Saturday 27 June 2015

Misikiti 80 kufungwa Tunisia.


Utawala nchini Tunisia unasema kuwa utafunga misikiti 80 katika kipindi cha wiki moja inayokuja kwa madai ya kuhubiri chuki na jihad.
null
Hii ni kufuatia shambulizi lililofanyika kwenye hoteli moja hapo jana ambapo takriban watu 39 wengi wao wakiwa raia wa mataifa ya ulaya waliuawa na mwanamme mmoja aliyejifanya kuwa mtalii.
Wapiganaji wanaoshirikiana na wanamgambo wa Kundi la kiislamu la Islamic State wamesema kuwa wao ndio waliotekeleza shambulizi hilo.
null
Miili ya watalii ilikuwa imetapakaa ufukweni
Waziri mkuu nchini Tunisia Hanib Essid anasema kuwa misikiti hiyo ndio iliokuwa ikitumika kueneza propaganda na kuunga mkono ugaidi.
null
Waziri mkuu ametangaza kuwa misikiti hiyo ndiyo imekuwa ikihubiri Jihad
Hali ya usalama umeimarishwa maradufu katika maeneo mengi mjini Tunis na karibu na majengo yenye watalii wengi.
null
Mpiganaji mmoja alijifanya kuwa mtalii kabla ya kuwafyatulia risasi watalii ufukweni
Tayari wanajeshi wa akiba wameamrishwa kuripoti mara moja katika kambi za jeshi zilizoko karibu nao.
Share:

Vuna mbegu za kiume mkiwa na miaka18.


Mbegu za uzazi wa wanaume zinapaswa kuvunwa na kuhifadhiwa pindi mtu anapotimiza umri wa miaka 18.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na mtafiti wa maswala ya uzazi nchini Uingereza, manii ya mwanaume huwa katika hali bora zaidi wakati huo na hivyo zinapaswa kuvunwa na kisha kutumika kupandikiza wanawake katika siku za usoni.
Daktari Kevin Smith, ambaye ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Abertay kilichoko Dundee Uingereza anasema kuwa baada ya utafiti wa kipindi kirefu amebaini kuwa ni bora kuvuna manii mapema ilikuepuka maradhi mengi yanayochangiwa na kuongezeka kwa umri.
null
Daktari Kevin Smith ameorodhesha ugonjwa wa akili ''autism'', na ule wa kuchanganyikiwa ama ''schizophrenia'' miongoni mwa magonjwa mengine mengi.
Dakta Smith, anasema kuwa wizara ya afya ya Uingereza inapaswa kuunda hifadhi maalum ya mbegu za uzazi ilikupunguza visa vya maradhi aliyoorodhesha.
Maoni yake hata hivyo yanapingwa na muungano wa wauguzi wa uzazi ambao wanasema kuwa hilo halitakuwa suluhisho la kudumu.
Badala yake shirika hilo linaitaka serikali ya Uingereza iweke sera zitakazowasaidia waingereza waliofikia umri wa uzazi kupata ajira.
null
Takwimu zinaonesha kuwa wanaume wanaanza kupata watoto wakiwa na umri wa miaka 33 ikiwa ni ongezeko kutoka kwa miaka 31 katika miaka ya tisini.
Akitetea wazo lake katika jarida la madaktari la ''The Journal of Medical Ethics, Dakta Smith nasema kuwa wale wanaotaka kupata watoto mapema basi wafanye hivyo lakini kwa wale ambao wamegonga maiaka 40 ni vyema watumie mbegu walizohifadhi kwa matokeo mazuri zaidi.
Profesa Adam Balen, wa shirika la British Fertility Society, ameonya kuwa mbegu ziliyohifadhiwa huwa hazina nguvu kama zile zinazotolewa moja kwa moja.
null
''Kwa mtazamao hawa vijana wanahitahitaji ajira na wapenzi basi watapata watoto pasi na matatizp yeyote.''alisema Profesa Balen
Wakati huo huo mwanasayansi mwenza Sheena Lewis, aliwashauri wanaume waanze kushughulikia swala la familia mapema katika ujana wao.
''ninataka kuwaelezea wazi kuwa umri mzuri wa kuzaa kwa wanaume na wanawake ni kati ya miaka ya 20 na 30."
Share:

Simba warejea Rwanda baada ya miaka 20..


