Sunday, 23 November 2014

Kenya yauwa al-Shabaab 100.........source BBC


Makamo wa rais wa Kenya, William Ruto, anasema kuwa askari wa usalama wa Kenya wamewaandama wapiganaji wa al-Shabaab hadi kwenye kambi yao nchini Somalia, baada ya shambulio dhidi ya basi kaskazini-mashariki mwa Kenya hapo jana ambapo raia 28 waliuliwa.
Bwana Ruto alisema wapiganaji zaidi ya 100 waliuliwa katika operesheni mbili tofauti. Alisema kambi ya al-Shabaab iliangamizwa. Habari hizo hazikuthibitishwa na upande wa pili.
Gavana wa Mandera - ambako shambulio la jana lilitokea - amelaumu vikosi vya usalama kwa kushindwa kuwalinda raia. Alisema polisi kawaida wanashindwa kufanya uchunguzi kamili baada ya mashambulio.
Share:

Mauaji yanalenga kuzua uhasama wa kidini...........BBC

Baadhi ya miili ya abiria waliouawa na Al-Shabaab eneo la Mandera, Kenya.

Basi lililotekwa na Al-Shabaab eneo la Mandera likiwa njiani kuelekea Nairobi.


Mshauri wa ngazi ya juu wa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa mauaji ya watu 28 waliokuwa wakisafiri kwenye basi moja yalilenga kusababisha vita vya kidini nchini kenya.
Kwenye mahojiano na BBC Abdikadir Mohammed alitoa wito kwa wakenya kutoka imani zote kuungana pamoja dhidi ya kile alichokitaja kuwa vitendo vya uhalifu.
Wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab waliwapiga risasi wasafiri ambao hawangeweza kukariri Koran.
Al Shabaab ilisema kuwa shambulizi hilo lilikuwa la kulipiza kisasi mauji ya hivi majuzi ya waislamu yaliofanywa na wanajeshi wa Kenya kwenye mji wa pwani wa Mombasa.

Serikali ya Kenya imesema kuwa imeanza kuwatambua waliotekeleza mauaji hayo na itawafikisha mbele ya sheria hivi karibuni.
Share:

Wanamgambo wawateka watoto 10 Mali.........BBC


Maafisa wa kijeshi nchini Mali wanasema kuwa watu waliokuwa na silaha wamewateka nyara watoto kumi na kuwaua wawili ambao walijaribu kupinga kutekwa karibu na mji wa Kidal.
Afisa mmoja alisema kuwa watoto hao walilazimishwa kuwa wanajeshi.

Maeneo yanayozunguka mji wa Kidal yanadhibitiwa na kundi la kiislamu lililojitenga ambalo lilidhibiti eneo la kaskazini nchini Mali mwaka 2012 lakini baadaye likatimuliwa na wanajeshi wa Ufaransa kwa ushirikiano na vikosi vya muungano wa Afrika.
Share:

Boko Haram wauwa 100 hivi karibuni.........BBC


Ripoti kutoka kaskazini-mashariki mwa Nigeria zinaarifu kuwa kundi la wapiganaji Waislamu la Boko Haram, limefanya mashambulio mawili makubwa katika siku chache za karibuni ambapo watu karibu 100 wameuwawa.
Kiongozi mmoja katika jimbo la Borno alisema kuwa wapiganaji waliuwa wauza samaki karibu 50 karibu na kijiji cha Doron Baga, kando ya Ziwa Chad.
Alisema wapiganaji wa Boko Haram wameweka kizuizi kwenye njia ya kuelekea Chad na kuwakamata wachuuzi waliokuwa wakienda kununua samaki.
Katika tukio jengine hapo awali watu karibu 50 waliripotiwa kuwa waliuwawa karibu na mpaka wa Cameroon pale Boko Haram walipovamia kijiji cha Azara Kuya, siku ambapo soko huwa na watu wengi
Share:

Saturday, 22 November 2014

Waliofanya shambulio la Mandera wasakwa...... BBC


Maiti za watu waliouliwa na al-Shabaab Jumamosi asubuhi nje ya mji wa Mandera, Kenya, karibu na mpaka wa Somalia, zilipelekwa na wanajeshi hadi mjini humo.
Serikali ilikuwa inajitayarisha kusafirisha miili hiyo hadi mji mkuu, Nairobi.
Basi lililokuwa limebeba abiria 60 lilitekwa nyara alfajiri na abiria 28 walipigwa risasi na kuuwawa.
Wengi waliouwawa ni kutoka maeneo mengine ya Kenya ambao wakifanya kazi Mandera.
Inasemekana kuwa wengi wao walikuwa waalimu na wafanyakazi wa wizara ya afya ambao walikuwa wanarudi nyumbani kuwa na familia zao wakati wa Noeli.
Msemaji wa wapiganaji wa Somalia, al-Shabaab, alidai kuwa walihusika na shambulio hilo.

