Sunday 30 November 2014

MHESHIMIWA PROF. ANNA TIBAIJUKA BORA UJIUZULU KULINDA HESHIMA YAKO NA CHAMA........source GLOBAL PUBLISHER












Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka.

Mheshimiwa Bi. Anna Tibaijuka (Mb), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ni moja wa viongozi wachache sana wenye ujasiri na kiongozi muwazi katika sakata zima la akaunti ya Tageta Escrow, kwani kiongozi huyu amekiri wazi kuwa amepokea fedha shilingi billion 1.6 kutoka kwa mmiliki wa kampuni ya VIP Engineering Bw. James Rugimalira.
Si jambo jema kumhukumu Mheshimiwa Anna Tibaijuka, lakini siyo vibaya kumshauri kwa kuwa amekuwa muwazi katika sakata hili, basi lingekuwa jambo la maana sana kama angejiuzulu madaraka aliyonayo katika serikali ili kulinda heshima yake na ya chama tawala.
Msomi yoyote yule anapofikia kuitwa Profesa na tena Waziri mwenye kushika dhamana ya nchi na wananchi yaani, Ardhi na Makazi, halafu akakubali kupokea fedha ya kiasi kikubwa hivyo bila ya kutia shaka yoyote kama ananuliwa kwa namna moja au nyingine kutokana na dhamana ya cheo chake, litakuwa ni jambo jema kwake kujiuzulu ili aonyeshe mfano bora kuwa yeye ni kiongozi mkweli na viongozi wengine wafuate nyao.
Msomi aliyefikia daraja la juu kabisa tunamwona kama kiongozi anayejua wazi kuwa yeye ni mojawapo wa Mawaziri wachache ambao Wizara zao zina dhamana kubwa ya nchi, leo hii akikubali kununuliwa kiurahisi au kufanya biashara akiwa katika madaraka mazito, tuna mashaka naye ikiwa atandelea kututumikia wananchi katika Wizara ambayo pia inahusika na mipaka ya ardhi ya nchi.
Watanzania tunajiuliza, hivi Mhe. Anna Tibaijuka yupo katika utumishi wa umma tena na huku akiwa Mkurugenzi wa Mashirika au Shule na miradi binafsi, ndiyo kusema cheo chake cha utumishi wa umma ndio dhamana ya biashara zake?
Hivi kuna hosptali ngapi hapa nchini hazina dawa? Je wakina mama wangapi wajawazito wanafariki wakati wa kujifungua kwa ukosefu wa vifaa vya mahosptalini? Shule ngapi za serikali hazina madawati?
Leo Mheshimiwa mabilioni ya fedha na kusema kuwa hakujua kama ni fedha chafu. Kwa vipi Watanzania tusiwe na mashaka naye?
Professor Anna Tibaijuka anafahamu wazi kuwa amevunja sheria ya maadili ya viongozi wa umma "(Sheria namba 13 ya mwaka 1995) ambayo inawataka viongozi watoe taarifa ya zawadi wanazopokea au malipo wanayolipwa."
Hivyo, sisi wananchi wenye kuiamini serikali hii hautuwezi kabisa kukubali au kuona kiongozi tena msomi anavunja dhamana ya wananchi na kumvunjia heshima mkuu wa nchi ambaye ndiye alimteua.
Litakuwa jambo la busara sana Mhe. Anna Tibaijuka ujiuzulu ili kulinda heshima yako kama msomi Professor, pia kulinda heshima serikali na Chama tawala. Huwezi kutumikia ofisi mbili, yaani utumishi wa umma na biashara.

Wanachi tunasikitika sana kuona katika sakata la fedha za umma mpaka baadhi watumishi wa Mungu ambao ni viongozi wa Kanisa nao wanahusika na bila ya woga. Wanapokea fedha bila ya hofu ya kujenga udini.
Share:

Helikopta ya maliasili(TANAPA) yadondoka Jijini dar....

Helikopta ya maliasili(TANAPA) Imedondoka maeneo ya Gongo la mboto, Moshi Bar jijini Dar na kuwa watu wote watano wakiwemo Rubani na Polisi



Share:

housegirl(dada wa kazi) aliyempiga mtoto uganda.....























Baada ya habari za yule msichana anayefanya kazi za ndani Uganda kuchukua headlines katika vyombo mbalimbali vya kimataifa Duniani, leo kipo alichkizungumza kwa mara a kwanza.

Jolly Tumuhiriwe ambaye kwa sasa amekamatwa na polisi, alisema sababu iliyomfanya amtese mtoto Arnella Kamanzi,ni kutokana na kuchanganyikiwa baada ya waajiri wake kutompatia pesa ili amtumie baba yake ambaye aikua anaumwa.

Amesema anajiona ni mwenye hatia kwa alichokifanya japo anadhani alifanya hivyo kama njia ya kumkanya mtoto huyo kwa kuwa alikuwa akimuona mama wa mtoto huyo akimpiga kama njia ya kumkanya.

Jolly amelalamika kuwa anajisikia vibaya pale ambapo wafungwa wenzake wamekua wakimtenga sana na wakitaka kumpiga.
Share:

WHO:Watu 7000 wamefariki na ebola........






















Hesabu mpya kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Ebola iliyotolewa na shirika la afya duniani WHO inaonyesha kuwa karibu watu 7000 wameaga duian kutokana na ugonjwa wa Ebola wengi wakiwa eneo la Afrika magharibi.
Hili ni ongezeko la zaidi ya watu 1000 tangu WHO itoe hesabu yake ya mwisho siku nne zilizopita.
Sehemu kubwa ya ongezeko hilo iliripotiwa nchini Liberia
Mkuu wa ujumbe wa umoja wa mataifa unaohusika na ugonjwa wa Ebola Antony Banburry anasema kuwa kwa sasa nchi iliyoathirika zaid ni Sierra Leone ambapo karibu visa 500 vya ugonjwa wa Ebola huripotiwa kila wiki.