Mfalme wa mwituni Simba ,atarejea Rwanda kwa mara ya kwanza tangu aangamie wakati wa mauaji ya kimbari mwaka wa 1994
Maafisa wanaowalinda wanyama pori wa Rwanda, wanasema kuwa simba watarudi nchini humo siku ya jumatatu kwa mara ya kwanza, tangu walipoangamizwa baada ya mauaji ya kimbari,ya mwaka wa 1994.
Simba wawili dume, na majike watano, wanasafirishwa kutoka mbuga ya wanyama ya Kwazulu Natal, Afrika Kusini, na Jumatatu watawasili Rwanda kwa ndege.
null
Simba hao saba watawekwa kwenye karantini kisha waruhisiwe kutembea huru katika mbuga ya wanyama.
Wanyama hao watapelekwa katika mbuga ya taifa ya Akagera.
Maafisa wakuu huko Rwanda walisema, kurejeshwa tena kwa simba nchini Rwanda ,ni Kilele cha juhudi kubwa ya kuhifadhi mazingira katika mbuga hiyo na kwa taifa zima kwa jumla.
null
Baada ya mauaji ya kimbari mwaka wa 1994, watu wengi waliokimbia makwao waliikalia mbuga hiyo ya Akagera.
Simba waliokuwa humo walikimbia au kuuawa, huku watu wakijaribu kulinda mifugo yao na maisha yao.
Share:

Siku 1 jela kwa kukojoa hadharani India.


Watu 109 wamehukumiwa kifungo cha siku moja jela kwa kukojoa hadharani huko India.
Polisi waliwakamata takriban watu 109 kwa kukojoa katika vituo vya usafiri wa umma na reli.
Wale wote waliokamatwa wanatuhumiwa kwa kupatikana na hatia ya kukojoa nje ama ndani ya vituo vya reli mjini Agra Kaskazini mwa India .
Waliokamatwa watahukumiwa kifungo cha saa 24 korokoroni ama walipe faini ya kati ya dola mbili na kumi au vyote.
null

Maafisa wa afya ya umma wanasema walifanya operesheni hiyo kwa ghafla ilikukabili uvundo wa mkojo unaoathiri afya ya mamilioni ya watu wanaotumia huduma hiyo ya reli nchini India.
Mkuu wa polisi katika eneo hilo GRP, Gopeshnath Khanna aliyeongoza operesheni hiyo anasema kuwa itaendelea hadi wahindi wanaolaumiwa kwa kuharibu mazingira kwa kutema mate ukutani baada ya kutafuna thambuu na tumbako iliyowekwa rangina kukojoa katika maeneo ya umma watakapo badili tabia zao.
Aidha wasafiri wa reli wanasemekana kupigwa na harafu mbaya ya mkojo pindi wanapoingia ndani ya vituo hivyo.
null
Operesheni hii ni sehemu ya kampeini ya Waziri mkuu mpya Narendra Modi ya kuimarisha afya ya umma al maarufu 'Swachh Bharat.
Operesheni hiyo ni sehemu ya kampeini ya waziri mkuu mpya wa India Narendra Modi ya kuimarisha afya ya umma al maarufu 'Swachh Bharat.
Waandishi wa habari katika eneo hilo la Agra wanasema hii ndio mara ya kwanza kwa maafisa wa kulinda afya ya umma kwa ushirikiano na serikali ya majimbo kuwakamata vikojozi.
Takwimu za afya nchini humo zinaonesha kuwa takriban watu milioni mia sita 600m ama nusu ya raia wa India hawana vyoo.
Share:

Kenyatta: al Shaabab yaishiwa nguvu..

