Wednesday 28 October 2015

Matokeo ya uchaguzi Zanzibar yafutwa....source BBC


Mwenyekiti wa ZEC amesema uchaguzi huo unafaa kurudiwa

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha ametangaza kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi visiwani humo akisema uchaguzi huo ulijaa kasoro nyingi.
Kulingana na mwanahabari wa BBC aliyeko hilo Sammy Awami, mwenyekiti huyo ametangaza hatua hiyo kupitia runinga ya serikali visiwani ZBC.
Bw Jecha amesema kuwa uchaguzi huo haukuwa wa haki na kwamba kulikuwa na ukiukaji mkubwa wa sheria za uchaguzi, kwa mujibu wa taarifa ambayo baadaye imetumwa kwa vyombo vya habari.
Amesema baadhi ya makamishna wa tume hiyo, badala ya kutekeleza majukumu yao inavyotakiwa kikatiba "wamekuwa ni wawakilishi wa vyama vyao".
"Kumegundulika kasoro nyingi katika uchaguzi huu miongoni mwa hizo ni kubainika kwa baadhi ya vituo hasa Pemba vimekuwa na kura nyingi kuliko daftari la wapiga kura wa kituo husika."
Amesema hilo ni jambo la kushangaza ikizingatiwa kwamba "baadhi ya wapiga kura hawakwenda kuchukua vitambulisho vyao vya kupigia kura".
Kadhalika, amesema kura hazikupata ulinzi mzuri hususan kisiwani Pemba ambako amesema kuwa baadhi ya mawakala wa baadhi ya vya vyama vya siasa katika kisiwa hicho walifukuzwa.
Ameongezea kuwa vijana katika eneo hilo walivamia vituo vya kupigia kura kwa lengo la kutaka kuzua ghasia, na pia vyama vya siasa vilionekana "kuingilia majukumu ya tume ikiwemo kujitangazia ushindi na kupelekea mashindikizo kwa tume."

Hii ni sehemu ya taarifa ya Bw Jecha

"Nimeridhika kwamba uchaguzi huu haukiwa wa haki na kuna ukiukwaji mkubwa wa sheria na taratibu za uchaguzi," amesema Bw Jecha.
"Hivyo, kwa uwezo nilionao natangaza rasmi kwamba uchaguzi huu na matokeo yake yote yamefutwa na kwamba kuna haja ya kurudia uchaguzi huu."
Tangazo la mwenyekiti huyo limetolewa huku hali ya wasiwasi ikiendelea kutanda visiwani humo.
Siku moja baada ya uchaguzi kufanywa, mgombea wa chama cha upinzani cha Civic United From (CUF) Seif Sharif Hamad alijitangaza kuwa mshindi, hatua iliyokemewa na chama cha CCM ambacho mgombea wake Dkt Ali Mohamed Shein amekuwa rais wa visiwa hivyo muhula unaomalizika.
Tume ya uchaguzi visiwani humo pia ilishutumu hatua ya mgombea huyo. Kabla ya kufutiliwa mbali kwa matokeo ya uchaguzi, tume hiyo ya uchaguzi ilikuwa imetangaza matokeo ya majimbo 31 kati ya majimbo 54 visiwani humo.
Hayo yakijiri Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania inaendelea kutoa matokeo ya uchaguzi wa urais. Kufikia sasa imetoa matokeo ya majimbo 155 kati ya majimbo 264.
Share:

Sababu 8 za kufutwa kwa uchaguzi Zanzibar... source BBC


Hizi ndizo sababu nane zilizotolewa na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wa kisiwani Zanzibar Bw Jecha Salim Jecha kuhusu kufutiliwa mbali kwa matokeo ya uchaguzi wa eneo hilo.
1. Makamishna wa uchaguzi katika tume hiyo walipigana kutokana na tofauti zao
2. Makamishna walikuwa na upendeleo fulani.
3. Katika vituo vyengine, hususan kisiwani Pemba,ambacho ni miliki ya Zanzibar, kura zilizopigwa zilikuwa zaidi ya zilizosajiliwa.
4. Masanduku ya kupigia kura hayakupewa ulinzi wa kutosha na maajenti pamoja na maafisa wa uchaguzi.
5. Maajenti wa vyama walifukuzwa katika vituo kadhaa.
6. Vijana walivamia vituo vya kupigia kura wakiwa na lengo la kuzua ghasia.
7. Vyama vya kisiasa vimekuwa vikiingilia tume hiyo.
8.Kura ziliharibiwa hususan zile kutoka Pemba
Share:

Lowassa apinga matokeo ya uchaguzi TZ... source BBC


Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha CHADEMA Edward Lowassa amesema kuwa hatokubali matokeo ya uchaguzi wa urais yanayoendelea kutolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania (NEC).
Kiongozi huyo amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha kwamba kuna udanganyifu uliofanyika.
Amesema kuwa kura za chama hicho zimepunguzwa katika vituo vingi vya kupigia kura.
Akihutubia wanahabari pamoja na viongozi wengine wa upinzani, amesema kwamba kura zilizohesabiwa katika maeneo tofauti haziambatani na matokeo yaliyotolewa.
Lowassa ameongezea kwamba maeneo yote ambayo walipata ushindi yamecheleweshwa. Aidha, amelalamikia kukamatwa kwa maajenti wa chama hicho akidai kuwa ni ishara za kutaka kuiba kura.
Share:

Jeshi lakomboa 300 kutoka kwa Boko Haram Nigeria... source BBC

Boko Haram
Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa limefanikiwa kuwakomboa watu 338 kutoka kwa wapiganaji wa Kiislamu wa Boko Haram.
Wapiganaji 30 waliuawa kwenye operesheni hiyo kwenye ngome moja ya kundi hilo katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo mnamo Jumanne.
Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa jeshi Kanali Sanni Kukasheka Usman, wanajeshi walishambulia kambi za wapiganaji hao kwenye msimu wa Sambisa na kukomboa watoto karibu 200, wanawake mia moja na wanaume wanane.
Mwandishi wa BBC aliye Abuja Chris Ewokor anasema kufikia sasa hakujatolewa maelezo zaidi kuhusu watu waliokombolewa.
Operesheni hiyo ni moja ya operesheni kubwa zaidi kufanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya wanamgambo hao.
Boko Haram
Jeshi linaonekana kujikakamua kutimiza makataa ya miezi mitatu ambayo walipewa na Rais Muhammadu Buhari kuwashinda Boko Haram, ingawa muda unayoyoma.
Wanamgambo hao wamekuwa wakitekeleza mashambulio ya kujitoa mhanga na kuua watu wengi kaskazini mashariki mwa taifa hilo, wengi wao waumini wa dini ya Kiislamu misikitini.
Share:

Ouattara ashinda uchaguzi Ivory Coast... source BBC



Alassane Ouattara ameshinda uchaguzi wa urais nchini Ivory Coast kwa wingi wa kura. Matokeo yalitangazwa kupitia runinga huku rais huyo akishinda kwa asilimia 83.66.
Hii inamaanisha kwamba hakutakuwa na duru ya pili ya uchaguzi.
Raia wa Ivory Coast waliamkia habari za ushindi wa Rais Alassane Outtara kama walivyotarajiwa kwamba rais huyo ataongoza kwa muhula mwengine wa miaka mitano.
Baada ya mwongo mmoja wa kutoimarika kwa uchumi na vita vya wenyewe kwa wenyewe, wengi watafurahia kwamba uchaguzi huo ulifanyika kwa amani.
Uchaguzi wa mwisho wa urais uliofanyika mwaka 2010 ulisababisha vita vya miezi mitano ambapo zaidi ya watu elfu 3000 waliuawa.
Rais wa zamani Laurent Gbagbo, yuko mjini the Hague katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita akingojea kesi inayomkabili.
Ijapokuwa rais huyo amekosolewa kwa kushindwa kuleta maridhiano na haki, amesifiwa kwa kuimarisha uchumi wa taifa hilo na kulifanya kuwa taifa lenye uchumi ulioimarika kama ilivyokuwa miaka ya sabini.
Share:

Wednesday 9 September 2015

Vifo vinavyotokana na nyoka kuongezeka?


Shirika la kimataifa la misaada, Medecins Sans Frontieres, limeonya kwamba vifo vitokanavyo na kuumwa na nyoka huenda vikaongezeka. Hali hii inasababishwa na kuisha kwa akiba za dawa inayotibu sumu ya nyoka. Inadhaniwa kwamba watu laki moja huuawa na nyoka kila mwaka.

Share:

Mtoto aliyeibiwa apatikana baada ya miezi 4.


Mahakama nchini El Salvador imeamuru mtoto aliyebadilishwa punde baada ya kuzaliwa kukutanishwa na wazazi wake halisi miezi minne baadaye
Mahakama hiyo iliamuru uchunguziwa kina kufanyika kuhusiana na daktari aliyeshutumiwa na mama kwa kumbadilishia mtoto wake wakati wa kujifungua.
Mama huyo, Mercedes Casanella,anasema kwamba mtoto aliyemuona muda mfupi baada ya kujifungua mwezi May alikua na ngozi nyeupe na maumbile
tofauti na yule aliyekabidhiwa baadae .
Mtoto Mweusi
''Mtoto niliyemuona alikuwa na rangi ya hudhurungi lakini yule aliyeletwa alikuwa ni mweusi titi ti''
Kipimo cha vinasaba DNA kimethibitisha kwamba mtoto huyo mchanga si wa mwanamke huyo kibayolojia.
Bi Casanella anasema kuwa daktari huyo Alejandro Guidos alikuwa amekusudia kufanya mabadiliko hayo.

Vyombo vya habari nchini humo vinasema kwamba matokeo ya uchunguzi wa vinasaba umebaini mtoto huyo si wa bi Casanella na mumewe.
Aidha hayo yalitiliwa pondo na matokeo ya uchunguzi uliofanywa kwa watoto wote waliozaliwa katika zahanati hiyo ya afya katika siku hiyo moja.
Wazazi wa mtoto huyo wamemshutumu dakatari , Alejandro Guidos, kwa kumuuza mtoto wao mweupe kwa wafanyabiashara haramu ya watoto , lakini alikana kufanya kosa lolote
Share:

Guterres aomba wakimbizi waruhusiwe Ulaya


Kamishna wa tume ya Umoja wa Mataifa, anayehusika na masuala ya wakimbizi, Antonio Guterres, ameyaomba mataifa ya Ulaya kuwakubali wakimbizi laki mbili wanaokimbia mapigano nchini Syria, Iraq na Afghanistan.
Bwana Guterres amesema kuwa jibu lao huenda likaathiri mustakabali wa muungano wa Ulaya.
Kamishna Guterres amewasihi viongozi wa Ulaya kutafuta namna ya kuwaruhusu wakimbizi halali kuingia Ulaya kwa urahisi.
Kamishna huyo wa Umoja wa Mataifa, ameonya kuwa nchi za Ulaya haziwezi kuendelea kushughulikia suala hili la wakimbizi kila moja kwa njia yake.
Amesema kuwa bara hilo likikosa kushikana kwa pamoja kuhusu suala hili watakaonufaika ni walanguzi wa binadamu na mawakala wa wahamiaji.

