Thursday 2 April 2015

Mazungumzo ya nyuklia ya Iran yaafikiwa..



Makubaliano kuhusu muundo wa baadaye wa mpango wa nyuklia wa Iran, yamefikiwa baada ya mazungumzo na mataifa sita makubwa yaliyokuwa yakifanyika nchini Uswisi.

Kwa mujibu wa mkataba huo, Iran itapunguza uwezo wake wa kurutubisha madini ya urani huku ikiahidiwa kuondolewa vikwazo kwa awamu.
Rais Barack Obama amesema ni "uelewano wa kihistoria" uliofikiwa na Iran.
Mataifa makubwa ya dunia na Iran sasa yanalenga kuandika mkataba kabambe ifikapo Juni 30.
Muundo wa mkataba ulitangazwa na Umoja wa Ulaya na Iran baada ya siku nane za majadiliano mjini Lausanne.
Mazungumzo kati ya mataifa makubwa matano jumlisha moja yaani-Marekani, Uingereza, Ufaransa, China na Urusi pamoja na Ujerumani- na Iran katika mkutano uliofanyika mjini Lausanne, uliendelea na kupitiliza muda uliopangwa wa kufikia tarehe 31 Machi.
Mwandishi wa BBC kutoka mjini Lausanne, Barbara Plett Usher, anasema baada ya kupitiliza muda uliopangwa na siku mbili za majadiliano ya kina kati ya Iran na mataifa sita makubwa duniani wameelezea muundo wao uliofikiwa katika mkutano huo kama mafanikio makubwa.

Mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya,Federica Mogherini, alisoma taarifa ya pamoja ikielezea vipengele vikuu, ambavyo ni kupunguza vinu vya uchakataji wa fito za nyuklia, kubadili zana za kutengenezea nyuklia na ahadi ya kuondolewa vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran.
Makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano huo si ya maandishi, sio rasmi, bali yanajenga msingi wa kufanyika mazungumzo ya kina.
Lakini waanzilishi wa mazungumzo haya wanasherehekea mafanikio makubwa yaliyofikiwa, ambayo wanasema ni ya kihistoria.
Iran imekuwa ikikana madai ya mataifa ya magharibi kuwa mpango wake wa nyuklia unalenga kutengeneza silaha za nyuklia. Iran imeingia katika mazungumzo haya ili kuona inaondolewa vikwazo.

Katika mahojiano na BBC, waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry amesema ilifikia hatua alishawishika kujitoa katika mazungumzo hayo lakini anasema cha msingi wameweza kupenya vikwazo vilivyojitokeza katika awali.
Rasimu ya mazungumzo hayo pia imepongezwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, ambaye amesema anaamini "yatachangia hali ya amani na utulivu katika eneo hilo".
Mkuu wa sera ya nje wa Umoja wa Ulaya Federica Mogherini ametangaza mkataba huo katika mkutano na waandishi wa habari akiwa pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif, akisema hiyo ni "hatua ya maamuzi" iliyofikiwa.

Urusi imepongeza mkataba huo kuwa ni hatua ya kutambua mpango wa nyuklia wa Iran usio na masharti na ambao ni salama.
Lakini kiongozi wa Israel, Benjamin Netanyahu amemwaambia Rais Obama kwa njia ya simu kwamba mkataba huo ambao umejikita katika muundo uliokubaliwa, unatishia uwepo wa Israel.
Kwa upande wake Rais Obama amemwambia Bwana Netanyahu kwamba mkataba huo kwa namna yoyote ile unaondoa wasiwasi kwao kuwa Iran ni kinara wa kufadhili ugaidi na vitisho dhidi ya Israel.
Mkataba huo pia umekosolewa na wajumbe wa baraza la Congress la Marekani ambao wanataka wabunge wa Marekani kuwa na haki ya kupitia kila makubalino ya mwisho yanayofikiwa katika mkataba huo.
Nao wananchi wa Iran wanaoishi nchini Uswisi wameelezea kufurahishwa na mpango huo.
Share:

Vigogo wa Siasa na mdahalo,Uingereza...


