Saturday 28 February 2015

Utafiti:Wanawake huwa na mpango m'badala..


Nusu ya wanawake huwa na mpango mbadala ama wa kando ambao wanaweza kukimbilia iwapo uhusiano wao utaharibika.
Utafiti uliofanywa miongoni mwa wanawake 1000 uligundua kuwa asilimia kubwa imeweza kuwaweka wanaume mbadala pindi tu uhusiano walionao unapoharibika.
Cha kushangaza ni kwamba wanawake waliomo katika ndoa huwa na mpango mbadala ikilinganishwa na wale walio katika uhusiano wa kawaida.
Pia imebainika kuwa mpango huo wa kando huenda akawa rafiki wa zamani ambaye amekuwa akimpenda mwanamke huyo.
Wengine huwa wapenzi wa zamani ama hata mume waliyeachana naye,rafiki ama mtu ambaye walikutana katika eneo la mazoezi.
Utafiti huo ulifanywa na kampuni ya utafiti wa mtandaoni wa Onepoll

Share:

Facebook kupambana na vitendo vya kujiua..


Mtandao wa Facebook umeanzisha Nyenzo mpya nchini Marekani kuwasaidia watumiaji wenye mashaka na marafiki ambao wako hatarini kujiua.
Nyenzo hii itawasaidia watu kuripoti ujumbe ambapo ripoti hizo zitaufikia mtandao wa facebook kwa haraka.
Afisa Mkakati wa Mtandao wa Facebook, Holly Hetherington amesema mara nyingi Marafiki na Familia wamekua wakishuhudia hali ya hatari kupitia ujumbe unaowekwa lakini wamekuwa wakishindwa kujua cha kufanya.
Awali watumiaji wa facebook walikuwa wakiandika ujumbe kwenye kurasa zao kuhusu kujitoa uhai lakini hakuna hatua zilizochukuliwa kwa wakati.
Share:

Wanaolala sana kushikwa na kiharusi..


Watu wanaolala kwa zaidi ya masaa manane kwa siku wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa kiharusi,utafiti umesema lakini wataalam hawajua sababu yake.
Utafiti uliofanywa kwa takriban watu 10,000 katika chuo kikuu cha Cambridge ulibaini kwamba wale wanaolala kwa takriban saa nane wana uwezekano mkubwa wa asilimia 46 kupata kiharusi.
Watu wazima hupendelea kulala kati ya saa sita na tisa ili kupumzika vizuri,lakini kulala zaidi hushirikishwa na matatizo ya afya kama vile ugonjwa wa sukari pamoja na ule wa kunenepa kupitia kiasi.
Hatahivyo haijabainika kutoka kwa utafiti huo iwapo kulala kwa zaidi ya saa nane huenda ndiko kunakosababisha matatizo hayo ambayo husababisha kiharusi ama iwapo ni miongoni mwa sababu za magonjwa yasiojulikana.
Utafiti huo ulifanywa miongoni mwa watu walioko na kati ya miaka 42 na 81.

Watafiti walichunguza mienendo yao ya kulala kwa kipindi cha miaka 10 ambapo watu 346 walipatwa na kiharusi.
Baada ya kuangazia athari kama vile miaka na jinsia, watu waliosema wamekuwa wakilala kwa zaidi ya masaa manane walipatikana na hatari ya asilimia 46 kupatwa na ugonjwa huo.
Wale walioweza kulala kwa chini ya masaa sita walipatikana na hatari ya asilimia 18
Share:

Mafuriko yawaua watu 14 Madagascar..


Watu 14 wameuawa kwenye mafuriko nchini Madagascar ambapo pia wengine 20,000 wamelazimika kuhama makwao.
Mafuriko hayo yaliukumba mji mkuu Antananarivo na maeneo yaliyo karibu.
Utawala unasema kuwa mvua nyingi siku zijazo huenda ikasababisha madhara zaidi.
Mvua kubwa imenyesha nchini humo kwa takriban wiki mbili.
Mwezi uliopita kimbunga Chedza kiliwaua watu 80 nchini Madagascar.
Share:

Rwanda:Serikali yaagizwa kuishtaki BBC...


