Tuesday 2 December 2014

Mashine yenye uwezo wa kufikiri kitisho..........




















Profesa Stephen Hawking, mmoja wa wanasayansi mahiri nchini Uingereza, amesema juhudi za kutengeneza mashine inayofikiria inatishia uwepo wa binadamu............>>>>>INGIA HAPA<<<<<
Share:

Wakuu wa usalama watimuliwa Kenya...........source BBC

Aliyekuwa waziri wa usalama Joseph Ole Lenku

Rais Uhuru Kenyatta amemwachisha kazi waziri wa usalama Joseph Ole Lenku na kumpendekeza waziri mpya wa usalama Joseph Nkaiseri kuchukua nafasi hio.
Wakati huohuo mkuu wa polisi nchini Kenya inspekta generali David Kimaiyo amejiuzulu kutokana na shinikizo dhidi yake afanye hivyo kwa kushindwa kukabiliana na utovu wa usalama nchini.
Rais Kenyatta alisema kuwa baada ya mazungumzo na Bwana Kimaiyo alikubali 'kustaafu' mapema kutoka kwa majukumu yake kwa sababu za kibinafsi.
Rais alitoa tangazo hilo wakati akihutubia taifa kufuatia shambulizi la hapo jana dhidi ya wachimba migodi 36 waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera Kaskazini ya Kenya.

Aliyekuwa mkuu wa polisi David Kimaiyo
Rais pia alitangaza kuwa amekubali ombi la Generali wa polisi David Kimaiyo kuachia wadhifa wake.
Kimaiyo na Ole Lenku wamekuwa wakikabiliwa na shinikizo za kuachia ngazi kufuatia kukithiri kwa utovu wa usalama nchini.
Hatua ya kuwatimua kutoka katika nyadhifa zao wawili hao bila shaka litakuwa jambo la kuridhisha kwa wakenya wengi ambao wamekuwa wakilalamikia utovu wa usalama na kuwataka waondoshwe ofisini.
Uteuzi wa Joseph Nkaisery kama waziri mpya wa usalama ni jambo jipya kwani atakuwa mwanasiasa wa kwanza kutoka kwa upinzani kuwa ndani ya serikali.
Alipokuwa anahutubia nchi,Rais Kenyatta aliwasihi wabunge kuongeza mda wa vikao vyao vya leo ili kumhoji na kumkagua Nkaisery aliyeteuliwa kuchukua nafasi ya waziri mpya wa usalama na maswala ya ndani ili wamuidhinishe.
Share:

Al Shabaab waua 36 Mandera,Kenya................

       
                 Kundi la wanamgambo nchini Somalia Al Shabaab limekiri kuwaua watu 36 katika                               shambulio lililotokea kwenye machimbo ya kokoto karibu na mji wa Mandera kaskazini                    mwa Kenya.
Katika taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa kundi hilo, wanamgambo hao wamesisitiza kuwa ndio waliowaua wakenya hao kwa sababu ya majeshi ya Kenya kuendelea kuwa nchini Somalia.
Taarifa za mauaji hayo zilitolewa kwa mara ya kwanza na Shirika la Msalaba Mwekundu.
Inaarifiwa kuwa wafanyakazi hao walipigwa risasi wakiwa katika mahema ya. Walioshuhudia shambulizi walisema kwamba wapiganaji hao waliwatenga waisilamu na wakristo huku wakiwachinja baadhi, na kuwapiga risasi wlaiosalia.
Wakazi wa eneo hilo wamesema waathirika wote wa tukio hilo ni watu wasio Waislam ambao walikuwa wakifanya kazi katika machimbo hayo yaliyopo Kormey kilomita 15 kutoka mji wa Mandera Kaskazini mwa Kenya.
Tukio hili linafuatia tukio la wiki moja iliyopita ambapo watu wapatao 28 waliuawa katika shambulio la basi la abiria huko Mandera.

