Wednesday 31 December 2014

Aua watu 8 naye ajiua Canada.



Polisi Nchini Canada wanasema kuwa watu 8 wameuawa kwa kupigwa risasi na mtu mmoja ambaye naye alijiuua katika kile kilichotajwa kama mfululizo wa unyanyasaji wa majumbani.
Siku ya jumatatu polisi walikuta mwili wa mwanamke mmoja katika mji wa Edmonton eneo magharibi mwa jimbo la Alberta.
Polisi pia waliikuta miili mingine ambayo ni ya wanawake watatu,wanaume wawili na watoto wawili wakati ilipokuwa ikishughulikia taarifa ya mtu huyo aliyejiua katika eneo jingine kwenye mji huo.
Muuaji huyo alijiua mwenyewe kwenye mgahawa mmoja katika eneo la kaskazini mwa Edmonton.
Polisi bado haijatoa majina wala uhusiano wa waathirika.
Share:

Miili 40 yaopolewa baharini.


Kufuatia kupotea kwa ndege ya shirika la ndege la Asia ndege namba QZ8501At ,miili arobaini imeopolewa kutoka baharini katika utafutaji wa mabaki ya ndege hiyo na utafutaji unaendelea.
Miili hiyo ilionekana ikielelea karibu na taka za bahari pwani ya Indonesia,eneo la Borneo moja ya eneo la utafutaji mabaki ya ndege hiyo.Na taarifa kutoka serikali ya Indonesia zimethibitisha kwamba miili hiyo inatoka katika ndege iliyopotea.
Ndege hiyo aina ya Airbus A320-200,ilikuwa imebeba abiria mia moja na sitini na wawili ikitokea Surabaya nchini Indonesia kuelekea Singapore,ilipotea siku ya Jumapili.
Utafutaji wa mabaki ya ndege hiyo umeingia katika siku ya tatu,na eneo la utafutaji limeongezwa na kufikia kanda kumi na tatu hii inashirikisha nchi kavu na baharini.
Wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliooneshwa wazi kwenye runinga ya taifa la Indonesia picha za taka bahari zilioneshwa zikiwa zimechanganyika na mabaki ya miili ya abiria ikielea majini.
Ndugu wa mabaki hayo walipoona picha hizo walipigwa na fadhaa kuu na walionekana kushtushwa na picha hizo.Baadaye askari wa majini nchini Indonesia wameeleza kuwa miili hiyo arobaini iliopolewa na meli ya kivita .
Mkurugenzi mtendaji wa AirAsia Fernandes ali ingia katika mtandao wa twitter na kueleza huzuni yake kwa ndugu waliopoteza ndugu zao katika ndege QZ 8501. Na kwa niaba ya shirika la ndege la AirAsia ametuma salamu za rambi rambi .
Utafutaji miili na mabaki ya ndege hiyo unashirikisha meli thelathini,ndege kumi na tano na chopa saba.
Share:

Boko haram wavamia kijiji na kuua 15.


Wapiganaji wanaodhaniwa kuwa ni Boko Haram wamevamia kijiji Kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuua watu takriban 15.
Shambulizi hilo lilitokea katika kijiji cha Kautikari katika jimbo la Borno, pale washukiwa wa Boko Haram walipowasili kijijini humo kwa magari yenye silaha, wakilenga askari wa ulinzi wa jadi wa mji huo.
Kijiji hicho kipo karibu na Chibok mahali ambapo kundi la Boko Haram, liliwateka nyara wasichana wa shule zaidi ya mia mbili mwezi Aprili mwaka huu.
Zaidi ya watu elfu kumi wameuwawa Nchini Nigeria na Boko Haram mwaka huu pekee.
Share:

Rais Jammeh:'Bado niko mamlakani.


Rais wa Gambia amesema kuwa bado analiongoza taifa hilo la Afrika magharibi baada ya vikosi vyake vya usalama kutibua jaribio la mapinduzi.
Yahya Jammeh amesema kuwa kamanda mmoja wa jeshi wa zamani alijaribu kuchukua udhibiti wa taifa hilo alipokuwa ziarani Ufaransa.
Hatahivyo hajulikani aliko.Milio mikali ya riasi ilizuka karibu na makao ya rais katika mji mkuu.
Bwana Jammeh alichukua mamlaka kupitia mapinduzi mwaka 1994 na wapinzani wake wamekuwa wakimkosoa kwa uongozi wake wa kiimla.
Duru za kidiplomasia na zile za kijeshi zinasema kuwa wanajeshi kutoka kwa jeshi la ulinzi wa rais wanadaiwa kufanya shambulizi hilo katika makao ya rais mjini Banjul mapema siku ya jummane.
Serikali imekana kwamba kulikuwa na jaribio la mapinduzi katika taarifa iliotangazwa katika radio ya taifa.
Hatahivyo,bwana Jammeh baadaye alikiri kuhusu shambulizi hilo na kusema kuwa wanajeshi waaminifu wa Lamin Sanneh aliyemtaja kama mwenye aibu walivamia mji mkuu wa Gambia kutoka Senegal katika jaribio la kutaka kuipindua serikali yake.
Amesema kuwa wavamizi hao hatahivyo walikabiliwa na vikosi vya usalama na kuwaua wanne kati yao huku wengine wanne zaidi wakikamatwa.
Share:

MTUHUMIWA ALIYEJARIBU KUTOROKA MAHAKAMA YA KISUTU APIGWA RISASI.


























Maofisa wa Polisi na Magereza wakiangalia mwili wa mtu aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya dawa za kulevya na kupigwa risasi wakati akijaribu kutoroka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam saa 2:00 asubuhi ya leo.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kinapasha kuwa mwili wa marehemu huyo ambaye bado jina lake halijatambulika umepelekwa kuhifadhiwa Hospitali ya Muhimbili. Picha kwa hisani ya Father Kidevu.
Share:

Monday 29 December 2014

Watoto wazuiwa kuitembelea Israel.


