Monday 27 April 2015

Yanga mabingwa wapya 2014/2015 Tanzania


Kikosi cha Yanga kilichotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa mwaka 2014/2015

Timu ya Yanga wamekuwa mabingwa wapya wa ligi kuu ya Tanzania kwa mwaka 2014/2015 na hivyo kuivua rasmi ubingwa Azam iliyokuwa ikishikilia taji hilo.
Ubingwa wa Yanga unakuja baada ya kuizamisha timu ya Polisi Morogoro kwa jumla ya mabao 4-1 katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Taifa Jumatatu, jijini Dar es Salaam, ilikuwa inahitaji ushindi wa pointi tatu kutangazwa bingwa mpya ikibakiwa na michezo miwili mbele.
Kabla ya mchezo huo Yanga ilikuwa inaongoza kwa pointi 52 ambapo sasa imefikisha pointi 55 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine yoyote ya ligi hiyo ya Vodacom.


Azam ambayo inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi 45 kwa sasa, endapo itashinda michezo yake iliyobaki itafikisha pointi 54 tu.
Vita ya kusaka nafasi ya pili sasa imebaki kwa Azam na Simba iliyo katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 41.
Timu za Prisons, Polisi na Ndanda ziko hatarini kushuka daraja.
Timu 14 zinashiriki ligi kuu ya Vodacom nchini
Tanzania.
Kocha wa Yanga Hans Pluijm

Share:

Babaake Kim Kardashian sasa ni mwanamke


Bruce Jenner aliyekuwa mwariadha bora duaniani kabla ya kuwa nyota wa kipindi cha televisheni na familia moja maarufu duniani ''The Kardashians''. sasa amefichua siri ambayo amekuwa akiificha kwa miaka mingi.
''Kwa nia na madhumuni yote, mimi ni mwanamke.'' Jenner aliambia Sawyer kutoka ABC katika mahojiano maalum yaliopeperushwa hewani siku ya Ijumaa.
''Watu wananiona tofauti,wananiona kama mwanaume, lakini moyo na roho yangu na kila kitu ninachofanya maishani ni sehemu yangu.'' Jenner ambaye ana umri wa miaka 65 amesema. '' Upande huu wa kike ni sehemu yangu.
hivi ndivyo mimi nilivyo.''

Katika masaa ya mahojiano na Diane Sawyer mjini New York na California, Jenner alielezea kwa kina mapambano yake ya kuwa na jinsia mbili tangu utotoni.
''Akili zangu ni za kike sana kuliko za kiume.'' Ameongezea. '' Ni vigumu sana watu kuelewa, lakini hivyo ndivyo nafsi yangu ilivyo.''
Jenner aliyejawa na hisia na mwenye nywele ndefu shati na suruali ndefu alisema kuwa amesubiri kwa miaka mingi ili kujitangaza kwa kuwa hakutaka kuwavunja moyo watu.
Kwa miongo kadhaa wake wa zamani wa Jenner na madada zake waliweka siri kuhusu jinsia yake na kwamba walikuwa watu waliokuwa wakijua siri hiyo.
Mtandao wa watu wanaojua siri hiyo hatahivyo ulipanuka hivi majuzi wakati Jenner alipomwambia mamaake na wanawe 10 .
Jenner ana watoto sita Burt,Cassandra,Brabdon,Brody,Kendall na Kylie pamoja na watoto wanne wa kambo akiwemo Kourtney,Kim,Khloe na Rob Kardashian.
Share:

Raia wa Uganda kupewa mafunzo ya kijeshi


Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameviagiza vikosi vya usalama kuanza kutoa mafunzo ya kijeshi kwa raia kama njia mojawapo ya kupigana vita dhidi ya kundi la kigaidi la Al Shabaab.
Amesema kuwa baada ya kundi hilo kushindwa na vikosi vya usalama vya umoja wa mataifa nchini Somalia,limeanza kuwashambulia raia wa kawaida na maeneo yasio na ulinzi,kama vile shambulizi la West gate na lile la Garissa nchini Kenya.
Kundi la Alshabaab pia lilitekeleza mashambulizi ya mabomu katika eneo la Kampala mwaka 2010 na kuwaua watu 70 waliokuwa wakiangalia mechi ya kombe la dunia.
Rais Museveni amewataka polisi ,jeshi na maafisa wa ujasusi kuwafunza raia wa Uganda ili kuwawezesha kuwalinda.

Kulingana na msemaji wa jeshi la Uganda Luteni Paddy Nkunda lengo lao sio Al Shabaab pekee.
Amesema kuwa sera hiyo inalenga kuwatuliza raia wenye ufahamu wa maswala ya usalama lakini hakuna atakayepewa silaha.
Maafisa wa serikali bado wanafanya mipango kuhusu ni lini mafunzo hayo yataanza pamoja na maelezo yao.
Kumekuwa na tamaduni ya wanafunzi wa shule za upili kupewa mazoezi wanapomaliza shule lakini mpango huo ulisitishwa katika miaka ya hivi karibuni.
Share:

Warundi 152,572 wawa raia wa Tanzania


Waliokuwa wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania zaidi ya 152,572 walioingia nchini humo tangu mwaka 1972, wamekabidhiwa vyeti vya uraia wa Tanzania na kuwa huru kuishi kama Watanzania wengine.
Wakimbizi hao walikuwa wameomba uraia wa Tanzania mwaka 2008 na kupewa na waziri wa mambo ya ndani mwaka 2010, sasa ni halali kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi mbalimbali za uongozi zikiwemo za udiwani na ubunge.
Akizungumza wakati wa ugawaji wa vyeti hivyo, mkuu wa makazi ya Mishamo, Frederick Nisajile alisema ugawaji wa vyeti hivyo ulianza Novemba 24 mwaka 2014 katika makazi ya Katumba mkoani Katavi magharibi mwa Tanzania ambako watu 56,554 walipewa vyeti vya uraia na baadaye kuhamia katika makazi ya Ulyankulu mkoani Tabora, magharibi mwa Tanzania ambako wakimbizi 43,453 tayari wamepewa vyeti hivyo.
Kwa upande wake msemaji wa wizara ya mambo ya ndani, Isaack Nantanga amesema hatua ya Tanzania kuwapa uraia wakimbizi hao ni kutokana na hiyari yao na kwamba serikali ya Tanzania ilishauriana na Burundi na hatimaye kukubaliana wapatiwe uraia wanaotaka wa kuwa Watanzania.
Hata hivyo si mara ya kwanza kwaTanzaniakutoa uraia kwa wakimbizi wanaoishi Tanzania kwa muda mrefu. Tanzania imefanya hivyo kwa wakimbizi wa Burundi na Somalia ambao wameishi Tanzania kwa miaka mingi.
Share:

Maandamano:Jeshi lasambazwa Burundi


Jeshi la Burundi limetawanywa nchini humo kujaribu kukabiliana na wale wanaopinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza kutangaza kuwania muhula wa tatu.
Polisi walivunja maandamano ya Wanaharakati na wapinzani nchini humo waliongia mitaani kwa siku ya pili kufanya maandamano.
Waandamanaji kadha walipigwa risasi jana Jumapili na watu wanne wanaripotiwa kufariki
Share:

Tetemeko laua zaidi ya watu 3,600 Nepal


Watu wapatao 3,617 wamefahamika kufa katika tetemeko kubwa la ardhi lililoipiga Nepal Jumamosi.
Kituo cha Taifa cha Dharura cha Majanga kimesema watu zaidi ya 6,500 wamejeruhiwa.
Watu kadhaa pia wameripotiwa kufa katika nchi jirani za China na India
Zaidi ya wapanda milima 200 wameokolewa kuzunguka Mlima Everest, ambao umekumbwa na athari za tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.8.
Wakaazi wengi wa mji mkuu Kathmandu wamekuwa wakilala katika mahema kwa wale wasio na makazi au wanaohofia kurudi majumbani kutokana na athari zaidi za tetemeko la ardhi zinazoendelea. Maelfu wamelala nje kwa siku ya pili Jumapili, baada ya tetemeko hilo kuipiga Nepal Jumamosi.
Maafisa wamesema idadi ya vifo au majeruhi ikaongezeka wakati huu ambapo vikosi vya waokoaji vimefanikiwa kufika katika ameneo ya milimani magharibi mwa Nepal.
Taarifa za awali zinasema jamii nyingi za watu, hususan wanaoishi karibu na kingo za mlima, wameathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na tetemeko hilo.
Mtu mmoja ambaye aliokolewa na helikopta kwenda katika mji wa Pokhara, kilomita 200 kutoka Kathmandu, amesema karibu kila nyumba katika kijiji chake chenye nyumba zaidi ya 1,000 kimeharibiwa, Bwana Darvas ameiambia BBC.
Share:

Saturday 25 April 2015

Je,michezo huathiri ubikra wa wasichana?


Mwalimu mkuu wa shule moja ya kiislamu mjini Melbourne, Australia amedaiwa kuwazuia wasichana katika shule hiyo kutoshiriki katika maswala ya michezo kwa hofu kwamba huenda wakapoteza ubikira.
Wanafunzi wa kike katika chuo cha Al-Taqwa mjini Truganina pia walizuiwa kucheza soka kwa kuwa majeruhi huenda yakawafanya kuwa tasa kulingana na fairfax.
Wasimamizi wa shule hiyo kwa sasa wanachunguza madai hayo yaliowasilishwa dhidi ya Mwalimu mkuu Omar Hallak ambaye awali alizua hisia kali baada ya kusema kuwa wapiganaji wa Islamic state walikuwa wakiungwa mkono na mataifa ya magharibi.
Katika barua iliondikwa na wizara na kuchapishwa na The Age,mwalimu mmoja wa zamani alisema kuwa:''Anaamini kwamba iwapo wasichana wataruhusiwa kukimbia huenda wakapoteza ubikra wao.Mwalimu huyo pia ana ushahidi wa kisayansi unaosema kuwa iwapo wasichana watajijeruhi,kupitia kuvunjika mguu wakati wanapocheza soka huenda ikawafanya kuwa tasa''..
Mwalimu huyo amedai kwamba Bwana Hallak aliwazuia wanafunzi wa kike kutoshiriki katika mashindano ya wilaya ya mbio za marathon mwaka wa 2013 na 2014.
Share:

Ng'ombe awala kondoo Kenya.


Mkulima mmoja nchi Kenya anasema kuwa mmoja wa ng'ombe wake amesusia lishe yake ya kawaida na kuanza kuwala kondoo.
Charles Mamboleo, ambaye anamiliki shamba kusini magharibi mwa kaunti ya Nakuru aligungua kuwa ng'ombe wake amemla kondo siku moja asubuni.
Jitihada zake za kumpa ng'ombe huyo chakula na maji hazikufua dafu, na siku iliyofuata ng'ombe huyo alimla kondoo mwingine.
Kulingana na afisa mmoja wa kilimo ni kuwa , huenda tabia ya ng'ombe huyo huenda imetokana na ukosefu wa madini yanayopatikana kwa mimea mbichi.
Hali ya kiangazi ambayo ilimalizika hivi majuzi huenda imesababisha mifugo kukosa madini yanayopatikaan kwenye nyasi mbichi. Mwaka 2007 ndama mmoja nchini India alinaswa kwenye mkanda wa video akila kuku.
Share:

Wahamiaji:Wanahabari wa UK washtumiwa


Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Zeid Ra’ad Hussein, amekuwa akifadhaishwa sana na lugha ya magazeti ya Uingereza wanayotumia dhidi ya wakimbizi, lakini ni taarifa ya hivi punde iliyochapishwa na makala ya
‘The Sun’ iliyomghadhabisha zaidi.
Makala hiyo iliwaita wakimbizi mende, matamshi ambayo Hussein anasesema ni sawia na yale yaliotumika Rwanda kabla ya mauaji ya kimbari.

Mkuu huyo wa Haki za Kibinadamu amesema taarifa hiyo ya The Sun ilikuwa mojawapo tu ya taarifa nyingi za chuki na za kibaguzi ambazo zimechapishwa kwa miongo mingi na magazeti ya Uingereza.
Alisema desturi hii ilikuwa inaongeza moto wa chuki na udhalilishaji wa binadamu wengine. Hussein alisema kuwa malalamishi kuhusu makala hizo tayari yamepelekwa kwa Polisi wa jiji na akataka kuchukuliwe hatua kali.

Matamshi haya, hasa kutoka kwa afisa wa juu sana wa umoja wa mataifa, umeashiria wasiwasi ulioko kuhusu mjadala unaoendelea bara Uropa kuhusu wakimbizi wanaovukia Meditteranean kuingia Ulaya .
Mjadala ambao unasemekana unaendeshwa na hisia kali kwenye vyombo vya habari, na kwamba maoni ya uma huenda hayaungi mkono hatua zinazohitajika kuokoa maisha ya wanaokufa maji huko mediterrenean
Share:

Washukiwa wa ugaidi wakamatwa Italia


Polisi nchini Italia wanasema kuwa wamewakamata watu 18 wanaoshukiwa kuwa wanachama wa Islamic State kutoka nchini Afghanistan na Pakistan katika oparesheni kubwa ya kupambana na ugaidi.
Wanasema kuwa wawili kati ya washukiwa hao wanaaminiwa kuwa walinzi wa aliyekuwa kiongozi wa al-Qaeda Osama Bin Laden na wengine wanashukiwa kuhusika kwenye mashambulizi nchini Pakistan likiwemo shambulizi lililotokea kwenye soko la Peshawar.
Oparesheni hiyo ilikuwa imeendeshwa kwenye kisiwa cha Italia cha Sardina .
Polisi walisema kuwa kundi linalofanyiwa uchunguzi lilikuwa limewapangia wanachama wake kuingia nchini Italia wakiwa na vyeti vya kufanya kazi au kama watafuta hifadhi.
Share:

Mwanaharakati maarufu auawa Pakistan


Mwanaharakati maarufu wa haki za binadamu nchini Pakistan Sabeen Mehmud ameuawa kwa kupigwa risasi kwenye mji mkuu Karachi.
Alivamiwa na watu wasiojulikana alipokuwa akielekea nyumbani kwake baada ya kuandaa warsha kuhusu kuhusika kwa jeshi la Pakistan katika kuwatesa na kuwaua wanaharakati wa kisiasa nchini humo.
Bi Sabeen ambaye alikuwa na umri wa miaka 38, alikuwa pia mkurugenzi wa shirika moja la misaada na wa duka moja la vitabu ambapo mazungumzo kuhusu haki za binadamu yalikuwa yakifanyika.
Duka hilo lilikuwa moja ya maeneo machache mjini Karachi ambapo wanafunzi na wanaharakati walikuwa wakikutana kujadili changoto zinazoikumba Pakistan.
Share:

Google yazindua huduma mpya ya simu


Kampuni ya Google imatangaza kuwa itazindua huduma mpya nchini Marekani ambayo inaweza kutumiwa nyumbani na wakati wa safari za mataifa ya kigeni.
Huduma hiyo inayo fahamika kama Project Fi inatapatikana kwa simu za Smartphone za Google Nexus 6.
Huduma hiyo itatumia maeneo yaliyo na Wi-Fi sambamba na huduma zingine za mawasilianoi nchini Marekani za Sprint na T-Mobile na inaweza pia kutumiwa kwenye nchi 120 bila malipo ya ziada wakati mtu anaposafiri nje ya nchi.
Huduma hiyo itatolewa kwa malipo ya dola ishirini kwa mwezi kwa huduma za kawaida na dola kumi kwa mwezi kwa kila gigabyte ya data inayotumika.
Google inasema kuwa huduma hiyo huwa inajiunga moja kwa moja na zaidi maeneo milioni yenye huduna za Wi-Fi na mteja ana uwezo wa kuhamiswa kutoka kwa mtandao mmoja hadi mwingine kulingana na ni upi unaotoa huduma bora zaidi.
Share:

Sherehe za miaka 100 zafanyika Gallipoli


Sanamu za makumbusho Gallipoli

Sherehe zimefanyika eneo la Gallipoli nchini Uturuki kuadhimisha miaka mia moja tangu uvamizi wa kijeshi uliofanywa eno hilo na wanajeshi wa muungano wakati wa vita vya kwanza vya dunia.
Zaidi ya watu 100,00 waliuwa kwenye uvamizi huo ulioendeshwa dhidi ya ufalme wa Ottoman.
Wageni kutoka nchi zote zilizopigana walihudhuria sherehe hizo wakiwemo viongozi kutoka Uturuki , Australia na New Zealnd, ambazo zote zilipoteza watu wengi.
Sherehe pia zilifanyika mapema nchini New Zealand na pia mjini Sydney. Zaidi ya wanajeshi 10,000 wa Australia na New Zealand waliuawa kwenye vita hivyo vilivyofeli.
Share:

Thursday 23 April 2015

Hasira zamfanya aipige kompyuta risasi


Mwamamme mmoja kwenye mji wa Colorado nchini Marekani huenda akachukuliwa hatua za kisheria kufuatia kisa ambapo alikasirishwa na kompyuta yake kisha akaitoa nje na kuifyatulia risasi mara nane.
Polisi wanasema kuwa Lucas Hinch alikuwa na matatizoya kiteknolojia ndipo akaipeleka kompyuta hiyo upande wa nyuma ya nyumba yake na kuiharibu ambapo alikamatwa muda mfupi baadaye.
Vyombo vya habari vilisema kuwa alichoka na kusumbuliwa na kompyuta yake lakini hakufahamu kuwa alikuwa akivunja sheria alipoiadhibu kwa risasi.
Gazeti moja lilisema kuwa wakati herufi za ctrl+alt+delete zilifeli , bwana Hinch alishikwa na hasira nna kuamua kulipiza kisasi kwa kuiharibu Kompyuta hiyo hadi kiwango ambacho haiwezi kutumika tena
Share:

Mashambulizi ya Yemen yawapa tuzo marubani


Mwana wa mfalme nchini Saudi Arabia ambaye ni miongoni mwa matajiri wakubwa nchini humo, ameshambuliwa katika mitandao ya kijamii baada ya kuwapa magari ya kifahari marubani wa ndege za kivita wa nchi yake ambao walishiriki katika kampeni ya kurusha mabomu na kuishambulia Yemen.
Mwanzoni mwa wiki hii Saudi Arabia iliweka bayana mwisho wa awamu ya kwanza ya kampeni yake ya kijeshi nchini Yemen.Katika sherehe za kufurahia matokeo ya kampeni hiyo ya kwanza mwana wa mfalme Al-Waleed bin Talal, ,aliweka maoni yake kwenye ukurasa wake wa twitter wenye wafuasi milioni tatu akisema kwamba; kwa kutambua na kuonesha nimethamini kile walichofanya askari wetu kwenye awamu hii ya kwanza ,ninajisikia fahari kuwazawadia askari ambao ni marubani pia wapatao mia moja magari aina ya Bentley kwa matokeo mazuri ya oparesheni yetu .
Pendekezo la zawadi hiyo kutoka kwa mawana wa mfalme lilikumbwa na upinzani mkali mara tu baada ya kuwekwa katika mtandao huo wa kijamii na kuwagawa wafuasi wake katika makundi mawili, zaidi ya wafuasi wake elfu ishirini na nane walitumiana ujumbe huo na zaidi ya wafuasi wake elfu tano waliupenda ujumbe huo.

Mwana wa mfalme huyo alisifiwa kwa moyo wake wa ukarimu na wasaudia wengi, ambao walitoa maoni yao juu ya uamuzi wake huo,na kusema kwamba marubani hao wanastahili magari hayo ya kifahari na zaidi ya hayo kwa kazi yao nzuri ya kutukuka waliyoifanya nchini Yemen.
Hata hivyo ujumbe huo wenye kutoa zawadi nono kwa marubani hao umefutwa katika akaunti yake ya twitter,ingawa hapo awali ujumbe huo ulishasambazwa na unaendelea kusambaa mitandaoni.
Na baadhi ya vyombo vya habari nchini Saudi Arabia vimeripotiwa kudai kuwa akaunti ya mwana wa mfalme ilikuwa imedukuliwa ,ingawa hakukuwa na taarifa yoyote hapo awali iliyolalamikia udukuzi huo ,na mwana wa mfalme huyo mpaka sasa ameamua kupiga kimya, wala hajasema neno.
Mwaka uliopita, mwana mfalme huyo,anayetambuliwa kwa mahaba yake ya kupenda maisha ya kifahari na mwenye mkono mwepesi wa kutoa zawadi kubwa kubwa ,mwaka huo inaarifiwa kuwa aliipatia timu ya mpira wa miguu ya nchi hiyo magari ishirini na matano baada ya kushinda michuano ya kandanda ya nchi hiyo,suala ambalo lilizua mjadala yakwamba nani anapaswa kutoa zawadi nchini humo na nani hastahili kutoa zawadi.
Share:

Raisi wa Everton afariki dunia

Rais wa heshima wa klabu ya Everton Sir Philip Carter amefariki akiwa na miaka 87.
Taarifa iliyotolewa na klabu ya Everton imethibitisha kifo hicho na Kueleza Carter alifariki akiwa nyumbani kwake Alhamisi asubuhi baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Carter, alikua mshabiki wa timu hii tangu utotoni ambapo mwaka 1973 alijiunga na timu kama mkurugenzi na mwaka 1978 akawa mwenyekiti wa timu.
utoto Everton shabiki, alijiunga na klabu kama mkurugenzi mwaka 1973. Yeye alipata nafasi ya mwenyekiti mwaka 1978 na aliendelea ataongoza kipindi cha mafanikio ndani na Ulaya
Wakati wa uongozi wake kama mwenyekiti akiwa na meneja Howard Kendall ,Carter , alishinda mataji mwaka ya FA cup 1985 na 1987, 1984 na Kombe la Ulaya 1985.
Alichaguliwa kuwa Raisi wa heshima wa maishan wa timu ya Everton mwaka 2004
Share:

Akiri kudanganya kuhusu tiba ya Saratani


Mwanablogu aliyelimbikiziwa sifa baada ya kudai kwamba alimiliki dawa za kuponya ugonjwa wa saratani ya ubongo kupitia tiba ya kiasili amekiri kwamba alidanganya kuhusu ugonjwa wake.
Belle Gibson alianza kazi iliojawa na mafanikio mbali na uzinduzi wa kitabu cha mapishi kufuatia madai ya afueni ya kimiujiza.
Lakini wengine walipoanza kumuuliza kuhusu habari hiyo aliliambia gazeti moja la nchini Australia kwamba hajawahi kuwa mgonjwa.
Alisema kuwa alipambana na maisha kuhusu kusema ukweli.
Shirika moja la wahisani wa saratani limewataka wagonjwa kuwa na hofu punde wanapoelezwa kuhusu tiba zisizoaminika.
Share:

Wanawake wanaokuwa watawa waongezeka UK


Idadi ya wanawake wanaokuwa watawa imeongezeka pakubwa katika kipindi cha miaka 25,kanisa katoliki nchini Uingereza na Wales limesema.
Takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya wanawake wanaokula viapo vitakatifu imeongezeka mara tatu katika kipindi cha miaka mitano kutoka wanawake 15 mwaka 2009 hadi 45 mwaka uliopita,ikiwa ni idadi kubwa tangu mwaka 1990.
Wanawake 14 walioingia katika utawa mwaka 2014 walikuwa na miaka 30 ama chini yake ,takwimu mpya zinaonyesha.
Kanisa hilo linasema kuwa wanawake wanajiingiza katika maisha ya kidini kutokana na pengo la utamaduni kutotiwa maanani.
Takwimu zinaonyesha kuwa mwaka 1980 takriban wanawake 80 walijiunga na utawa lakini idadi hiyo ilipungua hadi mwaka 2004 ambapo wanawake saba pekee walijiunga na utakatifu huo.
Idadi hiyo imeongezeka katika kipindi cha miaka 10 ambapo ilifika 45 mwaka 2014.
Share:

Alshabaab washukiwa kumteka nyara Chifu


Wanamgambo wanaoaminika kuwa Al Shabaab wamemteka nyara chifu na gari la miraa katika eneo la Arabia, kaunti ya Mandera.
Shambulizi hilo limetokea mapema siku ya Alhamisi , na maafisa wa usalama wako katika harakati ya kuwaokoa manusura waliotekwa nyara.
Viongozi wamesema washambuliaji walionekana kufahamu eneo hilo na pia Chifu waliyemteka nyara. Inasemekana kuwa Chifu huyo alikuwa akielekea Mandera wakati wa shambulizi hilo.
Awali katika idhaa yaa BBC Somali tuliweza kuzungumuza na mwakilishi wa kaunti katika wadi ya Arabia na kaweza kutuhakikishisa shambulizi hilo na vile vile alisema kuwa wanashuku wanamgambo wa Alshabab ndio waliofanya kitendo hicho.
Hadi sasa hakuna taarifa rasmi kutoka serikali kuhusiana na utekaji nyara na muda mfupi uliopita kulikuwa na taarifa isiyo thibitishwa kuwa chifu huyo ameuwawa na Alshabaab.
Kutokana na swala hili la Usalama wanasiasa jimbo la Mandera waliweza kuongea na wanahabari huku wakilaani kitendo hicho huku wakihimiza serikali kuimarisha usalama katika mkoa wa kaskazini mashariki mwa Kenya.
Share:

Boko Haram labadilisha jina Nigeria


Picha mpya zimetolewa kuhusu wapiganaji wa Boko Haram ambao wanajielezea kuwa Islamic State Jimbo la Magharibi mwa Afrika.
Kundi hilo limekuwa watiifu kwa wapiganaji wa Islamic State mwezi uliopita.
Baadhi ya wanajeshi wa Nigeria ambao wameshirikishwa katika oparesheni ya kulishinda kundi hilo katika msitu wa Sambisa uliopo Kazkazini mashariki wamelazimika kurudi nyuma kwa kuwa wanadhani kwamba huenda msitu huo umewekwa mitego.
Mwanachama wa kundi moja la kuweka usalama mtaani JTF ameiambia BBC kwamba mwanajeshi mmoja na walinzi watatu wa mitaani waliuawa wakati gari lao lilipopita juu ya mtego.
Share:

Obama:Mateka waliuawa kwa bahati mbaya


Ikulu ya Marekani imetangaza kuwa watu wawili waliokuwa wamezuiliwa na wapiganaji katika nyumba moja nchini Afghanistan, waliuwawa kimakosa na majeshi ya Marekani yanayopambana na ugaidi katika maeneo ya Afghanistan na Pakistan.
Akisoma taarifa kuhusiana na vifo hivyo, Rais Barrack Obama, amesema kuwa amesikitishwa mno na kisa hicho kilichofanyika Januari mwaka huu.
Anasema watu hao walikuwa wamezuiliwa na wapiganaji wa al Qaeda, kwa miaka kadha.
Wametajwa kama Mmarekani Warren Weinstein, na Giovanni Lo Porto raia wa Italia.
White House inasema pia kuwa, raia wengine wawili waliouliwa walikuwa waamerika, na wanachama wa kundi la al Qaeda.
Share:

Waandamana kupinga ubaguzi Afrika Kusini


Maelfu ya raia wa Afrika Kusini wanaandamana kupinga wimbi la visa vya hivi majuzi vya mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni.
Mikutano mikubwa imeandaliwa katika mji mkuu Johannesburg na katika mji wa Port Elizabeth ulioko kusini mwa nchi hiyo ambao ulishuhudia mashambulio kadhaa dhidi ya wahamiaji wa mataifa ya kigeni mnamo mwaka 2008.
Makundi ya kiusalama yanafanya misako katika majumba ya makaazi katika mji wa Alexandra mjini Johannesburg, mahala ambapo mashambulio kadhaa dhidi ya raia wa kigeni hasa Afrika yalifanyika katika kipindi cha majuma kadhaa yaliyopita.
Mwaandishi wa BBC anasema kuwa, kuonekana kwa walinda usalama barabarani kumeleta udhibiti na amani.
Share:

Tuesday 21 April 2015

Japan yavunja rekodi treni mwendo kasi


Treni ya kampuni ya Central Japan Railway (JR) ikirejea katika stesheni baada ya kuandika rekodi mpya ya dunia ya mwendo kasi

Treni ya Japan iendayo kasi imevunja rekodi yake duniani kwa kufikia mwendo wa kilomita 603 kwa saa, sawa na maili 374 kwa saa katika majaribio yake karibu na Mlima Fuji.
Treni hiyo imevunja rekodi yake ya mwendo wa kilomita 590 kwa saa iliyoweka wiki iliyopita katika jaribio lingine.
Treni ya maglev ambayo haitegemei kugusana na chuma bali inaendeshwa kwa nguvu ya umeme, inatumia sumaku zilizochajiwa kwa umeme kunyanyua na kuvuta mabehewa juu ya njia ya reli.
Treni ya Kati ya Japan, JR Central, ambayo inamiliki matreni hayo, inataka kuanzisha huduma yake kati ya Tokyo na mji wa Nagoya uliopo katikati ya Japan, ifikapo mwaka 2027.
Safari hiyo ya kilomita 280 itachukua dakika itachukua muda wa dakika 40 tu, pungufu ya nusu ya muda unaotumiwa sasa.
Hata hivyo abiria hawatashuhudia treni hiyo kukimbia mwendo wake uliovunja rekodi kwa sababu kampuni inasema treni zake zitakimbia kasi ya kilomita 505 kwa saa. Kwa kulinganisha treni za mwendo kasi kabisa za Japan aina ya shinkansen, au "bullet train" inakimbia mwendo kasi wa kilomita 320 kwa saa.