Viongozi wa vyama vitano vya siasa nchini Uingereza wameshiriki katika mdahalo ulioonyeshwa moja kwa moja katika televishen ambao ulilenga maeneo mhimu katika harakati za kuijenga Uingereza.
Kila kiongozi katika mdahalo huo viongozi hao walipewa muda wa kujibu maswali kuhusu masuala ya kiuchumi,uhamiaji,afya na mtazamo ujao kuhusu Uingereza. Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amekitetea chama chake cha Conservative kwamba kimekuwa na mipango mizuri ya kiuchumi na kukubali mapendeekezo yaliyotolewa na chama cha upinzani cha Labour.
Mwandishi wa BBC kuwa katyika mdahalo huo hakukuwa na mshindi,kwani hayo siyo yalikuwa malengo ya mkusanyiko huo,bali fursa ya kubainisha mamabo ya mhimu na kwamba hata baadhi ya vyama vidogo vingeweza kushiriki.
Share:

Kanisa Katoliki linautazamaje ushoga


Kadinali Raymond Burke mwenye asili ya Marekani ameenguliwa na Papa Francis katika wadhifa wake wa mwenyekiti wa bodi katika kanisa katoliki,ametoa onyo kwamba kuna viashiria vya kanisa hilo kuupigia chapuo ushoga, kauli hii Burke aliiotoa wakati alipokuwa akihojiwa na tovuti moja ya Italy ya La Nuova Bussola Quotidiana mara baada tu ya kuenguliwa kwenye wadhifa wake.
Mwandishi wa BBC anasema hii ni ishara nyingine ya jinsi viongozi wa dini waandamizi wanavyochukulia hatua juu ya masuala kama vile ushoga na talaka , wakati wengine wanatakiwa kuyachukulia mambo kwa utuvu na uangalifu wa hali ya juu.
Share:

Kura ya maoni yaahirishwa Tanzania..


Tume ya Uchaguzi wa taifa la Tanzania, kukabiliwa na na msisitizo wa muda mrefu wa wananchi juu ya kuahirishwa kwa tarehe ya kufanyika kura ya maoni kuhusu katiba inayopendekzwa na tume hiyo kutoa msimamo kwamba tarehe haitobadilika, leo hii tume hiyo imetoa kauli tofauti. Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi , Jaji Mstaafu Damian Lubuva ametangaza kuwa zoezi hilo la kura ya maoni limeahirishwa, jambo ambalo limezua hisia tofauti nchini humo.
Share:

Askari 15 wa Misri wauawa barabarani..


Maofisa wa serikali nchini Misri wameeleza kuwa mtu mmoja aliyekuwa na silaha amewaua askari kumi na watano katika shambulio la kizuizi cha barabarani katika eneo la kaskazini la pwani ya mlima Sinai .
Jeshi la Misri limeingia katika vita ya kulinda maeneo yaliyoko Kaskazini yam lima Sinai kwa muda mrefu ili kuwabaini askari washambuliaji kinyume na majeshi ya serikali .
Siku za hivi makundi ya kigaidi yenye nguvu na msimamo mkali yamekula kiapo cha utii kwa kundi la wanamgambo wa dola ya Kiislam IS.
katika eneo la kaskazini la pwani ya mlima Sinai .
Jeshi la Misri limeingia katika vita ya kulinda maeneo yaliyoko Kaskazini yam lima Sinai kwa muda mrefu ili kuwabaini askari washambuliaji kinyume na majeshi ya serikali .
Siku za hivi makundi ya kigaidi yenye nguvu na msimamo mkali yamekula kiapo cha utii kwa kundi la wanamgambo wa dola ya Kiislam IS.
Share:

Kasi ya kujiunga na ugaidi yaongezeka...


