30 iliyopita.
Nae muigizaji wa zamani Barbara Bowman amesema
alidhalilishwa na Cosby katika nyakati tofauti mwaka 1985 alipokuwa
na umri wa miaka 17.
Mwanzoni mwa mwezi huu Barbara alisema alishindwa
kupeleka mashitaka polisi kwa kuwa alihofu hataaminika.
Cosby hajawahi kushtakiwa kwa kosa lolote la kihalifu.
Mkuu wa kampuni ya ferry Korea jela....
Mahakama moja nchini Korea kusini imemhukumu miaka kumi gerezani mkurugenzi mkuu wa kampuni iliyoitengeza feri ya Sewol iliyozama mwezi Aprili na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 300, wengi wao wakiwa ni watoto.
Mahakama ya wilaya ya Gwangju imeelezwa kwamba feri hiyo ilikarabatiwa kuweza kubeba mizigo zaidi na mabadiliko hayo yaliongeza uwezekano wa chombo hicho kupindukia.
Mapema mwezi hu kapteni wa feri hiyo, alihukumiwa miaka 36 kwa kukwepa majukumu yake. Mmiliki wa kampuni hiyo alifariki akitoroka.
Wapiga mbizi waliiokoa miili 295 kabla ya serikali kusitisha shughuli hiyo ya kutafuta miili zaidi wiki iliyopita. Bado waathirwa tisa hawajulikani waliko.
Wednesday, 19 November 2014
Binti ajinasua na ndoa ya mwanamgambo.......source BBC
Mwanamke mmoja raia wa Uholanzi amewasili nchini Uturuki baada ya safari iliyojaa hatari nchini Syria kwa ajili ya kumchukua binti yake aliyekua mjini Raqqa, mji unaokaliwa na waasi wa Islamic State..............>>>>>INGIA HAPA<<<<<
Familia ya Bob Marley kuuza bidhaa za Bangi...... source BBC
Familia ya aliyekuwa mwanamuziki wa Jamaica, Bob Marley imezindua kampuni ambayo wanaitaja kama ya kwanza duniani kuuza bidhaa za Canbbisa au marujuana au Bangi kama wanavyoijua wengi.... >>>>INGIA HAPA<<<<
Bill Gates kusaidia kupambana na Ebola......source BBC
Mfuko wa Bill na Melinda Gates umeahidi kutoa kiasi cha dola milioni 5.7 kwa ajili ya mradi kusaidia matibabu dhidi ya maradhi ya Ebola nchini Guinea na nchi nyingine zilizoathiriwa na ugonjwa huo.....>>>>>INGIA HAPA<<<<<
Raia wa India awekwa Karantini...... source BBC
India imemuweka karantini mwanaume mmoja ambaye alipatiwa matibabu baada ya kuathirika na ugonjwa wa Ebola nchini Liberia, kwa hofu kuwa huenda akasambaza virusi vya Ebola kwa njia ya kujamiiana...........>>>>INGIA HAPA<<<<
Tuesday, 18 November 2014
AJILIPUA KWA MAFUTA YA TAA..........source Global Publisher
Kijana mmoja Nicholas Mhagama (25), mkazi wa Makongo Juu Dar, juzi kati alijilipua na mafuta ya taa kisa kikidaiwa kunyanyaswa na babu yake. Tukio hilo lilitokea eneo la Makongo Juu Makaburini usiku ambapo kijana huyo na babu yake aliyemtaja kwa jina moja la Mhagama waligombana.
Kijana Nicholas Mhagama (25) aliyejilipuwa na mafuta ya taa akidai kunyanyaswa.
Netanyahu aishutumu Palestina na Hamas........sourse BBC
Benjamin Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin
Netanyahu amewataka Waisrael kuungana bila kujichukulia sheria mkononi
baada ya Wapalestina wawili wakiwa na bunduki na mashoka kuwaua waumini
wanne katika hekalu moja mjini Jerusalem.
Ameyashutumu Mamlaka ya
Palestina na Hamas kwa kuchochea shambulio hilo. Lakini maafisa wa
Palestina wamemlaumu Netanyahu kwa kuchochea ghasia kubwa za hivi
karibuni, zilizosababisha Waisrael na Wapalestina kuuawa.Amesema kama taifa watakabiliana na ugaidi na wafadhili wao.Hata hivyo Netanyahu ameongeza kuwa kwa sasa wapo katika kampeni ndefu ya vita dhidi ya ugaidi na ambayo haikuanza leo.