Kundi la wapiganaji wa Kiislam la Al Shabab wamekiri kuhusika na mauaji hayo.
Mkuu wa Polisi eneo hilo, amesema bado wanafuatilia tukio hilo.
Katika tukio lingine, mtu mmoja ameripotiwa kuuawa nchini Kenya kufuatia mlipuko katika klabu moja ya usiku katika mji wa Wajir kaskazini mwa Kenya.
Kwa mujibu wa Kamishna wa Polisi wa Wajir, Frederick Sishia, shambulio hilo limefanyika saa mbili usiku na kuua mtu mmoja na watu wengine wanne wamejeruhiwa.
Washambuliaji hao walitumia magruneti na silaha nyingine za kijeshi kufanya shambulio hilo.
Wiki iliyopita watu wengi waliuawa eneo la Mandera kaskazini mwa Kenya.

Kenya imejikuta ikilengwa na mashambulio ya kigaidi tangu majeshi yake yapelekwe nchini Somalia kukabiliana na wapiganaji wa Al Shabab. Mbali na miji ya kaskazini mwa Kenya kushambuliwa kila mara, miji mikubwa nchini humo ya Nairobi na Mombasa imekuwa ikilengwa na mashambulio ya kigaidi.
Share:

Kenyatta:Kenya haitatikiswa na magaidi.............


Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema kuwa Kenya haitachoka katika vita vyake dhidi ya ugaidi kufuatia shambulizi lililofanywa dhidi ya wachimba migodi mjini Mandera Kaskazini ya Kenya.
Ametoa kauli hiyo katika hotuba yake kwa taifa baada ya shambulizi lengine lililofanywa na kundi la wanamgambo la Al Shabaab dhidi ya wakenya wasiokuwa na hatia.
Kundi hilo liliwavamia wachimba migodi 36 waliokuwa katika machimbo ya kokoto mjini Mandera.
Kundi hilo liliwaua wakenya wengine 28 waliokuwa wanasafiri kutoka mjini Mandera siku kumi zilizopita.
Kenyatta amelaani wanamgambo hao wa Al Shabaab kwa kutaka kuigawanya Kenya katika msingi ya kidini na kuwataka wakenya kuungana dhidi ya kile alichokitaja vita dhidi ya ugaidi.
Kenyatta aliwataka magaidi wa Al Shabaab kama wanyama walio na kichaa.
Aliwasihi wakenya kuungana katika vita dhidi ya magaidi.

Siku kumi zilizopita, Al Shabaab waliuwaua abiria 28 waliokuwa wanasafiri kwa basi kutoka mjini Mandera karibu na mpaka na Somalia kuelekea likizoni makwao. Wengi wa waliouawa walikuwa walimu wa shukle za umma.
Share:

Jela miaka 50 kwa kuwaharibu watoto Kenya.........


Mahakama nchini Kenya imemhukumu kifungo cha miaka 50 jela raia mmarekani kwa kutengeza na kusambaza picha chafu za video za watoto wakifanya vitendo vya ngono.
Terry Ray Krieger alikiri makosa yake mbele ya mahakama mwezi jana. Pia alipatikana na kosa la kuwadhalilisha watoto wadogo huku akinasa vitendo hivyo kwa kanda ya video.
Alikamatwa na maafisa wa usalama Kenya baada ya kupata taarifa kutoka kwa shirika la kimataifa la polisi kwamba alikuwa anasambaza video hizo zilizokuwa zinaonyesha watoto wakifanyiwa vitendo vichafu kwenye mtandao.
Krieger amewahi kushtakiwa kwa makosa sawa na hayo na kufungwa jela nchini Marekani miaka 20 iliyopita.
Polisi wa Kenya walipokea taarifda kutoka kwa polisi nchini Marekanmi wakiwaamiwa kuwa kuna raia mmarekani nchini Kenya anayetengeza na kusambaza video chafu za watoto wadogo wakihishwa na vitendo vya ngono.

Aliomba mahakama kumuonea huruma kutokana na maradhi anayougua ya mifupa lakini mahakama ilisema kuwa maradhi yake sio haiwezi kuwa sababu ya kutowajibishwa kwa makosa yake.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.