Rais Kenyatta huku amevaa sare ya jeshi
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amelaani siasa kali za baadhi ya Waislamu Afrika Mashariki.
Aliuambia mkutano wa kanda kuhusu usalama unaofanywa Nairobi kwamba kundi la Waislamu la al-Shabab limeishiwa nguvu na kwamba mashambulio yake ni ya kuinusuru tu al-Shabaab yenyewe, siyo kushinda.
Hapo Ijumaa, wapiganaji hao walishambulia kambi ya askari wa Umoja wa Afrika katikati mwa Somalia.
Wanajeshi wa kuweka amani kama 50 kutoka Burundi inaarifiwa waliuwawa.
Piya inaarifiwa kuwa wanajeshi wa Kenya walipambana na wapiganaji Ijumaa karibu na mji wa Dhobley, kusini mwa nchi.
Share:

15 kati ya waliouawa Tunisia ni Waingereza.


Maelfu ya watalii wanaondoka Tunisia baada ya shambulio katika hoteli ya watalii iliyosababisha vifo vya watu 38 wengi wao wazungu.
Maelfu ya watalii wanaondoka Tunisia baada ya shambulio katika hoteli ya watalii iliyosababisha vifo vya watu 38 wengi wao wazungu.
Makampuni ya utalii pia yanavunja safari za kwenda huko.
Katika uwanja wa ndege wa Hammamet, karibu na Tunis, watalii wamepanga foleni kusubiri kuondoka nchini humo.
Serikali ya Tunisia inasema kuwa ulinzi umezidishwa katika maeneo ya utalii huku wanajeshi wa akiba wakitakiwa kuripoti kazini mara moja.
null
Aidha serikali imetangaza kuwa itafunga misikiti 80, inayodaiwa kuwa inafundisha utumizi wa nguvu na Jihad.
Islamic State imesema imehusika na shambulio hilo.
Mshambuliaji aliyekuwa na bunduki, baadae alipigwa risasi na kuuawa.
null
Maelfu ya watalii wanatoroka Tunisia kufuatia shambulizi la kigaidi
Wakati huo huo inaaminika sasa kuwa 15 kati ya wale waliouawa huko Tunisia ni raia wa Uingereza.
Waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron, amesema shambulio hilo ni kumbusho la kikatili na kusitikisha, kwamba kuna tisho la ugaidi dunia nzima
"Nitahakikisha, tunafanya tuwezalo kusaidia, na kuwakinga watu na mashambulio ya kigaidi''.
null
''Tunawakumbuka na kuwaombea waliofiwa, na wale waliojeruhiwa''.
''Tunashirikiana na wakuu wa Tunisia, kujua idadi kamili ya Waingereza waliouliwa.''
Lakini wananchi wa Uingereza wanafaa kujitayarisha, kuwa wengi waliouwawa ni Wangereza."Alisema Cameroon.
Share:

Burundi:''Uchaguzi utafanyika Jumatatu''


Balozi wa Burundi katika umoja wa mataifa amekariri kuwa uchaguzi utaendelea mbele Jumatatu licha ya shinikizo uahirishwe
Balozi wa Burundi kwenye umoja wa mataifa amesema kuwa uchaguzi utaendelea jinsi ulivyopangwa siku ya jumatatu licha ya ombi kutaka uahirishwe kutoka kwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki moon.
Ban anasema kuwa ana wasiwasi kuhusu hali ya usalama nchini Burundi kufuatia mzozo wa kisiasa unaoendelea huko.
null
Balozi Albert Shingiro aliuambia mkutano wa usalama wa umoja wa mataifa kuwa watu wanataka uchaguzi ufanyike.
Balozi Albert Shingiro aliuambia mkutano wa usalama wa umoja wa mataifa kuwa watu wanataka uchaguzi ufanyike.
Vyama vya upinzani na mashirika yasiyokuwa ya serikali tayari yametangaza kuwa watasusia uchaguzi huo.
Waandamanaji wanapinga uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza wa kuwania urais kwa muhula wa tatu wakidai kuwa inakiuka katiba ya Nvhi hiyo.
null
Uchaguzi wa ubunge unatarajiwa kufanyika Jumatatu
Rais Nkurunziza naye anashikilia kuwa awamu ya kwanza aliteuliwa na wajumbe wala sio raia kama vile inavyohitajika kwenye katiba iliyoundwa baada ya makubaliano ya Arusha yaliyokomesha vita vya wenyewe kwa wenye nchini humo.
Takriban watu 50 wameuawa nchini Burundi tangu mwezi Aprili mwaka huu wakati rais Pierre Nkurunziza alipotangaza kuwa atawania muhula wa tatu.
null
Maelfu ya raia wengine wa Burundi nao wamehamia mataifa jirani kwa hofu ya kuzuka mamchafuko zaidi.
Uchaguzi wa ubunge unatarajiwa siku ya Jumatatu huku uchaguzi wa urais ukipangiwa kufanyika tarehe 15 Julai mwaka huu.
Share:

Ulaya yakataa kuiongeza Ugiriki muda zaidi.


Mawaziri wa fedha wa mataifa ya ulaya wamekatalia mbali ombi la Ugiriki la kutaka iongezewa muda zaidi wa kulipa deni lake kutoka Jumanne ijayo.
Ugiriki ina hadi Jumanne ijayo kulipa deni lake la zaidi ya dola bilioni moja nukta saba.
Serikali ya Uigiriki chini ya Alexis Tsipras ilikuwa imeombamuda wa majuma mawili iliiandae kura ya maoni
kuhusu makubaliano yaliyopendekezwa na wakopeshaji wa kimataifa wa nchi hiyo.
null
Waziri mkuu nchini Ugiriki Alexis Tsipras,anatarajiwa kuomba muda zaidi wa kulipa deni la IMF
Ikiwa itaidhinishwa kura hiyo itafanyika tarehe tano mwezi Julai.
Awali wagiriki walipiga foleni nje ya mabenki wakihofia kuwa watawekewa masharti dhidi ya kutoa pesa zao.
Mwandishi wa BBC mjini Athens anasema kuwa kulikuwa na uvumi kuwa kiwango kipya cha pesa ambacho mtu anaweza kutoa kwa benki kinaweza kuwa euro 80.
Bunge la Ugiriki nalo liliandaa kikao cha dharura kujadili pendekezo ya kufanyika kwa kura hiyo ya maoni.
Waziri mkuu nchini Ugiriki Alexis Tsipras, anasema kuwa masharti hayo yanayotaka kupunguzwa kwa matumizi ya umma hayawezi kustahimiliwa.
null
Watu nchini Ugiriki wameanza kupanga foleni nje ya mabenki wakihofia kuwa watawekewa masharti dhidi ya kutoa pesa zao
Baadaye atakutana na waziri wa fedha wa nchi za ulaya mjini Brussels kuomba kuongezwa muda zaidi wa kulipa kwa mkopo wa sasa wa Ugiriki.
Muda unazidi kuyoyoma kwa bwana Tsipras kuwa amelipa deni la dola mbilioni 1.7 kwa shirika la IMF ifikapo jumanne ijayo..
Share:

Monday 15 June 2015

Waislamu Uingereza watakiwa kufungua mapema


Kiongozi wa kidini anayehusishwa na wakfu wa kiislamu nchini Uingereza anasema kuwa waislamu nchini humo wanapaswa kupunguza muda wanaofunga kula na kunywa wakati wa ramadhan kwani muda wao unazidi saa 19.

Dakta Usama Hasan ambaye ni msomi katika shirika moja linalowashughulikia waislamu Quilliam anasema japo mafundisho ya dini yanamtaka muumini wa dini hiyo kufunga kula na kunywa kuanzia asubuhi hadi jua linapotua waislamu nchini Uingereza hulazimika kufunga kwa zaidi ya saa 19.

Wito wake hata hivyo unapingwa na baadhi ya waislamu ambao wanasema kuwa ni sharti maadili na mafundisho ya dini yaheshimiwe.

