Wednesday 28 January 2015

Gumzo:Michelle hakujitanda kichwa Saudia.


Mkewe Rais wa Marekani Barack Obama, Michelle Obama alipowasili nchini Saudi Arabia na mumewe bila ya kujitanda kichwa chake kwa kitambaa, wengi walitarajia kwamba mitandao ya kijamii nchini humo ingewaka moto kwa mingon'ono.
Lakini mambo yalikuwa tofauti maana kimya kilikuwa kikuu.
Ingawa vyombo kadhaa vya habari Ulaya, viliripoti kuhusu utata mkubwa kutokea kwenye mitandao ya kijamii, alama ya njia ya reli kwenye mtandao wa Twitter kwa lugha ya kiarabu...ikimaanisha ....''Michelle Obama bila mtandio''...ujumbe huo ilisambazwa kwenye mtandao huo zaidi ya mara 2,5000.
Hii sio idadi kubwa ya watu waliousambaza ujumbe huo lakini pia sio ndogo sana katika nchi yenye watumiaji wengi wa Twitter.
Pia inaarifiwa ujumbe huo ulizidiwa nguvu na ujumbe mwingine uliotumbwa kwenye Twitter dhidi ya ziara ya Rais Obama nkatika ufalme huo.
''Mfalme Salman amwacha Obama na kwenda kuomba,'' huu ndio ulikuwa ujumbe mwingine uliosambazwa sana kwenye Twitter kuhusu ziara ya Obama nchini humo.
Ujumbe huo: "Mfalme Salman amwacha Obama na kwenda kuomba,'' uliwavutia zaidi ya watu 170,000.

Wananchi katika ufalma huo walisambaza ujumbe huo kama njia yao ya kuonyesha wlaivyofurahishwa na mfalme mpya, Salman kumwacha Obama na kwenda kusali,kama ilivyoonekana kwenye video iliyowekwa kwenye Youtube.
''Huyu ndiye mwanamume aliyemwacha kiongozi wa nchi muhimu zaidi duniani akimsubiri wakati akienda kusali'', aliandika mtu mmoja kwenye mtandao wa Twitter.
Kitengo cha BBC cha Monitoring, ambacho kilikuwa kinafuatilia gumzo kwenye mitandao ya kijamii kuhusu ziara ya Obama nchini Saudia kilisema wengi walikuwa wanafanya tu utani kuhusu ufalme wa Ufalme wa Saudia ambao una sheria kali kuhusu mambo mengi tu.
Baadhi walikuwa wanatumiana picha ya Michelle akiwa amevalia kitambaa kichwani wakati wa ziara yake nchini Malaysia mwaka 2010 wakati wengine wakitoa wito kwa ufalme huo kuwaoa haki zaidi watu wake.
Ni watu wachache sana walionyesha kukerwa na hatua ya Michelle kutovalia kitambaa kichwani kama heshima tu kwa ufalme huo huku wengi kwenye Twitter wakikosoa ufalme huo kwa kile wanachosema ni kuwanyima uhuru wananchi.

Share:

'Ajioa' baada ya kukosa mchumba.


Yasmin Eleby hakupata mchumba wa kumuoa mtu ambaye alitaka awe mume wake atakapofikisha miaka 40--kwa hivyo akafanya kitendo ambacho kimewashangaza wengi, aliamua kujioa mwenyewe.
Kwa mujibu wa mtandao wa MySanAntonio.com,Eleby aliahidi kwamba ikiwa hatapata mchumba wakati atakapokuwa ametimiza miaka 40, basi atafanya harusi ya mtu mmoja yaani atajioa ili kusherehekea miaka yake 40.
Duru zinasema kuwa mwanamke Eleby alifanya harusi yake mwenyewe katika makavazi ya Houston akiambatana na jamaa na familia yake na wageni wengine waalikwa.
Kwa sherehe hii, dadake Eleby ndiye aliendesha sherehe hio, kwani ni kinyume na sheria kwa mtu kujioa mwenyewe. Harusi ya kawaida ni kati ya watu wawili.
Katika picha za kanisani sherehe ilionekana kuwa ya kawaida bila ya mchumba.
Kulingana na John Guess Jr afisaa mkuu wa makavazi hayo, sherehe hiyo ilionekana kuwa bila tashwishi na kuonekana kama jambo la kawaida kwani makavazi hayo huwakumbatia watu wa jinsia mbali mbali kuendesha harusi zao hapo.
Aliposikia kwamba Eleby, ambaye anaishi na kufanya kazi ugenini alikuwa anapanga kujioa mwenyewe, aliharakisha kwenda katika eneo hilo kujionea mwenyewe.
"Eleby alipofikisha umri wa miaka 40 bila ya kupata mpenzi na mtu mwenye nia ya kumuoa, aliamua angejioa mwenyewe,''alisema Guess Jr ambaye anasema harusi hiyo imewashangaza wengi na kuwa gumzo katika mitandao ya kijamii.
Anasema anakubaliana na Eleby na mtazamo wake wa mapenzi kwamba mtu anaweza kujipenda na kujioa kwa kukosa wa kumuoa kwani cha muhimu ni mtu kujipenda kwanza kabla ya kupendwa.
"watu wengu huolewa bila ya kutafakari mara mbili kuhusu yule anayemuoa, '' Guess Jr alisema.
Anadhani kwamba pindi watu watakapomuona Eleby anavyojishughulikia mwenyewe, huenda akapata ushindani.
"ni mrembo, anafanya kazi kwa bidii na anasifika duniani na pia anaona uamuzi wake umewapa gumzo watu wengi. ''
Share:

Msikiti mkubwa Afrika wajengwa Algeria.


Msikiti utakaoshindana na maeneo mengine ya Kiislam ya kuabudia makubwa kuliko yote duniani unajengwa katika pwani ya kaskazini mwa Algeria.
Nini malengo ya kujenga msikiti mkubwa kama huu?
Nusu ya eneo katika ghuba ya Algiers, jengo kubwa taratibu limeanza kuibuka kutoka ardhini.
Katika sehemu moja kitakuwa chumba cha kuabudia cha Msikiti Mkuu wa Algiers. Katika sehemu nyingine kutakuwa na mnara mrefu kuliko yote duniani, ukiwa na urefu wa mita 265 kwenda juu.
Kutakuwa na shule ya korani, maktaba na jumba la makumbusho, na maeneo na bustani zenye miti ya matunda mbalimbali.

Wageni watawasili katika magari, matreni na hata maboti. Jengo hilo, litakalokuwa na uwezo wa kuchukua watu 120,000 people, litaunganishwa na bandari katika bahari ya Mediterani katika njia mbili za mandhari ya kutembea.
Msikiti huu utakuwa wa tatu kwa ukubwa wa eneo duniani, kwa mujibu wa wataalam wa majengo na kuwa msikiti mkubwa kuliko yote barani Afrika.
"Ni moja ya miradi ya karne," amesema Ouarda Youcef Khodja, afisa mwandamizi katika wizara ya nyumba na mipango miji, wakati alipotembelea eneo hilo la ujenzi.
Bi Ouarda amesema Rais Abdelaziz Bouteflika alitaka msikiti huo kuwa"Mnara wa Uislam na kwa mashujaa wa mapinduzi ya Algeria" - vita vya kupigania uhuru kutoka Ufaransa.
Lakini pia unaamanisha kuwa ishara kwa siku za baadaye. "Mnara huu utakuwa kitu cha kurejelea katika mapinduzi ya sasa-mapinduzi ya maendeleo ya Algeria."
Kama ilivyo kwa miradi mingine mikubwa, inayofadhiliwa kutokana fedha inayotokana na mafuta, ujenzi wa msikiti huu unategemea wataalam na wafanyakazi kutoka nje. Umebuniwa michoro na wataalam wa majengo wa Ujerumani na unajengwa na kampuni ya ujenzi ya China iitwayo China State Construction Engineering Corporation, ambayo ina mamia ya wafanyakazi wanaoishi katika eneo la ujenzi.