Wanajeshi na polisi wametumwa huko kwenda kuwasaka wale waliohusika na shambulio hilo lakini hakuna taarifa kuwa wamekamatwa.
Share:

RAIS KIKWETE ATOLEWA NYUZI KATIKA MSHONO, AFYA YAKE YAZIDI KUIMARIKA......Global Publisher




Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland baada ya kutolewa nyuzi katika mshono baada ya kufanyiwa upasuaji wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na ushauri. Kulia kwake ni Daktari wa Rais Profesa Mohamed Janabi.

























Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amepumzika kwenye hoteli maalumu baada ya kutoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland alikotolewa nyuzi katika mshono baada ya kufanyiwa upasuaji wa Tezi Dume wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na ushauri.
Share:

BASI LA ABIRIA LAVAMIWA KENYA, WATU 28 WAUAWA.......source Global Publisher


 Habari kutoka Mandera, kaskazini mashariki mwa Kenya zinasema kuwa, abiria 28 wameuawa na wengine kujeruhiwa baada ya watu wenye silaha kuvamia basi walimokuwa wakisafiria leo alfajiri.
Habari zaidi zinasema wavamizi hao huenda ni wanachama wa kundi la kigaidi la al-Shabab. Mashuhuda wa tukio hilo wanasema wavamizi hao walikuwa wa asili ya kisomali na waliwaua abiria ambao si Waislamu. Jambo hilo linalenga kuzusha vita vya kidini nchini Kenya.

Ikiwa itathibitika kuwa al-shabab ndio waliohusika na hujuma hiyo,  hilo litakuwa shambulizi baya zaidi la kundi hilo kutokea katika miezi ya hivi karibuni. Polisi ya Kenya imekataa kutoa taarifa kuhusiana na tukio hilo na kusisitiza kuwa, itatoa maelezo punde baada ya kuchunguza kadhia hiyo.
Share:

Al Shabaab lakiri kutekeleza shambulizi......source BBC


Kundi la Al Shabaab nchini Somali linasema kuwa limefanya mashambulizi ya abiria 28 katika basi moja kazkazini mashariki mwa kenya.
Basi hilo ambalo lilikuwa likiwabeba abiria 60 lilitekwa katika jimbo la mandera lilipokuwa likelekea mjini Nairobi.
Abiria mmoja ambaye alinusurika ameiambia BBC vile raia wasio wa Somali walitengwa na wengine na wale ambao hawakuweza kusoma aya ya Quran walipigwa risasi kwa karibu.
Katika taarifa yake al Shabaab limesema kuwa mashambulizi hayo ni ya kulipiza kisasi mauaji ya waislamu huko Mombasa yaliotekelezwa na vikosi vya usalama vya kenya.

Kenya imekumbwa na misururu ya mashambulizi ya risasi na mabomu yanayodaiwa kutekelezwa na kundi la Alshabaa tangu vikosi vyake viingie nchini Somali
Share:

Ebola:Fuo za bahari kufungwa Liberia....source BBC


Polisi nchini Liberia wametangaza kuwa watafunga fuko zote za bahari kuanzia tarehe 29 mwezi Novemba hadi pale taifa hilo litakapo tangaza kuwa ugonjwa wa Ebola umemalizwa..
Tarehe hiyo itakuwa ni siku ya taifa la Liberia ya kuadhimisha kuzaliwa kwa raisi aliyeiongoza Liberia kwa miaka mingi William Tubman.
Polisi wanasema kuwa yeyote atakayetumia fuo hizo za bahari atakuwa amekiuka amri hiyo na atachukuliwa hatua za kisheria.
Polisi pia wamepiga marufuku mikutano yote ya umma isipokuwa ya kisiasa.
Karibu watu 3000 wameaga dunia kutokana na ugonjwa huo.
Share:

Friday, 21 November 2014

Basi linalotumia kinyesi lazinduliwa.......





