Kundi la Hamas limewazuia kundi la watoto kutoka ukanda wa Gaza wengi wakiwa ni wale waliowapoteza wazazi kwenye vita vya hivi majuzi kati ya Hamas na Israel waliotaka kuitembelea Israeli katika ziara ambayo waandalizi wake wanasema ililenga kuleta uwiano. Msemaji wa Hamas anasema kuwa ziara hiyo ilizuiwa ili kulinda tamaduni ya watu wa ukanda wa Gaza.
Wapiganaji wa kundi la Hamas wamezuia kundi la watoto kutoka Gaza wengi wao wakiwa ni wale ambao wazazi wao waliuawa katika vita.
Wanaharakati wa masuala ya Amani waliowasaidia watoto hao kufanya safari hiyo wamesema kuwa mamlaka ya Gaza waliruhusu watoto hao kufanya safari yao lakini wakabadili msimamo wao baadae.
Share:

Filamu ya Interview yatikisa mitandaoni.


Kampuni ya Sony Picutues inasema kuwa - the interview - ambayo ni filamu yenye utata ya dhihaka kuhusu njama ya kumuua kiongozi wa korea kasakzini Kim Jong un imekuwa yenye mafanikio zaidi mtandaoni.
Kampuni hiyo inasema kuwa filamu hiyo imenunuliwa na pia kukodishwa zaidi ya mara milioni mbili kwa muda wa siku nne tangu iwekwe kwenye mitandao.
Sony iliahirisha mpango wake wa filamu baada ya komputa za kampuni hiyo kudaiwa kuingiliwa na wadukuzi,huku Korea Kaskazini ikihusishwa katika udukuzi huo.
Share:

Upepo wakwamisha Uokoaji Meli iliyozama.


Waokoaji wamekuwa wakipambana na upepo mkali pamoja na mawimbi ya bahari gizani kuwakoa karibu abiria 300 ambao wamekwama ndani ya ferry moja ya Italia iliyokuwa imeshika moto kwenye bahari ya Adriatic.
Maofisa nchini Italia wanasema kuwa oparesheni ya uokoaji itandelea.Hadi sasa watu 190 wamekolewa kutoka kwa ferry hiyo.
Share:

Abiria miamoja wakwama:ATC


Zaidi ya abiria mia moja wa ndege ya ATC wamekwama nchini Tanzania, baada ya safari zao kuarishwa. Wengi wao wakielekea nchini Comoros na wengine wakiwa katika safari za ndani, kuelekea Mtwara na Kigoma wamekwama kwa siku mbili mjini Dar es salaam.
Abiria hao imebidi wakodiwe hoteli ilivyo ada wakisubiri muafaka wa namna watakavyosafiri kuelekea Comoro. Sharifu Hashim, Balozi wa heshima wa Comoro huko Chicago nchini Marekani, anasema mambo yake mengi yamekwama kutokana na tukio hili na hajapata uhakika ataondoka lini
Zenabal Mwarabu yeye hofu yake ni kwa namna gani ataweza kuiwahi ndege aliyokuwa aunganishe Kisiwani Comoro kuelekea katika kisiwa kingine cha Rarinyo.
Msawi Seifu anasema ijapokuwa tatizo hili limetokea lakini Air Tanzania ni mkombozi kwa wana Comoro….Lily Fungamtama, Mkuu wa Kitengo cha Biashara amesema tayari Air Tanzania inashughulika kuhakikisha abiria wote wanasafiri mapema kesho .
Sikukuu za mwisho wa mwaka ndilo tatizo la kukwama kwa abiria hao,kwani marubani hawajarejea kazini tangu walipoondoka, na walitegemewa kurejea kazini tarehe 27 mwezi huu, baada ya sherehe za Christimas, lakini haikuwa hivyo na kusababisha sintofahamu hiyo.
Share:

Sunday 28 December 2014

Feri ya abiria 460 yashika moto Ugiriki.


Amri imetolewa ya kuwataka abiria kuondolewa kwa ferry iliyo na karibu abiria 460 ambayo ilishika moto ilipokuwa safarini kutoka nchini Ugiriki kwenda Italia.
Abiria waliokuwa kwneye ferry hiyo walipiga simu kwa vituo vya runinga nchini Ugiriki wakisema kuwa mawimbi makali na upepo unatatiza shughuli za uokoaji.
Maafisa wa ulinzi wa pwani nchini Ugiriki wamesema kuwa ferry hiyo ya Norman Atlantic ilikuwa umbali wa kilomita 30 kutoka kisiwa cha Othonoi wakati walipotuma ujumbe .
Vyombo vya habari nchini Italia vinasema kuwa moto ulianzia kwenye eneo la kuegesha magari.
Share:

Mashindano ya Miss Tanzania yafungwa..


Serikali ya Tanzania imeyafungia kwa miaka miwili mashindano ya Miss Tanzania baada ya waandalizi kudaiwa kukiuka taratibu na kanuni.
Mashindano hayo yaliofunguliwa mwaka 1994 yamedaiwa kuwa na upendeleo mbali na rushwa kulingana na malalamishi yaliotolewa na wananchi pamoja na washiriki.
Kwa mujibu wa kaimu katibu mtendaji wa Baraza la Sanaa nchini Tanzania Basata , Godfrey Mngereza,kamati ya miss Tanzania ilikiuka kanuni na taratibu zinazoongoza mashindano hayo.
Alisema bwana Mgereza:"Ni kweli kwamba tumeifungia Miss Tanzania kwa miaka miwili, lakini haya si maazimio ya tathmini iliyofanyika mapema mwezi huu, bali kulikuwa na vikao mbalimbali vilivyofanyika na si kimoja, ni uamuzi mgumu ambao umekuja kutokana na sababu maalumu,"
Imedaiwa kuwa mashindano yaliyofanyika Desemba 12, mwaka huu hayakufikia uamuzi, bali vikao mbalimbali vilivyoendeshwa na wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo kwa kushirikiana na Basata ndivyo vilivyofikia hatua hiyo ili kutoa nafasi kwa waandaalizi kujipanga upya.
Baadhi ya maswala yaliobainika ni kwamba baadhi ya warembo walidaiwa kutumiwa kingono.Vilevile hakuna utaratibu wa kuwasajili warembo hao uliofuatwa kuanzia vitongojini hadi kufikia fainali.
Mngereza alisema baraza limegundua kuwa baadhi ya washiriki walichaguliwa kwa upendeleo bila ya kuwa na sifa zilizohitajika
Share:

Indonesia yasitisha utafutaji wa Airasia.