Waislamu wanahitajika kususia kula kuanzia alfajiri hadi jua linapotua
Ratiba ya kufunga wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadan inatarajiwa kutolewa wakati wowote tayari kwa waislmu kutekeleza nguzo hiyo muhimu ya dini hiyo.
Share:

Msafara wa baiskeli Tanzania


Mamia ya waendesha baiskeli walijitokeza kwenye msafara katika barabara za mji wa Dar es Salaam kwa lengo la kuhamasisha wananchi kutumia zaidi usafiri huo kwa ajili ya afya bora huku wakiitaka serikali kupinga uonevu unaofanywa na waendesha magari ambao husababisha ajali za barabarani.
Huu ni mwaka wa tisa sasa msafara huu umekuwa ukifanyika jijini Dar es salaam
Mbali ya kuwa ni tukio la burudani baina ya marafiki na familia, msafara huu una ujumbe maalumu
"msafara huu ni wito kwa serikali na wadau wa miundombinu kutenga sehemu mahususi ya kupitisha baiskeli"

Dar es Salaam ina watumia barabara zaidi ya laki tatu .
Mwenyekiti wa muungano wa vyama vya waendesha baiskeli mjini Dar es salaam UWABA Mejah Mbuya ,anasema idadi ya watumia baiskeli wanaofariki kutokana na ajali za barabarani ni asilimia 6 vifo vyote vitokanavyo na ajali barabarani.
''Anasema kuwa siku hii ni kubwa kutokana na kutokuwepo kwa waoneaji wa magari, lakini anatamani hali hii ingekuwa ni ya kila siku''
Hata hivyo, waandaaji wamesema tayari mabadiliko yanaonekana ndani ya miaka mitano iliyopita.

Shughuli hii inalenga kuondoa dhana kwamba ni chombo cha usafiri kwa watu maskini.
Anasema kuwa ''serikali imekuwa pamoja nao katika mipango yao ya miundombinu mijini kwa sababu ya misafara hii, na kuwa punguzo la vifo vya waendesha baiskeli''.
Shughuli hii inalenga kuondoa dhana kwamba ni chombo cha usafiri kwa watu maskini.
Na ukiangalia watu wanaotumia baiskeli siku hizi , unaona mambo yameanza kubadilika.
Utaona watu wenye uwezo wa kati na wale wa juu nao wameanza kuutumia.
Share:

Kasisi basha aishtaki kanisa kumbagua


Kasisi mmoja ambaye alinyimwa leseni ya kufanya kazi kama mhudumu katika zahanati ya afya kwa misingi ya kuwa katika ndoa ya jinsia moja ameishtaki kanisa kwa kumbagua.
Kasisi Jeremy Pemberton alikuwa amewasilisha pendekezo la kutaka kuhudumu kama Kasisi katika kanisa lililoko ndani ya hospitali.
Aidha kasisi Pemberton anadai kuwa maombi yake yalipingwa kwa kinywa kipana na kaimu askofu wa Southwell na Nottingham nchini Uingereza.
Rt Revd Richard Inwood alimkashifu kasisi Pemberton kuwa katika ndoa na mwanaume mwenza ambaye ni kinyume na mafundisho ya kanisa la Church of England.
Tume inayosimamia utoaji kazi nchini Uingereza inatazamia kuanza kuisikiza kesi hiyo leo.
Wadau wa maswala ya ajira wanasema kesi hiyo inatumiwa kama funzo na mtihani kwa tume hiyo ya ajira ya uingereza iwapo itazingatia haki za wafanyikazi ama zile za mwajiri.
Kasisi Pemberton alikuwa mhudumu wa kwanza kanisani kuoa nchini Uingereza.
Pemberton alifunga pingu za maisha mnamo mwezi wa Aprili mwaka wa 2014.
Askofu Inwood, alimnyima kazi kasisi Pemberton, na kisha akaiandikia barua bodi inayosimamia hospitali hiyo ya Sherwood Forest akiwashauri wasimpe kazi kasisi Pemberton.
Share:

Mwanajeshi wa Korea Kaskazini atorokea Kusini


Jeshi nchini Korea Kusini linasema kuwa mwanajeshi wa Korea Kaskazini ametoroka nchi hiyo na kuingia nchini Korea Kusini akipitia mpaka wa mkoa wa Gangwo

Mpaka wenye ulinzi mkali wa mkoa wa Gangwo
Kuhama kwa wanajeshi kupitia mpaka huo ulio chini ya ulinzi mkali si jambo la kawaida.
Korea Kusini ilichukua hatua za kuboresha ulinzi kwenye mpaka kufuatia tukio la mwaka 2012 wakati mwanajeshi mwingine kutoka Korea Kaskazini alivuka mpaka usiku wa manane na kuingia nchini Korea Kusini.
Share:

Amama Mbabazi atampinga rais Museveni


Waziri mkuu wa zamani wa Uganda Amama Mbabazi atampinga rais Yoweri Museveni kuwania tikiti ya urais wa chama cha NRM.
Bwana Amama Mbabazi anataka kuwania kiti cha urais dhidi ya mwandani wake wa zamani katika uchaguzi utakaokuwa mwakani.
Kupitia kwa taarifa aliyoichapisha kwenye mtandao wa Youtube, bwana Mbabazi aliahidi
''kufufua na kuleta muamko mpya nchini Uganda.''
Rais Museveni ametawala Uganda tangu mwaka wa 1986 na anatarajiwa kuwania urais kwa muhula wake wa nne.

Museveni alimfuta kazi bwana Mbabazi mwaka uliopita katika hatua iliyotafsiriwa na wachanganuzi wa kisiasa nchini humo kuwa mbinu ya kukandamiza mpinzani wake mkuu.
Bwana Mbabazi anakabiliwa na changamoto kubwa ya kushinda uteuzi katika chama tawala cha National Resistance Movement (NRM).
Rais Museveni tayari ameidhinishwa na kamati kuu ya chama japo anahitaji kupokea ithibati ya wanachama katika mkutano mkuu wa wajumbe.
Iwapo atakonga nyoyo za wajumbe wa NRM sasa Mbabazi sasa atawania urais dhifi ya Museveni
Mwandishi wa BBC Rachael Akidi anasema kuwa hii ndiyo itakayokuwa mtihani mkubwa zaidi kuwahi kumkabili rais Museveni ndani ya chama cha NRM.
Share:

Al Shabaab 1 raia wa UK auawa Kenya


Utafiti wa DNA unatarajiwa kuthibitisha kuwa mmoja wa wapiganaji 11 wa Al shabaab waliouawa na wanajeshi wa Kenya hapo jana alikuwa ni raia wa Uingereza.
Duru za kijasusi za jeshi la Kenya zinasema kuwa mmoja kati ya watu wawili wazungu waliouawa anafahamika kama Thomas Evans, 25, ambaye ni raia wa Uingereza na anayetokea Buckinghamshire.
Bwana Evans, alisilimu na kubadili jina lake na kuitwa Abdul Hakim.
Familia yake imeiambia BBC kuwa inasubiri hakikisho kutoka kwa serikali ya Uingereza kuwa ndiye aliyeuawa.
Shambulizi hilo lilitokea jana alfajiri katika kambi ndogo ya kijeshi iliyoko Baure karibu na Lamu ambapo wanajeshi sasa wamethibitisha kuwa waliwauawa watu 11 na kupata bunduki 13 na mizinga mingine tano.

Maafisa wa utawala nchini uingereza wanashirikiana na utawala nchini Kenya kubaini haswa ni nani aliyeuawa.
Kwa mujibu wa polisi katika bonde la Thames nchini Uingereza , mamake Thomas bi Sally Evans amenukuliwa akisema kuwa ''yeye na mwanaye Michael wanasubiri thibitisho kutoka kwa duru za polisi''
Awali Familia yake ilikuwa imeilaumu idara ya uhamiaji ya Uingereza kwa kumruhusu kuondoka nchini humo.
Evans alisafiri kuelekea Misri mwaka wa 2011 punde baada ya kunyimwa ruhusa ya kuenda Kenya.

Mnamo mwaka wa 2012 Evans inafahamika alimuarifu mamake kuwa amesafiri hadi Somalia kujiunga na wapiganaji wa kundi la Al Shabaab.
Takriban raia 50 wa Uingereza wanaaminika kuwa wamejiunga na al-Shabaab nchini Somalia.
Kundi hilo ndilo linalolaumiwa kwa kutekeleza mashambulizi kadha nchini Kenya na pia Somalia.
Iwapo mwili huo utathibitishwa kuwa wa Evans basi itakuwa ndio mara ya kwanza kwa raia wa Uingereza kuuawa cnhini kenya akipigania kundi la wanamgambo wa Al Shabaab.
Share:

Bashir amewasili mjini Khartoum Sudan..


