Friday 5 December 2014

Volkswagen kuikabili Mercedes F1......

 Kampuni ya Volkswagen ya pili kwa utengenezaji magari duniani, inafanya upembuzi yakinifu kuhusu kuingiza magari yake katika michezo ya Formula 1.
Vyanzo vya habari vinasema uchambuzi huo unafanywa na mkuu wa zamani wa timu ya Ferrari Stefano Domenicali, ambaye alikodishwa na kampuni ya magari ya Audi ya VW mapema mwaka huu.
Hamu yake imechochewa na mafanikio ya kampuni pinzani ya Mercedes, ambayo ni mabingwa wapya wa mbio za magari ya langa langa ya Formula 1
Lakini uamuzi wa kujiunga na F1 kutategemea mabadiliko ya uongozi katika kampuni ya VW au F1.
Ferdinand Piech, mkuu wa bodi ya usimamizi wa makampuni ya VW, na mkuu wa matngazo wa F1 Bernie Ecclestone wamekuwa katika uhusiano mbaya kwa muda mrefu.
Angalau mmoja wao atatakiwa kuondoka katika vyeo vyao vya sasa kabla ya kampuni ya VW kuingia katika F1.
Share:

Aishi na maiti akitarajia itafufuka......


Familia moja nchini Canada iliishi na maiti katika chumba cha juu cha nyumba yao kwa miezi sita kwa kuwa waliamini marehemu atafufuka iwapo wataendelea kumuomba mungu,lakini mwili huo ukapatikana baada ya familia hiyo kushindwa kulipa mkopo waliochukua kununua nyumba hiyo.
Kaling Wald mwenye umri wa miaka 50 alipatikana na makosa ya kushindwa kuwaarifu maafisa wa polisi kwamba mumewe alifariki ,kosa ambalo na akahukumiwa kuwekwa katika muda wa majaribio na ushauri,wakili wake alikiambia chombo cha habari cha Reuter siku ya Jumanne.
Peter Wald mwenye umri wa miaka 52 alifariki mnamo mwezi machi mwaka 2013 kwa kile mamlaka inasema ni sababu za kawaida kufuatia maambukizi ya mguu wake yanayodaiwa kusababishwa na ugonjwa wa sukari.
Mkewe Kaling Wald alimwacha kitandani na kufunga chumba hicho katika nyumba yao ya Hamilton ,Ontario ili kuzuia harufu kali iliokuwa ikitoka chumbani humo kuwafikia watu waliokuwa wakiishi nyumbani humo.
Kama vile Yesu alivyomfufua Lazaro baada ya siku ya nne ,pia yeye aliamini kwamba Mungu atamfufua mumewe wakili wa mwanamke huyo alisema.
Share:

Wataka Sokwe apewe haki za kibinadamu..........

 Sokwe hawana haki sawa na binadamu na wala sio lazima wanyama hao kuachiwa huru na wale wanaowafuga. Hii ni kwa mujibu wa uamuzi wa mahakama nchini Marekani.
Uamuzi huu ulitolewa katika kesi kumhusu Sokwe kwa jina Tommy ambaye wanahakatari wa kutetea wanyama walitaka aachiliwe huru na mmiliki wake na pia atunzwe kama binadamu.
Jaji katika mahakama ya rufaa mjini New York aliyeisikiliza kesi hio, amesema Sokwe wanaokuwa wamefugwa hawawezi kutunzwa sawa na binadamu kwani hawawezi kuwajibishwa kama anavyoweza binadamu.
Shirika moja la kutetea haki za wanyama lilikuwa limedai kuwa Sokwe walio na usawa fulani na binadamu wanapaswa kuwa na haki sawa na na binadamu ikiwemo kupewa uhuru.
Shirika hilo limesema litakata rufaa katika kesi hiyo.
Katika uamuzi wake , jaji aliandika: '' Sokwe hawawezi kuwa na haki sawa na binadamu kwani hawawezi kuwajibishwa wala kupewa majukumu.''
Mahakama hio iliongeza kuwa hakuna sheria inayoshurutisha kwamba wanyama hao wapewe haki sawa na binadamu.
Mnamo mwezi Okotoba, shirika hilo la kutetea haki za wanyama, lilikuwa limetetea kwamba, Sokwe wanapaswa kutambuliwa kama binadamu katika sheria, na kisha kupewa haki sawa na uhuru kama binadamu.
Shirika hilo limesema litakata rufaa dhidi ya hukumu hio katika mahakama ya juu zaidi nchini humo.
Share:

ICC yatupilia mbali kesi ya Kenyatta......


Mahakama ya kimataifa ya ICC imetupilia mbali kesi ya jinai inayomkabili Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Mwendesha mkuu wa mashitaka Fatou Bensouda ameondoa kesi dhidi ya Kenyatta ambaye alidaiwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007/2008.
Mahakama ilikuwa imempa Bensouda wiki moja kuamua ikiwa ataendelea na kesi dhidi ya Kenyatta au la inagwa alisema muda huo haukutosha kwake yeye kuandaa ushahidi zaidi dhidi ya Kenyatta.
Kenyatta alishtakiwa kama mshukiwa mkuu wa ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007/2008 akituhimiwa pamoja na William Ruto ambaye ni naibu Rais kwa kutenda uhalifu dhidi ya binadamu.
Zaidi ya watu elfu moja waliuawa wakati wa ghasia hizo. Uhuru alikuwa mtu maarufu zaidi kufikishwa mahakamani na pia mshukiwa mkuu kwani alifikishw amahakamani akiwa Rais aliye mamlakani.
Hili ni pigo kubwa kwa upande wa mashitaka, wengi wlaioana keshi dhidi ya Kenyatta kama mtihani mkubwa katika historia ya mahakama hio.
Upande wa mashitaka ulitaka mahakama kuupatia muda zaidi ili upate ushahidi zaidi,dhidi ya Kenyatta kama vile taarifa za akaunti yake ya benki.
Upande wa utetezi uliteta kuwa ikiwa hakuna ushahidi wa kutosha kesi hio inapaswa kutupiliwa mbali.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.