Amesema kuwa maziko ambayo ndiyo chanzo kikubwa cha maambukizi bado hayafanywi kwa njia iliyo salama.
Share:

Polisi aliyemuua kijana mweusi ajiuzulu........BBC


Wakili wa Darren Wilson ambaye ni afisa wa polisi aliyempiga risasi na kumuua kijana mweusi Michael Brown kwenye eneo la st Louis nchini Marekani mwezi Agosti anasema kuwa polisi huyo amejiuzulu.
Mapema wiki hii bwana Wilson aliondolewa mashtaka hatua iliyozua ghadhabu miongoni mwa waamerika weusi.
Afisa huyo amekuwa likizoni tangu mauji hayo yafanyike, mauaji ambayo yalisababisha majuma kadha ya maandamano.
Gazeti la St Louis limesema kuwa afisa huyo mwenye miaka 28 aliamua kujiuzulu baada ya kitengo chake cha polisi kupokea vitisho kwamba ghasia zitafutia iwapo ataendelea kuhudumu kama mfanyikazi.
Gazeti hilo lilichapisha kile lilichodai kuwa barua yake ya kujiuzulu ambayo ilisoma:''nimearifiwa kwamba iwapo nitaendelea kuwa mfanyikazi wa idara ya Polisi basi hatua hiyo itawachochea maafisa wa polisi na raia wa eneo la Furguson kuishi kwa hofu,hali ambayo siwezi kuikubali hata kidogo.

Share:

Saturday 29 November 2014

Rais Kikwete asema amepona Saratani.......


Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema amepona saratani baada ya kufanyiwa upasuaji mapema mwezi huu nchini Marekani.
Kiongozi huyo wa Tanzania mwenye umri wa miaka 64 ametoa hotuba kwa taifa kuelezea afya yake..
"Niligundulika kuwa na hatua ya pili ya saratani ya kibofu, ambayo baadaye ikaonekana kuwa ni hatua ya kwanza," alisema Kikwete katika hotuba iliyotangazwa moja kwa moja kupitia televisheni akiwa uwanja wa ndege wa Dar Es Salaam baada ya kurejea kutoka Marekani.
Aliongeza kuwa madaktari wamesema sasa hali yake shwari: "Madaktari walisema saratani haikuenea katika sehemu nyingine za mwili na baada ya upasuaji sasa wamesema nimepona saratani."
Alisema aligundulika kuwa na saratani ya kibofu zaidi ya mwaka mmoja uliopita na alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya Johns Hopkins Hospital tarehe nane Novemba.
Kikwete ambaye anamaliza muhula wake wa pili mwakani amesema wananchi wajenge tabia ya kupima afya zao ili wagundue maradhi mapema.
Share:

Nigeria:Raia watakiwa kuwa waangalifu.........


Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amewataka watu wote nchini Nigeria kuwa waangalifu na kushirikiana na vikosi vya usalama vya nchi hiyo ili kujaribu kuzuia mashambulizi zaidi yanayotekelezwa na wanamgambo wa Boko Haram kaskazini mwa nchi.
Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulizi hilo lililotokea kwenye msikiti mmoja mkubwa ulio kwenye mji wa Kano ambapo watu kadhaa waliuawa.
Hata hivyo shambulizi hilo linaaminika kutekelezwa na Boko Haram ambalo kampeni yake dhidi ya serikali imesababisha vifo vya maelfu ya watu mwaka huu.
Polisi walitibua njama ya shambulizi jingine kwenye mji ulio kaskazini mwa Nigeria wa Maiduguri ambapo mabomu sita yaliharibiwa ndani ya msikiti mmoja na kwenye soko lililo karibu.
Share:

Friday 28 November 2014

Bunge lasambaratika Tanzania........


Mzozo mkubwa umesababisha Bunge la Tanzania kuvunjika usiku huu wakati likiendelea na mjadala wa kashfa ya Escrow, baada ya wabunge kushindwa kukubaliana njia sahihi ya kuwawajibisha baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaotuhumiwa kuhusika na sakata la wizi wa Zaidi ya fedha za Tanzania shilingi bilioni 300 kutoka Benki Kuu ya nchi hiyo.
Taarifa ya mwandishi wa BBC Baruan Muhuza imesema kuwa Bunge hilo, leo limeweka rekodi ya kuwa na mjadala wa muda mrefu Zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Hadi kufikia kuvunjika kwa kikao hicho ilikuwa ni saa 4.30 usiku kwa saa za Afrika Mashariki. Spika wa Bunge hilo Anne Makinda karibu muda wote wa kikao hicho alijikuta akitoa tahadhari kwa wabunge wake kujilinda na hatua za kuingilia mihimili mingine ya utawala ya Tanzania ambayo ni Mahakama na Serikali. Hatua hiyo kwa namna Fulani iliamsha hisia tofauti kutoka upande wa kambi ya upinzani pamoja na wajumbe wa kamati ya hesabu za Serikali ambao walitishia kutoka nje hadi viongozi wanaodaiwa kulindwa na bunge hilo wawajibike wenyewe. Bunge hilo linategemewa kuendelea na kikao chake hapo kesho.


Share:

Ikulu ya Tanzania yahusishwa na Escrow..........BBC


Bunge la Tanzania hapo jana liliambiwa kwamba afisa mmoja wa ikulu ya rais bwana Prosper Mbena aliandika barua ili kushinikiza hatua ya kutolewa kwa billioni 306 fedha za Escrow kutoka banki kuu ya Tanzania.
Bwana Mbena ambaye anafanya kazi kama katibu katika afisi ya rais aliandika barua mwaka uliopita akiiagiza wizara ya fedha kuzitoa fedha hizo kama ilivyoamrishwa na mwanasheria mkuu.
Kushirikishwa kwa ikulu ya ya rais kulizuka baada ya wabunge kujadili ripoti kuhusu kashfa hiyo ambayo imeikumba serikali ya Tanzania katika miezi kadhaa iliopita.
Kiongozi wa upinzani katika bunge,Bwana Freeman Mbowe pamoja na kinara wa bunge upande wa upinzani bwana Tandu Lissu alifichua jukumu lililochukuliwa na afisa huyo wa ikulu kushinikiza madai kwamba baadhi ya maafisa wakuu serikalini walihusika katika utoaji wa mabilioni hayo ya fedha.

Ripoti hiyo imesema kuwa fedha hizo za Escrow ni za walipa ushuru wa Tanzania na kwamba zilitolewa kwa njia ya ufisadi na kugawanywa miongoni mwa watu maarufu.
Share:

Mtoto mchanga anusurika kuuawa Kenya.....