Tume ya uchunguzi nchini Rwanda imebaini kwamba kipindi cha shirika la habari la BBC kilichopeperushwa hewani na kuuliza maswali mengi kuhusu mauaji ya halaiki ya mwaka 1994 hakikufikia kiwango kinachohitajika cha kitengo cha uhariri cha shirika hilo.
Mkuu wa tume hiyo Martin Ngoga alipendekeza serikali ya Rwanda kuanzisha kesi ya jinai dhidi ya shirika hilo.
BBC imesema kuwa imesikitishwa na matokeo ya uchunguzi huo na inatathmini athari zake.
Serikali ya Rwanda ilisimamisha matangazo ya shirika la BBC kupitia huduma yake ya kinyarwanda baada ya kipindi hicho kilichopeperushwa na runinga ya BBC na kuwashtumu watayarishaji wake.
Share:

Mbunge John Komba wa Tanzania afariki...






marehemu Komba akiongea na wanahabari nyumbani kwake Mbezi tangi Bovu akielezea kuimarika kwa afya yake aliporejea kutoka India kwenye matibabu, Julai 27, 2012.

Mbunge na Mwimbaji maaarufu wa nyimbo za Siasa nchini Tanzania, Keptain John Komba amefariki dunia siku ya jumamosi jioni.
Kwa mujibu wa Katibu wa Itakadi na Uenezi wa Chama tawala cha Tanzania chama cha Mapinduzi Nape Nnauye Mbunge huyo ambaye alikuwa maarufu kwa utunzi na uimbaji wa nyimbo za kampeni za chama hicho kifo cha chake kimetokea siku ya jumamosi majira ya jioni.
Marehemu Kaptain Komba alizaliwa Marchi 18 mwaka 1945 alipata elimu ya msingi huko nchini Tanzania katika shule ya Lituhi baadae elimu ya sekondari katika shule ya sekondari ya Songea iliyopo kusini mwa Tanzania kuanzia 1971 hadi mwaka 1974.
Mwaka 1975 hadi mwaka 1976 Marehemu John Komba alijiunga na chuo cha ualimu kilichopo Kleruu Iringa, Kusini Magharibi mwa Tanzania ambapo alihitimu cheti cha ualimu.
Marehemu John Komba ni mwanajeshi ambaye alipata mafunzo ya uafisa wa Jeshi katika chuo cha Maafisa wa Jeshi kilichopo Monduli kaskazini mwa Tanzania mwaka 1978 hadi mwaka 1978.
Keptain John Komba pia alipata mafunzo mengine ya siasa kutoka chuo Kikuu cha Washngton International ambapo alitunukiwa shahada ya siasa mwaka 2006 hadi mwaka 2008.
Share:

Thursday 26 February 2015

Nyong'o aibiwa vazi lake la bei Mbaya..


Nguo iliyobuniwa na kampuni ya Calvin Klein yenye thamani ya dola 150,000, na kuvaliwa na msanii maarufu wa kike Lupita Nyong'o katika tuzo za Oscar imeibiwa Hollywood .
Gauni hilo lililobuniwa kwa namna ya pekee na kupambwa kiasilia na konokono weupe zaidi ya 6,000 toka baharini, lilichukuliwa kwenye hoteliya London magharibi mwa Hollywood.
Lupita Nyong'o kutoka nchini Kenya aliibuka msanii bora wa kike mwaka jana baada ya miaka kumi na mbili ya utumwa, Lupita alikuwa mtangazaji wa sherehe za jumapili.
Baadhi ya magazeti yanamwita Lupita Nyong'o mrembo wa mwaka 2014.
Sheriff William Nash anasema nguo hiyo inaonekana kuibiwa siku ya jumatano jioni na polisi wanaendelea kufanya uchunguzi kupitia kamera maalum za CCTV.
Share:

Chinja chinja wa IS akamatwe:Ndugu..