Basi la kwanza nchini Uingereza linalotumia kinyesi na uchafu unaotokana na chakula limeanza safari yake ya kwanza>>>>>INGIA HAPA<<<<<
Share:






wanawake wakiandamana huku wakiomboleza nchini Uganda
shughuli za mazishi ya mtoto wa miaka miwili zimefanyika nchini Uganda, mtoto ambaye kifo chake kimezua ghadhabu baada ya mtoto huyo kugongwa na gari la halmashauri ya jiji la Kampala ,baada ya mama yake kukamatwa akiuza matunda kinyume cha sheria.
Familia ya Ryan Ssemaganda na wanasiasa wa upinzani walitishia kutomzika mtoto huyo mpaka maofisa hao watakapo wajibika kwa kitendo hicho.Mwili wake ulichukuliwa wakati wakiandamana kuelekea bungeni siku ya alhamisi.
Raia wa Uganda wanaona kuwa halmashauri hiyo inatumia nguvu nyingi kupambana na wachuuzi wa mitaani.
Mama wa mtoto Ryan alikamatwa siku ya jumatatu baada ya kukutwa akiuza matunda huku akiwa hana leseni.
Siku iliyofuata, Bibi wa mtoto huyo alimpeleka katika Ofisi za Mamlaka ya mji wa Kampala ambako mama mtoto alikuwa akishiliwa , nia ilikua kumpa mama mtoto ili amnyonyeshe.
Maafisa wa Ofisi hiyo walikataa na wakati wakijadiliana kuhusu hilo, mtoto alichoropoka kutoka kwa mama yake na kugongwa na gari linalomilikiwa na Mamlaka hiyo.

Siku ya Alhamisi polisi ilizuia kupelekwa kwa mwili katika Bunge, wakisisitiza mwili huo uzikwe ili marehemu apumzike kwa amani, na kuwataka waepuka jambo hilo kushughulikiwa kisiasa.
Share:

Mkanyagano hatari wawaua 11 Zimbabwe.......

Watu 11 wamefariki katika mkanyagano nchini Zimbabwe baada ya ibada ya kidini kufnayika katika uwanja wa soka.
Polisi wanasema kuwa watu wanne walifariki katika uwanja huo ulio mjini Kwekwe wakati wengine saba wakifariki hospitalini.
Mkanyagano huo ulitokea wakati maelfu ya waumini wakikimbilia kuondoka uwanjani humo baada ya ibada iliyoongozwa na mhubiri wa kipentekoste Walter Magaya.
Mhubiri huyo anadai kuwaponya watu kwa kufanya miujiza.
Baadhi ya walioshuhudia mkanyagano huo wanatuhumu polisi kwa kufunga baadhi ya milngo ya kuondokea uwanjani humo, huku watu wakiondoka kupitia mlango mmoja tu.
Hata hivyo polisi wanakana kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya.

Bwana Mugaya ambaye ni mkuu wa kanisa la 'Prophetic Healing and Deliverance' aliambia vyombo vya habari kuwa alipopata habari ya kutokea vifo hivyo alihuzunika sana.
Share:

Shambulio laua tena Mombasa Kenya.....source BBC

Mtu mmoja ameripotiwa kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mapigano katika mji wa Mombasa pwani ya Kenya. Polisi walipambana na vijana walioingia katika Msikiti wa Swafaa eneo la Kisauni na mpaka sasa zaidi ya vijana 400 wanashikiliwa tangu kuanza kwa msako huo, mapema wiki hii.
Mwandishi wa BBC, Emmanuel Igunza anasema Msikiti huo ulifungwa jana baada ya polisi kuuvamia Jumatano, ambamo walipata magruneti, mabomu ya petroli na silaha nyingine. Hali ya wasi wasi bado imetanda katika mji huo wa pwani. Serikali imekwishafunga misikiti minne ambayo wanasema ina uhusiano wa watu wenye misimamo mikali ya imani ya kidini.
Pamoja na kukamata silaha mbalimbali, polisi pia walikamata bendera nyeusi, alama ya kuunga mkono kundi la kigaidi la Al-Shabab la nchini Somalia

Awali polisi mjini Mombasa pwani ya Kenya walisema wamepata silaha nyingine zaidi yakiwemo mabomu katika msikiti wa tatu ambao ulifanyiwa upekuzi                                               Msako huo katika msikiti wa Swafaa mtaani Kisauni unakuja baada ya msako mwingine wa Jumatatu ambapo polisi pia walipata silaha ndani ya msikiti ambao wanasema hutumika kutoa mafunzo yenye itikadi kali.
Mtaa wa Kisauni ndiko vijana waliokuwa wamejihami kuwadunga visu watu wanne na kuwaua. Pia waliwashambulia kwa silaha nyingine.
Waziri wa usalama wa ndani, Joseph Ole Lenku anasema kuwa msako huo ulifanywa katika misikiti ambayo hutumiwa na watu wanaoeneza itikadi kali za kiisilamu kwa vijana ambao inadaiwa wanajiunga na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab nchini Somalia.
Viongozi wa kiisilamu wamelaani misako hiyo katika Misikiti wakisema kuwa itachochea zaidi vijana kuendeleza itikadi kali za kidini.
Share:

Rais Obama awatangazia neema wahamiaji.....source BBC


Rais Barack Obama amelihotubia taifa kueleza mageuzi makubwa katika mfumo wa uhamiaji wa Marekani. Amesema atachukua hatua za kikatiba kutoa ruhusa ya muda kisheria kwa takriban wahamiaji haramu milioni tano. Obama amesema nchi hiyo ilijengwa kwa uhamiaji na ameshutumu wanachama wa Republican kwa kuzuia mageuzi hayo. Wanachama hao wametishia kuchukua hatua.
Amesema watakaohalalishwa watalazimika kulipa kodi na wasiwe na rekodi ya uhalifu. Hata hivyo amesema urejeshwaji makwao kwa watu wenye makosa utaharakishwa.
Bwana Obama ametangaza mpango wake, ambao anaupitisha bila baraza la Congress, katika hotuba aliyoitoa kupitia televisheni.
Kwa upande wao wajumbe wa Republican wamesema hatua ya Rais Obama inavuka mipaka yake na uhusiano na rais utaingia dosari
Kuna wahamiaji wasio halali wapatao milioni 11 nchini Marekani na mwaka huu watoto wanaovuka mpaka wamesababisha tatizo.
Rais Obama ameliambia taifa kuwa kile anachopendekeza sio msamaha
"Ninachokieleza ni uwajibikaji - akili ya kawaida, mtazamo wa kawaida," amesema.
"Kama unatimiza vigezo, unaweza kujitokeza na kuishi maisha ya kawaida ukiendana na sheria."
"Iwapo ni mhalifu utarejeshwa ulikotoka.Kama unapanga kuingia Marekani kinyume cha sheria, nafasi ya kukamatwa na kurejeshwa ulikotoka ni kubwa." anasema Rais Obama.
Rais Obama amesema mfumo mpya wa uhamiaji utawawezesha watu wanaoishi nchini Marekani kinyume cha sheria, kujulikana na kuchangia katika uchumi wa taifa kwa kuwa watakuwa huru kufanyakazi.
Kuamuru kufanyika kwa mageuzi hayo kumesababisha malalamiko ya hasira kwa wanachama wa Republicans ambao wanasema hatua hiyo ni kutolishirikisha baraza la Congress na kuendesha mambo kwa mfumo wa Kifalme. Baadhi wanasema hawatatoa ushirikiano katika maeneo mengine ya kisera, na wengine wamemtaka Bwana Obama ashitakiwe.

Rais Obama anasema anachukua hatua hiyo kwa sababu baraza la Congress mara kadha kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu limeshindwa kurekebisha mfumo wa uhamiaji ambao umeharibika.
Share:

Msichana kutoka Syria ashitakiwa.....

Monique akiwa mbele ya TV akiomba binti yake kurejea nyumbani Uholanzi miezi miwili iliyopita
Msichana wa kiholanzi aliyerejea kutoka Syria ambako alikwenda huko kujiunga na wapiganaji wa jihadi lakini baadaye alirudishwa nyumbani na mamake anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kushukiwa kutishia usalama wa taifa.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 19, akijulikana kama Aicha, alikamatwa aliporejea nyumbani kwao katika mji wa Maastricht.
Aicha, aliyebadili dini hivi karibuni kuwa Mwislam, anaaminika kusafiri kwenda kujiunga na wapiganaji wa Islamic State (IS) katika ngome ya Raqqa nchini Syria kuoana na mpiganaji mmoja.
Mama yake Monique alisaidia kumrejesha nyumbani Uholanzi na si mtuhumiwa.
Aicha ni mmoja wa idadi ndogo ya wasichana na wanawake kutoka Ulaya ambao wamekwenda Syria na Iraq katika miezi ya karibuni.
Baadhi wanaaminika kusafiri kwenda hukokupata mafunzo ya kiitikadi, wakati wengine wanasemekana kuoana na wapiganaji, wakiwemo wanaopigana bega kwa bega na wapiganaji wa IS.
Mahakama nchini Uholanzi Ijumaa itasikiliza kesi hiyo bila wasikilizaji na itaamliwa Aicha anaweza kushikiliwa kwa muda gani.