Mtoto X amelala kwa utulivu, akiwa amefunikwa na Blanketi lenye kumpa joto na kukumbatiwa na Mama yake katika Nyumba moja ya kulelea Watoto yatima nchini Kenya.
Mtoto huyu ni wa miezi miwili hivi sasa, alizaliwa kufuatia tendo la ngono kati ya msichana na Mjomba wake, mtoto huyu anaelezwa kupatikana katika mazingira ya miiko.
Katika nyumba ya watoto wa Kanduyi, mjini Bungoma magharibi mwa Mji wa Nairobi, kama ilivyo kwa Watoto wengine , Mtoto huyu aliokolewa kutoka kwenye Familia yake kulipokua na mipango ya kuuawa.
Katika tukio hilo,siku mbili tu baada ya kuzaliwa Mtoto X, baada ya kupewa Taarifa vikosi vya usalama vilivamia makazi ya mtoto huyo na kumchukua wakiyaokoa maisha yake kutokana na kifo kilichokuwa kinamkabili mbele yake, kifo kilichaoamriwa na wazee wa kimila wa jamii iitwayo Bukusu.
Kuna watoto kama yeye katika nyumba hii ya Kunduyi wenye umri kati ya siku moja mpaka miaka 18.
Watoto waitwao 'mwiko'
Kujamiiana kwa maharimu ni mwiko nchini Kenya kama ilivyo katika maeneo mbalimbali, kwa mujibu wa Sheria ya Kenya, hilo ni kosa lenye kuadhibu kwa kifungo cha miaka mitano,au kifungo cha maisha kwa kujamiiana na binti wa umri mdogo

Lakini kwa Karne nyingi, adhabu ya kimila katika Jamii nyingi za Kenya ni kifo,na katika jamii ya Bukusu si lazima Mwanaume na Mwanamke waliohusika, lakini pia mtoto atakayezaliwa kutokana na uhusiano ulio mwiko.









Waziri wa utamaduni katika Kaunti ya Bungoma,Stephen Kokonya amesema kumekuwa na mahusiano ya namna hii yameenea katika jamii na kuongeza kuwa si sheria kwa jamii kutoa adhabu ya kifo, ni Jaji pekee anayeweza kuhukumu.Kokonya amesema katika maeneo ya kijijini hii ni sehemu ya Sheria za kijamii watoto kuonekana kuwa wamelaaniwa.
Watu wa jamii ya Bukusu huwaita Watoto hawa ''be luswa'' wakimaanisha ''Watoto haram'' wakihofu kuwa watasababisha kupata laana kama utasa na magonjwa ya akili.
''Kila mara tunaposikia mtoto anayedaiwa kuwa haramu amezaliwa katika eneo lolote huwa tunakimbia upesi kumuokoa vinginevyo unaweza kufika na kuambiwa tayari Mtoto alishakufa''Afisa anayetunza Watoto katika nyumba ya Watoto wa Kanduyi,Alice Komotho ameiambia BBC.
Kokonya amesema Serikali inatoa elimu ya uelewa kuhusu vitendo vya adhabu zitolewazo kinyume cha sheria ya nchi na Wazee wa jamii ya Bukusu.
Kisa cha Msichana.
Mama wa miaka 15 ambaye mtoto wake aliokolewa amerudi shuleni,binti huyu wa miaka 15 alibakwa na Mjomba wake. Msichana huyu amesema Mjomba wake alimtishia kuwa atampiga ikiwa atatoa taarifa kuhusu tukio la kubakwa, binti huyu alibakwa na mjomba wake mwenye umri wa miaka 17.
Msichana huyu hivi sasa amerudi shuleni kurudia mwaka wake alioupoteza alipokua mjamzito.
Binti huyu anaeleza kuwa hana mapenzi na Mjomba wake wala mtoto wao.
Mama huyu mdogo ameiambia BBC kuwa anapenda kuwa Daktari atakapomaliza masomo.
Maafisa wanasema kuwafundisha wazee wa kimila itakua ni njia nzuri ya kumaliza mila na desturi mbaya katika maeneo ya vijijini.
Mjomba wa Msichana huyo alikataa kuzungumza na BBC baada ya kuwasiliana nae.
Haki ya Kuishi
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wazee wa Bukusu anaeleza namna mtoto anavyouwawa,anakataa kuzungumzia kisa cha Mtoto X lakini anaeleza namna mtoto wanayedai kuwa haramu anavyouawa, anaeleza..
''Wakati binti anapokaribia kujifungua,huwakusanya baadhi ya Wanawake ambao hujifanya kama wanakwenda kumsaidia mzazi badala yake humziba pumzi mtoto kwa kuzibana nyonga za mama na kumuua Mtoto.
Wakinamama hawa hufanya haya kwa makini wakiamini kuwa ni budi mtoto kufa ili mzazi aishi katika jamii kwa amani.
Mzee mwingine anasema pia Wanakijiji wakati mwingine huua uzao wa pili ambao huwa pacha kwa madai kuwa huleta hali ya bahati mbaya, ambao wanapenda kubaki na watoto wao hulazimishwa kuondoka kijijini hapo.
Lakini Waziri wa utamaduni anasema kuwa angependa kuwakumbusha Wazee wote ambao hukaa na kuamua maamuzi ya mauaji kuwa wanaingilia haki ya msingi ya kuishi.
Share:

Msikiti washambuliwa nchini Nigeria..........BBC






















Taarifa kutoka mjini Kano, Kaskazini ya Nigeria, zinasema kuwa watu wengi wamefariki na wengine wengi kujeruhiwa katika shambulizi la bomu.
Ni baada ya milipuko mitatu inayoaminika kuwa ya mabomu kutokea katika msikiti mkubwa zaidi mjini humoulio katikati mwa jiji karibu na eneo anakoishi Emir au kiongozi wa waisilamu nchini humo Muhammad Sanusi.
Emir huyo kwa sasa yuko nchini Saudi Arabia.
Mabomu hayo yalilipuka wakati maombi ya Ijumaa yalipokuwa yanaendelea.
Mtu mmoja aliyeshuhudia tukio hilo, alihesabu karibu miili 50 ya waliofariki katika shambulizi hilo.
Taarifa zingine zinasema watu waliokuwa wamjihami waliaingia msikitini humo na kuanza kufyatua risasi baada ya mabomu kulipuka.
Wapiganaji wa Boko Haram, wamekuwa wakifanya mashambulizi katika mji huo ambao ni mkubwa zaidi Kaskazini ya Nigeria.
Mapema mwezi huu , Emir alitoa wito kwa watu kujikinga dhidi ya mashambulizi yanayofanywa na Boko Haram.
Aliwashauri wakazi kujihami na kufanya kila wawezalo kujikinga dhidi ya mashambulizi yanayofanywa na kundi hilo.