Indonesia imesitisha utafutaji wa ndege ya AirAsia hadi kesho iliopotea na takriban abiria 160 waliokuwa wakielekea Singapore kutoka mji wa Surabaya nchini Indonesia.
Ndege za kijeshi kutoka indonesia na singapore zilikuwa zikiisaka ndege hiyo kusini magharibi mwa pwani ya Borneo ambapo ndege hiyo ilitoweka.
Takriban abiria 162 walikuwa wakiabiri ndege hiyo aina ya Airbus 320 wengi wao wakiwa raia wa Indonesia.

Rubani wa chombo hicho anadaiwa kutaka kubadilisha njia ili kuepuka kimbunga lakini hakuomba usaidizi wowote.
Baadhi ya meli katika eneo hilo zinaendelea kuitafuta ndege hiyo,licha ya hali mbaya ya hali ya anga
Familia na marafiki wa waathiriwa wamekongamana nchini Singapore na uwanje wa ndege wa surabaya wakingojea habari kuhusu ndege hiyo.
Share:

Saturday 27 December 2014

Tibaijuka:Nitatetea kiti changu.


Siku kadhaa tu baada ya rais Kikwete kumfuta kazi Anne Tibaijuka kama waziri wa ardhi,nyumba na makao ,kiongozi huyo amewaambia wakaazi wa bunge lake kwamba hawakumchagua kama waziri bali kama mwakilishi wao wa bunge, kulingana na gazeti la The citizen nchini Tanzania.
Tibaijuka alipigwa kalamu kutokana na maadili yake kufuatia kashfa ya akaunti ya tageta escrow ambapo alipokea sh.billioni 1.6.'' Mungu anayetoa ndiye aliyechukua jina la mungu libarikiwe alisema tibaijuka akimaanisha kuwa yule aliyempa kiti hicho cha uwaziri ndiye aliyekichukua.
Katika kile alichoelezea kama harakati za kukitetea kiti chake katika uchaguzi wa 2015,Tibaijuka aliwaonya wapinzani wake wa kisiasa kwamba yeye ndiyo chagua bora la wapiga kura.
Kulingana na The Citizen kiongozi huyo aliwashukuru wapiga kura wa eneo bunge lake kwa kumchagua kuwa mbunge,wadhfa aliodai kumfungulia milango ya kupewa uwaziri.
''Lazima muelewe kwamba ninyi mulinipigia kura mimi ili niwahudumie bungeni na sio kama waziri,kwa hivyo yaliotokea si ndwele tugange yajayo kwa kuwa tayari kashfa ya escrow imezikwa'',aliwaambia wakaazi wa Muleba.
Hatahivyo bi Tibaijuka amesema kuwa yuko tayari kufanya kazi na viongozi wa upinzani waliochaguliwa katika uchaguzi wa madiwani wa hivi karibuni.
Share:

Korea Kazkazini yamtusi Obama.


Tume ya taifa ya ulinzi nchini Korea Kaskazini inasema kuwa Marekani inavuruga mifumo ya mitandao ya nchi hiyo huku ikimfananisha rais wa marekani Barack obama na tumbili wa misitu ya tropiki mbali na kumshutumu kwa kuhusika katika kuonyeshwa kwa filamu yenye utata inayojulikana kama The Interview.

Filamu hiyo iliyotengenezwa na kampuni ya Sony ambayo ni ya ucheshi inayoonyesha kuuawa kwa kiongozi wa korea kaskazini Kim Jong Un.
Korea kaskazini imekana kuhusika kwenye uhalifu wa mtandao dhidi ya kampuni ya Sony uliosababisha kampuni hiyo kusitisha maonyesho ya filamu hiyo.
Share:

Wanaume waliooana wapunguziwa hukumu.


Mahakama moja ya Misri imepunguza hukumu ya watu wanane waliodaiwa kushiriki katika ndoa ya watu wa jinsia moja kutoka miaka mitatu hadi mwaka mmoja.
Mwezi Uliopita ,wanane hao walipatikana na hatia ya kuchochea uasherati.
Walishtakiwa baada ya kanda moja ya video kusambaa katika mitandao ikiwaonyesha wakisherehekea katika boti moja lililokuwa mto Nile huku wanaume wawili wakionekana wakivalishana pete na kukumbatiana.

Watu hao baadaye walikataa kwamba ilikuwa harusi ya watu wa jinsia moja.
Ushoga ni kinyume na utamaduni wa Misri ,ijapokuwa si kinyume na sheria.
Wanaharakati wa kupigania haki za kibinaadamu wanasema kuwa kampeni dhidi ya mashoga imeimarishwa katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni nchini Misri.
Share:

Kiongozi wa Al-Shabaab akamatwa.