Treni ya Maglev ikiwa katika majaribio

Majaribio ya treni hiyo yalifanyika katika reli ya majaribio katika mkoa wa Yamanashi ulioko katikati mwa Japan.
Ujenzi wake unakadiriwa kugharimu karibu dola za kimartekani bilioni 100 au pauni za Uingereza bilioni 67 kwa ujenzi tu wa kwenda Nagoya, ambapo asilimia 80% ya gharama itakwenda katika ujenzi wa mahandaki ya kupitia treni hiyo.
Ifikapo mwaka 2045, treni hizo za mwendo kasi za maglev zinatarajiwa kusafiri kati ya miji ya Tokyo na Osaka kwa muda wa saa moja tu na kupunguza urefu wa safari kwa nusu ya muda uliokuwa ukitumika yaani saa mbili.
Watu wapatao 200 walijipanga kando ya reli kushuhudia majaribio ya treni hiyo yaliyofanyika Jumanne.
"Jinsi treni inavyokwenda kwa mwendo kazi zaidi, ndivyo inavyozidi kutulia- nafikiri ubora wa treni umeimarika," amesema mkuu wa utafiti wa treni ya JR Central, Yasukazu Endo.
Treni hiyo inatumia sumaku iliyochajiwa kwa umeme kunyanyua na kuvuta mabehewa juu ya njia ya reli.
Share:

Ethiopia yaanza siku 3 za maombolezi.


Islamic State wakienda kuwaua raia wa Ethiopia

Ethiopia imeanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kwa heshima za raia wake waliouawa na wanamgambo wa kundi la Islamic State nchini Libya.
Bendera zitapepea nusu mlingoti wakati nalo bunge la nchi hiyo likikutana kujadili hatua ambazo litachukua kufuatia mauaji hayo ya raia wake zaidi ya ishirini.
Msemaji wa serikali Redwan Hussein, alisema kuwa waathiriwa hao wanaaminika kuwa wahamiaji waliojaribu kusafiri kwenda barani ulaya.
Mungano wa Afrika ambao una makao yake makuu nchini Ethiopia ulilaani mauaji hayo na kusema kuwa utafanya mikakati ya kuhakikisha kuwepo usalama nchini Libya.
Wanamgambo wa Islamic State walitoa kanda ya video ambayo inakisiwa kuonyesha mauaji hayo yanayoonyesha watu hao wakipigwa risasi na kukatwa vichwa.
Share:

Mkenya ashinda tuzo la Goldman


Phyllis Omido mshindi wa tuzo la Goldman

Phyllis Omido, kutoka Kenya, alikuwa miongoni mwa washindi sita waliokabidhiwa tuzo hilo huko San Francisco, Marekani, Jumatatu usiku. Omindo alipata tuzo hilo kwa kutetea wakaazi wa mtaa wa mabanda wa Owino Ohuru ulioko Mikindani kaunti ya Changamwe mjini Mombasa.
Wakaazi hao wameathirika na sumu aina ya ''lead'' kutokana na kiwanda cha kukarabati betri kuu kuu kilichojengwa karibu na mtaa huo wa mabanda. Ukarabati wa betri kuu ulisababisha umwagikaji wa madini ya sumu aina ya "lead" na kuwadhuru kiafya wakaazi hao kiasi kwamba baadhi ya wanaume sasa wameshindwa kutekeleza majukumu yao ya nyumbani.
Kiwanda hicho kilianza kazi mwaka wa 2009 lakini Omido alitetea wakaazi hao wa Uwino Uhuru kwa kufanya maandamano ya mara kwa mara hadi kikafungwa miaka mitatu baadae.

Omido apongezwa kwa ushindi wake

Anastacia Nambu anatueleza jinsi mumeo ameumia:''Sasa sisi tunaishi tu kama dada na ndugu kwa sababu mzee sasa hawezi kazi na si kupenda kwake ni kwa sababu ya hicho kibanda. Sisi tuliakua tunaishi karibi sana na hicho kibanda ndio kwa maana huo moshi ukaumiza mzee wangu. Ni jambo ka kusikitisha sana maanake tulitaka tupate watoto wengine lakini sasa hatuwezi. Tuna watoto wanne.''
Mzee wa kijiji Alfred Ogolla anatueleza juhudi zao za kuhimiza serikali ya Kenya iwape matibabu zimegonga mwamba. Ogolla anatueleza zaidi:''Sote hapa wazee, kina mama na watoto tunaumia sana. Mimi ninakohoa kila mara, wasichana hawawezi kuzaa kwa sababu huo moshi uliharibu nyumba zao za uzazi na watoto nao wengine miguu imejipinda na wengine nao ni vibofu hawawezi kuona. Pesa ya matibabu ni nyingi sana hatuwezi kupata dawa kila siku.''
Tuzo hilo la Omido limeandamana na kitita cha dola 175,000.

Omido afurahia tuzo lake

Je, Omido atatumiaje fedha hizo ambazo ni kama shillingi milioni 17 za Kenya?:''Kiasi kikubwa cha pesa hizi nitatumia kwa wakili maanake kesi ya wakaazi wa Owino Uhuru ingali kotini. Tunataka serikali iwape fidia na kuwalipia matibabu. Fedha zingine nitazitumia kuendeleza shirika langu lisilo la kiserikali (Centre for Justice, Governance and Environmental Action) maanake kuna mengi nataka kufanya licha ya vitisho kwa maisha yangu kwa sababu ya kupigania wakaazi wa Owino Uhuru.
''Kwa kweli nimefurahia sana kupata tuzo hili ambalo linanipa morali zaidi kwa kuwa kazi yangu imetambuliwa kote duniani. Nataka kufuata nyayo za mwanaharakati mwingine wa mazingira, merehemu Wangari Maathai. Nitazidi kutetea wanyonge kwa sababu ni wengi sana wanaumia.''
Share:

Uharamia wapungua duniani


Maharamia

Halmashauri ya kimataiafa ya safari za baharini IBM imetoa ripoti yake ya hivi punde kuhusu uharamia.
Halmashauri hiyo inasema kuwa uharamia sasa unaripotiwa kusini mashariki mwa bara Asia, huku meli ndogo za kusafirisha mafuta zikishambuliwa baada ya kila wiki mbili.