Msemaji wa Polisi alisema matamshi ya Emir, yalikuwa ya uchochezi na kwamba watu wanapaswa kumpuuza.
Share:

Thursday 27 November 2014

Saudia yawakataa mayaya wa Uganda........BBC



















Yaya wa Uganda aliyemtesa mtoto wa miezi 18

Mamlaka ya Saudia mjini Kampala imewaonya raia wake nchini Saudia dhidi ya kuwaajiri mayaya kutoka Uganda.
Onyo hilo linajiri baada ya kanda za video za CCTV kumuonyesha Jolly Tumuhiirwe,22,akimtesa mtoto wa miezi 18.
Bwana Haza Al-Otabi ,naibu wa ujumbe wa Saudi Arabia alinukuliwa na gazeti la kiingereza nchini saudi akiwaonya wawanchi wa taifa hilo dhidi kuwaajiri raia wa kigeni kutoka Uganda kuwa mayaya wao wenyewe.
''Uajiri ni sharti ufanyike kupitia makubaliano rasmi''bwana Al-Otaibi alisema.
Harakati ya gazeti la the monitor nchini Uganda kuwasiliana na afisa huyo ziligonga mwamba baada ya kudaiwa kuwa mikutanoni siku nzima.
Mtoto aliyechomwa na yaya aonyesha jareha alilopata

Inadaiwa kuwa Gazeti hilo la Saudia linasema kuwa bwana Al-Otaibi aliitoa kanda hiyo ya video kwa makusudi kwa kampuni zinazowaajiri wafanyikazi wa nje na ambazo mwezi mmoja uliopita ziliweka makubaliano na wizara ya wafanyikazi nchini Uganda ili kuwaajiri mayaya na madereva.
''Walioajiriwa kutoka Uganda hawatapewaza Viza kuingia nchini Saudia iwapo makubaliano hayo hayatafanyika kwa njia rasmi'',alinukuliwa akisema.
Katika mktaba huo kati ya Uganda na Saudia takriban viza 500 zilitarajiwa kupewa mayaya 400 wa Uganda na madereva 100 kufanya kazi nchini humo.
''Kumekuwa na matatizo na uajiri unaoshirikisha raia wa Uganda nchini Saudi Arabia.
Wengi ya mayaya wa Uganda wanaowasili Saudi Arabia huondoa mda mfupi baadaye na kushindwa kumaliza siku 20 n wafadhili wao'' mjumbe huyo alisema.
Amesema kuwa mayaya hao hulalamika kwa balozi yao kwamba wanahitaji haki zao za kifedha.Lakini Wafadhili wa saudia wanadai kwamba hawawezi kuwalipa kwa kuwa wameshindwa kufanya kazi kwa mwezi mmoja.
Lakini msemaji wa wizara ya maswala ya kigeni nchini Uganda Fred Opolot ,amesema kuwa ubalozi wa Saudia haujatoa lalama yoyote kuwahusu.
Share:

Bi harusi wa miaka 14 ampa sumu mumewe....


Bi harusi wa miaka 14 nchini Nigeria ameshtakiwa kwa kuwaua watu wanne akiwemo mumewe wa miaka 35 baada ya kuweka sumu ya panya katika chakula alichoandaa kwa sherehe za haruysi yake.
Kesi hiyo imewashangaza wahaharakati wa haki za kibinaadamu ambao wamesema kuwa msichana aliyeozwa kwa mume aliye mara mbili umri wake anafaa kuchukuliwa kama mwathiriwa na wala sio muhalifu.
Wasila tasiu kutoka familia masikini katika eneo la waislamu la kazkazini huenda akakabiliwa na kifo iwapo atahukumiwa.
Shahidi wa kwanza wa kiongozi wa mashtaka Lamido Abba Sorron-Dinka alikuwa msichana wa miaka 7 anayejulikana kama hamziyya,ambaye alikuwa akiishi katika nyumba moja na Tasi'u pamoja na mumewe Umar sani,wakati bi haru huyo alipoweka sumu ya panya katika chakula hicho.
Hamziyya alijulikana tu kama dadaake mke wa kwanza wa bwana Sani,mwanamke aliyeolewa na marehemu awali katika eneo ambapo ndoa za wake wengi zimekithiri.
Msichana huyo wa miaka 7 alisema kwamba Tasi'u alimpa fedha ili kununua sumu ya panya kutoka duka moja jirani mnamo tarehe 5 mwezi Aprili,siku ambayo bwana Sani alifariki.
''Alisema kuwa panya wanamsumbua katika chumba chake'',Hamziyya aliiambia mahakama.Upande wa mashtaka baadaye ulisema kuwa badala yake Tas'u aliweka sumu hiyo ya panya katika chakula ambacho alikuwa amekiandaa kwa sherehe za baada ya harusi kwa kuwa alijuta uamuzi wake wa kumuoa bwana Sani.
Msichana huyo alikataa kuzungumza mahakamani.
Jaji Mohammed Yahaya,katika mahakama ya Gezawa alitoa hukumu kwamba Tasi'u ambaye alikataa kuongea katika mahakama hana hatia katika kusikizwa kwa kesi mnamo mwezi Octoba ambapo alisomewa mashtaka.
Jaji huyo alikataa ombi la upande wa mshtakiwa la kesi hiyo kupelekwa katika mahakama ya watoto.
Ushahidi wa Hamziyya uliungwa mkono na Abuwa Yussuf muuzaji duka katika mji wa Unguwar Yansoro ambaye alithibitisha kuuza sumu hiyo kwa mtoto huyo.
Jirani ya Bwana Sani mwenye umri wa miaka 30 ambaye ni mkulima, Abdulrahim Ibrahim alitoa ushahidi ambapo alisema kwamba alipewa chakula hicho kilichopikwa na Tasiu.''Nilipoletewa chakula hicho niliona vipande vipande vyeusi''aliiambia mahakama.
Alikula vipande vinne vya madonge vilivyotengezwa na maharagwe lakini hakupendelea ladha yake'',alisema na kuongezea kuwa ni Umar pekee aliyeendelea kula.
Baadaye alisema kuwa alimuona bwana Sani katika bustani ,akiwa mgonjwa na kumpeleka nyumbani.
Lakini alipokuwa akijaribu kumuuguza bwana sani ,aligundua kwamba watu wengine watatu ambao walikuwa wamekula chakula hicho wamefariki kwa ghafla.
Viongozi wa mashtaka walidai kwamba chakula cha Tasiu kilichowekwa sumu kiliwaua watu wanne na hivyobasi kuwajumuisha wanne hao katika kesi moja ya mauaji.
Nigeria haijawahi kumyonga mtoto aliyefanya uhalifu tangu mwaka 1997,ambapo taifa hilo liliongozwa na dikteta Sani Abacha,kulingana na shirika la kibinaadamu la Human Rights Watch.
Share:

Misikiti iliofungwa yafunguliwa Mombasa.........