Zaidi ya wapiganaji wa kigeni elfu ishirini na watano kutoka mataifa mia moja walisafiri kwa nia na malengo ya kujiunga na makundi ya kijeshi kama al-Qaeda na Islamic State (IS), taarifa ya umoja wa mataifa imeeleza hayo.
Taarifa hiyo imeeleza pia kwamba wapiganaji wageni ulimwenguni idadi yao imeongezeka mpaka kufikia asilimia sabini na moja katikati ya mwaka 2014 na march mwaka huu.
Nchi za Syria na Iraq ndizo nchi zinazolengwa kwa ukaribu zaidi na ndicho kitovu cha vijana wanaomaliza mazomo yao na kugeuka kuwa wenye msimamo mkali wa kidini.
Na pia taarifa hiyo imebainisha kuwa endapo kundi la IS lingeshindwa nchini Syria na Iraq,sasa wapiganaji hao kutoka nchi za kigeni wamesambaa ulimwenguni .
Nalo baraza la usalama la umoja wa mataifa liliwaomba wataalamu wa masula ya kijeshi miezi sita iliyopita kuchunguza vitisho vya askari wa kigeni wanaojiunga na kundi la Is na makundi mengine ya kigaidi.
Katika ripoti iliyowasilishwa kwenye baraza hilo mwishoni mwa mwezi uliopita ,na wataalamu wakaeleza kuwa ongezeko la wapiganaji wa nchi za kigeni zinazidi kuongezeka kulinganisha na muongo mmoja uliopita .
Maelfu ya wapiganaji wa kigeni ambao hufanya safari hadi nchini Syria ,Falme za Kiarabu na Iraq huko hufanya makao na kufanya kazi na kumalizia masomo ya elimu ya juu kwa wenye msimamo mkali kamalivyowahi kutokea kwatika nchi ya Afghanistan miaka ya 1990 .
Syria na Iraq inasemekana ina makaazi elfu ishirini na mbili kwa wapiganaji hao wa kigeni ,pia nchini Afghanistan makaazi elfu sita na mia tano na maelfu ya makaazi nchini Yemen, Libya, Pakistan na Somalia.
Share:

Mtu mwenye umri mkubwa duniani afariki...


Mtu aliyekuwa na umri mkubwa duniani kutoka nchini Japan amefariki wiki kadhaa baada ya kusherehekea miaka 117 tangu azaliwe.
Misao Okawa alifariki katika kituo cha uangalizi mjini Osaka,mji ambao alizaliwa mwaka wa 1898.
Okawa amewaacha vitukuu sita na wajukuu wanne .
Kufuatia kifo chake kuna madai kwamba kumesalia watu wanne pekee wanaodaiwa kuwa hai ambao walizaliwa karne ya kumi na tisa.
Wote ni Wanaume huku mwanamume wa mwisho akifariki mwaka 2013.
Share:

Meli ya uvuvi ya Urusi yazama..


Boti ya uvuvi ya Urusi imezama katika visiwa vya Kamchatka , ikiwa na mabaharia wapatao hamsini na wanne ambao inadhaniwa kuwa wamekufa maji wote.
Watu wapatao sitini na watatu wameopolewa ambao nao walikuwa ndani ya boti hiyo ya uvuvi,wengine wamekumbwa na homa ya mapafu na wengine kumi na watano wameripotiwa kuwa hawaonekani.
Taarifa za awali zinasema kwamba kabla meli hiyo ya uvuvi haijazama ilikuwa na watu wapatao miamoja na thelathini na mbili ,uchambuzi unaeleza kuwa sabini na nane kati yao ni raia wa Urusi na arobaini na wawili ni raia wa Myanmar. Wengi wao walikuwa wanatokea maeneo ya Vanuatu, Latvia na Ukraine na nahodha ni miongoni mwa waliopoteza maisha.
Kikosi cha uopoaji kinaendelea na kazi ya oukozi ambapo mpaka sasa wanatafuta abiria hao waliopotea wapatao kumi na watano .
Nahodha wa kikosi cha uongozi ambaye ni miongoni mwa mabaharia wa kikosi cha uopoaji ishirini na sita anasema kwamba pengine chanzo cha ajali hiyo ni hali mbaya ya hewa, na wakati meli hiyo ilipokuwa ikizama ,kulikuwa na barafu,upepo mkali, mawimbi yenye urefu wa futi kumi. Na maji ya bahari yalikuwa karibu yanaganda kwa nyuzi joto 32 .
Inaelezwa kwamba manusura wa ajali hiyo walikuwa wanauwezo wa kudumu katika maji hayo kwa dakika ishirini tu,ingawa mpaka sasa chanzo cha ajali hiyo ni cha kukisia tu.
Maji yalifurika kwenye chumba cha ingini ya meli hiyo na kuanza kuzama ndani ya dakika kumi na tano kimesema kitengo cha dharula cha Urusi,na kusema kwamba pengine meli hiyo iligonga eneo la karibu na chumba cha ingini na kuwa sababu ya ajali hiyo.
Sergei Khabarov amesmea kwamba kiwango cha abiria na mizingo katika meli za wavuvi lazima kizingatiwe na kisizidi uwezo wa vyombo hivyo.
Share:

Buhari aahidi kutokemeza Boko Haram..


Rais mteule wa Nigeria, Muhammadu Buhari, amezitaja vurugu zinazosababishwa na kundi la wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram kuwa ni tatizo kubwa linalokabili nchi.
Katika mahojiano maalumu na BBC, kiongozi huyo mstaafu wa jeshi amesema anatarajia kulishinda kundi hilo baada ya dhamira mpya kutoka jeshini na msaada wa nchi jirani. "Kwa ushirikiano na majirani zetu Cameroon, Chad, Niger na jumuia ya kimataifa na dhamira ambayo tutapata kutoka katika jeshi, Nafikiri itachukua muda mfupi zaidi kukabiliana nao."
Jenerali Buhari amesema tayari ameainisha msingi wa tatizo linalokabili nchi ya Nigeria, lakini amewataka raia wa nchi hiyo kuwa wavumilivu.
"Tumebaini matatizo makubwa matatu. Ambayo ni kukosekana kwa usalama nchini, tatizo ambalo kila mmoja analifahamu na lingine ni ukosefu wa ajira, hii ina maana uharibifu wa uchumi ikiwa ni kutokana na vitendo vya rushwa na rushwa yenyewe. Matatizo haya matatu makuu, Wanigeria wote wanafahamu na tunaomba ushirikiano wa wananchi wa Nigeria, wasitarajie miujiza kutokea katika kuyapatia ufumbuzi matatizo haya katika kipindi cha miezi michache baada ya kutwaa madaraka kwa sababu uharibifu umechukua miaka mingi, miaka kumi na sita ya utawala wa chama tawala cha nchi hii." Anasema rais huyo mteule wa Nigeria.
Share:

Amri wafugaji kuwapiga picha ngombe wao...


Polisi nchini India wamewalazimu wafugaji wa ngombe kuwapiga picha ilikufanikisha sheria mpya inayoharamisha uuzaji wa nyama ya ngombe.
Maafisa katika mji wa Malegaon, ulioko katika jimbo la Magharibi la Maharashtra wanasema kuwa pich hizo zitasaidia katika kutekelezwa kwa sheria hiyo mpya.
Sheria hiyo imeharamisha kuchinja na kuuza nyama ya ng'ombe kwa mjibu wa jarida la the times.

Sheria hiyo ya jimbo la Maharashtra ilianza kutekelezwa Machi tarehe mbili 2 baada ya mjadala uliodumu zaidi ya miaka 19.
" hizi picha tutazihifadhi kisha tutazitumia tu kukiwa na haja ya kutoa ushahidi'' alisema afisa mkuu wa jimbo hilo Mahesh Sawai.
"endapo mtu atamshaki mwenzake kwa kukiuka sheria hizi picha zitatumika kama itibathi ya umiliki wa ng'ombe''.

Polisi walitangaza sheria hiyo mmpya baada ya watu watatu kushtakiwa kwa kuvunja sheria hiyo mpya.
Hiyo ndiyo iliyokuwa kesi ya kwanza chini ya sheria hiyo mpya.
Jimbo hilo la Maharashtra liliharamisha uchinjaji wa ngombe mwaka wa 1976, lakini sheria hii mpya sasa inaharamisha hata kuchinja mafahali ambao kwa kawaida hufugwa kwa ajili ya nyama.