Maafisa nchini Somali wanasema kuwa kiongozi mkuu wa kundi la wapiganaji wa Alshabaab amekamatwa karibu na mji mmoja karibu na mpaka wa Kenya na Somali.
Kamishna wa Wilaya ya El Wak mjini Gedo ameiambia BBC Somalia kwamba vikosi vya usalama vilimkamata Zakariya Ismail Ahmed Hersi katika maficho yake ndani ya nyumba moja baada ya kupashwa habari.
Mwaka 2012 Marekani ilitoa zawadi ya dola millioni 3 kwa yeyote yule ambaye angeweza kutoa habari za Hersi.
Kundi la Al Shabaab limejiondoa kutoka miji kadhaa nchini Somalia tangu uzinduzi wa mashambulizi makali dhidi ya kundi hilo yanayotekelezwa na vikosi vya AMISOM vikishirikiana na wanajeshi wa serikali ya Somalia.
Bwana Hersi alikuwa kiongozi wa kundi la Alshabaab upande wa Amniyat.
Mapema mwaka huu alikosana na kiongozi wa kundi hilo Ahmed Abdi Godane ambaye aliuawa katika mashambulizi ya Marekani mnamo mwezi Septemba.
Share:

Monday 22 December 2014

Ndoto ya mjasiriamali


Hii ni Makala ya mwisho katika mfululizo wa ndoto ya Africa Makala ambayo ilikuwa ikiwaangazia wajasiriamali wa bara hili kwa muda wa wiki nane sasa.kila Makala ilikuwa na changamoto zake mwanzoni mwa biashara,hivyo muda wote wa mfululizo huu,ulikuwa na fursa ya kujifunza namna ya kuifikia ndoto yako, ama ndoto zao,na kama walifaulu,na inawezekanaje kwa wengine pia.
Binti huyu alionja ladha ya tasnia ya vyombo vya habari akiwa na umri mdogo wakati huo akimsindikiza babake.hata hivyo binti huyo amehitimu masomo ya sheria Kemi Adetiba baada ya muda mfupi alijitosa katika burudani na kuwika nchini mwake Nigeria nan chi zote za ukanda wa Jangwa la Sahara.
Leo hii tunapomzungumzi Adea Kemi, amekwaa tuzo ya uongozaji,mzalishaji na upigaji picha bora mjini Lagos, Nigeria Kemi anamiliki kampuni ya masuala ya filamu iitwayo K-Alpha Innovations. Na hapa anatumegea kidogo siri ya mafanikio katika biashara ya tasnia ya burudani.
Tuanze na suala ambalo liko katika vichwa vya watu wengi.ni kawaida kusikia katika tasnia ya burudani kinachogomba ni UNAMJUA NANI , wengine wana dhana kuwa ukimjua mtu ndio umefanikiwa na kumjua mtu hii inafanya kazi hata kama huna muingiliano na watu wengi.sio kweli.kama biashara zingine zote,inategemea juhudi zako binafsi changanya na uvumilivu.
Tuanze kuzitazama njia za mafanikio na kuitendea haki ndoto yako.

HATUA YA 1
Andaa mpango kazi amba unaainisha misingi ya awali kampuni ya kampuni ya kuandaa picha za video,ujuzi ulionao kama mzalishaji (producer) na pia mgango wa mauzo.Ambatanisha na orodha ya vitendea kazi unavyomiliki ambavyo unajua kuvitumia pia na bajeti ya kununua mifumo ya utendaji kazi kama ya uhariri wa picha za video,mashine za kurudufu kazi zako na taa.

HATUA YA 2
Andaa vyanzo vya mapato.pata orodha ya makato ya kodi mapema.

HATUA YA 3
Nunua vifaa vya kazi. Mzalishaji wa picha za video anapaswa kuwa na camera mbili hadi tatu ,microphone isotumia waya ,taa,komputa ya uhariri ambayo imewekewa mfumo wa final cut , ama adobe primier na lenzi tofauti tofauti kwa muujibu wa kamera ulizonazo.pia itategemea na vifaa ulivyonavyo kampuni ya uzalishaji picha za video inakadiriwa kuanza na mtaji wa dola za kimarekani 15,000 kwa kuwa na vyombo hitajika kwa ujumla wake .

HATUA YA 4
Tayarisha alama ya utambulisho ya kampuni yako,businesscard na mtandao ambao utakuwa ukionesha kazi zako ulizozifanya za video.

HATUA YA 5
Andaa kazi yako ya video yenye urefu wa dakika tatu hadi tano.tumia kamera nzuri lakini pia kuwa mbunifu katika namna ya upigaji picha zako kwa jicho la tofauti,nenda kapige picha nje ya eneo lako la kazi ili uongeze uhifadhi maktaba.

HATUA YA 6
Buni bei za bidhaa zako.hii ina maana utaanza kutoza bei kwa huduma kuanzi saa moja ama kwa bidhaa.toa huduma ya kazi iliyokamilika,ikiwezekana fanya video ya familia ya mteja na kuzirudufu.

HATUA YA SABA
Weka mfumo wa utembezaji kazi zako za video gurudumu litakalo muwezesha mteja kupitia kazi zako bila usumbufu ,lazima uwe na mtandao na wateja wako, na uwasambazie kadi zenye maelezo ya kazi zako na watakavyokufikia yakiwemo mawasiliano.picha,michezo ya kuigiza,kwa wapenzi wa huduma zako kwa mtindo wa DVD.

Share:

Kwa wivu,Mume amjeruhi mkewe kwa shoka.






















Mama mwenye watoto watatu anapata matibabu hospitalini nchini Malaysia baada ya mumewe kuvamia mikono yake na miguu nakumcharanga kwa shoka la kucharangia nyama,na baadaye mwanamume huyo kujinyonga .
Mama huyo anatajwa kama K Menaga,amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Kluang upande wa kusini mwa jimbo la Johor baada ya shambulio hilo hatari lililotokea mapema mwezi huu.
Ingawa taarifa kutoka hospitalini hapo zinaarifu kuwa mama huyo ameshatolewa katika chumba cha wagonjwa mahututi baada ya hali yake kuendelea vyema,na amelazwa katika wodi ya wagonjwa wa kawaida.
Inasemekana mume wa mwanamke huyo ana umri wa miaka 47 na asiye na kazi maalumu baada ya kumcharanga mkewe na kuona damu tele imtokayo mkewe, aliamua kunywa sumu na baadaye kujinyonga .Mke wa bwana huyo alikuwa akifanya kazi ya kuosha vyombo huko Singapore kwa muda wa miaka 15 sasa .
Majirani wanaeleza kuwa familia ya mwanamke huyo ilikuwa inaishi kwa kutegemea mshahara wa mwanamke huyo, wakati mumewe alikuwa hana chanzo cha mapato.Na mwanamke huyo alikuwa na utaratibu wa kurejea nyumbani kwake mara moja kwa mwezi kuwaona watoto wake akiwemo mama mkwe wake.
Mashuhuda hao wanasema kwamba,kila mwanamke huyo arejeapo kutoka kibaruani, mumewe alikuwa akimshutumu kwa kukosa uaminifu na kumshutumu kuwa ana bwana ambaye humrejesha kutoka Singapore,nao polisi wameeleza kuwa matokeo ya tukio hilo ni wivu wa mwanamume huyo,na baada ya tukio hilo kaka wa mwanamke huyo anaeleza kuwa watoto wa mwanamke huyo wamechukuliwa na jamaa zao kwa matunzo.
Share:

Rais Kikwete azungumza na wazee.