Maeneo yaliyoathirika na uharamia

Kwenye ripoti yake ya kila baada ya miezi mitatu, IMB inasema kuwa licha ya kupungua kwa mashambulizi kote duniani miaka ya hivi majuzi, visa vya uharamia viliongezeka katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka 2015.
Ripoti hiyo inasema kuwa kwa mara ya kwanza hakuna visa vyovyote vya uharamia vilivyorekodiwa pwani ya Somalia na Ghuba ya Aden.
Inasema kuwa uharamia ulianza kushuhudiwa mwaka 2007 eneo hilo lakini ukapungua kuanzia mwaka 2011 wakati doria za meli za kijeshi zilipo ongezeka.
Ripoti hiyo pia imetaja visa kadha vya uharamia pwani ya magharibi mwa Afrika. Inasema kuwa mwaname moja aliuawa wakati wa kutekwa kwa mashua ya uvuvi pwani ya Ghana.
Share:

Mawaziri 16 waapishwa Afghanistan


Baada ya miezi kadha ya mizozo ya kisiasa, rais wa Afghanistan Ashraf Ghani amewaapisha mawaziri 16 wapya kwenye sherehe zilizofanyika mjini Kabul.
Hii inamaanisha kuwa baraza la mawaziri sasa limekamilika. Nafasi ya waziri wa ulinzi imesalia wazi kufuatia kutoelewana kwa serikali ya umoja.
Wale wote walioteuliwa hawajashikilia nyadhifa kama hizo na wengi ni vijana na waliosoma. Wanne kati ya mawaziri hao ni wanawake.
Kinyume na ilivyo kuwa awali, rais Ghani ameahidi kuwateua watu walio na ujuzi badala ya mibabe wa kivita na wapiganaji kuongoza serikali.
Share:

Morsi ahukumiwa miaka 20 gerezani


Makahama nchini Misri imemhukumu aliyekuwa rais wa zamani Mohammed Morsi kifungo cha miaka 20 jela kutokana na kuuawa kwa waamdamanaji wakati akiwa madarakani.
Hii nidyo hukumu ya kwanza kutolewa kwa Morsi tangu aondolewe madarakani, na moja ya hukumu zinazomuandama.
Morsi aliondolewa madarakani na jeshi mwaka 2013 kufuatia maandamano makubwa mitaani ya kupinga uongozi wake.

Wafuasi wa Morsi

Yeye pamoja na viongozi wengine wa Muslim Brotherhood walilaumiwa kwa kuwachochea wafuasi wao kumuua mwandishi wa habari na waandamanaji wa upinzani wakati wa makabiliano nje ya ikulu ya rais mwishoni mwa mwaka 2012.
Wakati umati ulipokusanyika nje ya ikulu bwana Morsi aliwaamrisha polisi kuwatawanya lakini wakakataa kufanya hivyo.
Baadaye Muslim Brotherhood waliwaleta wafuasi wao ambapo watu 11 waliuawa kwenye makabiliano, wengi kutoka kwa Muslim Brotherhood.
Kabla ya kutolewa hukumu ya leo, Muslim Brotherhood walimlaumu rais wa sasa Abdul Fatta al-Sisi kwa kutumia mahakama kama silaha.
Share:

Jeshi kutuliza ghasia Afrika kusini


Waziri wa ulinzi nchini Afrika kusini ametangaza kuwa jeshi litatumwa wakati ghasia dhidi ya wageni zikiwa zimesababisha vifo vya watu Saba.
Nasiviwe Mapisa-Ngqakula anasema kuwa ombi la kutumwa kwa wanajeshi liliamuliwa baada ya polisi kuomba msaada.
Lakini hakusema ni wanajeshi wangapi watatumwa mitaani. Jeshi litatumwa kwenda maeneo yanayoshuhudia ghasia nyingi ikiwemo mikoa ya Kwa Zulu Natal na Guateng.
Wakati wa ghasia kama hizo mwaka 2008 jumla ya watu 63 waliuawa. Serilali ya Afrika Kusini pia imetangaza kuwa zaidi ya watu 900 wamerudi kwa hiari kwenda nchi zao.
Share:

Monday 20 April 2015

Mama aliyeua Watoto Marekani ahukumiwa


Mwanamke mmoja katika Jimbo la Utah nchini Marekani ambaye alikiri kuua watoto wake wachanga sita wa kuzaa mwenyewe huenda akahukumiwa Kifungo cha maisha gerezani.
Megan Huntsman, 40, alikamatwa mwaka mmoja uliopita baada ya miili ya Watoto kukutwa kwenye maboksi katika gereji ya Nyumba yake ya zamani.
Mwezi Februari alikutwa na hatia kwa makosa sita ya mauaji.
Jaji wa mjini Provo alitoa hukumu dhidi ya mwanamke huyo ya takriban miaka 30 mpaka kifungo cha maisha.
Polisi wamesema Watoto hao walizaliwa kati ya mwaka 1996 na 2006 na kueleza hali ya Watoto hao kuwa mauti iliwakuta kwa kukosa hewa au kwa kukabwa na Huntsman mara tu baada ya kuzaliwa.
Polisi wamesema miili aliiweka kwenye mifuko ya plastiki na kuiweka kwenye maboksi.
Mwanamke huyo aliacha maboksi hayo katika Nyumba aliyoishi alipokuwa akihama, miili iligunduliwa na mumewe,Darren West, mwezi Aprili mwaka jana.Mtoto wa saba pia anaaminika alipoteza maisha wakati mwanamke huyo alipokuwa akijifungua.
Polisi wanasema Huntsman alikuwa akitumia dawa zenye nguvu ziitwazo methamphetamine, dawa zinazosisimua neva mwilini ili kuwezesha akili na mwili kufanya kazi kwa uchangamfu, pia mwanamama huyo hakuwataka Watoto hao.
Maafisa wanasema West ni Baba wa Watoto lakini yeye si mshukiwa wa tukio hilo.Yeye na Huntsman wana Watoto watatu.
Mwezi Aprili mwaka 2014 West aliachiwa huru baada ya kutumikia kifungo cha miaka minane gerezani kwa makosa ya kujihusisha na uhalifu wa madawa, hivyo alikwenda kwenye nyumba kwa ajili ya kukusanya vitu vyake ndipo alipogundua miili ya Watoto.
Uamuzi wa mwisho kuhusu muda ataotumikia Huntsman gerezani uko mikononi mwa jopo la wanasheria.Waendesha mashtaka wamesema huenda akatumikia kifungo cha maisha.
Share:

Ulaya kumaliza vifo vya Wahamiaji?


Mkuu wa sera za kigeni ndani ya Umoja wa Ulaya amesema kuwa uharaka unahitajika katika kushughulikia majanga yanayojitokeza katika bahari ya Mediterania.
Federica Mogherini ameainisha mambo tisa ya mpango wa kumaliza tatizo la vifo vya wahamiaji.
Operesheni ya uokoaji itaimarishwa na kutakuwa na Kampeni maalumu ya kuteketeza boti zilizotumiwa kusafirisha watu.
Waziri Mkuu wa Italia, Matteo Renzi, amesema Roma ina mpango wa kupambana na wale waliowaita Wafanyabiashara wa utumwa.
Imeelezwa kuwa hatua zitachukuliwa kupunguza idadi ya wahamiaji na kuwarejesha wale wanaoingia barani Ulaya.
Mpango huu utajadiliwa na Viongozi wa Ulaya siku ya Alhamisi.
Wakati hayo yakijiri,Polisi nchini Italia inawashikilia watu wawili miongoni mwa walionusurika kwenye ajali ya boti.
Mtu mmoja mwenye asili ya Tunisia ambaye anaaminika kuwa nahodha wa chombo hicho na mwenzake Raia wa Syria walikamatwa wakishukiwa kuhusika na vitendo vya kusafirisha watu kinyume cha sheria.
Watu hao walikamatwa baada ya meli moja yenye manusura wa ajali kuwasili katika bandari ya Catania katika kisiwa cha Sicily.
Share:

Zwelithini alaani mashambulio AK.