Misikiti minne iliofungwa na maafisa wa polisi wiki iliopita baada ya kuchukuliwa na vijana wenye itikadi kali za kiislamu hatimaye imefunguliwa.
Hatua ya kuifungua misikiti hiyo ya Minaa,Sakina,Musa na Swafaa inajiri baada ya siku mbili za mazungumzo kati ya viongozi wakuu wa kiislamu,wataalam na uongozi wa kaunti ya Mombasa.
Maelezo ya mazungumzo hayo yalioandaliwa na Gavana wa Mombasa Hassan Joho na kaunti kamishna Nelson Marwa yamefanywa kuwa siri.
Kabla ya misikiti hiyo kufunguliwa ,viongozi wa kiislamu pamoja na wataalam walilazimika kuajiri kiongozi wa dini wa kila msikiti na kubuni kamati maalum ya kusimamia misikiti hiyo ya kisauni na majengo mjini Mombasa.





''Hatutaki wajisikie kana kwamba serikali ina wakandamiza.Tumewapa mda wa kuzungumza na kuamua kuhusu kamati za misikii hiyo na viongozi w dini ambao watakuwa wakisimamia ibada.Watatupatia majina na kufikia kesho{leo} misikiti hiyo itafunguliwa'',alisema bwana Marwa ambaye ndio mwenyekiti wa kamati ya usalama kaunti ya Mombasa.
Duru zinaarifu kuwa miongoni mwa wale walioalikwa katika mazungumzo hayo ni viongozi wakuu wa kiislamu wakiwemo wawakilishi kutoka baraza kuu la waislamu nchini Kenya SUPKEM,barasa kuu la ushauri wa maswala ya kiislamu na baraza la maimamu na wahubiri nchini Kenya CIPK.
Misikiti hiyo ilifungwa wiki iliopita na maafisa wa usalama baada ya uvamizi katika Msikiti wa Musa pamoja na msako wa kuwanasa zaidi ya watu 250 ambao baadaye walishtakiwa kwa kuwa wanachama wa makundi ya kigaidi.
Maafisa wa polisi pia walionyesha baadhi ya silaha na nakala ambazo wanasema zilipatikana katika msikiti huo.
Muda mchache baada ya kukamatwa kwao,magenge ya vijana walizua ghasia na kuanza kuwashambulia raia wasio kuwa na hatia katika vituo vitatu vya mabasi pamoja na makaazi katika eneo la kisauni.
Wakati wa ghasia hizo watu watatu walidungwa visu na kufariki huku wengine saba wakijeruhiwa vibaya.
Viongozi wa kiislamu mjini Mombasa na maeneo mengine ya nchi wamekuwa wakitaka kufunguliwa kwa misikiti hiyo ambayo imekuwa katikati ya utata kuhusu madai kwamba ilikuwa inatumiwa kuwafunza vijana itikadi kali mbali na kuhifadhi silaha kinyume na sheria.
Share:

Chanjo ya Ebola yaonesha matumaini...........BBC


Wanasayansi wamepongeza matokeo ya majaribio ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Ebola, na kusema dawa zinaonesha kuwa salama na itasaidia mfumo wa kinga ya mwili kuvitambua virusi hivyo.
Watu 20 waliojitolea kutoka nchini Marekani, walipatiwa kinga maradhi hiyo, ikiwa ni hatua muhimu ya kujikinga na virusi hivyo vya ugonjwa wa Ebola.
Utafiti wa chanjo hiyo ya ebola kama huenda ikaokoa maisha wa maelfu walio hatarini kuambukizwa virusi hivyo. Dr Anton Fauci ni mkuu wa Taasisi ya Marekani ya magonjwa ya kuambukiza :
"Kwa upande wa usalama na uwezo wa kuleta matokeo mazuri nadhani tunaweza kuita majaribio haya ya chanjo haikufanikiwa. Japokuwa katika mkondo wa awali imeonyesha mafanikio makubwa." Amesema Fauci
Hata hivyo watafiti wanasema matokeo hayo sio uthibisho kwamba chanjo hiyo inafanya kazi lakini kama majaribio ya awali yamekuwa na mafanikio basi chanjo ya ebola itatolewa kwa maelfu ya wafanyakazi wa afya huko Afrika Magharibi kuanzia mwezi Januari mwakani.
Zaidi ya watu elfu tano mia tano wamefariki kutokana na kuambukizwa virusi vya ebola.Kwa sasa chanjo imekuwa ikifanyiwa utafiti na kampuni GlaxoSmithKline.
Dr Colin Brown ni mtaalamu wa magonjwa ambaye amepokea habari za chanjo hiiyo kama habari njema.
"Kwa vile suala la usalama limepewa umuhimu tunayo furaha kwamba hakuna madhara yaliyotokana na chanjo. Ambapo imeonyesha wagonjwa wa awali wapatao 20 wakuwa na tatizo lolote. Ninadhani tutarajie kuona itasaidia hasa kwa upande wa wafanyakazi wa afya kujilinda wakiwa kazini. " Alisema Bwana Brown
Share:

Baridi yagandisha breki za ndege Siberia.....