Dragana Haines mke wa David Haines,mamlaka zinapaswa kumsaka na kumkamata akiwa hai mtu aliyemuua mume wake kwa kumchinja baada ya kutekwa na kundi la wapiganaji wa dola ya kiislam Islamic State wakati akifanya kazi na shirika la misaada la Uingereza.Mtu aliyemchinja David Haines na wengine tayari amefahamika kuwa ni Mohamed Emwazi.
Bi.Dragana amesema tangu alipojua kuwa mmewe David amechinjwa alijipa matumaini moyoni mwake kuwa ipo siku muuaji huyo atafahamika na hatimaye kukamatwa.Lakini baada ya kupatika kwa taarifa hizi za muuaji huyo anasema kuwa itakuwa faraja ya pekee kwa familia za kila aliyeuawa kinyama na wauaji hao, kwa sababu kama atakutwa amekufa anaona hicho kitakuwa ni kifo cha heshima kwa Mohamed Emwazi, lakini maombi yake ni kwamba kukamatwa akiwa hai na afe baadaye.
Kwa upande wake Barak Barfi ambaye ni msemaji wa familia ya Sotloff iliyopoteza ndugu yao pia, anasema kuwa hawana wasiwasi juu ya kukamatwa kwake muuaji huyo Mohamed Emwazi ama JIHAD JOHN.
"Tuna Imani kubwa sana na nchi ambayo vyombo vyake vya usalama na kiintelijensia vitawakamata watu hawa.Tungependa kwenda kumuangalia muuaji huyu ana kwa ana wakati wa mashtaka yake katika mahakama ya Marekani,na pia kuona akitumikia kifungo chake, katika gereza maalumu ambako ataishi huko pekee yake katika upweke.hiyo ndiyo sheria ya Marekani na hivyo ndivyo nchi yetu inavyoshughulikia matatizo kama haya"amesema Barak.
Share:

Kofi Annan atua Cuba kutatua migogoro,...


Katibu mkuu wa zamani wa umoja wa mataifa Kofi Annan amewasili nchini Cuba kuhamasisha mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Colombia na nchi zenye makundi ya waasi.
Mazungumzo hayo yanayofanyika mjini Havana ni mwendelezo wa hjjitihada za kusaka Amani katika nchi kwa zaidi ya miaka miwili hadi sasa.
Hata hivyo katika mazungumzo hayo ya Amani lengo ni kumaliza migogoro iliyodumu kwa zaidi ya miongo mitano.
Annan amesema atakutana na pande zote mbili za viongozi na kuwa na mazungumzo nao ya pamoja na kwamba atatumia uzoefu wake wa utatuzi wa migogoro katika nchi alizowahi kuwa msuluhishi.
Share:

UJUMBE WA RAIS JAKAYA KIKWETE KUTOKA KWA BI. CLARA PETER JUU YA MAUAJI YA WALEMAVU WA NGOZI...habari na matukio blog


Nilizaliwa kwenye familia ya watoto sita nikiwa mtoto pekee mwenye albinism. Mama alitupenda na anatupenda sawa bila kujali hali yangu na kunifanya nijione sawa na wenzangu. Tunapendana sana. (Pichani ni Bi. Clara Peter akiwa na mwanae).
Nilizaliwa kwenye familia ya watoto sita nikiwa mtoto pekee mwenye albinism. Mama alitupenda na anatupenda sawa bila kujali hali yangu na kunifanya nijione sawa na wenzangu. Tunapendana sana.