Netanyahu amesisitiza kuwa kuna watu baadhi ya watu wanaotaka kuwandoa katika mji mkuu wa Israel Jerusalem, suala ambalo amesema haliwezekani kwani huo ni mji mkuu wao milele
Bi harusi apewa talaka siku ya harusi..... source BBC
Bi harusi apewa talaka siku ya harusi.Picha niaba ya gazeti la Daily Mirror nchini Uingereza
Bwana harusi mmoja kutoka Saudi
Arabia amempa talaka mkewe siku ya harusi baada ya kumuona uso wake kwa
mara ya kwanza wakati mpiga picha alipotaka kuwapiga picha.
Maharusi
hao kutoka mji wa magharibi wa Saudia,Medinah walikubaliana kuoana
licha ya kutoonana uso kwa uso,swala ambalo ni utamaduni mkubwa wa
mataifa ya mashariki ya kati.Lakini wakati mwanamke huyo alipofungua kitambara alichokuwa amejifunika uso na kutabasamu katika kamera,mumewe alishtuka na kuondoka wa ghafla.
Kulingana na gazeti moja katika eneo hilo kwa jina Okaz,mwanamume huyo alianguka na kuzirai huku wageni waalikwa wakijaribu kuingilia kati ili kutatua kilichokuwa kikiendelea.
Hata hivyo Bwana harusi alisema kuwa hakuweza kumwona bi harusi kabla ya harusi yao gazeti hilo la Okaz liliripoti.
'' Si wewe msichana niliyetaka kuoa,si wewe kamwe niliyedhani '' kwa hivyo nakupa talaka''alisema bwana harusi.
Na alipompa talaka bi harusi naye alianguka na kuzirai na kuifanya harusi hiyo kuwa usiku wa majonzi.
Shahidi mkuu kuhusu Rwanda atoweka Kenya
Kumbu kumbu ya mauaji ya Kimbari nchini Rwanda
Shahidi mmoja muhimu wa uchunguzi
unaofanyika kuhusu mauaji ya kimbari ya Rwanda ambaye alikuwa
akitarajiwa kuhojiwa na majaji Nchini Ufaransa kuhusu kudunguliwa kwa
ndege ya aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, anasemekana
kutekwa nyara na kutoweka jijini Nairobi.
Idara ya Polisi Nchini Kenya imekanusha kumtia mbaroni Emile Gafirita.Majirani wa Emile Gafirita wanasema kuwa walisikia milio ya breki za gari na kamsa pale alipokuwa akirejea nyumbani muda mfupi kabla ya usiku wa manane Jumatatu usiku na kuwaona watu wawili wakimtia pingu na kumrusha kwenye gari.
Idara ya Polisi Nchini Kenya inasema kuwa hawajamtia mbaroni.
Jina la bwana Gafirita liliibuka katika kesi ya hivi majuzi Nchini Rwada, pale alipotajwa kama askari wa zamani katika kikosi cha ulinzi cha Rais Paul Kagame.
Majaji wawili wa Ufaransa, Marc Trevidic na Nathalie Poux, walikuwa wakipanga kumhoji ili atoe ushahidi mjini Paris kuhusiana na mzinga ulioshambulia na hatimaye kuiangusha ndege iliyombeba Rais wa zamani wa Rwanda hayati Juvenal Habyarimana mnamo mwezi Aprili ya mwaka 1994.
Mauaji ya Habyarimana yaliibua mapigano makali ya kikabila yaliyosababisha mauwaji ya zaidi ya watu laki nane, wengi wao waTusti na wahutu wenye siasa za kadri.
15 wakamatwa kwa mauaji Mombasa
Polisi mjini Mombasa wamewakamata watu 15 kuhusiana na mauaji ya watu wanne usiku wa kuamkia leo mjini humo.
Lakini
wamekanusha kuwa mauaji hayo yalihusishwa na msako wa polisi dhidi ya
misikiti inayotoa mafunzo ya itikadi kali mjini humo. Hali ya taharuki bado iko juu katika baadhi ya maeneo mjini humo huku polisi wakiendelea kushika doria mjini humo.