Rais Omar al Bashir wa Sudan amewasili mjini Khartoum Sudan kutoka nchini Afrika Kusini.
Rais Bashir amekariri kuwa hana hatia yeyote wala hajui kwanini mahakama ya kimatiafa ya ICC inasisitiza kumchafulia jina.
Shirika la habari ya AFP limemnukuu rais Bashir akifoka ''Allah Akbar'' aliposhuka kutoka kwa ndege iliyombeba.
Aidha aliinua mkongojo wake juu na kushabikiwa na wafuasi wake.
Waziri wa maswala ya kigeni wa Sudan Ibrahim Ghandour aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali ya Afrika Kusini ilikuwa imemkariria rais Bashir kuwa kuwepo kwake mjini johannesburg ilikuwa ni tukio la kushabikiwa na lenye heshima kubwa kwa hivyo hakukuwa na uwezekano wowowte wake kukamatwa.

Rais Huyo alikuwa ameratibiwa kuhutubia umma lakini kinasa sauti kikaharibika na akaondoka.
Rais bashir aliingia katika gari lake lililowazi na akaondoka uwanjani huku akishabikiwa na wafuasi wake.
Awali kuondoka kwake nchini Afrika Kusini kulikumbwa na atiati, baada ya mahakama moja kuamuru rais huyo asiondoke nchini humo hadi mahakama hiyo itakaposikiza kesi na kuamua iwapo atakamatwa na apelekwe mjini the Hague Uholanzi au la.
Awali Mwandishi wa BBC aliyeko Afrika Kusini Nomsa Maseko, alisema kuwa ndege ya rais al Bashir ilijazwa mafuta jana usiku na kuwekwa mstari wa mbele tayari kabisa kuondoka katika uwanja wa ndege wa kijeshi.

Rais Bashir aliondoka licha ya kuwepo amri ya mahakama ya kumzuia kuondoka nchini humo hadi kesi dhidi yake itakaposikizwa na kuamuliwa.
Mahakama hiyo ilikuwa inapaswa kuamua ikiwa Bwana al-Bashir atakabidhiwa mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai ICC yenye makao yake mjini Hague Uholanzi ilikukabiliana na mashtaka ya uhalifu wa kivita na mauaji yahalaiki yanayomkabili .
Majaji watatu waliokuwa wanasikiza kesi hiyo dhidi yake wamemtaka waziri wa usalama wa ndani nchini humo kueleza ni vipi rais Bashir aliruhusiwa kukaidi amri ya mahakama .
Share:

Friday 12 June 2015

WHO:Ebola yaongezeka Guinea na S Leone..


Shirika la afya duniani WHO limeelezea wasiwasi wake kwamba visa vipya vya maambukizi ya maradhi hatari ya Ebola vimeongezeka huko Guinea na Sierra Leone katika kipindi cha wiki tatu zilizopita.
WHO liliripoti kesi 31 mpya katika mataifa hayo mawili.
Uchunguzi unaonyesha kuwa tamaduni za mazishi ndizo zinachangia kusambaa kwa kasi kwa maradhi hayo licha ya tahadhari na mafunzo kupewa raia wa nchi kwamba waripoti visa vyovyote vinavyoshukiwa kuwa vya maambukizo ya Ebola na kuachia maafisa wa matibabu shughuli za mazishi ili yafanyike kwa utaratibu uliofuatwa.
Share:

Nigeria na mikakati dhidi ya Boko Haram...