Awali wajumbe kutoka tume ya Ulaya, walianza ziara katika kisiwa cha Kos, nchini Ugiriki, ambako maelfu ya wakimbizi wamekuwa wakiwasili kila siku.
Wengi wa wakimbizi hao, wamelalamika kuwa inawachukua muda mrefu, kabla ya kupata stakabadhi wanazohitaji kuondoka kisiwani humo.
Serikali ya Ugiriki imeahidi kuharakisha shughuli hiyo, lakini kamishna wa Ugiriki, anayehusika na masuala ya uhamiaji amesema kuwa ni lazima mataifa yote ya Ulaya, yashirikiane kutafuta suluhisho la kudumu.
Ziara hii ya tume ya Ulaya, ndio ya punde zaidi katika msururu wa juhudi za kutafutia ufumbuzi janga la uhamiaji barani Ulaya.
Share:

Punda na farasi ni marufuku Nigeria


Jeshi la Nigeria limepiga marufuku matumizi ya farasi na punda katika jimbo la Kaskazini Mashariki la Borno, kama sehemu ya juhudi za vita dhidi ya Boko Haram .
Kundi hilo limekua likitumia farasi kutekeleza mashambulizi dhidi ya wanavijiji

Huku jeshi la Nigeria likionekana kupata mafanikio katika vita vyake dhidi ya Boko Haram, kundi hilo linaripotiwa kukabiliwa na kibarua kigumu kupata mafuta ya kuweka kwenye magari yake kwa hivyo hutumia farasi kwa usafiri mbadala.
Lakini tayari kuna marufuku ya matumizi ya piki piki ambazo zilikuwa zikitumiwa na wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram kuwasafirisha wapiganaji wake katika mashambulizi.

Pikipiki hizo zilirahisisha kutoroka kwa washambulizi , kwa hivyo kwa sasa kuna hofu kwamba marufuku ya sasa itadhoofisha zaidi uchumi wa maeneo ya vijijini na kuathiri maisha ya watu wa kawaida.
Punda hutumiwa kwa kusafirishia bidhaa na mara nyingi farasi huendeshwa katika tamasha za kidini na kitamaduni.
Share:

Papa Francis kurahisisha sheria ya talaka.


Papa Francis anatarajia kurahisisha taratibu zinazoruhusu wafuasi wa kanisa katoliki waliooana kutoa talaka na kuolewa tena huku wakibakia kuwa wafuasi wa katika kanisa hilo .
Maelezo ya taratibu hizo yanatarajiwa kutangazwa mjini Vatcan baadaye leo .
Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa mbinu ya kurekebisha taratibu hizo zinazoruhusu wanandoa kuachana na kupunguza gharama .

Bila sheria hiyo wanandoa wa kikatoliki wanaotalikiana na kuolewa upya hutazamwa kama wazinifu na hawaruhusiwi kupokea komunio.
Mwandishi wa BBC mjini Vatican anasema kuwa Papa Francis hatabadilisha mafunzo ya katoliki kuhusu kuachana kwa wanandoa , lakini atawezesha kurahisisha wanandoa wenye matatizo kuthibitisha kuwa ndoa yao haikuwa ya maana tangu mwanzo
Share:

Mpango wa kutega mabomu watibuliwa Kenya


Wanaume watatu wamakamatwa mjini Nairobi nchini Kenya baada ya mtu mmoja kuzuiwa wakati anajaribu kuingia katika jengo la maduka akiwa na kifaa cha kilipuzi katika mkoba wake.
Kifaa hiko kiliharibiwa na polisi wa kitengo cha kutegua mabomu nchini kenya.
Shuhuda anasema watu hao watatu walisimamishwa na walinzi wa usalama wakiwa wanajaribu kuingia katika jengo moja la maduka la Garden city Mall kwenye kitongoji kimoja Nairobi.
Mmoja wa wanaume hao alikataa kukaguliwa hivyo ilibidi walinzi wamdhibiti wa kumpiga ngumi.
Milipuko iligunduliwa katika mkoba wake.
Wateja na wafanyakazi wa maduka hayo waliondolewa na kifaa hicho kiliharibiwa na kitengo maalum cha kudhibiti mabomu.
Polisi anasema wanaume wote watatu wanaoshukiwa kuwa ni raia wa Kenya wamekamatwa.
Inaaminiwa kuwa bomu hilo ni kilipuzi kidogo chenye betri na kilichounganishwa kwenye simu ya mkonon ambayo ingetumia kulipua bomu hilo.
Miaka miwili iliyopita watu 67 waliuawa baada ya wanamgambo wa Al Shabaab kuvamia maduka ya Wastegate mjini Nairobi.
Share:

Waandamanaji wafanya vurugu Uturuki


Maelfu ya waandamanaji waliokuwa wakipepea bendera za Uturuki wamevamia makao makuu ya chama kikuu cha Kikurdi cha HDP.
Jengo hilo lililoko katika mji mkuu wa Ankara baada ya kuvamiwa lilichomwa moto.
Chama hicho baadaye kilitoa maelezo kwamba majengo yake mengine yaliyoko kwenye miji mingine yalilengwa pia,mjini Kabul ambamo ziko ofisi za gazeti moja la Hurriyet zilishambuliwa kwa mara ya pili katika kipindi cha wiki mbili .
Naye waziri mkuu wa Uturuki Ahmet Davutoglu amelaani vikali mashambulizi na uvamizi huo katika ofisi za kisiasa na hata kwa nyumba za habari na ametoa wito wa kusitisha ghasia.
Mpaka sasa askari jeshi kumi na wanne wa Uturuji wanaarifiwa kupoteza maisha mapema wiki hii katika shambulio la bomu upande wa mashariki mwa nchi hiyo.
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema majeshi yake yatapambana na magaidi wa nchi hiyo.
"Hatujaacha matarajio ya watu wetu na hatutaacha kwa magaidi, kwa makundi ya wanaotaka kuipindua nchi na washirika wao. Uturuki ambaye imewezakushinda mambo mengi hapo nyumba hadi sasa, itashughulikia suala la magaidi. Nchi yetu na wanajeshi wake, polisi na maafisa ujasusi wanajitahidi kupambana na makundi ya kigaidi nayogawa nchi pamoja silaha zao. Hadi sasa uharibufu mkubwa umefanywa na makundi hayo, kutoka ndani na nje ya mipaka yetu. matukio ya hivi sasa ni ya ziada, na kuchanganyikiwa kwa makundi hayo ni jambo tulilolizoea." amesema Erdogan.
Share:

Saturday 29 August 2015

Waandishi wa Al Jazeera miaka 3 Jela


Mahakama nchini Misri imewahukumu waandishi watatu wa kituo cha runinga cha Al jazeera miaka mitatu jela.
Wakati wa kutolewa kwa hukumu hiyo, Mohamed Fahmy, Peter Greste na Baher Mohamed walipatikana na hatia ya kutangaza habari za uongo na kulisaidia kundi la Muslim Brotherhood ambalo kwa sasa linatambuliwa kuwa kundi la kigaidi.
Baher Mohamed pia alihukumiwa kifungo kingine cha miezi sita.
Hata hivyo Peter Greste, yuko nje ya nchi baada ya kutimuliwa kutoka nchini humo mwezi Ferbruari.
Share:

Mkutano wa usalama kufanyika Ufaransa


Mawaziri wa masuala ya ndani wa nchi za ulaya wakutana mmji Paris hii leo kujadili njia za kuboresha usalama kwenye usafiri wa reli baada ya shambulizi lililotibuka wiki iliyopita kwenye treni iliyokuwa safarini kutoka Amsterdam kwenda Paris.
Ufaransa inataka kutangaza hatua kali za usalama ikiwemo vifaa vya kutambua chuma kwenye treni za kimataifa, kuweka wahudumu waliojihami na mifumo ya mawasiliano iliyoboreka kufuatilia mienendo ya wanamgambo walioshukiwa.

Raia wa Morocco ambaye alikuwa amejihami vikali (Ayub al-Khazani) ambaye alishindwa nguvu na abiria baada kupanda treni mjini Brussels alikuwa akifanya safari kote barani Ulaya hata baada uhispania kutoa onyo kuwa huenda mtu huyo alikuwa ni gaidi.
Share:

Ban aitaka ulaya kuwasaidia wahamiaji


Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki Moon ametoa wito kwa serikali zote zinazolishughulikia suala la wakimbizi barani ulaya kutenga maeneo salama kwa wahamiaji na kuonyesha utu.
Ban amesema kuwa idadi kubwa ya wakimbizi na wahamiaji ni ishara ya matatizo makubwa kama ya vita vilivyo nchini Syria ambapo ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuonyesha moyo wa kutatua mizozo kama hiyo.

Ban amesema kuwa masuala hayo yatapewa kipaumbele wakati viongozi wa dunia watapokusanyika kwenye mkutano wa umoja wa mataifa mwezi ujao.
Mapema umoja wa mataifa uliwataka viongozi wa nchi za ulaya kuzuia vifo vya wahamiaji baada ya mamia kuaga dunia siku tatu zilizopita.
Share:

Mafuriko yaua 20 Dominica


Waziri mkuu nchini Dominica anasema kuwa watu 20 wanariporitiwa kuaga dunia kwenye mafuriko yaliyosababishwa na kimbunga Erika.
Kwa njia ya televisheni Roosevelt Skerrit alisema kuwa mamia ya nyumba, madaraja na barabara vimeharibiwa na kisiwa hicho kumerudishwa nyuma miaka ishirini.
Kimbunga kwa sasa kinazikumba Haiti na Jamhuri ya Dominica kikiwa na upepo unaovuma kwa kasi ya karibu kilomita 85 kwa saa.
Watabiti wa hali hewa wanaseme kuwa hata hivyo kinaonyesha dalili za kupoteza nguvu zake.
Share:

Yaliomo kwenye makubaliano ya S.kusini


Hivi ndio vipengee vikuu kwenye makubaliano ya amani ambayo rais wa Sudan kusini Salva Kiir anatarajiwa kusiani Juba:
Mapigano yasite mara moja. Wanajeshi wasalie kweny kambi zao kwa siku 30, vikosi vya nje viondoke katika siku 45 na watoto wanaotumiwa jeshini na wafungwa wa vita waachiliwe huru.
Vikosi vyote vya usalama vitoke umbali wa kilomita 25 kutoka Juba, nabadala yake vikosi maalum na polisi ya pomoja vichukuwe nafasi hiyo.
Waasi wapewe cheo cha "makamu wa kwanza wa rais"
Serikali ya mpito ya muungano wa kitaifa iidhinishwe katika muda wa siku 90 na iongoze nchi kwa miezi 30.
Uchaguzi ufanyike siku 60 kablaya ya kumalizika kipindi cha mpito.
Serikali ipate uwingiwa nyadhifa serikalini katika kiwango cha kitaifa na katika majimbo 7 kati ya 10 yaliopo.
Katika majimbo yanayokumbwa na vita - Jonglei, Unity, na Upper Nile - waasi wanapata uwakilishi ulio sawana serikali.
Tume ya ukweli na mapatano ichunguze ukiukaji wa haki za binaadamu.
Share:

Kidimbwi kinachounganisha majumba 2 UK


Kidimbwi cha kuogelea chenye urefu wa mita 25 kinachounganisha kilele cha majumba mawili marefu yenye ghorofa 10 kitajengwa mjini London.
Kidimbwi hicho kinachoitwa ''Sky Pool'' ni cha kwanza duniani na kitakuwa na eneo la chini lililo wazi.Uwazi huo utawasaidia waogoleaji kuwaona raia wanaotembea chini ya majumba hayo kwa urefu wa mita 35.
Kampuni ya Eckersley O'Callaghan ambayo imeshirikiana na ile ya Apple kuhusu mtindo wa kidimbwi hicho cha kuogelea itatengeza mradi huo.
Kidimbwi hicho ni miongoni mwa miradi ya ujenzi ya maeneo ya kujivinjari kwa jina Embassy Gardens at Nine Elms,karibu na kituo cha umeme cha Battersea

Inatarajiwa kuwa mradi huo utakamilika ifikiapo mwaka 2019,lakini mtindo huo una changamoto zake hususan kutokana na hatua kwamba kidimbwi hicho kitazuiliwa na misukumo itakayotoka kutoka kuta za majumba hayo mawili ambayo yamejengwa na misingi tofauti.
''Upepo unapovuma majumba hayo huyumba tofauti na hivyobasi kuwa changamoto kwa watengezaji wa kidimbwi hicho'' kulingana na Brian Eckersley
Share:

Treni iliyosheheni dhahabu yapatikana


Afisa mmoja wa serikali ya Poland, amesema kuwa ana imani kuwa treni moja ya kijeshi ambayo imefichwa tangu vita vya pili vya dunia, zaidi ya miaka sababini iliyopita, na kusemekana kubeba vitu vya dhamani, imepatikana, chini ya ardhi Kusini Magharibi mwa nchi hiyo.
Naibu waziri wa utamaduni amesema shehena iliyoko kwenye treni hiyo bado haijulikani.
Kwa mujibu wa ripoti treni hiyo ilipotea ikiwa imejaa shehena ya dhahabu kutoka mji wa Breslau nchini Ujerumani, mji ambao kwa sasa unajulikana kama Wroclaw and sehemu zingine za Poland, wakati wanajeshi wa Ujerumani walipokaribi mji huo.
Afisa mkuu wa makavazi ya kitaifa, Piotr Zuchowski, amesema anaimani kuwa treni hiyo itapatikana chini ya ardi karibu na mji wa Walbrzych.
Amesema ameona picha zilizopigwa na kifaa maalum chini ya ardhi ikionyesga treni hiyo yenye urefu wa karibu mita mia moja ikiwa na bunduki juu yake.
Amesema hamna anayefahamu kile treni hiyo ilikuwa imebeba wakati huo na asema anatarajia iwe na vitu vya Sanaa vilivyoibiwa nchini Ujerumani wakati wa utawala wa Kinazi.
Raia wawili ambao hawajatambuliwa kutoka Ujerumani na Poland waliifahamisha utawala wa eneo hilo kuwa wanafahamu eneo lililofichwa treni hiyo, na wamedai wapewe asilimia kumi ya vitu vitakavyopatikana ndani yake.
Watu hao wanasema kuwa walipewa habari hizo na mtu mmoja ambaye alikuwa miongoni mwa walioficha treni hiyo, muda mfupi tu kabla ya mtu huyo kufariki.
Share:

Wednesday 5 August 2015

Wasifu wa Edward Lowassa


Umoja usio rasmi wa vyama vinne vya upinzani nchini Tanzania unajulikana kwa jina la Katiba ya Wananchi (UKAWA), baada ya kusubiri kwa muda hatimaye umemtangaza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.
Lowassa anagombea kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), huku vyama vingine vitatu vikimuunga mkono. Hii inatokana na sheria za Tanzania ambayo haitambui umoja wa vyama.
Kabla ya kujiengua chama Tawala chama cha Mapinduzi CCM, Edward Lowassa amekuwa mwanachama wa CCM kwa muda wa miaka 38, ambapo alijiunga na chama hicho mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka 1977.
Hatua ya mwanasiasa huyo mashuhuri nchini Tanzania kuamua kujiunga na chama cha upinzani Chadema, ikiwa imebaki miezi mitatu tu kuelekea uchaguzi mkuu, kumebadilisha kabisa upepo wa kisiasa nchini Tanzania, na hasa uchaguzi mkuu ujao.