Upande wa mashitaka unatarajiwa kumwomba jaji kuongeza muda wa kumshikilia Aicha wakati wakichunguza ushahidi.
Share:

Thursday, 20 November 2014

Obama kutangaza mabadiliko ya uhamiaji......source BBC



Ikulu ya Marekani imesema Rais Obama atatumia muda ambao watazamaji wa televisheni nchini humo wanaangalia zaidi matangazo siku ya Alhamisi kutangaza mabadiliko makubwa ya mfumo wa uhamiaji wa nchi hiyo.
Inatarajiwa kuwa Rais Obama atasema kuwa atatumia madaraka yake aliyopewa kikatiba kuzuia wahamiaji wapatao milioni tano kurejeshwa makwao na badala yake wapatiwe vibali vya kufanya kazi nchini humo.

Rais Obama amesema hayo katika video iliyotumwa katika ukurasa wa facebook kabla ya hotuba yake.Tangu kuingia madaraka Obama amekuwa akipigania baadhi ya mabadiliko ikiwemo huduma ya utoaji wa huduma za afya kwa mfumo wa bima ya afya.
Share:

Bill Cosby ashutumiwa kuwa mdhalilishaji......source BBC


Televisheni ya NBC imesitisha mradi wa kurusha kipindi cha mchekeshaji maarufu duniani, Bill Cosby baada ya kukabiliwa na shutuma zaunyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake .
Katika taarifa hiyo, kampuni imethibitisha kusimamishwa kwa kipindi hicho.
Siku ya jumanne kamouni inayotoa huduma ya vipindi vya video kwa njia ya internet, Netflix iliahirisha kipindi kilichomuhusu Cosby baada ya mwanamitindo mmoja kudai kuwa alidhalilishwa kijinsia mwaka 1982.
Mtandao wa Netflix ulikataa kutoa sababu ya kusitisha uzalishaji wa kipindi, lakini umesema kuwa maandalizi ya uzalishaji ulikua haujaanza. Cosby amekana kuhusika na vitendo hivyo.
Hatua hii imekuja baada ya mwanamitindo na mtangazaji kipindi cha Televisheni Janice Dickinson kusema kuwa alidhalilishwa na Cosby walipokutana kwa ajili ya chakula cha usiku huko California mwaka 1982.
Janice amesema aliandika katika kitabu kinachohusu maisha yake kuhusu tukio hilo lakini alipata shinikizo kutoka kwa Mwanasheria wa Cosby na mchapaji wa kitabu chake kuondoa sehemu hiyo.
Mwanasheria wa Cosby Martin Singer amesema madai ya Dickinson ni ya uongo na hayana msingi.
Dickinson ni miongoni mwa wanawake kadhaa waliomshutumu kuwadhalilisha kijinsia miaka takriban 30 iliyopita.
Nae muigizaji wa zamani Barbara Bowman amesema alidhalilishwa na Cosby katika nyakati tofauti mwaka 1985 alipokuwa na umri wa miaka 17.
Mwanzoni mwa mwezi huu Barbara alisema alishindwa kupeleka mashitaka polisi kwa kuwa alihofu hataaminika.

Cosby hajawahi kushtakiwa kwa kosa lolote la kihalifu.
Share:

Mkuu wa kampuni ya ferry Korea jela....


 Mahakama moja nchini Korea kusini imemhukumu miaka kumi gerezani mkurugenzi mkuu wa kampuni iliyoitengeza feri ya Sewol iliyozama mwezi Aprili na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 300, wengi wao wakiwa ni watoto.
Mahakama ya wilaya ya Gwangju imeelezwa kwamba feri hiyo ilikarabatiwa kuweza kubeba mizigo zaidi na mabadiliko hayo yaliongeza uwezekano wa chombo hicho kupindukia.
Mapema mwezi hu kapteni wa feri hiyo, alihukumiwa miaka 36 kwa kukwepa majukumu yake. Mmiliki wa kampuni hiyo alifariki akitoroka.
Wapiga mbizi waliiokoa miili 295 kabla ya serikali kusitisha shughuli hiyo ya kutafuta miili zaidi wiki iliyopita. Bado waathirwa tisa hawajulikani waliko.
Share:

Wednesday, 19 November 2014

Binti ajinasua na ndoa ya mwanamgambo.......source BBC


Mwanamke mmoja raia wa Uholanzi amewasili nchini Uturuki baada ya safari iliyojaa hatari nchini Syria kwa ajili ya kumchukua binti yake aliyekua mjini Raqqa, mji unaokaliwa na waasi wa Islamic State..............>>>>>INGIA HAPA<<<<<
Share:

Familia ya Bob Marley kuuza bidhaa za Bangi...... source BBC


Familia ya aliyekuwa mwanamuziki wa Jamaica, Bob Marley imezindua kampuni ambayo wanaitaja kama ya kwanza duniani kuuza bidhaa za Canbbisa au marujuana au Bangi kama wanavyoijua wengi.... >>>>INGIA HAPA<<<<
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.