Serikali ya Nigeria na nchi nyengine nne majirani zimekubaliana kuunda vikosi vya jeshi la pamoja ili kupambana na wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram.
Kikosi hicho kitapiga kambi katika mji mkuu wa Chad, Ndjamena, lakini kitakuwa chini ya usimamizi wa Nigeria.Nchi ya Chad, Cameroon, Niger na Benin pia zitatoa wanajeshi wake.
Baada ya mkutano huo uliofanyika katika mji mkuu wa Nigeria Abuja, katibu mkuu wa wizara ya ulinzi ya Nigeria, Aliyu Ismail, amesema kikosi hicho kitakuwa tayari kuanza kazi ifikapo mwezi July mwaka huu:"viongozi wa nchi na serikali za nchi za ukanda wa ziwa Chad na Benin zimechukua uamuzi ufuatao.
kupitisha dhana ya ufanyaji kazi, mikakati ya ufanyaji kazi na nyaraka zinazohusiana na kuundwa kwa vikosi vya pamoja katika kupambana na kundi la kigaidi la wapiganaji wa Boko Haram, kupitisha kupelekwa kwa vikosi hivyo katika makao makuu ya Ndjamena, Chad, kwa utekelezaji wa rasilimali watu na mahitaji ya kifedha.
Share:

Gari linalohisi mashimo barabarani..


Watafiti wa gari aina ya Landrover Jaguar wametengeza gari ambalo linaweza kuhisi mashimo yalio barabarani wakati linapoendeshwa.Sensa zilizopo katika gari hilo hubaini mashimo hayo na hutuma ujumbe wa data hiyo kwa haraka kwa madereva na mamlaka ya eneo hilo.
Share:

Mtoto azaliwa kutokana na mayai yaliohifadhiwa..


Mwanamke mmoja nchini Ubelgiji amekuwa wa kwanza duniani kujifungua mtoto kwa kutumia upandikizaji wa mayai ya mwanamke yaliowekwa katika jokovu alipokuwa mtoto.
Msichana huyo wa miaka 27 alikuwa na mayai yaliotolewa akiwa na umri wa miaka 13 kabla ya kuanza kupewa matibabu ya anemia ya seli.
Mayai yake yaliosalia yalifeli kutokana na matibabu hayo hatua ambayo ingeathiri uwezo wake wa kushika mimba bila upandikizaji huo.
Wataalam wanatumai kwamba mpango huo huenda ukawasaidia wagonjwa wengine wadogo.
Mwanamke huyo alijifungua mvulana mwenye afya nzuri mwezi Novemba mwaka 2014 na maelezo kuhusu swala hilo yalichapishwa siku ya jumatano katika jarida la kizazi cha binaadamu.
Mwanamke huyo ambaye hakutaka kujulikana alipatikana na ugonjwa wa anemia ya seli alipokuwa na umri wa miaka mitano.

Alihamia kutoka jamhuri ya Congo na kuelekea Ubelgiji ambapo madaktari waliamua ugonjwa wake ulikuwa hatari kwa yeye kufanyiwa upandikizaji wa uboho kwa kutumia tishu za kakaake zinazofanana na zake.
Lakini kabla ya kuanza upandikizaji huo walitakiwa kutumia kemikali ili kutibu mgonjwa huyo kwa lengo la kudhoofisha kinga yake ili kuzuia kutokataa tishu hiyo.
Matibabu ya kutumia kemikali yanaweza kuharibu kazi ya mayai hayo,kwa hivyo walitoa mayai yake ya upande wa kulia na kuyaweka katika jokovu.
Wakati huo,alikuwa akionyesha ishara za kubalekhe ,lakini alikuwa hajaanza kupata hedhi.Mayai yake yaliosali yalifeli akiwa na umri wa miaka 15.
Miaka kumi baadaye ,aliamua kwamba angetaka kupata mtoto,hivyobasi madaktari wakapandikiza mayai yake katika mayai yaliokuwa yamesalia na mayai mengine 11 katika sehemu zake nyingine mwilini.

Mgonjwa huo alianza kupata hedhi baada ya miezi mitano na kushika mimba akiwa na umri wa miaka 27.
Mkunga aliyeongoza tiba hiyo ya kumwezesha mgonjwa huyo kuweza kushika mimba Daktari Isabelle Demeestere alisema kuwa kuna matumaini kwamba mpango huo unaweza kuwasaidia vijana wengine ambao wanakabiliwa na hatari ya kufeli kwa mayai yao ya uzazi,hasa kutokana na ongezeko la idadi ya waathiriwa wa muda mrefu wa magonjwa ya damu wakiwa watoto.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.