Lowassa alikuwa Maziri Mkuu kati ya mwaka 2005 na 2008 kabla ya kujiuzuLu wadhifa huo kufuatia sakata la kashfa ya rushwa iliyohusisha kampuni ya kuzalisha umeme ya ki-Marekani Richmond Development Company LLC ya Houston Texas.
Hata hivyo wakati anatangaza kuhamia kwake Chadema, Lowassa alikanusha katu katu kuhusika kwa namna yoyote na kashfa hiyo na kudai kuwa yeye alifuata tu amri kutoka kwa ‘wakubwa’ walio juu yake.
“Kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi basi na aende mahakamani ama sivyo anyamaze” alisema Lowassa

Kuhama kwake kunamfanya Lowassa kuwa ndie kiongozi wa kwanza wa ngazi ya juu kabisa wa CCM kukihama chama hicho tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania mnamo mwaka 1992.
Mwanajeshi wa zamani na aliyewahi kupigana wa vita kati ya Uganda na Tanzania mwaka 1978/79, Lowassa aliiambia hadhara kwamba akiwa kama mtu mwenye uchungu na nchi yake isingekuwa rahisi kubaki ndani ya CCM huku akiona chama hicho kimepoteza mwelekeo na sifa ya kuongoza nchi.
Lowassa amekimbilia upinzani baada jina lake kukatwa wakati alipoomba kuwa mgombea urais kupitia chama tawala CCM katika uchaguzi mkuu ujao utakafanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Wakati mchakato wa CCM wa kumtafuta mgombea wao wa urais ulipoanza, Lowassa ndiye aliyekuwa kinara wa wagombea wote 42. Kila kona aliyozunguka, mikutano yake ya hadhara ilivutia maelfu ya watu waliomuunga mkono.
Wakati chama cha CCM kilimtaka kila mgombea apate sahihi za wadhamini 450 lakini Lowassa alipata sahihi za wadhamini zaidi ya 700,000.

Hata hivyo mchujo wa chama ulipofanyika jina lake lilikatwa mapema kabla hata ya kupelekwa kwenye vikao vya vya juu vya chama hicho. Ambapo baadae Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli ndiye aliyeibuka kidedea na kuwa mgombea kupitia chama tawala CCM.
Lowassa ameushutumu mchakato CCM wa kutafuta mgombea urais akiuita kuwa ulijaa chuki na mizengwe dhidi yake, hali ambayo aliifananisha na ‘ubakaji wa demokrasia’
“Nitakuwa mnafki nikisema bado nina imani na CCM. CCM niliyoiona Dodoma si CCM niliyokulia”, alisema, na kuongeza “kama Watanzania hawapati maendeleo kupitia CCM basi wakayatafute nje ya CCM”
Wakati sakala la Richmond lilipoibuka miaka michache tu iliyopita, Chadema ilimfanya limsakama Lowassa kuwa ni mmoja wa mafisadi wakubwa nchini. Lakini wakati chama hicho kinamkaribisha kuwa mwanachama wao, kiligeuka na kusema hakuna mtu msafi nchini na kwamba hawawezi kuacha kumpokea mwanasiasa mwenye mtaji mkubwa wa wafuasi kama Lowassa.
Wakati akiwa Waziri Mkuu, Lowassa alisifika kama mchapakazi hodari na msimamiaji wa moja kwa moja wa shughuli za serikali. Bado anaendelea kufahamika kwa jina la utani la ‘mzee wa maamuzi magumu’.

Moja ya mafanikio makubwa ya uwaziri mkuu wake ni jitihada kubwa na mafanikio ya upatikanaji wa fedha za kujenga chuo kikuu cha Dodoma. Chuo hiki kikuu cha umma kilichopo katikati ya Tanzania kilianzishwa mwaka 2007.
Lowassa ni mashuhuri pia kwa kusimamia mpango wa serikali uliofanikiwa wa ujenzi wa shule za kata ambazo uliiletea Tanzania sifa kubwa kwa kutoa fursa ya watoto wengi kupata nafasi shuleni.
Mtoto wa Mzee Ngoyai Lowassa, ambaye aliwahi kuwa mtumishi wa serikali ya kikoloni, Lowassa ameanza harakati zake za kuwania urais tangu mwaka 1995 lakini inaarifiwa kwamba rais wa kwanza wa Tanzania Mwl Julius Nyerere alimkatalia kushika nafasi hiyo. Wafuasi wa Lowassa wamekuwa wakiyatupilia mbali madai hayo
Ulipofika uchaguzi wa mwaka 2005, Lowassa hakutaka kuwania urais, lakini badala yake alimnadi rafiki yake wa siku nyingi Rais wa sasa Jakaya Kikwete ambaye alipata ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 80.
Share:

China ni haramu kuhifadhi mayai ukiwa hujaolewa


Mjadala mkali umeibuka nchini China baada ya serikali kupiga marufuku kwa uhifadhi wa mayai kwa wanawake ambao hawajaolewa.
Aidha mayai ya wanawake walioolewa wanaweza kuhifadhi mayai iwapo tu wanapata matibabu ya saratani ama matibabu ambayo yatadhuru kizazi chao.
Marufuku ya aina hii si jambo geni kwa raia wa China ambao tayari wanastahimili sheria kali ya kupanga uzazi.
Hata hivyo,ripoti zilipoibuka kuwa muigizaji Xu Jinglei alikwenda Marekani kuhifadhi mayai yake ya uzazi ndipo wachina wakang'amua kuwa huenda sheria hiyo inawalemga maskini.