Abiria waliokuwa wanafanya safari na shirika ka ndege la Serbia walilazimika kushuka katika ndege hiyo na kuisukuma baada ya breki zake kuganda na kushindwa kuondoka.
Ndege hiyo ilikuwa inaanza kuruka kutoka katika mji wa Kirusi wa Igarka,lakini ilishindwa kusogea baada ya hali ya hewa kuwa -52C.
Abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo idadi yao kubwa walikuwa wafanyakazi wa ndege hiyo waliombwa kutoa msaada wa dharura wa kuisukuma ndege hiyo kwa hofu ya kutowachelewesha endapo watasubiri msaada Zaidi.
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Katekavia baada ya muda ilimudu kuendelea na safari zake na baadaye kutua salama katika mji wa Krasnoyarsk.kwa muujibu wa mashuhuda wa tukio hili kiwango cha baridikwa muujibu wa mashuhuda wa tukio hili ,wanaeleza kuwa kiwango cha baridi kilishuka hadi kufikia nyuzi joto 52, na kugandisha mfumo wa breki za ndege hiyo .
Mkuu wa kitengo cha huduma za ndege hiyo Oxana Gorbunova, anaeleza kwama abiria hawakulazimishwa kuisukuma ndege hiyo bali kwa hiyari waliamua kusaidia kuisukuma ,japokuwa kitendo hicho hakiruhusiwi kwakuwa kitendo hicho kinaweza kuathiri bodi ya nje ya ndege hiyo ,na wanasheria nao wanachunguza endapo uwanja wa ndege,shirika la ndege,wafanyakazi wa ndege ama abiria endapo wamevunja sheria za usalama wa anga.
Uwanja huo wa ndege unatumiwa na abiria takribani elfu moja kwa mwaka ,wengi wao hufanya kazi katika makampuni ya mafuta yanayomilikiwa na Urusi.
Share:

Wednesday 26 November 2014

Lawama kwa viongozi wa kiisilamu Kenya.............BBC


Baraza makanisa nchini Kenya(NCCK) limewalaumu vongozi wa kiislamu na serikali kushindwa kuzuia mashambulizi dhidi ya wakristu.
Wakizungumzia mauaji yanayosemekana kutekelezwa na kundi la Al-Shabaab na kuwaua wakristu 28 Jumamosi asubuhi.
Baraza hilo limesema kuwa halitafanya mazungumzo mengine na viongozi wa dini ya kiislamu kwa sababu wameshindwa kuwathibiti waumini wao ambao NCCK inadai kuwa wamekuwa wakiwashambulia wakristu kwa maeneo ya ibada na kwingineko.
Kwa siku nyingi baraza la makanisa limekuwa likichukua msimamo wa kadri kunapotokea mashambulizi nchini Kenya ama kwa jumla kuhusu suala la usalama.
Ila leo walikuwa na msimamo mkali sana kuhusiana na mauaji yaliyotokea Mandera wakalaumu kwana viongozi wa kiislamu kwa kutokuwa wakakmavu kuwashauri waumini wao.
Huyu hapa katibu Mkuu wa baraza hilo Peter Karanja alisema kuwa wamekuwa na mikutano mingi na viongozi wa dii ya kiislamu lakini kumekuwa na mshambulizi mengi yanyowalenga wakristu
Japokuwa walionyesha kukerwa na tukio la Mandera, viongozi hao wamesema kuwa serikali na viongozi wa kiislamu hawajashughulikia tatizo la vijana wanaoshikilia mismamo mikali ya dini katika maeneo ya Pwani na Kaskazini ya nchini ambao wamekuwa hatari kwa usalama




Hata hivyo viongozi wa kiislamu hawajachukulia kwa wepesi sula hilo. Dr Hassan Kinyua ambaye ni mkurugenzi wa masuala ya kidini katika baraza kuu la waislamu(SUPKEM) anataka NCCK iendelee kufanya mazungumzo na SUPKEM.
Ameongeza kuwa ni makosa kila mara kuhusisha suala la ugaidi na dini ya kiislamu
Lakini viongozi hao wanapoishambulia serikali hususan vikosi vya usalama kwa kulegea katika vita dhidi ya ugaidi Rais uhuru Kenyatta amewatetea maafisa wa usalama akisema kuwa suala la usalama ni la wakenya wote.
Na hata watu wanapotaka wakuu wa usalama wajiuzulu Rais Uhuru anasema vikosi vya usalama havitavumilia dini kutumia majengo ya ibada kuendeleza ugaidi
Hapo jana makundi kadhaa ya kutetea haki za binadamu yaliandamana yakimtaka Rais Uhuru Kenyatta kuwaachisha kazi wakuu wa uslama kwa kushindwa kuzuia mashmbulizi dhidi ya wakenya.
Kumekuwa na mashmbulizi mengi nchini Kenya tangu jeshi la Kenya liingie Somalia kuwakabili wanamgambo wa Al Shabaab ambao wanadhaniwa kuwa wamekuwa wakitekeleza mashambulizi nchini Kenya na kutorokea Somalia.
Baadhi ya mashambulizi makubwa kuwahi kufanyika lile la Westgate jijini Nairobi ambako zaidi ya watu sitini waliuawa na huko Mpeketoni katika pwani ya Kenya.
Serikali ya Kenya imesisitiza kuwa jeshi la Kenya liliwaua zaidi ya wapiganaji 100 wa Al-shabaab wanaodaiwa kuhusika na mauji ya watu 28 waliokuwa wakisafiri kwenye basi kutoka Mandera kuelekea katika sehemu nyingi za nchini ila baadhi wananchi wanatilia shaka kauli hiyo.
Share:

Kauli ya Bi Maria Nyerere kuhusu Escrow........BBC


Mjane wa Hayati Baba wa Rais wa kwanza wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere, Maria Nyerere, amezungumzia sakata ya ESCROW iliyozungumziwa bungeni mjini Dodoma na kupendekeza ripoti ya mgogoro huo wa IPTL kujadiliwa kwa uwazi ili kupata ufumbuzi na wahusika kuwajibishwa kwa manufaa ya umaa.
Share:

Vyuo vya Tanzania vyafeli katika mjadala........ BBC


Vyuo vikuu vitatu vya Tanzania ambavyo vilishiriki katika mashindano ya mjadala wa Afrika kuhusu Sheria za kimataifa za haki za kibinaadamu yalioandaliwa na kamati ya kimataifa ya shirika la msalaba mwekundu ICRC vimeshindwa kufika katika raundi ya mwisho.
Badala yake vyuo hivyo viliondolewa katika raundi za mapema ambapo mataifa manane ya Afrika yalishiriki.
ICRC imekuwa ikiandaa hafla kama hizo kwa kipindi cha miaka 14 sasa mjini Arusha.
Kulingana na gazeti la the Citizen nchini Tanzania, vyuo vilivyoiwakilisha Tanzania ni chuo cha kanisa katoliki cha Ruaha kutoka Iringa,Chuo cha Iringa na Chuo kikuu cha Zanzibar.
Katika raundi ya mwisho ya mashindano hayo yaliofanyika mwishoni mwa wiki katika mahakama maalum ya kimataifa inayochunguza mauaji ya kimbari nchini Rwanda ICTR mjini Arusha,chuo cha Strathmore University kutoka Kenya kiliibuka mshindi na kufuatiwa na chuo cha Christian University kutoka Uganda huku chuo cha Kunduyi pasi kutoka Zimbabwe kikiibuka mshindi wa spika bora.
Raundi ya mwisho ya mjadala huo ilisimamiwa na jaji wa mahakama hiyo Vagn Joensen,jaji wa mahakama kuu ya Tanzania Stella Mugasha,jaji wa mahakama ya haki katika Afrika mashariki Fanstin Ntezilyayo,John Joseph Wamwara na Mutsa mangezi kutoka ICRC.
Judge Joensen, ambaye alitoa zawadi kwa washindi aliyapongeza mashindano hayo kama kifaa cha kuwahamasisha wanafunzi wa vyuo vikuu wanaofanya sheria na kwamba itasaidia kuimarisha maono yao katika siku za usoni.
Share:

Kashfa ya ESCROW vigogo watajwa TZ..........