Rais Jakaya Kikwete ametengua nafasi ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka kupitia hotuba aliyotoa kuzungumzia kashfa ya upotevu wa fedha kutoka akaunti ya Tegeta Escrow.
Hatua hiyo imechukuliwa na Rais Kikwete mbele ya wazee wa Dar Es Salaam aliokuwa akiongea nao na matangazo kurushwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa na vyombo vingine.
Uchunguzi uliofanywa na kamati ya hesabu za umma ya Tanzania (PAC), ilidai kuwa Profesa Tibaijuka ni mmoja wa watu walionufaika kinyume cha sheria kwa kupata fedha zilizotoka katika akauti hiyo iliyofunguliwa kutunza fedha kusubiri ufumbuzi wa mgogoro wa kibiashara kati ya kampuni ya kusambaza umeme TANESCO na kampuni binafsi ya kuzalisha umeme ya IPTL.
Siku chache zilizopita Profesa Tibaijuja aliitisha mkutano na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam kubainisha kuwa hakuwa akikusudia kujiuzulu kutokana na tuhuma zilizokuwa zikimkabili.
Hata hivyo Rais Kikwete hakutangaza kuwachukulia hatua watumishi wengine waliodaiwa kuhusika na tuhuma hiyo kwa maelezo kuwa uchunguzi zaidi unatakiwa kwa kila mtuhumiwa.
Kumekuwa na ubishi mkubwa kujadili endapo fedha ambazo ni mabilioni zilizochukuliwa zilikuwa za umma au la. Na hata Rais Kikwete amesema maelezo aliyopewa na wataalam yanaonyesha hazikuwa mali ya TANESCO.
Share:

Sunday 21 December 2014

Korea kazkazini sasa yaionya Marekani.


Korea Kazkazini sasa inataka uchunguzi wa pamoja na Marekani kufanywa kuhusu wizi wa mtandaoni uliosababisha kampuni ya Sony Pictures kuahirisha maonyesho ya filamu ya ucheshi inayomdhihaki raia wa Korea kazkazini Kim Jong-un.
Imesema kuwa shtuma hizo za shirika la ujasusi nchini marekani FBI kwamba Pyongyang ndio iliotekeleza uovu huo inaliharibia jina taiafa hilo.
Chombo rasmi cha habari nchini humo kilimnukuu waziri wa maswala ya kigeni ambaye jina lake halikutajwa akisema kuwa taifa lake litachukua hatua kali iwapo Marekani itakataa ombi hilo.
Taifa la Korea Kazkazini hapo awali lilikuwa limeunga mkono uvamizi huo wa kampuni ya Sony likisema kuwa ni kitendo cha haki.
Rais Obama amesema kuwa Marekani itajibu shambulizi hilo la mtandaoni wakati utakapowadia.
Share:

Wanaume 28 washtakiwa kwa uasherati..


Watu 28 wamefikishwa mahakamani mjini Cairo Misri kutokana na mashtaka ya uasherati katika kile kinachoonekana kama ishara za kampeni dhidi ya ushoga.
Baadhi ya washtakiwa walikuwa wakilia baada ya kufikishwa mahakamani wakiwa wamefungwa pingu.
Mmoja alilalama kwamba yeye na wafungwa wenzake walipigwa na polisi.
Wanaume hao walikamatwa mapema mwezi huu katika kidimbwi cha kuoga kwa jina hammam mjini Cairo.
Wanahabari wa chombo kimoja cha habari walichukua filamu ya uvamizi huo wa polisi.
Miezi miwili iliopita,watu wanane walifungwa miaka 3 jela baada ya kunaswa katika kanda ya video ambayo wakuu wa mashtaka wanasema ilionyesha wakifanya harusi ya watu wa jinsia moja mjini Cairo.
Share:

Kura zaanza kuhesabiwa Liberia.


Kura zimeanza kuhesabiwa nchini Liberia ambapo uchaguzi wa Useneta umefanyika licha ya mlipuko wa ebola.
Idadi ya watu waliojitokeza kupiga kura ilikuwa chini huku watu wengi wakisalia majumbani mwao kwa hofu ya maambukizi ya ugonjwa huo.
Viwango vya joto vya wapiga kura vilichukuliwa ,huku wakiambiwa kusimama kwa umbali wa mita moja mmoja baada ya mwengine na kuosha mikono yao kabla ya kupiga kura na hata baada ya kushiriki katika shughuli hiyo.
Matokeo ya mapema yanatarajiwa baadaye siku ya jumapili.
katika mji mkuu wa Monrovia ,mwana wa rais Ellen Johnson Sirleaf anakabiliana na mwanasoka mkongwe George Weah ambaye aliwania urais mwaka 2005.
Share:

Somalia yawakataa wanajeshi wa S.Leone.