Na kama ilivyo kwa miradi mingine, mradi huu umechelewa kutekelezwa. Wizara ya nyumba na mipango miji hivi karibuni ilichukua jukumu la kusimamia ujenzi wa msikiti huo kutoka wizara ya masuala ya dini. "Mungu akipenda", anasema Bi Youcef Khodja, kwa sasa utakamilika mwishoni mwa mwaka 2016, japo hata hiyo tarehe, ujenzi utakuwa umechelewa kwa zaidi ya mwaka mmoja kutoka muda uliokuwa umepangwa.
Vipimo vya msikiti huo, na eneo lake na gharama yake inakadiriwa kuwa dola za Kimarekani bilioni 1-1.5, ikionyesha kuwa ni kipaumbele cha serikali.
Sababu moja ya kutekelezwa kwa mradi huu ni uungwaji mkono na Bwana Bouteflika ambao utakuwa ukumbusho wa urais wake nchini Algeria.
Sababu nyingine inaweza kuonekana kwa ushindani wa mara kwa mara na majirani zake, Morocco. Msikiti wa Algiers utaupita kidogo msikiti wa Hassan wa Pili ulioko Casablanca kwa ukubwa wa eneo na kwa urefu wa mnara.
Lakini msukumo mkubwa huenda ukawa jaribio la serikali kujenga utambulisho wa taifa kidini na kutangaza Uislam kwa kuweka udhibiti juu ya misikiti na maimam wanaosalisha humo.
Jitihada hiyo iliyoanza pamoja na harakati za uhuru mwaka 1962 na kupata dharura na mgogoro wa kiraia na wapinzani wa Kiislam katika miaka ya 1990, wakati huo serikali ilipoteza udhibiti wa baadhi ya misikiti kwa wahubiri waliochochea upinzani dhidi ya utawala wa serikali.

Ni kwa mantiki hiyo Algeria inajenga msikiti mkubwa wa kisasa, kitu ambacho kilikuwa kinakosekana mpaka sasa - anasema Kamel Chachoua, mtaalam wa Algeria wa masuala ya dini katika Taasisi ya Utafiti na Elimu katika Ulimwengu wa Kiarabu na Kiislam mjini Marseille.
Uamuzi wa kujenga msikiti huu ulikuwa "ukimaanisha kuwadhibiti wapiganaji wa Kiislam. Ni wazo la kuunda Uislam wa kitaifa baada ya kitisho cha miaka ya 1990 na kuundolea Uislam taswira mbaya na kuufanya kuwa karibu zaidi na serikali na kupambana na misimamo mikali ya kidini."
Msikiti huu una maana ya kuwa ishara muhimu katika sehemu ya Algiers ambayo imeshuhudia vitendo vingi vya misimamo mikali ya kidini katika miaka ya 1990, amesema.
"ni njia ya kuficha misikiti midogo na kuidunisha. Ni namna ya kusema: 'Tunapenda Uislam, lakini Uislama wa kisasa'. "Unaweza kujenga miskiti midogo 1,000 lakini haionekani - haionyeshi kuwa serikali iko katika mchakato wa kuonyesha udhibiti wake juu ya Uislam na kwamba inajivunia Uislam."
Wazo la kuhamasisha utaifa wa dini ya Kiislam ambayo inaondokana na itikadi zenye misimamo mikali kutoka nchi za Ghuba au kwingineko linaonekana katika jitihada za serikali za kutangaza na kushirikisha Sufi zawaya, au sheria za kidini. Pia inajidhihirisha katika utaalam wa ujenzi wa msikiti mpya wa Afrika Kaskazini, wenye mnara mmoja wa muundo wa pembe nne.

Mnara utakwenda juu ya eneo la Mohammedia, na juu ya mabaki ya ukoloni uliopita nchini Algeria. Moja kwa moja nyuma ya eneo la ujenzi ni jengo kubwa lililotumika kukaliwa na wachungaji wa kimisionari kutoka Ufaransa waliojulikana kama "peres blancs, au white fathers". Chini kidogo ya barabara ni eneo la kiwanda cha zamani cha mvinyo.
Msikiti huo umebuniwa kuwa ishara ya utambulisho wa Algeria mpya, lakini utambulisho huo bado unapiganiwa.
Baadhi ya wakosoaji wanauona msikiti huo kuwa zaidi kuwa ishara ya maelewano baada ya mgogoro na wanasiasa waislam kuliko kuwa njia ya kupambana na wasilam wenye misimamo mikali.
"Kipaumbele ni kusema: 'Angalia tulivyo nchi ya Kiislam," anasema Amira Bouraoui, mfuasi wa vuguvugu la upinzani la Barakat. "Ni njia nyingine ya kuwanyamazisha wapinzani wa Kiislam na kuwapaka mafuta kwa mgongo wa chupa."
Bi Bouraoui hivi karibuni alitishiwa katika mtadao wa kijamii wa Facebook baada ya kuuliza kama sauti ya vipaza sauti ingeweza kupunguzwa. Wananch iwa Algeria wasiofungamana na dini wanaona hili kama mfululizo wa mifano ya kufuatilia uislam na kukosekana kwa uvumilivu wa kidini.
Hata hivyo kwa kawaida, iwapo Wa-Algeria wanaonekana kuwa watazamaji zaidi, hiyo ni hali ya juu juu, anasema Nacer Djabi, mwana sociolojia katika chuo kikuu cha Algiers. "katika kiwango cha kijamii si fikirii kama wanadini hasa, anasema Djabi.
"Ni watu wasiotaka mabadiliko sana, mabadiliko wanayoonyesha ni ya juu juu. Unaweza kuona hilo katika mitaa ya Algiers - kuna wasichana wengi wenye hijab, lakini hizo haziwazuii kuwa na wapenzi wa kiume, kunywa bia.
"Wa- Algeria wengi, wafanyabiashara, wanakwenda Mecca, wanaswali mara tano kwa siku", anasema."Lakini hali halibadili tabia yao kama wananachi kama Waislam."
Kwa upande wao wakazi wa Mohammedia wanaonekana kutofurahishwa na ujenzi wa msikiti mkubwa katika maeneo yao, wakisema fedha hiyo ingetumika katika mambo mengine.
"Unatakiwa kuanza na elimu na afya, na baadaye unaweza kufikiria kuenzi dini," anasema Racim, mwanafunzi mwenye umri wa miaka 22.
"Katika mtazamo wa Kiislam, mahali pa kuswalia si muhimu sana - ni kile kilichoko moyoni."

Share:

Hezbollah lashambulia jeshi la Israel.


Kundi la wapiganaji wa Washia wa Lebanon walio chini ya vugu vugu la Hezbollah, linasema kuwa limetekeleza shambulio dhidi ya msafara wa wanajeshi wa Israeli katika mpaka wa mataifa hayo mawili.
Kwa upande wake, Jeshi la Israeli linasema wanajeshi wake wanne wamejeruhiwa pale kombora lililorushwa kwa kifaru kupiga gari lake la kijeshi karibu na mpaka wa Lebanon.
Taarifa nyingine kutoka kwa Hezbollah zinasema kuwa zaidi ya waisraeli 15 yamkini wameuwawa au kujeruhiwa.
Kundi la Hezbollah linasema kuwa lilikuwa likijibu mashambulio ya angani yaliyofanywa na Israeli yaliyomuua jenerali mmoja wa Iran na wapiganaji kadhaa wa Hezbollah Nchini Syria siku kumi zilizopita.
Israel ilijibu mashambulizi hayo kwa kurusha makombora Kusini mwa Lebanon
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu alionya kwamba jeshi la Israel liko tayari kutumia nguvu dhidi ya mashambulizi yoyote kutoka kwa washambuliaji.
Share:

Amnesty yakosoa jeshi la Nigeria.


Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu, Amnesty International, limelishutumu jeshi la Nigeria kwa kushindwa kuwalinda raia katika mji wa Baga uliopo kaskazini mashariki mwa Nigeria, licha ya kuwepo onyo kwamba wanamgambo wa Boko Haram wangelitekeleza shambulio.
Linanukuu duru ambayo haikutajwa jina aliyesema kwamba wanamgambo hao waliwaambia wakaazi miezi miwili awali kwamba walikuwa wanapanga shambulio.
Amnesty International linasema waanjeshi walitazama tu jinsi vikosi vya Boko Haram vilivyokuwa vikiongezeka. Inakadiriwa kwamba kati ya watu 150 hadi 2000 waliuawa katika shambulio hilo lililotokea mapema mwezi huu.
Shirika hilo linadai kwamba limeelezea wasiwasi wake mara kadhaa awali kwamba vikosi vya usalama haviwajibiki vya kutosha kuwalinda raia dhidi ya unyanyasaji na ukiukaji wa haki za binaadamu unaotekelezwa na Boko Haram.
Tangu mwaka 2009, Boko Haram limekuwa likiwalenga raia na kufanya uvamizi, kuwateka raia na mashambulio ya mabomu, huku mashambulio yao yakiongezeka kwa idadi na ukubwa. Malefu ya watu wameuawa katika mashambulio hayo, mamia kutekwa na maelfu wengine wameachwa bila makaazi baada ya kulazimika kutoweka mapigano.
Share:

Profesa Lipumba afikishwa mahakamani.


Kikao cha Bunge la Tanzania leo kimevurugika kutokana na vurugu za baadhi ya wabunge waliokuwa wakibishana kuhusu suala la kiongozi wa chama cha upinzani cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kushambuliwa na polisi Jumanne kwa madai kuwa alihusika katika maandamano kinyume cha sheria.
Hoja iliamshwa na mbunge ambaye pia ni kiongozi wa upinzani aliyetaka suala hilo lijadiliwe kwa dharura. Hayo yametokea huku Profesa Lipumba akifikishwa mahakamani kusomewa mashtaka ya jinai.
Chanzo ni pale aliposimama James Mbatia mbunge wa kuteuliwa kutaka suala la polisi kumshambulia na kumdhalilisha Profesa Ibrahim Lipumba, kiongozi wa chama cha CUF lijadiliwe kwa dharura bungeni humo.
Licha ya jitahada za Spika Makinda kueleza kuwa suala hilo litajadiliwa kesho, kwa kuwa serikali inahitaji muda wa kuwasilisha majibu, mambo yakavurugika.
Huku wabunge wakiwa wamesimama wima wakishinikiza hoja hiyo ijadiliwe, Spika Makinda aliendelea na msimamo wake wa kutaka hoja ijadiliwe Alhamisi baada ya serikali kuwasilisha majibu, hapo ndipo mkorogano ulipozidi na kuleta kutoelewana kati ya wabunge wa upinzani na Spika.
Spika Makinda alilazimika kuahirisha kikao hicho mpaka jioni baada ya hali kuwa ngumu, na hata jioni likaahirishwa tena mpaka kesho, Alhamisi.
Kiongozi huyo wa upinzani inadaiwa alifika eneo ambako maandamano yaliyopangwa kufanyika Jumanne yalikuwa yamepigwa marufuku, ingawa uongozi wa chama cha CUF unadai Profesa Lipumba alikusudia kuwashawishi wafuasi wake watawanyike kutii amri ya polisi ndipo akashambuliwa.
Wakati huo huo Profesa Lipumba amefikishwa mahakamani mjini Dar Es Salaam ambako amesomewa mashtaka ya kufanya maandamano bila kuwa na kibali.
Hata hivyo kwa muda Profesa Lipumba alikimbizwa hospitalini baada ya afya yake kudhoofika, ikidaiwa ni sababu ya kupigwa na polisi, madai ambayo BBC haijaweza kuyathibitisha.
Hata hivyo alirejeshwa mahakamani baada ya kupata nafuu, na kesi yake imeahirishwa na itatajwa tena mahakamani tarehe 26 Februari 2015.
Ameachiwa kwa dhamana ya watu wawili kwa kiasi cha shilingi milioni mbili kila mmoja.
Share:

Monday 26 January 2015

ANGALIA BIBI WA MIAKA 90 ANASOMA DARASA LA NNE.


Gogo akiwa darasani na wanafunzi wenziwe.

Akiwa na umri wa miaka 90 mwanamke wa Kenya ambaye anahudhuria masomo akiwa na wajukuu zake wapatao sita inaaminika ndiye mwanafunzi mzee zaidi anayesoma shule ya msingi duniani.
Akiwa ameketi dawati la mbele kabisa darasani ,yuko darasa la tano na amevalia nguo za shule , Priscilla Gogo Sitienei anamsikiliza mwalimu anayefundisha kwa makini hukua akiandika majina ya wanyama kwa kiingereza kwenye daftari lake.
Prissilla alijiunga na shule hii ya Leaders Vision Preparatory School miaka mitano iliyopita lakini pia aliwahi kuwahudumia wakaazi wa kijiji chake cha Ndalat kilichoko kwenye bonde la ufa kama mkunga miaka sitini na mitano iliyopita.
Darasani Priscilla anawasaidia wengine wafanye vyema ambao wana umri kati ya miaka 10 hadi 14 na mar azote huwaambia ujumbe wake hasa mabinti kuwa elimu ndiyo urithi wao.
Priscilla anajulikana kama Gogo maana yake bibi katika lugha ya jamii ya wakalenjini,anasefurahia masomo akiwa na umri wa miaka 90 katika umri huo anajua kuandika na kusoma pia fursa aliyoikosa alipokuwa mdogo.
Lugha ambayo Priscilla anajiona yuko huru kuitumia ni lugha mama kwake ki Kalenjin kuliko kiingereza,pindi anapotakiwa kujieleza kwanini aliamua kujiunga na shule katika umri wake.
Sababu kubwa ambayo amekuwa akiitoa,ni ajue kusoma ili amudu kusoma bibilia,lakini pia kwa umri wake anataka awahamasishe watoto kupata elimu,kwani anawaona watoto wengi wakiwa hawako shuleni na watoto hao wana watoto.
Gogo apitapo mitaani haoni shida kukabiliana na watoto ambao hawako shuleni katika muda wa masomo na kuwauliza kwanini hawako shuleni.
Gogo anasema watoto hao humjibu kwamba hawaendi shule kwakuwa umri wao ni mkubwa,name huwaambia mimi ni mkubwa sana kwenu lakini niko shuleni hivyo nanyi jiungeni na shule.
Kikubwa kinachomuumiza Gogo ni kuwaona watoto wengi waliopoteza muelekeo,wengi wao hawana baba na wanazurura hovyo mitaani,bila msaada wowote.kutokana na hali hiyo nataka kuwahamsisha waende shuleni.
Share:

Kwa nini waafrika wanajibadilisha rangi?.