Goodwill Zwelithini
Mfalme wa kabila la Zulu, Goodwill Zwelithini, ameelezea kama jambo la aibu mashambulio dhidi ya raia wa mataifa mengine yanayofanyika nchini Afrika Kusini, ambayo tayari yamesababisha vifo vya watu saba.
Mwaandishi habari wa BBC mjini Durban mahala ambapo mfalme huyo alitoa matamshi hayo anasema kuwa hata ingawa anakanusha kuwa amenukuliwa visivyo, matamshi yake dhidi ya raia wa kigeni imesababisha athari mbaya.
Amesema kuwa umma uliwapigia kelele mabalozi wanaoziwakilisha mataifa yaliyoathirika zikiwezo Msumbiji na Zimbabwe.
Polisi nchini humo wameakamata washukiwa kadhaa miongoni mwao wanaume watatu ambao wanatuhumiwa kuhusika na mauaji ya rais mmoja wa Mozambique katika eneo la Alexandra viungani mwa mji mkuu wa Johannesburg.
Picha kadhaa zimeonyesha Emmanuel Sithole akindungwa kisu huku umati mkubwa ukitizama.



Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma, amesema mashambulio hayo yanakwenda kinyume na maadili yote wanayoamini.
Makundi kadhaa yaliyojihami yameshambulia na kupora maduka kadhaa yanayomilikiwa na wahamiaji kutoka mataifa mengine ya Afrika.
Huku idadi ya watu wasio na kazi nchini humo, ikikadiriwa kuwa zaidi ya asilimia Ishirini na nne, raia wengi wa taifa hilo wamewashutumu raia wa kigeni kwa kuchukua nafasi zao za kazi.
Maelfu ya raia hao wa kigeni, wamekimbia makwao na sasa wanaishi katika kambi za muda, ili hali mataifa jirani wameanza shughuli ya kuwahamisha raia wao.
Siku ya Jumapili, serikali ya Zimbabwe imetuma mabasi kadhaa mjini Durban kwenda kuwachukua raia wake wapatao mia nne.
Takwimu rasmi za serikali zinakadiria kuwa kuna raia milioni mbili wa kigeni wanaoishi nchini Afrika Kusini, lakini wengi wanahoji kuwa idadi hiyo huenda ni kubwa zaidi.
Share:

Huenda 800 waliangamia baharini


Umoja wa Mataifa unasema unahofia kuwa huenda watu 800 walifariki siku ya Jumapili, pale mashua waliyokuwa wakilitumia kuvuka bahari ya Mediterenean ilipozama karibu na Libya.
Shirika la Umoja wa mataifa linalowashughulikia wakimbizi UNHCR, limekuwa likizungumza na manusura baada ya kuwasili katika kisiwa cha Sicily mapema leo Jumanne.

Mkuu wa sera kwenye Muungano wa Ulaya Federica Mogherini anasema kuwa pana haja ya kuwepo hatua za haraka ili kushughulikia suala kuhusu wahamiaji katika bahari ya Mediterranean, huku akizindua mikakati kumi ya mpango wa kutanzua vifo vya wahamiaji.
Mogherini, anasema kuwa mipango hiyo ni hatua kubwa ya kuzuia kupotea kwa maisha ya watu. Majukumu ya muungano huo ni kuzidisha operesheni ya uokozi, pamoja na mipango mipya ya kuharibu mashua zinazotumiwa na walanguzi wa binadamu wanaowavusha watu baharini.
Share:

Sunday 19 April 2015

Jacob Zuma aapa kukabiliana na ghasia

Rais Jacob Zuma amewatembelea watu walioathirika na ghasia hizo, mauwaji pamoja na kuibwa kwa mali zao huku akiahidi kukabiliana vilivyo na wimbi la mashambulio hayo.

Bwana Zuma alifutilia mbali ziara yake nchini Indonesia, ili kukabiliana na vurumai hizo zilizoanza majuma mawili yaliyopita.Amesema kuwa ghasia hizo ni kinyume na maadili ya taifa la Afrika kusini.

Maafisa zaidi wa polisi wametumwa katika maeneo yenye mashambulio dhidi ya raia wa kigeni nchini Afrika Kusini.

Yamkini watu sita wameuawa na makundi yenye silaha, ambayo yanawalaumu wahamiaji wa kiafrika kwa kuchukua kazi zao nchini Afrika Kusini.

Nchini Harare Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, alilaani ghasia hizo.

Ghasia hizo zilianza baada ya mfalme mmoja wa Kizulu, Goodwill Zwelethini, kusema kuwa raia wa kigeni sharti waondoke Afrika Kusini.

Akiongea katika kambi hiyo iliyoko mjini Durban kiongozi mkuu wa jimbo la Gauteng, David Makhura, anasema kuwa uhasama na ghasia hizo zinazoshuhudiwa, haundamani na uhuru wa miaka mingi ambayo Afrika Kusini ilipigania.





Share:

Vita vya kikabila:Watu 45 wauawa Nigeria


Takriban watu 45 wameuawa kwenye mapambano ya kikabila katika jimbo la Benue, katikati mwa Nigeria.

Polisi wanasema ghasia hizo baina ya jamii za Ologba na Egba, zilizuka kutokana na umiliki wa bwawa la samaki.

Watu zaidi waliuawa pale kundi moja liliposhambulia mazishi ya mtu aliyekufa katika ghasia za awali.

Watu wengi wamelitoroka eneo hilo.

Kumetokea mapambano mengi katika jimbo la Benue katika miaka ya karibuni, lakini mara nyingi ni mizozo baina ya wafugaji na wakulima.
Share:

Dawa ya magugu yauwa watu Nigeria


Shirika la Afya Duniani, WHO, linasema inavoelekea dawa ya kuuwa magugu ndio chanzo cha vifo vya watu 18 vilivyotokea kusini-magharibi mwa Nigeria, bila ya sababu kujulikana.

Katika siku chache zilizopita wakaazi katika jimbo la Ondo wamekufa saa chache baada ya kuhisi macho hayaoni sawasawa na kuumwa na vichwa, Baadae wakazimia.