Wanajeshi wa kulinda amani kutoka Sierra Leone wameondoka nchini Somali na hakuna wanajeshi wengine wa taifa hilo watakaochukua mahala pao kufuatia wasiwasi wa ugonjwa wa Ebola.
Umoja wa Afrika una mpango wa kutafuta wanajeshi wengine kutoka mataifa yenye wanajeshi wake nchini humo.
Zaidi ya wanajeshi 800 wa Sierra Leone walio kusini mwa bandari ya Kismayu wameondoka kuelekea nyumbani.
Walitarajiwa kuondoka mapema lakini safari yao ikacheleweshwa kwa zaidi ya miezi sita baada ya mmoja wa wanajeshi wa Sierra Leone waliotarajiwa kuchukua mahala pao kupatikana na ebola
Share:

Thursday 18 December 2014

Gari linaloweza kujiegesha kwa kutumia saa.
























>>>> SOMA ZAIDI HAPA<<<<
Share:

Purukushani bungeni nchini Kenya.


Wabunge wa Kenya wametofautiana vikali bungeni na kuvuana mashati huku wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswada tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.
Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani walipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.

Mwenyekiti wa kamati ya usalama wa bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyaja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo wakisema 'bado mapambano.'
Spika wa bunge Justin Muturi wakati mmoja aliamuru walinzi wa bunge kuwaondoa baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.
Mswada huo ambao umewasilishwa bunge kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.


Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.
Pia ikiwa mswada huo utapistihwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa faini ya hadili shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.
Mswada huu umetolewa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab wakilalamika na kutaka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia
Rais Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikzo kuimarisha usalama wa tangui mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Share:

JK:Akatiza ziara ya Mizengo Pinda.... Source BBC


Waziri Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli maalumu.
Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu, ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji, amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow.
Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.
Katika barua yake ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa.

Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya B2B pamoja na kutembelea maeneo mengine lakini ziara hiyo imefutwa na badala yake anaondoka asubuhi kurudi nyumbani.
Baadaye leo Pinda alitakiwa kwenda Doha, Qatar kwa ziara kama hiyo hadi Desemba 23.
Baada ya kukamilisha jukumu aliloitiwa, Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea Falme za Kiarabu Jumamosi kuendelea na ziara yake.
Share:

M'marekani ahusishwa na fedha bandia UG.


Mamlaka ya Marekani imemkamata raia mmoja wa taifa hilo kwa kuongoza kashfa ya kimataifa ya fedha bandia,BBC imebaini.
Ryan Gustafson mwenye umri wa miaka 27 alishtakiwa kwa njama ya kuwa na fedha bandia nje ya Marekani baada ya fedha hizo kutumika katika biashara tofauti za Marekani.
Shirika la kijasusi la Marekani lilifuatilia fedha hizo hadi Kampala ,ambapo walibaini kuna njama ya fedha hizo bandia inayotengeza yuro,rupee pamoja na fedha tofauti za nchi za Afrika.
Mshukiwa huyo anakabiliwa na kifungo cha miaka 25 gerezani.

Maajenti wa FBI waligundua fedha hizo zinatumwa kutoka Uganda.
Alama ya kidole kutoka kwa kifurushi cha fedha hizo ilitoa maelezo ya fedha hizo kutoka kwa bwana Gustafson,raia wa Marekani.
Shirika hilo la maafisa wa ujasusi lilishirikiana na mamlaka ya Uganda ili kuanzisha uchunguzi wa siri kwa lengo la kununua fedha hizo kutoka kwa mshukiwa huyo.
Alikamatwa ,na msako kufanywa katika nyumba yake ambapo fedha bandia za Uganda,Francs za Congo,Cedis za Ghana,Rupees za India na Yuros pamoja na vifaa vya kutengeza fedha bandia.
Mamlaka ya Marekani inakisia kwamba washukiwa hao waliingiza takriban dola millioni 2 fedha bandia katika soko.
Share:

Wednesday 17 December 2014

Kijana mzungu abadilika kuwa m'masai..


Aliposafiri nchini Kenya mwaka 2011 kama mtu aliyejitolea katika shirika moja lisilo la kiserikali ,uamuzi wa kuwa kijana wa kimasai wa Ilchamus lilikuwa wazo la mwisho katika akili ya Max Roing,ambaye ni raia wa Sweden.
Lakini miaka mitatu baadaye ,Max mwenye umri wa miaka 25 amependa sana utamaduni wa watu hao walio wachache katika fukwe za ziwa Baringo.
Max pia alikuwa miongoni mwa vijana 5,000 wa Ilchamus katika kaunti ya Baringo waliotawazwa kuwa wanaume kamili baada ya kupashwa tohara.

''Nilikuja nchini Kenya kama mtalii na pia kusaidia kuhifadhi mazingira kupitia upandaji wa miti katika kaunti ya kajiado''bwana Roing aliliambia gazeti la Nation nchini Kenya baada ya kuhitimu.
Kwa sasa anafuata mila yake mpya inayoshirikisha mavazi yanayovaliwa pamoja na shuka nyeusi,simi iliofungwa katika ukanda wake wa rangi ya hudhurungi,viatu vyeusi na nguo iliorembeshwa kwa shanga.
Hafla hiyo ya kuhitimu imemfanya kuingia katika umri wa Ilmeng'ati.
''Mimi ni Max Lemeyan Le Kachuma kutoka kabila la Ilchamus na ukoo unaojiita Iltoimai''alisema jina lake huku akinywa maziwa yalio chungu katika kikombe.
Share:

Ebola:Msako wa wagonjwa kufanywa S.Leone


Rais wa Sierra Leone Ernest Bai Koroma ametaka kufanyika kwa msako wa nyumba hadi nyumba kwa waathiriwa wa ugonjwa wa ebola nchini humo

Rais Ernest Bai Koroma wa Sierra Leone amesema kuwa msako wa nyumba kwa nyumba unaanza kote nchini humo kuwatambua watu walio na ugonjwa hatari wa ebola.
Aidha, Rais huyo amepiga marufuku biashara siku ya Jumapili.....  >>>>INGIA HAPA<<<<


Share:

Mwanasheria Mkuu wa Tanzania ajiuzulu.



Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Jaji Frederick Werema amejiuzulu nafasi yake hiyo kuanzia jana, Jumanne, kufuatia sakata.......  >>>>INGIA HAPA<<<<
Share:

Pakistan yaomboleza mauaji ya watoto



Raia nchini Pakistan wanaadhimisha siku tatu za maombolezo kuwakumbuka zaidi ya watu 140 waliouwawa,karibia wote wakiwa...>>>>INGIA HAPA<<<<
Share:

Tuesday 16 December 2014

Tahadhari:'Hatari za urembo bandia'.

Kilio cha uchungu baada ya upasuaji wa pua ili kunyooshwa
Huwezi kuepuka matangazo ya mauzo kila utembeapo katika Mji wa Seoul,utapata wito wa kukutaka ubadilishe umbo kwa njia ya upasuaji wa kuongeza urembo bandia.
Katika mtaa wa ukwasi wa Gangnam,kila ukuta una ishara ya kukuelekeza sehemu ya upasuaji wa aina hii
Kwenye treni na mitaani,unaelezewa kuwa ''unaweza kurudisha uchanga usoni mwako.''kuweka ama kuondoa mikunjo usoni'' inapendekezwa kufanyiwa-''upasuaji wa matiti'',''kuzuia kuzeeka'' ''kubadili kope za macho''''kupunguza nyama na ngozi inayolegea mwilini''..........>>>INGIA HAPA<<<
Share:

Mtoto amuibia nyanyake na kuwashangaza wengi.


Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 11 aliiba maelfu ya dola kutoka kwa nyanyake na kisha kukodi taxi kumpeleka eneo la mbali kukutana na kijana mwenye umri wa miaka 16 ambaye walikuwa wakiongea naye tu kupitia mtandao wa Internet.
Wawili hao hawajawahi kuonana hata siku moja.
Msichana huyo Alexis Waller yuko salama na bukheri wa afya na hatakabiliwa na kesi yoyote baada ya kitendo chake ambacho kimewashangaza wengi.
Maafisa wanasema Waller aliiba dola elfu kumi kutoka kwa chumba cha nyanyake katika mji wa Bryant, jimbo la Arkansas.
Baada ya kitendo chake cha wizi, msichana huyo alikodisha taxi na kumtaka dereva kumpeleka kwa kijana huyo katika jimbo la Florida.
"nilisema nitaka kwenda mjini Jacksonville, Florida," Waller aliambia shirika la habari la KARK. "kijana huyo aliniuliza kama nina pesa na nikamwambia ndio. ''
Gharama ya safari yake ilikuwa dola 1,300.
Jarida la Arkansas Democrat-Gazette linasema kuwa Waller alikuwa tayari amesafiri umbali wa maili 500 kuelekea kwa kijana huyo lakini polisi waliweza kuwasiliana na dereva wa taxi hio na kuwafuata.
Wazazi wake walisema Waller aliwakasirisha sana lakini ni afunei kwao kwani mtoto wao aliweza kurejea nyumbani
Share:

Alipanda kreni kumposa mpenzi.Yalomkuta?


Mwanamume mmoja raia wa udachi amejikuta akikimbilia usalama wake baada ya jaribio la kutaka kumposa mpenzi wake kwa mbwembwe kwenda mrama.
Mtu huyo ambaye hakutajwa kwa jina anayeishi mjini Ijsselstein alikodisha 'kreni' au Crane na kuipanda akipanga kwamba kreni hilo imtoe chini na kumpanidhs hadi dirishani mwa mpenzi wake ambapo angemchezea wimbo na kisha kumposa.
Badala yake yaliyomkuta hakuyatarajia kabisa.Kreni hiyo ilianguka chini na kupita dirishani kwa mpenzi wake huku ikiangukia nyumba za majirani.
Mwanamume huyo alilazimika kukimbilia usalama wake na hakuna aliyejeruhiwa katika tukio hilo lililowaacha wengi wakiangua kicheko.
Kwa mujibu wa jarida la Algemeen Dagblad, mpenzi wake mwanamume huyo alimkubali na kusema yuko radhi kuolewa naye licha ya tukio hilo.
Baada ya kuongea na polisi, wawili hao walisafiri kwenda mjini Paris Ufaransa kusherehekea.
Kreni hio ilianguka tena kwa mara ya pili ilipokuwa inainuliwa na hata kuharibu zaidi nyumba za majirani. Meya wa mji huo, amezomewa na wengi baada ya eneo hilo kusemekana kutokuwa salama.
Share:

Roboti zapata ajira mgahawani China


Hadimu hivi karibuni huenda wakakosa ajira maana roboti zimezinduka
Mgahawa mmoja nchini China umeanza kutumia Roboti badala ya kuwaajiri hadimu au wafanyakazi wa hotelini kuwapakulia chakula na vinywaji wageni.
Share:

Wafungwa Philippines waponda raha.


Polisi mjini Manila wamevamia gereza moja na kuushangaza umma wa Philippines baada ya kung'amua maisha ya anasa yanayoendelea ndani ya gereza hilo kwa kikundi cha baadhi ywa wafungwa wenye upendeleo wa kipekee.
Uvamizi huo umefanywa katika gereza hilo la Bilibid lenye wafungwa wengi nchini humo kufuatia taarifa kwamba mtandao wa dawa za kulevya nchini humo unafanya kazi katika gereza hilo kwa njia za panya.

Baada ya uvamizi huo maafisa wa polisi walikuta wafungwa hao wakiwa wamefunga viyoyozi,mabafu ya kuogea ya kisasa yenye marumaru na kupambwa kwa mawe ya thamani,makasha ya kuhifadhia fedha,saa za gharama na fedha lukuki.
Wafungwa hao walifanikiwa pia kununua pombe kali za gharama kubwa ,komputa na hata simu za kisasa za gharama kubwa.kufuatia tukio hilo serikali ya Philippine imeahidi kufanya uchunguzi wa kina.
Share:

''Niliokoa Kenya 2013'' asema Moreno Ocampo.