Katika mfululizo wa Barua kutoka kwa Waandishi wa habari wa Afrika, Mwandishi na Mtunzi wa Riwaya,Tricia Nwaubani anaangazia mada ya kung'arisha Ngozi.
Kwa kipindi cha miaka michache iliyopita, nilijenga tabia ya kuwauliza waafrika wenzangu kutoka nchi tofauti tofauti wanafikiria bara letu lingekuwaje kama wafanya biashara ya utumwa na Wakoloni wasingeingia Afrika.
Baadhi wanaona kuwa jamii za kiafrika zingekuwa na maendeleo, ikienda sambamba na maendeleo ya dunia.
Wengine wanaona kuwa Afrika ilikuwa na maendeleo sawa na maendeleo ya dunia nzima, lakini utumwa na ukoloni viliingilia kati na kukwamisha maendeleo.
Wengine wanaamini kuwa sisi waafrika tungeuana kwa mapigano ya kikabila na migogoro, bara lingekuwa na makundi machache ya kikabila yaliyo mbali mbali.
Ninapenda kufikiria kuwa sisi waafrika tungeweza kujisimamia kwa mambo mengi.Tungegundua umeme ,tungetengeneza viyoyozi na majokofu, tungejiuliza ni vitu gani vinaonekana kwenye bahari, kisha tukkatuma wanaume kwa wanawake kufanya uchunguzi.

Ingeweza kuchukua miongo mingi, hata karne, lakini jamii za kiafrika zingeweza kupata hadhi ya kuwa moja ya bara la ulimwengu wa kwanza.
Pia nafikiri kuwa, kwa kiasi fulani ,mwafrika alipaswa kufikiria''Nywele zangu zimejinyonga nyonga na zimependeza.lakini swali ni je zingekuwaje kama zingenyooshwa.
''ingekuwaje kama nywele zangu zingekuwa za bluua au nyeusi kama za gold?''
Mwafrika wa namna hii angetengeneza dawa za nywele na rangi ya nywele, ingawa haonekani na nywele ndefu.
Kusingekuwa na kasumba ya kutaka kufanana na Watu weupe.

Waafrika wangeweza kuangalia uwezekano wa kubadili rangi za ngozi.
''baadhi yetu rangi zetu za ngozi ni nyeusi na nzuri,wengine ngozi ni angavu nao pia ni wazuri.je itakuwaje mwenye rangi nyeusi akataka awe mweupe na mweupe kuwa mweusi?''
'weusi ung'aao'
Wanawake wengi wa Nigeria ninaowafahamu wanaotumia vipodozi vya kung'arisha ngozi si kwamba ngozi zao za asili ni weusi.
Na kuna wanawake wenye ngozi nyeupe lakini wanataka kuongezea zaidi ya rangi waliyonayo.
Kumekuwa na kasumba kuwa kuwa na ngozi nyeupe kumeonekana kuwa kwa kipekee zaidi kwenye jamii ya watu wengi walio na ngozi nyeusi.
Share:

Alikaidi wazazi lakini sasa anajuta.


Je unakumbuka kisa cha wapenzi wawili waliozua gumzo nchini Kenya?
Msichana mhindi Sarika Patel kutoka familia tajiri na Timothy Khamala mbukusu kutoka familia maskini kutoka Magharibi mwa Kenya kuoana? wakati yao mapenzi yao yalijulikana kama Bukusu Darling, sifa kwa wanakoishi wawili hao.
Taarifa sasa ni kwamba mapenzi yao yamefika kikomo. Familia ya msichana Sarika ililaani sana mapenzi hayo kwani Timothy alikuwa anafanya kazi kwao kama mfanyakazi wa nyumbani.
Na Sarika alipoamua kwenda kuishi na Timothy kama mume na mke familia yake ilimfukuza na kisha kumfuta kazi Timothy.
Wawili hao walioana kinyume na matakwa ya familia ya Sarika ambayo kwao ilikuwa ni kama aibu kubwa sana kwa mtoto wao kutoka familia tajiri kuolea na kijana asiyekuwa na mbele wala nyuma.
Wakati taarifa ya wawili hao ilipogonga vichwa vya habari nchini Kenya, Sarika na mume wake walipata kazi katika kiwanda cha kutengeza Sukari kutoka kwa wahisani.
Lakini sasa kuna madai kwamba ndoa yao imevunjika baada ya Sarika kulalamika kwamba Timothy amekuwa akimdhulumu na kumtusi kila mara hali iliyosababisha wawili hao kutalakiana.
Mtandao wa Standard Digital umemnukuu Sarika akisema: "nilipokuwa mgonjwa , hakuwa hata na muda wa kunipeleka hospitalini badala yake wazazi wake ndio walionipeleka kutafuta matibabu. Mbali na hayo amekuwa akinichapa, '' alisema Sarika huku akibubujikwa na machozi.
Kwa sasa inaarifiwa anajuta sana kwa nini alikaidi amri ya wazazi wake.
''Ninajuta sana kwa nini sikuwasikiliza wazazi wangu na kuolewa kinyume na mapenzi yao. Ninaomba radhi, natumai watanikubali kurejea nyumbani. ''
Sarika ambaye ni mtoto wa nne katika familia ya watoto watano, ameamua kurejea nyumbani na kusema kamwe hatawahi kuwa na uhusiano wa kimepenzi tena. Lakini wazazi wake wamempa masharti, mwanzo aishi na rafiki yake huku akifanya uamuzi wa mwisho kuhusu anakotaka kuishi.
Anasema anahofia kwamba jamii ya wahindi haitamkubali tena kwani hakuwasikiliza wakati walipomshauri kutoolewa na mwanamume mwafrika.
Share:

Unywele wa Lincoln wauzwa dola 25,000.


Vitu vya kumbukumbu vya aliyekuwa rais wa 16 wa Marekani Abraham Lincoln vimeuzwa katika mnada mjini Dallas nchini Marekani na kupata dola 800,000.
Msokoto mmoja wa nywele za rais huyo aliyeuawa umeuzwa kwa dola 25,000 lakini barua iliokiri kwamba vita vya wenyewe kwa wenyewe havikuwa vizuri haikuuzwa.
Barua iliotiwa sahihi na naibu wake John Wlkes Booth iliuzwa kwa dola 30,000 huku agizo lake la kijeshi likitia kibindoni dola 21,250.





















Vitu vya Lincoln vilipigwa mnada mjini Dallas marekani.

ukusanyaji wa vitu hivyo 300 ulianzishwa mwaka 1963 na mmiliki wa jumba la sanaa Donald Dow aliyefariki miaka mitano iliopita.
Mwanawe Greg amesema kuwa ni wakati wakusanyaji wengine wapate fursa ya kuifurahia.
Amesema kuwa babaake alikuwa ameanza ukusanyaji huo kutokana na maslahi yake katika vita vya wenyewe kwa wenyewe pamoja na historia ya kijeshi,lakini baadaye alikuwa na hamu na Lincoln na mauaji yake.
Share:

Asilimia moja ya watu m.atajiri duniani

Aliko Dangote tajiri mkubwa barani Afrika.

