Wednesday 28 October 2015

Matokeo ya uchaguzi Zanzibar yafutwa....source BBC


Mwenyekiti wa ZEC amesema uchaguzi huo unafaa kurudiwa

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi visiwani humo akisema uchaguzi huo ulijaa kasoro nyingi.
Kulingana na mwanahabari wa BBC aliyeko hilo Sammy Awami, mwenyekiti huyo ametangaza hatua hiyo kupitia runinga ya serikali visiwani ZBC.
Bw Jecha amesema kuwa uchaguzi huo haukuwa wa haki na kwamba kulikuwa na ukiukaji mkubwa wa sheria za uchaguzi, kwa mujibu wa taarifa ambayo baadaye imetumwa kwa vyombo vya habari.
Amesema baadhi ya makamishna wa tume hiyo, badala ya kutekeleza majukumu yao inavyotakiwa kikatiba "wamekuwa ni wawakilishi wa vyama vyao".
"Kumegundulika kasoro nyingi katika uchaguzi huu miongoni mwa hizo ni kubainika kwa baadhi ya vituo hasa Pemba vimekuwa na kura nyingi kuliko daftari la wapiga kura wa kituo husika."
Amesema hilo ni jambo la kushangaza ikizingatiwa kwamba "baadhi ya wapiga kura hawakwenda kuchukua vitambulisho vyao vya kupigia kura".
Kadhalika, amesema kura hazikupata ulinzi mzuri hususan kisiwani Pemba ambako amesema kuwa baadhi ya mawakala wa baadhi ya vya vyama vya siasa katika kisiwa hicho walifukuzwa.
Ameongezea kuwa vijana katika eneo hilo walivamia vituo vya kupigia kura kwa lengo la kutaka kuzua ghasia, na pia vyama vya siasa vilionekana "kuingilia majukumu ya tume ikiwemo kujitangazia ushindi na kupelekea mashindikizo kwa tume."

Hii ni sehemu ya taarifa ya Bw Jecha

"Nimeridhika kwamba uchaguzi huu haukiwa wa haki na kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria na taratibu za uchaguzi," amesema Bw Jecha.
"Hivyo, kwa uwezo nilionao natangaza rasmi kwamba uchaguzi huu na matokeo yake yote yamefutwa na kwamba kuna haja ya kurudia uchaguzi huu."
Tangazo la mwenyekiti huyo limetolewa huku hali ya wasiwasi ikiendelea kutanda visiwani humo.
Siku moja baada ya uchaguzi kufanywa, mgombea wa chama cha upinzani cha Civic United From (CUF) Seif Sharif Hamad alijitangaza kuwa mshindi, hatua iliyokemewa na chama cha CCM ambacho mgombea wake Dkt Ali Mohamed Shein amekuwa rais wa visiwa hivyo muhula unaomalizika.
Tume ya uchaguzi visiwani humo pia ilishutumu hatua ya mgombea huyo. Kabla ya kufutiliwa mbali kwa matokeo ya uchaguzi, tume hiyo ya uchaguzi ilikuwa imetangaza matokeo ya majimbo 31 kati ya majimbo 54 visiwani humo.
Hayo yakijiri Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania inaendelea kutoa matokeo ya uchaguzi wa urais. Kufikia sasa imetoa matokeo ya majimbo 155 kati ya majimbo 264.
Share:

Sababu 8 za kufutwa kwa uchaguzi Zanzibar... source BBC


Hizi ndizo sababu nane zilizotolewa na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wa kisiwani Zanzibar Bw Jecha Salim Jecha kuhusu kufutiliwa mbali kwa matokeo ya uchaguzi wa eneo hilo.
1. Makamishna wa uchaguzi katika tume hiyo walipigana kutokana na tofauti zao
2. Makamishna walikuwa na upendeleo fulani.
3. Katika vituo vyengine, hususan kisiwani Pemba,ambacho ni miliki ya Zanzibar, kura zilizopigwa zilikuwa zaidi ya zilizosajiliwa.
4. Masanduku ya kupigia kura hayakupewa ulinzi wa kutosha na maajenti pamoja na maafisa wa uchaguzi.
5. Maajenti wa vyama walifukuzwa katika vituo kadhaa.
6. Vijana walivamia vituo vya kupigia kura wakiwa na lengo la kuzua ghasia.
7. Vyama vya kisiasa vimekuwa vikiingilia tume hiyo.
8.Kura ziliharibiwa hususan zile kutoka Pemba
Share:

Lowassa apinga matokeo ya uchaguzi TZ... source BBC


Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha CHADEMA Edward Lowassa amesema kuwa hatokubali matokeo ya uchaguzi wa urais yanayoendelea kutolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania (NEC).
Kiongozi huyo amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha kwamba kuna udanganyifu uliofanyika.
Amesema kuwa kura za chama hicho zimepunguzwa katika vituo vingi vya kupigia kura.
Akihutubia wanahabari pamoja na viongozi wengine wa upinzani, amesema kwamba kura zilizohesabiwa katika maeneo tofauti haziambatani na matokeo yaliyotolewa.
Lowassa ameongezea kwamba maeneo yote ambayo walipata ushindi yamecheleweshwa. Aidha, amelalamikia kukamatwa kwa maajenti wa chama hicho akidai kuwa ni ishara za kutaka kuiba kura.
Share:

Jeshi lakomboa 300 kutoka kwa Boko Haram Nigeria... source BBC

Boko Haram
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa limefanikiwa kuwakomboa watu 338 kutoka kwa wapiganaji wa Kiislamu wa Boko Haram.
Wapiganaji 30 waliuawa kwenye operesheni hiyo kwenye ngome moja ya kundi hilo katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo mnamo Jumanne.
Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa jeshi Kanali Sanni Kukasheka Usman, wanajeshi walishambulia kambi za wapiganaji hao kwenye msimu wa Sambisa na kukomboa watoto karibu 200, wanawake mia moja na wanaume wanane.
Mwandishi wa BBC aliye Abuja Chris Ewokor anasema kufikia sasa hakujatolewa maelezo zaidi kuhusu watu waliokombolewa.
Operesheni hiyo ni moja ya operesheni kubwa zaidi kufanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya wanamgambo hao.
Boko Haram
Jeshi linaonekana kujikakamua kutimiza makataa ya miezi mitatu ambayo walipewa na Rais Muhammadu Buhari kuwashinda Boko Haram, ingawa muda unayoyoma.
Wanamgambo hao wamekuwa wakitekeleza mashambulio ya kujitoa mhanga na kuua watu wengi kaskazini mashariki mwa taifa hilo, wengi wao waumini wa dini ya Kiislamu misikitini.
Share:

Ouattara ashinda uchaguzi Ivory Coast... source BBC



Alassane Ouattara ameshinda uchaguzi wa urais nchini Ivory Coast kwa wingi wa kura. Matokeo yalitangazwa kupitia runinga huku rais huyo akishinda kwa asilimia 83.66.
Hii inamaanisha kwamba hakutakuwa na duru ya pili ya uchaguzi.
Raia wa Ivory Coast waliamkia habari za ushindi wa Rais Alassane Outtara kama walivyotarajiwa kwamba rais huyo ataongoza kwa muhula mwengine wa miaka mitano.
Baada ya mwongo mmoja wa kutoimarika kwa uchumi na vita vya wenyewe kwa wenyewe, wengi watafurahia kwamba uchaguzi huo ulifanyika kwa amani.
Uchaguzi wa mwisho wa urais uliofanyika mwaka 2010 ulisababisha vita vya miezi mitano ambapo zaidi ya watu elfu 3000 waliuawa.
Rais wa zamani Laurent Gbagbo, yuko mjini the Hague katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita akingojea kesi inayomkabili.
Ijapokuwa rais huyo amekosolewa kwa kushindwa kuleta maridhiano na haki, amesifiwa kwa kuimarisha uchumi wa taifa hilo na kulifanya kuwa taifa lenye uchumi ulioimarika kama ilivyokuwa miaka ya sabini.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.