Msemaji wa WHO alieleza kuwa ukaguzi uliofanywa hadi sasa kutafuta virusi au bacteria haukugundua kitu
Alisema kwa sasa mawazo yao ni kuwa vifo hivyo vilisa-babishwa na dawa ya kuuwa magugu.
Share:

IS watoa tena video ya mauaji


Kundi la wapiganaji wadola ya Kiislam IS limetoa video inayo onyesha mauaji ya zaidi ya watu 30 raia Ethiopia ambao ni Wakristo wakiuawa wengine kwa kuchinjwa katika ufukwe wa bahari na wengine kwa kupigwa risasi kichwani jangwani. Hata hivyo video hiyo inabainisha wazi kwamba kundi hilo la IS linawaua watu hao kwa sababu ni wakristo. Serikali ya Ethipia imesema kuwa inajaribu kufuatilia utambulisho wa utaifa wa watu hao kupitia ubalozi wa Cairo nchini Misri. Hali ya usalama nchini Libya imetetereka tangu kuangushwa kwa utawala wa Kanal Muamar Gadaf, ambapo pia ustawi wa kundi la kigaidi wa wapiganaji wa dola ya Kiislam umekuwa mkubwa.
Share:

Saturday 18 April 2015

Balotelli ndiye aliyebaguliwa zaidi EPL


Mario Balotelli ndiye mchezaji aliyebaguliwa sana katika ligi ya Uingereza ,huku mchezaji huyo akipokea zaidi ya ujumbe 8000 ,asilimia 50 zikiwa ni za kibaguzi.
Takwimu hizo za kushtua zimeripotiwa na Kick it Out ,ambao walibaini kwamba raia huyo wa Itali alilengwa sana katika mitandao ya Twitter huku mshambuliaji wa Arsenal Danny Welbeck akipokea ujumbe 1700 asilimia hamsini zikiwa za kibaguzi.
Mshambuliaji mwenza wa Balotelli katika kilabu ya Liverpool Daniel Sturridge pia alionekana kulengwa katika mitandao ya kijamii baada ya kupokea ujumbe wa 1600 asilimia 60 ikiwa ni ujumbe wenye mwelekeo wa kijinsia.
Utafiti huo pia umebaini kwamba kilabu ya Chelsea ndio kilabu iliobaguliwa zaidi kwa ujumbe 20,000 huku liverpool ikiwa ya pili na ujumbe 19,000 Arsenal ikiwa ya tatu kwa ujumbe 12,000 huku Manchester City na Manchester United zikipokea ujumbe 11,000.
Share:

Obama: mabadiliko ya hewa hayakanushiki

Mwanamme mbele ya moto Colorado, Marekani,  Juni 2013,
Rais Obama ameonya kuwa mabadiliko ya hali ya hewa hayawezi tena kukanushwa au kudharauliwa, na amesema ndio tishio kubwa kabisa linalokabili dunia.
Katika hotuba yake ya kila juma, Rais Obama alisema anataka aweze kuwatazama watoto na wajuukuu wake machoni na kusema kuwa kila liwezalo limefanywa kupambana na msukosuko huo.
Bwana Obama hivi karibuni aliahidi kupunguza sana kiwango cha gesi inayozidisha joto inayotolewa na Marekani - kiwango cha pili kikubwa kabisa duniani - kabla ya mkutano wa viongozi wa dunia mwezi wa Disemba.
Mipango yake inapingwa vikali na wanasiasa wengi wa chama cha Republican ambao wanadai kuwa itaumiza makampuni ya Marekani.
Share:

Saudia kutoa msaada unaohitajika Yemen


Saudi Arabia, inayoongoza mashambulio ya ndege dhidi ya wapiganaji nchini Yemen, imeahidi kutoa idadi ya fedha ambayo Umoja wa Mataifa imesema inahitajika nchini Yemen.
Umoja wa Mataifa uliomba msaada huo wa kimataifa hapo jana, kwa shughuli za dharura za usaidizi nchini Yemen.
Shirika la habari la taifa la Saudi Arabia, linasema kuwa nchi hiyo itatoa dola laki mbili na 74 milioni, kama msaada wa kiutu kwa Wayemeni walioathirika na vita.

Taarifa rasmi ilisema Saudi Arabia inasimama pamoja na ndugu zake wa Yemen.
Oparesheni inayoongozwa na Saudi Arabia, dhidi ya wapiganaji wa Houthi (na askari wanaopigana kwa niaba ya rais wa zamani, Ali Abdullah Saleh, ilianza wiki tatu zilizopita.
(Umoja wa Mataifa unasema mamia ya watu wamekufa, na maelfu ya familia zimekimbia makwao wakati vita vikizidi.)
Share:

Ghasia zasababisha mauaji ya watu Libya


Zaid ya watu kumi wameuawa katika msururu wa ghasia viungani mwa mji mkuu wa Libya Tripoli.
Ghasia hizo kutoka maeneo mawili zilikuwa kati ya wanamgambo walio watiifu kwa serikali ya tripoli na wale walio watiifu kwa serikali inayatombuliwa na jamii ya kimataifa iliopo mashariki mwa taifa hilo.
Milipuko ya mabomu ya mara kwa mara pamoja na milio ya risasi imesika katika eneo la Fashloum ambapo baadhi ya watu wamekamatwa na wapiganaji walio watiifu kwa serikali ya Tripoli.
Share:

Jacob Zuma aahirisha ziara ya Indonesia


Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ameahirisha ziara yake ya ughaibuni kutokana na hali ya ghasia za kibaguzi dhidi ya wageni katika taifa lake.
Alitarajiwa kuhudhuria mkutano nchini Indonesia. Rais Zuma ambaye amekosolewa kwa kushindwa kuonyesha uongozi anatarajiwa kuitembelea kambi ya wakimbizi ya Chatsworth mjini Durban.
Polisi nchini Afrika Kusini wamewaagiza raia kutotuma ujumbe usiothibitishwa kuhusu mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni kwa sababu hatua hiyo inazua hofu.
Polisi wanesema kuwa kuna wasiwasi kuwa uvumi huo unachochea ghasia dhdi ya wahamiaji.Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ameahirisha ziara yake ya ughaibuni kutokana na hali ya ghasia za kibaguzi dhidi ya wageni katika taifa lake.
Alitarajiwa kuhudhuria mkutano nchini Indonesia. Rais Zuma ambaye amekosolewa kwa kushindwa kuonyesha uongozi anatarajiwa kuitembelea kambi ya wakimbizi ya Chatsworth mjini Durban.
Polisi nchini Afrika Kusini wamewaagiza raia kutotuma ujumbe usiothibitishwa kuhusu mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni kwa sababu hatua hiyo inazua hofu.
Polisi wanesema kuwa kuna wasiwasi kuwa uvumi huo unachochea ghasia dhdi ya wahamiaji.

Watu 30 waliakamatwa wakati wa ghasia za usiku kucha mjini Johannesburg.
Biashara kadha zinazomilikiwa na raia wa kigeni ziliharibiwa.
Takriban watu watano wameuawa kwenye mashambulizi yaliyaonza baada mfalme wa kizulu Goodwill Zwelethini kusema kuwa wageni wanahitajka kuondoka Afrika Kusini.
Share:

Watu zaidi ya 30 wauawa Afghanistan


Shambulizi la kujitoa mhanga kwenye mji ulio mashariki mwa Afghanistan wa Jalalabad limewaua watu 33 na kuwajeruhiwa karibu wengine 100.
Ripoti zinasema kuwa shambulizi hilo lilitokea karibu na benki ambapo wafanyikazi wa serikali wanalipwa misharaha yao.
Maafisa wanasema kuwa mtu aliyeendesha shambulizi hilo alikuwa na pikipiki.
Kulitokea shambulizi la pili karibu na madhabahu mjini Jalalabad lakini haijulikani kama kulikuwa na madhara yoyote.
Hakuna kundi lililokiri kuhusika, lakini mji wa Jalalabad umekuwa ukilengwa kila mara na kundi la Taliban.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.