Huku wafanyibiashara na wanasiasa wa ngazi za juu wakikutana katika mkutano wa kiuchumi duniani mjini Davos wiki hii ,hisia tofauti zimetolewa kuhusiana na kuwepo kwa ukosefu wa usawa duniani bila kuisahau asilimia moja ya watu Matajiri duniani.
Matajiri hao wanaishi katika visiwa vya kibinafsi,lakini je, hao ndio matajiri wanaojulikana Pekee?.
Ripoti moja ya shirika la wahisani la Oxfam iliotolewa sanjari na mkutano huo wa Davos,ilizua hisia kali baada ya kubashiri kwamba asilimia moja ya matajiri duniani huenda ikamiliki idadi yote ya watu duniani.
Ilitoa utafiti wake kutoka kwa benki ya Credit nchini Uswizi ambayo inakadiria jumla ya utajiri katika kila nyumba kuwa dola trillioni 263.
Huo ni itajiri na wala si mapato.
Watu matajiri kama vile Bill gates ,Warren Buffet na Mark Zuckerberg ni miongoni mwa asilimia 1.
Bill Gates na Warren Buffet.
Lakini je, ni nani mwengine aliyeorodheshwa katika asilimia hiyo?.
Kulingana na ripoti hiyo ya benki ya Credit watu wengine millioni 47 wana utajiri wa dola 798,000 kila mmoja.
Hiyo inashirikisha watu wengi katika mataifa tajiri ambao pengine wasingejitambulisha kama matajiri,lakini ambao wanamiliki nyumba ama wamelipa kiwango kikubwa cha mkopo.
Miongoni mwao ni:
Watu millioini 18 wanatoka Marekani
Millioni 4 inatoka Japan
Watu millioni 3.5 wanatoka Ufaransa
Watu millioni 2.9 wanatoka Uingereza
Millioni 2.8 wanatoka Ujerumani
Millioni 4 inatoka Japan
Na millioni 1.6 inatoka China
Share:

Tumesambaratisha IS,.Wakurdi

Serikali ya Kurdi imesema tayari imekwisha sambaratisha kikundi cha wapiganaji wa Islamic State katika mapigano yaliyodumu kwa takriban miezi minne.
Wapiganaji wa kundi la Islamic State walikuwa wakishikilia eneo la Kaskazini mwa Syria Kobane.
Wakrud katika eneo la jubilant wameanza kusherehekea kutokana na ushindi huo wa kuwaondoa wapiganaji wa IS.
Hata hivyo kumekuwa na maoni wapiganaji wa Kikurdi bado hawana udhibiti wa eneo la Mashariki. Wachambuzi wanasema kuwa kama mji wa Kobane umechukuliwa na majeshi ya Kurdi basi hiyo ni hatua mhimu katika kudhoofisha nguvu ya Islamic state.

Share:

Kasisi wa kwanza mwanamke aapishwa UK.

Kanisa moja nchini Uingereza hii leo limemuapisha mwanamke wa kwanza kuwa kasisi.
Mchungaji Libby Lane kama anavyojulikana sasa atakuwa kasisi wa Stockport katika sherehe iliofanyika katika eneo la York Minster,ikiwa ni miezi sita tu baada ya kanisa hilo kumpigia kura ili kumaliza utamaduni wake wa wanaume kuwa makasisi.
Kasisi huyo amesema kuwa iwapo uchaguzi wake utawafanya wanawake kubaini uwezo wao basi anafurahia.
Hatua hiyo imeendelea kuzua hisia tofauti miongoni mwa wafuasi wa kanisa hilo la kianglikana duniani.

Share:

Ongwen afikishwa katika mahakama ya ICC.

Kiongozi mmoja wa kundi la waasi nchini Uganda, Dominic Ongwen, amekuwa mwanachama wa kwanza wa kundi la Lord's Resistance Army LRA, kufika mbele ya mahakama ya kimataifa ya ICC.
Wakati wa kusikizwa kwa kesi yake huko The Hague, Bwana Ongwen alithibitisha kuwa ndiye, huku akijieleza kuwa ni mwanajeshi wa zamani wa LRA.


Anakabiliwa na makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu na makosa mengine ya kivita, ikiwemo mauwaji na utumwa.
Awali mwezi huu alikuwa amezuiliwa nchini Afrika ya kati, miaka kumi tangu ICC ilipotoa ilani ya kumkamata.

Share:

Saturday 17 January 2015

Huduma ya kuokoa watumishi wa Umma Kenya..

Serikali ya Kenya imeanzisha mpango kabambe wa kutoa huduma za kuokoa kwa kutumia ndege na magari kwa watumishi wa umma nchini humo. Huduma hiyo imezinduliwa kwa ushirikiano na shirika la bima ya afya,shirika la msalaba mwekundu na kundi lamadaktari wanaosafiri kwa ndege la AMREF. Kenya inakuwa nchi ya pili baada ya Afrika Kusini kutoa huduma ya aina hii. Victor Kenani alkuwepo kwenye uzinduzi wa mpango huo ambapo Rais Uhuru Kenyatta alihudhuria.




Share:

Bondia Muhammad Ali anaendelea vizuri..


Hali ya afya ya gwiji wa zamani wa ndondi Duniani Muhammad Ali inaendelea vizuri
Bondia huyo alirudishwa hospital kwa tatizo la maradhi ya maambukizi ya njia ya mkojo.
Msemaji wa familia Bob Gunnell alisema "Ali yuko imara na anatarajiwa kutolewa leo,kulikua na uchunguzi zaidi juu ya maambukizi yake.
Ali mwenye miaka 72 kabla alitolewa hospitali mapema mwezi huu baada ya kupatiwa mabaibatu kwa wiki mbili kwa maradhi yanayomsumbua.
Bondia huyo aliwahi kuwa bigwa wa dunia kwa uzito wa juu alistaafu mchezo huo mwaka 1981.
Share:

Marekani yalaani ICC kuhusu Israel.


Marekani imelaani hatua ya mahakama ya kimaitaifa ya uhalifu wa kivita ICC kuanzisha uchunguzi kuhusu uwezekano wa kuwepo kwa uhalifu wa kivita kwenye utawala wa Palestina.
Msemaji wa wizara ya ndani nchini Marekani anasema kuwa ni jambo lisiloaminika kuwa Israeli ambayo imekuwa ikishambuliwa kwa makombora yanayofyatuliwa katika ardhi yake kuwa sasa ndiyo inayochunguzwa na ICC.
Mapema Isreal iliitaja hatua hiyo kama yenye lengo la kuizuia isijilinde kutokana na vitendo vya kigaidi.
Uchunguzi huo ambao ICC inasema utakuwa huru utatumiwa kuamua iwapo kutafanyika uchunguzi ulio kamili.
Share:

Dubai inaongoza kwa uaminifu..


Dubai imejinyakulia sifa ya kipekee katika kupima Imani za jamii kwa pochi iliyoangushwa mtaani,na ikarejeshwa kwa mhusika mara moja.
Katika utafiti uliofanywa na mtengeneza Filamu mwenye asili ya Uingereza katika mitaa ya Dubai, alijaribu mara arobaini na tano kuidondosha kwa makusudi na katika kila tukio msamaria aliyeiokota aliirejesha pochi hiyo kwa mmiliki wake.
Daniel Jarvis, mwenye miaka 26,akiwa ameificha kamera yake na kurekodi mfululizo wa matukio hayo ya makusudi akiwa pamoja na rafikiye aliyejipachika jina la utani la 'Digi' ama Dan, mwenye miaka 25, walibarizi katika viunga vya Downtown na Bur vilivyoko Dubai,siku za karibuni na kuweka swali je unaweza kuiba Dubai? Kutaka kuichunguza jamii na kurushwa vipande vyake katika YouTube ambapo mpaka kufikia jana usiku watazamaji walikuwa ni zaidi ya 70,000 .
Jarvis aliiambia 7DAYS walishangazwa na utafiti huo na kikubwa kilichowasangaza ni kwamba waliookota pochi hiyo hawakujishughulisha kutazama ndani kuna nini? Wakati pochi hiyo ilikuwa imesheni euro za kutosha na fedha ya Falme za Kiarab dirham kadhaa.
Mtaa wa kwanza walioufanyia majaribio ni mtaa uliko katika barabra ya Sheikh Zayed karibu na soko kuu la kibiashara na jirani kabisa na mnara wa Emirates lakini kila aliyeiona pochi hiyo aliirejesha,lakini baadaye tukafikiri sababu ya kurejeshwa pochi hiyo kuwa walioko eneo hilo ni matajiri.
Basi utafiti wetu tukauhamishia eneo la Bur ,Dubai, mahali ambapo palionekana duni kidogo cha ajabu watu waliendeleza utamaduni ule ule wa kurejesha pochi kama ilivyo, na hali eliendelea hivyo mara kadhaa.
Jarvis anasema wameshafanya utafiti kama huo katika mji wa London nchini Uingereza. Na huko walistaajabu walipoidondosha tu aliyeiokota alianza kukimbia nayo wa nako hakuna aliyethubutu kuichukua pochi hiyo.
Jarvis, alivalia suti nadhifu na kuigiza kudondosha pochi anaonekana kwenye video hiyo anaeleza hisia za kurejeshewa kitu ulichondondosha kuwa ni raha iliyoje .lakini akaendelea kusema kuwa anadhani vyombo vya habari hupotosha ukweli,kwakuwa kulikuwa na kichwa cha habari kuwa kuna mtu alihukumiwa miaka 15 jela kwa kuiba mdoli wenye taswira ya dubu, utafiti wetu umegundua tofauti na wayasemayo.
Trollstation ina wanachama wapatao 230,000 na utafiti wao kutoka Falme za Kiarab unaelekezwa Ulaya, Marekani na hatimaye Afrika .
Inawezekana katika maeneo watakayopita kuvunja rekodi ya Dubai tusubiri wakati uwadie, ni kauli yake Jarvis .
Share:

Mavazi ya mhubiri yawaacha vinywa wazi..


Mhubiri mmoja nchini Iran amewaacha watu vinywa wazi kwa kuvalia vazi la rangi ya manjano.
Hoseyn Khademian alionekana kwenye televisheni akivalia shati la manjano , viatu na hata saa ya rangi hiohio. Taarifa hii ni kwa mujibu wa shirika la habari la Mehr.
Wahubiri nchini Iran, kwa kawaida huvalia mavazi meupe na joho la rangi isiyong'aa sana huku viatu vyao vikiwa vyeusi au vya hudhurungi.
Lakini mavazi ya Khademian yalikejeliwa na kufanyiwa gumzo sana kwenye mitandao ya kijamii.
Wakati baadhi ya watu kwenye Facebook walimzomea wakisema anajitakia tu sifa, wengine walimfananisha na ndizi lilioivaa kupitiliza. ''
Msomaji mwengine alisema, '' angependeza zaidi ikiwa angevalia kilemba cha waridi,basi angependeza sana''.
Wakati mwonekano wake umegonga vichwa vya habari nchini Iran, bwana Khademian anasema yeye haoni kwa nini watu wanamsema sana kwani sio mara yake ya kwanza kuvalia mavazi ya manjano.
Mara ya mwisho alionekana kwenye TV akiwa amevalia mavazi ya waridi, anahoji ''kwa nini watu hawakunisema sana wakati huo,''ikilinganishwa na sasa rangi ya mavazi yangi sio kitu kipya,'' alisema Bwana Khademian. Rangi ya manjano ni rangi ya kawaida kama rangi nyinginezo''.
Share:

Viatu vinavyojifunga kamba vyenyewe...


Ni miaka 26 tangu tuone viatu vikijifunga kamba zenyewe kama ilivyokuwa kwenye matangazo ya biashara ya viatu vya Nike vyake Marty McFly vikijifunga miaka hio. hio
Hilo lilikuwa tu tangazo la bishara zamani sana lakini kuna mtu ambaye aliwaza hivyo miaka hiyo na kusema atakuja kuzindua viatu vyenye uwezo wa kujifunga kamba. Na kwake ndoto hio imetimia.
Wahandisi nchini Ujerumani wamebuni viatu ambavyo vina uwezo wa kujifunga kamba.
Walifanikiwa kufanya hivyo kwa kuweka 'cherger'mfano kama ile ya simu kwenye viatu hivyo ambavyo vinatumia kawi kujionea wenyewe itakavyokuwa kwenye miguu tofauti.
Pindi unapovaa kiatu hicho, sensa ya kiatu inakiambia kwamba mguu uko sawasawa na kuchochea kawi kwenye kiatu kile kuamrisha kamba kujifunga zenyewe.
Wakati unataka kuvua viatu utahitajika kubonyeza au kugonga wayo wa kiatu kile mara mbili na vile vile kuna miale inayoamrisha kamba za viatu vile kujifungua kwa kuzilegeza kamba.
Wanasema kiatu hicho hakihitaji kuwekwa kwenye charger au kubadilisha betri kwa sababu kawi inatokana na hatua za kuukanyaga mguu chini kwa mvaaji au anapotembea zile hatua ndizo zinakipatia kiatu nguvu au kawi.
Mmoja wa wahandisi waliokitengeza kiatu hicho, anasema kwamba kiatu hicho kitawasaidia watu wengi.
Miongoni mwa watakaofaidi ni watu wanaokumbwa na ulemavu wa miguu au wenye matatizo ya kutembea lakini pia vinaweza kuwasaidia watoto au kwa wanaotaka tu kubadili mfumo wao wa maisha.
Saa moja ya kutumia viatu hivyo inatosha kuweza kurejesha kawi ya kufunga kamba.
Bwana Ylli na kikundi cha wahandiisi wengine wanashughulikia kifaa kingine ambacho kitawezesha viatu kumuonyesha mvaaji mwelekeo anakokwenda.
Share:

Boko Haram ishughulikiwe kimataifa.


Rais wa Ghana, John Mahama, ameiambia BBC kwamba msaada wa kimataifa unahitajika kuweza kulishinda kundi la wapiganaji Waislamu, Boko Haram, nchini Nigeria.
Rais Mahama alisema nchi moja pekee haiwezi kuwashinda wapiganaji hao na kwamba ugaidi kila pahala ni tishio la dunia nzima.
Rais wa Ghana alisema viongozi wa nchi za Afrika Magharibi watakutana juma lijalo kuomba idhini ya Umoja wa Afrika kuunda kikosi cha kimataifa ili kupambana na Boko Haram, lakini aliongeza kusema kuwa kutuma kikosi hicho kunaweza kuchukua miezi.
Wanajeshi wa Chad wameanza kujongea Cameroon, kama sehemu ya ushirikiano zaidi wa kanda hiyo dhidi ya Boko Haram.
Share:

Charlie Hebdo:Makanisa yachomwa Niger

Ripoti kutoka Niger zinasema kuwa makanisa matatu yamechomwa katika mji mkuu wa Niamey katika siku ya pili ya maandamano dhidi ya uchapishaji wa vibonzo vya mtume Mohammed uliofanywa na gazeti la vibonzo la Charlie Hebdo.
Baadhi ya biashara zimeripotiwa kushambuliwa kama vile vibanda vya kampuni ya simu ya Orange.
Ubalozi wa Ufaransa umewataka raia wake wanaoishi mjini Niamey kusalia majumbani mwao

Polisi wa kukabiliana na ghasia kwa sasa wameweka ulinzi mkali katika kanisa la Cathedral mjini humo ambapo makundi ya vijana wanaowarushia mawe.
Siku ya ijumaa watu wanne walifariki huku wengine 45 wakijeruhiwa baada ya waandamanaji kuyapekua makanisa matatu kabla ya kuyachoma mbali na kukichoma kituo kimoja kilicho na utamaduni wa Ufaransa huko Zinder.
Share:

Friday 2 January 2015

BAADA YA KUKAA KIMYA HATIMAYE YULE ASKOFU ALIYEKULA PESA ZA ESCROW AELEZA ALIVYOPEWA MGAO HUO.