Ripoti ya Kamati ya bunge ya Hesabu za Serikali imewataja baadhi ya vigogo wanaohusika na kashfa ya IPTL Nchini Tanzania akiwemo Waziri Mkuu na kuwataka kuwajibika kisiasa na kisheria.
Sakata hiyo ya IPTL inahusihswa na upotevu wa mamilioni ya fedha na kwa muda mrefu umezusha mjadala mzito katika bunge la Tanzania.
Katika ripoti hiyo iliyowasilishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Zitto Kabwe na makamu mwenyekiti Deo Filikunjombe, imethibitisha kuwepo mazingira ya udanganyifu na ufisadi katika mchakato wa malipo yaliyofanyika na kueleza kuwa upotevu huo wa fedha ungeweza kudhibitiwa kama kungekuwa na uwajibikaji wa kutosha kwa baadhi ya viongozi.
Kamati hiyo imewataja viongozi wengine wanaotakiwa kuwajibika kutokana na kashfa hiyo kuwa ni mwanasheria,Waziri wa nishati na Madini, Naibu Waziri wa Nishati pamoja na viongozi wengine wa bodi.
Kashfa nyingine zilizowahi chukua uzito mkubwa katika bunge la Tanzania na kusababisha viongozi kuwajibika wakiwemo Waziri Mkuu ni pamoja na kashafa ya Richmond,EPA na sasa hii ya ESCROW ambayo kwa mara nyingine kamati hiyo imeonyesha wazi mapendekezo yake ya kutaka kuwajibika kwa waziri mkuu, Mawaziri na viongozi wengine.
Share:

Tuesday 25 November 2014

Jengo laanguka, Kumi wafa Misri........ BBC


Watu kumi wamepoteza maisha baada ya jengo la ghorofa kuanguka mjini Cairo nchini Misri, maafisa wameeleza.
Watu saba wamejeruhiwa baada ya jengo la ghorofa nane kuanguka usiku.
Mkuu wa Idara ya dharula Jenerali Mamdouh Abdul Qader amesema vikosi vya uaokoaji vinawasaka Watu 15 wanaokisiwa kunasa kwenye kifusi.
Mara kadhaa majengo yameanguka nchini humo, sababu kubwa ikiwa ujenzi usiofuata kanuni na Sheria pia usimamizi mbovu wa taratibu za ujenzi.
Jenerali Qader ameliambia shirika la Habari la Ufaransa kuwa hawajui chanzo cha ajali hiyo,lakini walipatiwa taarifa kuwa ghorofa mbili za juu zilijengwa kinyume cha sheria.
Wakazi wa majengo ya karibu na lilipoanguka jengo hilo wameondoka katika makazi yao kwa nia ya kujihadhari.
Mwezi Januari Mwaka jana,Watu 28 walipoteza maisha baada ya jengo la ghorofa nane kuanguka mjini Alexandria.
Share:

Mfanyakazi mkatili matatani Uganda.......


Polisi wamebadilisha mashtaka ya mfanyikazi wa nyumbani aliyenaswa kwa kamera akimpiga na kumtendea unyama mtoto wa mwaka mmoja na nusu, kutoka kwa kosa la kutesa na sasa anakabiliwa na kosa la jaribio la mauaji.
Video hiyo iliwaudhi watu wengi sana kwenye mitandao ya kijamii ila babake mtoto huyo alisema walisambaza video hiyo ili kuwatahadharisha wazazi wenegine.
Mfanyakazi huyo wa nyumbani Jolly Tumuhirwe, alikuwa amezuiliwa katika gereza la Luzira na mahakama ya Nakawa kwa kosa la kutesa chini ya kifungo cha 41 kwenye katiba kinachoongelea dhidi ya mateso.
Mwanamke huyo sasa anatarajiwa kufikishwa mahakamani tarehe 8 Disemba.
Hata hivyo, msemaji wa polisi Bwana Fred Enanga, amesema "shtaka dhidi ya mwanamke huyo lilibadilishwa baada ya kupitiwa mwendesha mkuu wa mashitaka.
Tumuhirwe alikubali kosa la kumpiga mtoto huyo kwa kurunzi, tuki olililonaswa kwa kamara ya CCTV. Polisi walimfanyia Tumuhirwe uchunguzi wa kiakili na kubaini kuwa ana akili timamu.
Afisaa mkuu wa polisi Fred Enaga, amewaonya waajiri kuchunguza mbinu zinazotumika kuwachagua wasichana wa kazi, kwa sababu matendo kama haya yanaweza kutokana na matatizo ya kisaikologia.
Waziri wa Jinsia, Kazi na maendeleo ya jamii Bi Mary Karooro Okurut alipongeza juhudi za wazazi wa mtoto huyo Arnella "kutokana na kitendo hicho kwa mtoto. Ingekuwa mtu mwingine angemuua mischana huyo wa kazi lakini alifuata sheria. Pia tunapeleka marekebisho katika katiba kuhusu maslai ya watoto bungeni kuimarisha sheria zinazowajali watoto," alisema waziri huyo.
Polisi wamesema kuwa nia ya shambulio hilo haijatambulika na pia msichana huyo amefanyia kazi familia hiyo kwa siku 26 pekee. Wazazi wamesema kuwa mtoto huyo ametolewa hosipitalini na hali yake ya afya inaimarika.
Kulingana na msemaji wa polisi Fred Enaga, kesi hiyo iliripotiwa na Baba ya mtoto Erick Kamanzi mnamo tarehe 13 Novemba katika kituo cha polisi cha Kiwatule baada ya kuona video hio.
Kesi hiyo ilipelekwa kwa kitengo cha polisi cha Kiira. Baada ya uchunguzi, msichana huyo wa kazi alihukumiwa na shataka la mateso katika mahakama ya Nakawa na kuzuuliwa katika gereza la Luzira.
Bwana Enaga alisema Bi Tumuhirwe alishtakiwa chini ya kifungo cha tatu kwenye katika kinacholinda maslahi ya watoto. Kifungo hicho kinajumuisha mashataka kama ya kutesa inayopeana uwezekano wa kumfunga mtu hadi miaka 15 gerezani.