Kamishna mkuu wa Mombasa, Nelson Marwa anasema kuwa wale wote waliohusishwa na mauaji hayo ya watu wanne kwa kuwadunga visu, walikodiwa na mwanasiasa katika mtaa wa Kisauni.
Marwa hata hivyo amesema idadi ya wale waliouawa sio watu wanne bali ni watatu.
Hata hivyo jamaa wa waliouawa walithibitisha idadi yao kuwa watu wanne ambao walifariki baada ya kudungwa visu.
Wengine zaidi ya 12 walijeruhiwa kwenye tukio hilo ambalo limejhusishwa na vijana wenye itikadi kali za kidini.
Zaidi ya vijana 250 walikamatwa baada ya kupatikana na maguruneti pamoja na silaha nyinginezo kwenye msako uliofanywa Jumatatu asubuhi.
Viongozi wa kiisilamu na mashirika mengine ya kutetea haki za binadamu wamelaani msako huo ambao wanasema utarejesha tu hisia za waisilamu kulengwa na maafisa usalama.
Monday, 17 November 2014
KIVUKO KIPYA CHA DAR-BAGAMOYO CHAPOKELEWA NA WAZIRI MAGUFULI....... Global Publisher
Kivuko hicho mabacho kitakuwa kikipita katika vituo saba kati ya miji hiyo mwili, kimefungwa vyombo vya kuongozea vya kisasa (Navigational Equipment) vikiwemo GPS Compass, Automatic Identification System (AIS), Radar, Echo Sounder, CCTV Cameras na kina vyombo vya kutosha vya kuokolea watu kama ‘life jackets’, ‘life bouys’ na ‘life rafts’.
Akizungumza na GPL, Waziri Magufuli alisema” “Kuanza kwa kivuko hiki kutasaidia kwa kiasi kupunguza foleni kwa wakazi wa jijini la Dar es Salaam, kwani kina uwezo wa kubeba abiria 300 kwa kukaa.
Kivuko kipya cha MV Dar es Salaam-Bagamoyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar e s Salaam, Mecky Sadick, akizungumza na wadau bandarini.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sofia Mjema akizungumza jambo.
Mkurugenzi wa Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko (TEMESA) Japhet Massele, akitoa ufafanuzi kuhusu kivuko hicho.
Sehemu ya ndani ya kivuko inavyoonekana.
Wito kwa wakazi kujihami dhidi ya Boko Haram..........BBC
Emir wa Kaskazini mwa Nigeria,
ambaye ni mmoja wa viongozi wa kiisilmau wenye ushawishi mkubwa, ametoa
wito kwa watu nchini humo kuchukua silaha na kujilinda dhidi ya
mashambulizi ya kundi la wanamgambo wa kiisilamu wa Boko Haram.
Emir huyo wa Kano, Muhammad Sanusi, amewaambia wakazi wasisubiri wanajeshi kuwalinda kutokana na magaidi.Emir huyo ambaye alikuwa gavana wa benki kuu nchini humo kabla ya kuchukua wadhifa wake wa Emir, alitoa matamshi yake ya kutatanisha kwenye mkutano wa maombi.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria amesema kauli kama hii sio kawaida kutolewa kwani Emir huyo huyo hazungumzii sana maswala ya kisiasa.
Wapiganaji wa Boko Haram wamekuwa wakiwahangaisha wananchi kwa miaka mitano sasa
Wapiganaji wa wa Boko Haram wanaendelea kufanya mashambulizi ya mara kwa mara katika sehemu kadhaa za Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, huku wakiteka miji na mijiji ambko wamekuwa wakiwataka wakazi kufuata sheria kali ya kiisilamu.
Sanusi alikuwa mkosoaji mkuu wa serikali alipokuwa anafanya kazi yake ya benki, alisema kuwa watu hawapaswi kuogopa wanamgambo hao na kwamba wanapaswa kufanya wawezalo kujikinda kutokana na mashambulizi ya kundi hilo.
Mwandishi wa BBC anasema ingawa Emir huyo hakutaka kundi la Boko Haram, ilikuwa hatua ya kipekee kwa kiongozi kama huyo kuwataka watu kujihami dhidi ya Boko Haram.
Aanasema hii ni dalili tu ya mambo yalivyo nchini humo hasa katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.










.jpg)