Askofu Nzigilwa.












Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa, amevunja ukimya kuhusu mgao wa Sh. milioni 40 alioupata kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya VIP Engineering & Marketing Limited, James Rugemalira.

Ukimya wa Askofu Nzigilwa unatokana na sakata la uchotwaji wa zaidi ya Sh. bilioni 300 kutoka akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Akaunti hiyo ilifunguliwa baada ya waliokuwa wanahisa wa Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ikiwamo VIP kuingia katika mgogoro na Shirika la Umeme nchini (Tanesco).

Taarifa kwa vyombo vya habari jana ilisema fedha alizopewa Askofu Nzigilwa na Rugemalira, zilikuwa za matoleo kwa ajili ya maendeleo ya Kanisa.

Alisema kiutaratibu siyo vibaya kwa waumini kutoa michango na matoleo kwa Kanisa na watumishi wake.

Katika taarifa hiyo ambayo Askofu Nzingilwa alipotafutwa alithibitisha kwamba ni yake, alifafanua kuwa alifahamiana na familia ya Rugemalira tangu akiwa Paroko Msaidizi wa Parokia ya Makongo Juu, Dar es Salaam na hata baada ya kuteuliwa kuwa Askofu Msaidizi wameendelea kushirikiana na kuwasiliana katika masuala mbalimbali ya kikanisa na kijamii.

“Samahani nipo kwenye kazi fulani hatuwezi kuongea kwa sasa.

 Ni kweli kuna taarifa nimeitoa leo kwa Tumaini Media na nimewaambia waitume pia kwa vyombo vingine vya habari,” alisema Askofu Nzingilwa alipowasiliana na NIPASHE kwa kutumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms).

Askofu Nzingilwa katika taarifa hiyo aliyoisaini juzi, alisema mwanzoni mwa Februari 2014, Rugemalira alimuomba namba ya akaunti yake ya benki ya Mkombozi ili aweke matoleo yake.

Alisema aliombwa akaunti yake na Rugemalira mapema Februari, mwaka jana na kwamba hakuwahi kufahamu kiasi cha fedha kilichowekwa kwenye akaunti yake hadi alipoangalia taarifa ya benki Februari 27, mwaka jana iliyoonyesha aliingiziwa Sh. milioni 40.4.

“Niliwasiliana na Rugemalira na kumwambia nimeona kiasi kikubwa cha fedha katika akaunti yangu, naye akaniambia hayo ni matoleo yake ambayo anaamini yatasaidia katika shughuli zetu za kitume na kichungaji. Nikamshukuru kwa ukarimu huo mkubwa,” alibainisha Askofu huyo.

Alisema matoleo hayo yalipokelewa kwa moyo mnyofu kutoka kwa mtu anayefahamika kwa ukarimu wake katika kusaidia Kanisa na watumishi wake.

“Kampuni anazomiliki na biashara anazofanya Rugemalira kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, haviwezi kumpa shaka mtu anayemfahamu kuhusu uwezo wake au kampuni yake kutoa mchango mkubwa kama huo,” alisema.

Alisema ni desturi ya kawaida katika Kanisa kwa waamini kutoa michango na matoleo mbalimbali kila mmoja kwa kadri ya uwezo na ukarimu wa moyo wake na kwamba matoleo ya waamini hutumika katika shughuli za uinjilishaji na uendeshaji wa Jimbo, Parokia na taaisi zake.

Askofu huyo aliongeza kuwa hutumika katika miradi maalum iliyokusudiwa na matoleo hayo na kwa kadri ya matakwa na lengo la mtoaji.

“Nilipokea matoleo hayo kwa roho safi na moyo mweupe na wa shukrani kama tunavyofanya siku zote tunapopokea ukarimu wa michango na matoleo ya waamini wetu. Na tangu matoleo hayo yalipotolewa Februari, mwaka jana, hakuna mamlaka yoyote iliyowahi kuniuliza ,” alifafanua na kuongeza:

“Nawaomba waamini tuendelee kujitoa kwa hali na mali katika kulijenga Kanisa la Mungu; kila aliyepewa talanta na Mungu aitumie kwa kuzalisha matunda mema ili kulijenga kanisa letu na hatimaye kuurithi ufalme wa mbinguni.”

Hata hivyo, alisema Kanisa hilo litaendelea kuwa mstari wa mbele katika kutetea haki, ukweli na uadilifu, na halitarudi nyuma wala kukaa kimya katika kukemea maovu katika jamii.

UHUSIANO NA FAMILIA YA RUGEMALIRA
Alisema familia ya Rugemalira ni waumini wakatoliki wanaosali katika Parokia ya Bikira Maria Malkia wa Rozari Takatifu, Makongo juu katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam na kwamba ni washiriki wazuri katika shughuli za ibada na wamekuwa na moyo mkubwa wa ukarimu katika kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo ya Kanisa ndani na nje ya jimbo.

“Binafsi, nimeifahamu familia hii muda mrefu kutokana na majitoleo yao katika shughuli za Kanisa na uhusiano baina yangu na familia hiyo ulizidi kuimarika pale alipopangwa kufanya huduma za kichungaji katika Parokia ya Makongo Juu nikiwa Paroko Msaidizi, mwaka 2008,” alibainisha na kuongeza:

“Kipindi hicho ilikuwa katika harakati za ukamilishaji wa ujenzi wa nyumba ya mapadre na mikakati ya ujenzi wa Kanisa jipya la Parokia na walikuwa wachangiaji wazuri katika kufanikisha.”
Hata hivyo, aliwaomba waumini wa kanisa hilo kuendelea kujitoa kwa hali na mali katika kulijenga Kanisa la Mungu.

Aidha, Askofu huyo alisema utume wa kanisa siku zote umekuwa ukiwezeshwa na kutegemezwa kwa nguvu ya Mungu Roho Mtakatifu anayeliongoza kanisa katika ukweli wote, na kwa sadaka, matoleo na michango mbalimbali ya hali na mali kutoka kwa waamini na watu wengine wenye mapenzi mema waliopo ndani na nje ya nchi.

“Kwa waumini kutoa michango na matoleo kwa kanisa na watumishi wake ni jambo la kawaida katika desturi za imani yetu tangu nyakati za mitume,” alisema Askofu Nzigilwa.

KASHFA YA ESCROW
Mei, mwaka jana, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, aliibua kashfa ya kuchotwa kwa zaidi ya Sh bilioni 306 katika akaunti ya Tegeta Escrow, ambayo ilipingwa vikali na baadhi ya wabunge na viongozi wa serikali na Mbunge huyo kutakiwa kufuta kauli kwa kulidanganya Bunge.

Mbunge huyo aliendelea na msimamo wake na kutaka Bunge kuunda kamati ya kuchunguza sakata hilo.Juni mwaka jana, Bunge liliagiza Ofisi ya CAG kufanya ukaguzi wa fedha hizo na ripoti yake kuwasilishwa Bungeni.

Baada ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kukamilisha kazi yake, ripoti hiyo ilikabidhiwa kwa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), chini ya uenyekiti wa Zitto Kabwe.
 
Kamati hiyo ilifanya uchunguzi na kuweka wazi ripoti na mapendekezo yake ya awali ambayo yalizua mjadala mkali bungeni kiasi cha kutishia Bunge kushindwa kufikia maamuzi ya pamoja na baadaye Spika Anne Makinda, aliunda kamati ya maridhiano ambayo ilikubaliana katika maazimio yaliyowasilishwa Bungeni na Zitto.

Novemba 26, mwaka jana, Zitto, aliwasilisha ripoti iliyowataja viongozi wa dini, serikali na watu wengine waliopokea fedha za Tegeta Escow.