Maelfu ya wachina wameikashifu sheria hiyo wakisema kuwa ni ya kibaguzi kwa misingi ya jinsia.
Aidha wengine wanahoji kwanini serikali inaingilia kati maswala ya kibinafsi na mambo ya kijamii.
Mjadala huu ulitibuka mwezi Julai baada ya Xu Jinglei alipokiri kuwa ni kweli amehifadhi mayai yake huko Marekani tangu mwaka wa 2013.

Muigizaji huyo mwenye umri wa miaka 41 alisema alichukua uamuzi huo kwani hajui ni lini hamu ya kupata mtoto itamwandama.
Siku ya jumapili televisheni ya kitaifa ya CCTV ilitoa ripoti kuhusiana na swala hilo na kuonyesha athari zake na kusema marufuku hiyo haina uhusiano na upangaji uzazi.
Ripoti hii ilisisimua watu katika mitandao ya kijamii ambao wengi wamekuwa wakiitupia dongo serikali.
Share:

Boti la abiria lazama ziwa Victoria Kenya


Boti moja iliyokuwa imebeba abiria 23 imegongana na mtumbwi wa wavuvi na kuzama katika ziwa Victoria Magharibi mwa Kenya.
Taarifa za awali zilikuwa zimetoa idadi hiyo kuwa 200 lakini maafisa wa usalama nchini Kenya wamethibitisha kuwa idadi ya abiria kwenye boti hiyo ilikuwa 23.
Watu 21 wameokolewa.
Miili ya watoto wawili imepatikana ikielea kwenye ziwa hilo.
Afisa huyo ameiambia BBC kuwa waliwaokoa watu 14 walipowasili katika eneo la tukio kabla ya kuwanusuru wengine saba waliporejea mara ya pili.
Wavuvi wanne waliokuwa kwenye mtumbwi wa pili pia waliokolewa.
Kwa mujibu wa walionusurika, boti hilo lililokuwa limewabeba abiria liligonga mtumbwi wa wavuvi kisha zote mbili zikazama majini.
Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi hii leo.

Ajali hiyo imetokea karibu na visiwa viwili vidogo ndani ya ziwa Victoria viitwavyo Kiwa na Remba Magharibi mwa Kenya.
Boti hiyo iliyokuwa na abiria ilikuwa inaelekea Sori kutoka kisiwa cha Remba.
Shughuli za uokoaji zinaendelea huku maafisa wa idara za serikali ya Kenya na wavuvi wakishirikiana kuwanusuru abiria hao.
Share:

Japan yakumbuka shambulio la Heroshima


Raia wa Japan leo wanaadhimisha kumbukumbu ya miaka 70 tangu shambulio la kwanza la bomu la Atomiki kutekelezwa mjini Heroshima.
Takriban watu laki moja na arobaini walikadiriwa kupoteza maisha baada ya Ndege ya Marekani kudondosha bomu ambalo liliuharibu mji huo tarehe 6 mwezi Agosti mwaka 1945.
Watu elfu sabini walipoteza maisha papo hapo, huku wengine wa idadi kama hiyo walipoteza maisha kutokana na athari za mionzi ya sumu.
Katika hotuba yake, Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe alisema kumbukumbu ya Heroshima inasisitiza uhitaji wa kufanya jitihada ya kupiga vita matumizi ya Nuklia.
Shambulio la Heroshima lilifuatiwa na shambulio jingine la bomu la Atomiki katika mji wa Nagasaki.
Japan ilijisalimisha siku kadhaa baadae, hatua iliyomaliza vita ya pili ya dunia.
Share:

Hofu baada ya boti iliyojaa wahamiaji kuzama Libya


Waokoaji wanaendelea na shughuli ya kuwasaka mamia ya wahamiaji waliotumbukia baharini baada ya boti walimokuwa wakisafiria kwenda Ulaya kuzama majini katika bahari ya Mediterrania karibu na ufuo wa Libya.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa takriban watu 700 walikuwa kwenye mtumbwi huo uliozama baada ya kukumbana na mawimbi makali.
Wanajeshi wa majini kutoka Ireland wanakisia kuwa idadi kubwa ya watu wamekufa maji.
Aidha shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka Medecins Sans Frontieres (MSF) limeonya kuwa huenda kukazuka maafa makubwa kufuatia idadi kubwa ya abiria waliokuwa kwenye mtumbwi huo uliozama.
Inakisiwa kuwa takriban wahamiaji 2,000 walikufa maji kwanza mwanza wa mwaka huu wakijaribu kufika ulaya kupitia bahari hiyo ya Mediterranea
Meli nne za uokozi na ndege tatu zimetumwa huko kujaribu kunusuru maisha ya wahamiaji hao.

Walinzi wa Ufuo wa bahari ya Uitaliano wamesema boti hiyo ya uvuvi iliyokuwa imebeba mamia ya wahamiaji.
Inavyoelekea boti hiyo ilikumbwa na dharuba lakini pia ilipenduka pale watu walipokurupuka upande mmoja walipoona chombo kingine kilichokuwa kikienda kuwasaidia.
Zaidi ya watu 150 wameokolewa lakini wengine wengi wanahofiwa wamekufa maji.
Msemaji wa shirika linalohusika na maswala ya wahamiaji IOM, Leonard Doyle ameiambia BBC kuwa
''Lazima tukumbuke kuwa hawa ni watu ambao hawajazoea usafiri wa baharini kwahivyo waliogopa.''
''Na wakati walipoona chombo kingine kinakuja kuwaokoa wakataharuki na kukurupuka upande mmoja''.