Kiongozi wa zamani wa mashitaka katika mahakama ya jinai ya ICC, ameteta uamuzi wake wa kumshitaki Rais Uhuru Kenyatta licha ya kesi hiyo kutupiliwa mbali.
Bwana Luis Moreno Ocampo anasema kua mashitaka hayo dhidi ya Uhuru yalizuia ghasia kutokea tena katika uchaguzi wa mwaka 2013.
Kenyatta alishinda uchaguzi huo baada ya kugombea kwa tiketi ya chama cha TNA, huku akiituhumu mahakama hiyo kwa kuingilia maswala ya ndani ya Kenya.
Alishtakiwa kwa kosa la kuchochea ghasia za baada ya uchaguzi mwaka 2007.
Wiki jana mrithi wa Ocampo, Fatou Bensouda, alitupilia mbali kesi hio dhidi ya Kenyatta akisema amekosa kupata ushahidi wa kutosha kuthibitisha mashitaka dhidi ya Uhuru.
Kenyatta hata hivyo tangu mwanzoni alikanusha madai ya kutenda uhalifu dhidi ya Binadamu.
Alikuwa Rais wa kwanza aliye mamlakani kuwahi kufikishwa katika mahakama hio ambayo wengi wanasema ni ya kisiasa.
Watu 1,200 walifariki na wengine 600,000 kutoroka makwao katika ghasia hizo ambazo ndio mbaya zaidi kuwahi kushuhdiwa nchini humo tangu ijinyakulie uhuru.
Ocampo aliambia BBC kwamba kushitakiwa kwa Uhuru kulizuia ghasia kutokea tena nchini Kenya, wakati wa uchaguzi mwaka 2013. ''Mahakama ya ICC ilibadilisha siasa za Kenya, '' alisema Ocampo.
Wiki jana Rais was Uganda Yoweri Museveni alirejelea wito wake kwa mataifa ya Afrika kujiondoa ICC akisema kuwa mahakama hio inakandamiza mataifa ya Afrika.
Hata hivyo Ocampo amesema mahakama ya ICC ilikuwa kizingiti kwa viongozi kumi ambao walitegemea na kutumia sana ghasia ili kusalia mamlakani.
Share:

Idadi ya waliouawa Pakistan yafika 130.



Vikosi vya usalama nchini Pakistan vinakabiliwa na hali ngumu kuweza kudhibiti shule iliyovamiwa na wapiganaji wa Taliban katika jimbo la Peshawar Kaskazini Magharibi mwa Pakistan
Takriban watu miamoja na thelathini wamefariki , wengi wao wakiwa watoto.
Msemaji wa jeshi anasema washukiwa sita wameuawa huku operesheni hio ikiendelea.
Shule hio inasimamiwa na jeshi na wanafunzi wengi ni watoto wa wanajeshi.
Wakuu wa Hospitali wanasema kuwa zaidi ya watu 40 wanasemekana kujeruhiwa japo idadi hiyo inatarajiwa kupanda zaidi.
Maafisa mjini Peshawar wanasema kuwa wanaume watano ama sita waliokuwa na silaha waliingia shuleni humo wakiwa wamevalia magwanda ya kijeshi .


Wanafunzi mia tano na waalimu walikuwa katika shule hiyo ya umma ya kijeshi wakati sham,bulizi hilo lilipotokea .
Wakazi wa eneo hilop wanasema kuwa walisikia milio ya bunduki iliyodumu kwa dakika kadhaa .
Wanasema pia kuwa walisikia sauti za kelele za wanafunzi na waalimu .


Haijabainika wazi ni kwa namna gani wanamgambo wa Talebain waliweza kupenya hadi kuingia ndani ya majengo hayo yanayomilikiwa na jeshi.
Jeshi la Pakistan limesema operesheni ya uokozi ilikuwa ikiendelea na kwamba wengi wa wanafunzi na waalim wameokolewa toka eneo la hatari.
Shambulio hilo limetokea wakati operesheni kubwa ya kijeshi ikiendelea dhidi ya wapiganaji wa Taleban wa Pakistan na wanamgambo wengine wanaoendesha harakati zao kaskazini mwa jimbo la Waziristan.
Share:

Sunday 14 December 2014

Vikosi vya Libya vyatibua shambulizi.


Wapiganaji wazidi kushambuliana nchini Libya tangu kuanguka kwa utawala wa Muamar Gadaff....

Shambulizi lililolenga kituo muhimu cha mafuta mashariki mwa Libya halikufua dafu kutokana na mashambulizi ya angani yaliotekelezwa na vikosi vya serikali vinavyotambuliwa kimataifa.
Kamanda mmoja wa jeshi la wanahewa anasema kuwa mashambulizi ya angani yaliwalenga watu wenye silaha waliokuwa wakisonga mbele katika kituo cha mafuta cha Al-Sidra ambapo watu wengi waliuawa.

Zaidi ya miaka mitatu tangu kuanguka kwa utawala wa kanali Muamar Gadaffi serikali hasimu bado zinapigania madaraka nchini Libya.
Share:

Jenerali aliyempinga Museveni arudi UG........























Jenerali Sejusa aliyeitoroka uagnda baada ya kutofautiana na rais Musevenei hadharani

Mwanajeshi wa Uganda ambaye alitofautiana hadharani na rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni mwaka uliopita amerejea nchini Uganda bila kutarajiwa kutoka nchini Uingereza ambapo alikuwa amekimbilia uhamishoni.
Jenerali David Sejusa aliitoroka Uganda baada ya kumshutumu rais Museveni kwa kujaribu kubuni familia ya kifalme akitaka kumkabidhi uongozi mwanawe wa kiume.
Sejusa pia alidai kuwa kulikuwa na njama ya kuwaua watu fulani katika serikali na jeshini ambao walikuwa wakipinga mpango huo.





















Rais Museveni anayedaiwa kumtayarisha mwanawe ili kuchukua utawala wa Uganda

Alipowasili mjini kampala Jenerali Sejuse alikutana na mkuu wa ujajusi ambapo pia aliwaambia waandishi wa habari kuwa rais Museveni alifahamu kuhusu kurejea kwake.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.