Viongozi wa dini waliotajwa na Zitto kiasi cha fedha walichopokea kwenye mabano ni Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini (Sh. milioni 80)  Askofu Eusebius Nzigirwa na Padri Alphonce Twimanye Simon (Sh. milioni 40.4), ambao walipewa fedha hizo kupitia Benki ya Mkombozi.

VIONGOZI WA SERIKALI WALIOWAJIBIKA
Desemba 16, mwaka jana, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema, alijiuzulu nafasi kutokana na ushauri alioutoa.

Desemba 22, mwaka jana, Rais Jakaya Kikwete, alimfukuza kazi Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ambaye katika kashfa hiyo alipokea kiasi cha Sh. bilioni 1.6, huku akimuweka kiporo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Desemba 23, mwaka jana, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alimsimamisha kazi Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi, ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake.

VIONGOZI WENGINE WALIOPATA MGAWO
Viongozi waliopata mgawo wa Rugemalira Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (bilion 1.6); Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (milioni 40.4); Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Daniel Yona (milioni 40.4); Mbunge mstaafu Paul Kimiti (milioni 40.4); Msajili wa zamani wa Hazina na Mjumbe wa Bodi ya Tanesco, Dk. Enos Bukuku (milioni 161.7).

Wamo pia Jaji Profesa Eudes John Ruhangisa (milioni 404.25) na Jaji Aloysius Mujulizi (milioni 40.4).

Watumishi wa umma ni aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa wa Rita, Philip Saliboko (milioni 40.4); aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Emmanuel Ole Naiko (milioni 40.4) na Mtumishi wa TRA, Lucy Appolo (milioni 80.8).
Share:

PANYA ROAD WAZUA TAFRANI DAR..



































Picha hii ni moja ya vingozi wa kundi hilo ambao kamishna kova aliwahi kuudhibitishia mtandao huu kuwa wamefanikiwa kuukamata mtandao wa wahuni hao lakini sasa wameibuka tena jijini Dar es salaam
Hali ya sintofahamu imetanda katika maeneo mengi ya jiji la Dar es salaam usiku huu baada ya vijana wanaofanya fujo maarufu kama PANYA ROAD kuingia barabarani usiku huu kufanya fujo na kuvuruga hali ya amani katika maeneo kadhaa ya jiji la Dar es salaam.vijana hao wameanzia fujo hizo katika maeneo ya magomeni kagera na kusambaa maeneo yote ya magomeni,mabibo na kuelekea maeneo ya sinza na kufanya shughuli zote za kiuchumi kufungwa ikiwa ni pamoja na maduka na shughuli za ushafiri kusimama kwa muda kupisha vijana hao ambao haieleweki wanadai nini ila wao wanapiga kila wanayekutana naye mtaani.
maeneo ya sinza muda huu kukiwa hakuna shughuli zinazoendelea na badala yake wananchi wanalazimika kukaa majumbani mwao kuokoa maisha yao juu ya vijana hao ambao wanatembea kimakundi wakiwa na silaha a jadi kama mapanga,mawe na siaha nyingine.
Baadhi ya wanachi waliozungumza, wamelitupia lawama jesho la polisi kwa kushindwa kuwadhibiti vijana hao kwani wameanza harakati hizi zamani lakini jeshi la polisi limekuawa likishindwa kuwachukulia hatua madhubuti kwa lengo la kuwasaidia wananchi ambao wamekuwa hawakai kwa amanai kuogopa fujo hizo.

Wananchi wanaoishi maeneo ya sinza,kwa mtogole,magomeni,mabibo na viunga vyake wanashauriwa kutokuzurura ovyo mitaani muda huu kwani vijana hao wapo maeneo hayo na bado hawajaondoka.

Share:

Ajali ya pikipiki Magomeni Usalama.




kumetokea ajali mbaya maeneo ya magomeni usalama ikihusisha pikipiki (bodaboda) na coaster ambapo dereva wa pikipiki na abiria wake wameumia vibaya.

Dereva pikipiki amevunjika mguu katika ajali hiyo na abiria wake amevunjika mkono na kuumia vibaya kichwani.

Polisi waliokuwa eneo hili wamewachukua majeruhi hao na kuwapeleka hospitali kwa ajili ya kupata huduma ya kitabibu.

Usafiri wa pikipiki kwa upande mwingine unasaidia sana
hasa katika dharura au foleni ya magari. Ajali za pikipiki zinakuwa nyingi kwa sababu madereva walio wengi hawana ujuzi na uzoefu wa kuendesha pikipiki.
Share:

Utafiti waelezea sababu za saratani.














Utafiti mpya unasema aina nyingi za ugonjwa wa saratani ni matokeo ya bahati mbaya, kuliko malezo ya vinasaba, mazingira na mtindo wa maisha.
Watafiti nchini Marekani walichunguza aina 31 za saratani na kugundua kwamba theluthi mbili zilisababishwa na mgawanyiko holela wa seli. Kwa mgawanyiko wa kila seli kuna hatari ya mabadiliko yanayoweza kusababisha saratani.
Wanasayansi hao wanasema kuimarisha mtindo wa maisha na mazingira kunasaidia kudhibiti magonjwa kama ya saratani ya ngozi na saratani ya mapafu.
Share:

Idara ya polisi yaongoza kwa ufisadi TZ. source BBC


Idara ya polisi ndio taasisi inayochukua hongo zaidi nchini Tanzania kulingana na ripoti ya ufisadi katika jumuiya ya Afrika mashariki.
Ripoti hiyo inasema kuwa maafisa wa polisi walipokea asilimia 25 ya hongo zote zilizotolewa kwa wafanyikazi wa taasisi za uma mwaka uliopita.
Ya pili ni idara ya mahakama,ambayo wafanyikazi wake walitia mfukoni asilimia 18 ya hongo,huku mashirika yalio na majukumu ya usajili na utoaji wa leseni yakiwa katika nafasi ya tatu kwa asilimia 10.
kwa mujibu wa gazeti la The Citizen, Idara ya Polisi nchini Tanzania imetajwa kuwa ya tatu kwa ufisadi katika jumuiya ya Afrika mashariki.
Polisi wa Uganda wanaongoza wakifuatiwa na wale wa Kenya katika nafasi ya pili na wale wa Burundi wakiwa katika nafasi ya nne.
Kulingana na ripoti hiyo maafisa wa polisi wa Rwanda ndio wasiochukua hongo ya juu Afrika mashariki.
Utafiti huo ulifanywa mwezi Julai na Agosti mwaka uliopita na shirika la lenye na maslahi ya kimaendeleo barani afrika ForDIA likishirikiana na Jukwaa la uwazi nchini tanzania Trafo.
Share:

UN:Itachukua mda mrefu kuangamiza EbolaUN:Itachukua mda mrefu kuangamiza Ebola.


Kiongozi wa ujumbe wa ebola katika shirika la Umoja wa Mataifa amesema kuwa harakati za kukabiliana na ugonjwa huo zinazochukuliwa hazijafikia kiwango cha kuuangamiza katika eneo la Afrika Magharibi.
Katika mkutano na vyombo vya habari nchini Ghana,Tony Banburry amesema kuwa jamii ya kimataifa imekuwa ikikabiliana na ugonjwa huo na huenda ikachakua mda mrefu kabla ya kudhibitiwa.
Hatahivyo amesema kuwa anaamini jamii ya kimataifa itafaulu katika kuuangamiza mlipuko huo mwaka 2015.
Virusi vya ugonjwa huo vimewaua takriban watu 8000 hususan nchini Sierra Leone ,liberia na Guinea.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.