Hilo ndilo tunalokariri kuwa hao walanguzi wa kusafirisha watu hawajali kabisa kuhusu maisha ya wahamiaji hao licha ya kuwa wamewalipa pesa nyingi kwa safari hizo hatari''.
Kwamba mkasa wa aina hii unaweza kutokea wakati ambao hata watu wamepelekewa chombo cha kuwaokoa karibu yao ni jambo la kusikitisha sana.
Share:

Monday 20 July 2015

Buhari akutana na Obama


Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari anafanya mazungumzo mjini Washington na rais wa Marekani Barack Obama.
Mazungumzo baina ya viongozi hao wawili yanalenga ushirikiano katika vita dhidi ya wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
null
Awali Marekani ilikubali kuisaidia Nigeria katika vita dhidi ya makundi ya uasi hasa baada ya kutekwa nyara kwa wasichana zaidi ya 200 wa shule kutoka Chibok mwaka jana.
null
Hata hivyo uhusiano baina ya Marekani na utawala ulioondoka madarakani wa Goodluck Jonathan ulidhoofika , baada ya shutuma za makundi ya kutetea haki za kibinadamu kuhusu ukiukaji wa haki za kibinadamu unaotekelezwa na jeshi la Nigeria.
Bwana Buhari pia ameahidi kushughulikia ufisadi na amesema atarejesha mabilioni ya dola yaliyofichwa kwenye benki za Marekani Uswiss na kwingineko.
Share:

Ziara ya mfalme wa Saudia Ufaransa yazua Ubishi


Ubishi umeibuka nchini Ufaransa, baada ya ufukwe maarufu wa bahari wa Riviera kufungwa ilikumruhusu mfalme wa Saudi Arabia na familia yake kujivinjari kwa amani faraghani.
Viongozi wa mji wa Vallauriswametangaza kuwa watafunga sehemu kubwa ya ufukwe huo ilikuhakikisha usalama wa mfalme huyo familia yake na takriban ujumbe wa watu 400.
Familia hiyo ya kifalme, inatarajiwa kuishi katika jumba la kifahari lililoko huko.
Jumba hilo lililowahi wakati mmoja kuwa jumba la mapumziko la Sir Winston Churchill linatarajiwa kuzingirwa na maafisa wa usalama.
Maafisa wa Vallauris iliyoko kwenye mwambao wa Cote d'Azur, kilomita 10 kutoka kwenye ufukwe huo wanasema wamethibitisha kuwa shughuli kwenye ufukwe wa Milandore zitafungwa kwa muda wote wa majira ya kiangazi.
null
Hatua hiyo imewagadhabisha wakazi wa maeneo hayo ya mwambao , ambao wametishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mpango wa kuziba barabara ya ardhini kuelekea kwenye ufukwe huo.
Familia hiyo ya kifalme ya Saudi Arabia , ikiongozwa na Mfalme Salman, inamiliki jumba la kifahari ambalo Rita Hayworth alitumia kama mahala pa mapokezi ya wageni wakati wa harusi yake .
Sir Winston Churchill na Elizabeth Taylor walikua miongoni mwa wale waliolitumia kama makazi ya mapumziko.
null
Wakazi wa eneo hilo wamekasirishwa na shughuli za ukarabati katika eneo hilo, hasa baada ya kuwekwa kwa sakafu kubwa ya saruji kwenye mchanga ulioko ufukweni, zimeleza ripoti za wakazi wa eneo hilo.
Blandine Ackermann, rais wa shirika la wanaharakati wanaolinda mazingira katika maeneo ya Golfe-Juan na Vallauris amesema anapanga kuchukua hatua za kisheria kama ufukwe huo hautaendelea kuwa wazi na kurejeshwa katika hali yake
Maafisa wa kulinda bahari wamesema tayari kuwa chombo chochote hakitaruhusiwa kukaribia eneo hilo kwa takriban mita 300 ndani ya bahari.
Share:

Burundi:AU huenda isishiriki uchaguzi.


Yaelekea Muungano wa Afrika hautaweza kupeleka wanajeshi na waangalizi wa haki za kibinadamu nchini Burundi kabla ya uchaguzi wa urais unaotarajiwa kufanyika kesho Jumanne.
Katika taarifa kwa waandishi wa habari, Muungano huo wa Afrika wanasema kupelekwa kwa maafisa hao kumesababishwa na masharti mapya ya Burundi kwamba waangalizi sharti wawe na vibali vya kuingia Burundi mbali na vyeti vyao vya kusafiria vya kibalozi.
null
Mazungumzo baina ya serikali na upinzani yalivunjika mwishoni mwa juma baada ya pande hizo mbili mbili kushindwa kufikia makubaliano.
Upinzani unadai kuwa rais Nkurunziza anakiuka katiba ya taifa na mapatano ya Arusha yaliyokomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe.
null
Burundi imezama katika mgogoro wa kisiasa uliokumbwa na ghasia tangu rais wa nchi hiyo kutangaza kugombea nia ya kuwania muhula wa tatu .
Zaidi ya raia laki moja wa Burundi wamekimbia nchi hiyo tangu mwezi Aprili kulipozuka ghasia kupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.