Hata hivyo nyama ya nyati ni halali katika jimbo hilo.
Adhabu ya hukumu ya miaka mitano gerezani inawasubiri wale wote watakaopatikana na hatia.
Haijulikali makataa hayo ya kutochinja ngombe itaathiri vipi idadi ya mifugo ambayo ilisemekana kuwa takriban milioni 21 ukilinganishwa na hesabu ya jumla ya watu milioni 112 kulingana sensa ya mwaka 2012.
Share:

Awekwa moyo wa mtu aliyekufa Uingereza...


Madaktari wa upasuaji huko Cambridgeshire wamefanya upandikizaji wa kwanza wa moyo barani Ulaya kwa kutumia moyo mwengine uliosimama kufanya kazi.
Myoyo hiyo hupatikana kutoka kwa watu waliokufa lakini ambao myoyo yao bado inafanya kazi.
Katika upasuaji huo,moyo huo ulitoka kwa mtu ambaye mapafu yake na moyo wake ulikuwa haufanyi kazi.
Hospitali ya Papworth inasema kuwa mbinu hiyo huenda ikaongeza idadi ya myoyo inayopatikana kwa asilimia 25.
Mgonjwa aliyewekwa moyo mpya kwa jina Huseyin Ulucan, mwenye umri wa miaka 60, kutoka London,alikabiliwa na shinikizo la moyo mwaka 2008.
Alisema:kabla ya upasuaji,sikuweza kutembea na nilichoka sana,kwa hakika siku na maisha mazuri.

Lakini anasema kuwa amefurahishwa na kuimarika kwa afya yake tangu upandikizaji huo.
Kwa sasa najisikia mwenye nguvu kila siku,na nimetembea hadi haospitalini asubuhi hii bila tatizo.
Kumekuwa na visa 171 vya upandikizaji wa myoyo katika kipindi cha miaka 12 iliopita nchini Uingereza.
Lakini mahitaji yanashinda myoyo iliopo ,hivyobasi wagonjwa wengine hungoja kwa miaka mitatu kupata kiungo kinachowafaa.
Wengi ya wagonjwa hao hufariki kabla ya kiungo kupatikana.
Share:

Sura ya mke yamtisha mumewe harusini...


Duniani kuna mambo, kuna vibweka na vibwakuro pia , twende sawa,Kang Hu, mwenye umri wa miaka 33,aliwashtua wageni waalikwa siku ya harusi yake, pale alipoamua kuwaomba radhi wakiwemo familia yake na bi harusi Na Sung,mwenye umri wa miaka 30,kwa kumwambia dhahiri shahiri kuwa ana sura mbaya na hafai kuolewa.

Bwana harusi harusi huyo alikanganyikiwa mara baada tu ya kumwona bi harusi wake kwa mara ya kwanza na kujaribu kujitosa majini.
Mara akaamua kutoka eneo la tukio, kwenye ukumbi wa sherehe katika mji wa Shiyan mji ulioko nchini China jimbo la Hubei na baadaye alioneka akitembea kando ya mto akiwa na mawazo meeengi,mto ambao alijirusha ndaniye mara moja.

Pal Chan Wang alisema kwamba : familia ya bi harusi ilivurugikiwa,familia ikashikwa na ghadhabu,na familia ya mwanaume yao ikafura na marafiki zake walifadhaika mnoo kwa matamshi yake .
Kang alikuwa na uchaguzi wa bi harusi amtakaye na alikuwa akilazimishwa kumuoa bi harusi huyo, ndo alipoamua kumfanyia kituko hicho.
Wapiti njia ndio waliomgundua Kang mtoni ndipo walipowaita polisi na kuharakisha kushuka mtoni kumuopoa.

Qan Tsui, mwenye umri wa miaka25, yeye ndiye aliyepiga picha hizi anaeleza kwamba bwana harusi huyo alipojitosa mtoni alikuwa na nguo zake zote na alikuwa akielea uso ukiwa unaelekea chini kwenye maji,akiwa hajiwezi na mara nikasema anaweza kufa asipopata msaada wa haraka.
polisi walipowasili eneo la tukio,mmoja wao alijitosa mtoni na kumdaka mara moja,na mwingine aliwarushia Kamba ili wamvutie nje ya maji ya mto huo baadaye wamtoe maji yaliyoko kifuani.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.