Hata hivyo, Bwana Enaga anashauriana na mkurugegenzi wa pande za mashtaka kurebisha hukumu hilo kuwa kifungu cha maisha.
Share:

Sunday 23 November 2014

Kenya yauwa al-Shabaab 100.........source BBC


Makamo wa rais wa Kenya, William Ruto, anasema kuwa askari wa usalama wa Kenya wamewaandama wapiganaji wa al-Shabaab hadi kwenye kambi yao nchini Somalia, baada ya shambulio dhidi ya basi kaskazini-mashariki mwa Kenya hapo jana ambapo raia 28 waliuliwa.
Bwana Ruto alisema wapiganaji zaidi ya 100 waliuliwa katika operesheni mbili tofauti. Alisema kambi ya al-Shabaab iliangamizwa. Habari hizo hazikuthibitishwa na upande wa pili.
Gavana wa Mandera - ambako shambulio la jana lilitokea - amelaumu vikosi vya usalama kwa kushindwa kuwalinda raia. Alisema polisi kawaida wanashindwa kufanya uchunguzi kamili baada ya mashambulio.
Share:

Mauaji yanalenga kuzua uhasama wa kidini...........BBC

Baadhi ya miili ya abiria waliouawa na Al-Shabaab eneo la Mandera, Kenya.

Basi lililotekwa na Al-Shabaab eneo la Mandera likiwa njiani kuelekea Nairobi.


Mshauri wa ngazi ya juu wa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa mauaji ya watu 28 waliokuwa wakisafiri kwenye basi moja yalilenga kusababisha vita vya kidini nchini kenya.
Kwenye mahojiano na BBC Abdikadir Mohammed alitoa wito kwa wakenya kutoka imani zote kuungana pamoja dhidi ya kile alichokitaja kuwa vitendo vya uhalifu.
Wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab waliwapiga risasi wasafiri ambao hawangeweza kukariri Koran.
Al Shabaab ilisema kuwa shambulizi hilo lilikuwa la kulipiza kisasi mauji ya hivi majuzi ya waislamu yaliofanywa na wanajeshi wa Kenya kwenye mji wa pwani wa Mombasa.

Serikali ya Kenya imesema kuwa imeanza kuwatambua waliotekeleza mauaji hayo na itawafikisha mbele ya sheria hivi karibuni.
Share:

Wanamgambo wawateka watoto 10 Mali.........BBC


Maafisa wa kijeshi nchini Mali wanasema kuwa watu waliokuwa na silaha wamewateka nyara watoto kumi na kuwaua wawili ambao walijaribu kupinga kutekwa karibu na mji wa Kidal.
Afisa mmoja alisema kuwa watoto hao walilazimishwa kuwa wanajeshi.

Maeneo yanayozunguka mji wa Kidal yanadhibitiwa na kundi la kiislamu lililojitenga ambalo lilidhibiti eneo la kaskazini nchini Mali mwaka 2012 lakini baadaye likatimuliwa na wanajeshi wa Ufaransa kwa ushirikiano na vikosi vya muungano wa Afrika.
Share:

Boko Haram wauwa 100 hivi karibuni.........BBC


Ripoti kutoka kaskazini-mashariki mwa Nigeria zinaarifu kuwa kundi la wapiganaji Waislamu la Boko Haram, limefanya mashambulio mawili makubwa katika siku chache za karibuni ambapo watu karibu 100 wameuwawa.
Kiongozi mmoja katika jimbo la Borno alisema kuwa wapiganaji waliuwa wauza samaki karibu 50 karibu na kijiji cha Doron Baga, kando ya Ziwa Chad.
Alisema wapiganaji wa Boko Haram wameweka kizuizi kwenye njia ya kuelekea Chad na kuwakamata wachuuzi waliokuwa wakienda kununua samaki.
Katika tukio jengine hapo awali watu karibu 50 waliripotiwa kuwa waliuwawa karibu na mpaka wa Cameroon pale Boko Haram walipovamia kijiji cha Azara Kuya, siku ambapo soko huwa na watu wengi
Share:

Saturday 22 November 2014

Waliofanya shambulio la Mandera wasakwa...... BBC


Maiti za watu waliouliwa na al-Shabaab Jumamosi asubuhi nje ya mji wa Mandera, Kenya, karibu na mpaka wa Somalia, zilipelekwa na wanajeshi hadi mjini humo.
Serikali ilikuwa inajitayarisha kusafirisha miili hiyo hadi mji mkuu, Nairobi.
Basi lililokuwa limebeba abiria 60 lilitekwa nyara alfajiri na abiria 28 walipigwa risasi na kuuwawa.
Wengi waliouwawa ni kutoka maeneo mengine ya Kenya ambao wakifanya kazi Mandera.
Inasemekana kuwa wengi wao walikuwa waalimu na wafanyakazi wa wizara ya afya ambao walikuwa wanarudi nyumbani kuwa na familia zao wakati wa Noeli.
Msemaji wa wapiganaji wa Somalia, al-Shabaab, alidai kuwa walihusika na shambulio hilo.

Wanajeshi na polisi wametumwa huko kwenda kuwasaka wale waliohusika na shambulio hilo lakini hakuna taarifa kuwa wamekamatwa.
Share:

RAIS KIKWETE ATOLEWA NYUZI KATIKA MSHONO, AFYA YAKE YAZIDI KUIMARIKA......Global Publisher




Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland baada ya kutolewa nyuzi katika mshono baada ya kufanyiwa upasuaji wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na ushauri. Kulia kwake ni Daktari wa Rais Profesa Mohamed Janabi.

























Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amepumzika kwenye hoteli maalumu baada ya kutoka katika hospitali ya Johns Hopkins iliyopo Baltimore Maryland alikotolewa nyuzi katika mshono baada ya kufanyiwa upasuaji wa Tezi Dume wiki iliyopita. Rais Kikwete anatarajiwa kurudi tena hospitalini hapo Jumatatu kwa ukaguzi wa maendeleo ya kidonda na ushauri.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.