Hali hii ilinifanya nisijute na wala haitokaa itokee nijute kuzaliwa na hali (mwenye albinism). Mungu aliniumba kwa kusudi lake, kusudi maalum na wala si kwa bahati mbaya. Ila kusudi hili linaharibiwa na kukatishwa na baadhi ya wapumbavu (wauaji) wenye fikra mgando. Ila bado sijakata tamaa nitapambana mpaka dakika za mwisho za pumzi yangu.

Moyo wangu unavuja damu, damu na maji, japo bado nina tumaini la kuishi, moyo wangu huu umekunja ngumi ambayo sijui itatua kwa nani kwani adui yangu simjui. Je Ni familia, wazazi na ndugu zangu, majirani na marafiki au watu kuja nisowajua?

Hivi ni nani hasa anayedhamini mauaji haya ya kikatitili kwa watu waenye albinisim? Hakika hii ni system pana tena pana sana yenye kujitosheleza katika kila Nyanja. System inayolindwa kama nyara za serikali ama hata zaidi ya nyara hizo, kwani siamini kama serikali yetu hii ya maisha bora kwa kila mtanzania imeshindwa kuwakamata wahusika.

Muda mwingine najiuliza hivi mauaji haya yanasababishwa na imani za kishirikina tu au kuna mengine chini ya mwamvuli huu mpana wa imani za kishirikina? Mh! Mimi na wewe hatujui. Na je soko kuu la bidhaa hizi haramu lipo wapi na nani ana hisa nyingi? Pia mimi na wewe hatujui. Kuna connection gani kati ya hawa majasusi wauaji na watunza usalama? Mbona inakuwa ngumu kuwatia mikononi mwa sheria? ama kwa hakika kuna jambo zito ambalo limejificha chini ya kapeti ambalo mimi na wewe hatuljui.

Naamini kwa kutumia teknolojia ya sasa na hasa ya mawasiliano kuyakamata haya majitu mauji kuanzia jani, tawi, shina na hata mzizi wake, mwezi ni mrefu.

Mtukufu Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete watu wenye albinism tunakulilia baba tunaomba utuokoe sisi wana wa Israel tunapukukutika kwani tunaamini AMRI yako itasaidia kusitisha tatizo hili ikiwemo ya kunyongwa mpaka kufa kwa wote waliobainika kuhusika na uchafu huu.

Tunaomba haki itendeke kwa familia zilizopoteza wapendwa wao na wahanga wote. Tunahitaji uhuru katika inchi yetu, amani na upendo. Mbona tunaishi kwa kuificha kama wahalifu katika nchi yetu? Hatuna hatia wala hatuna bahati yeyote badaala yake tumekosa vimelea vinavyosababisha rangi ya asili (melanini), MSITUUE hakuna tulichotofautiana.

                                                 WE NEED NO,  WE DEMAND JUSTICE
Share:

HATIMAYE KINYESI CHA MWALIMU CHATEKETEZWA...


 Kinyesi kikiwa kimehifadhiwa ndani ya chumba cha mwalimu


Maulid Liuguyo ambaye ni mfanyakazi wa Manispaa ya Temeke kitengo cha usafi akishiriki katika zoezi hilo.


Mfanyakazi wa Manispaa ya Temeke Kitengo cha Usafishaji, Ramadhani Athuman akiweka dawa katika vyombo alivyokuwa akitumia kuhifadhia kinyesi mwalimu Gaudensia Albert wa Shule ya Sekondari Kibasila jijini Dar es Salaam, kabla vyombo hivyo havijaenda kutupwa dampo. (Picha na Francis Dande)



 Umati wa watu ukiwa nje ya nyumba wakati zoezi la kuteketeza kinyesi likiendelea.


 Mlango ukivunjwa ili maofisa wa afya waweze kuingia ndani ya chumba cha mwalimu.


Manispaa ya Temeke leo imeteketeza kinyesi kilichokutwa katika chumba cha mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kibasila Gaudensia Albert baada ya maofisa wa afya wa manispaa hiyo kuchukua hatua hiyo ili kunusuru afya za wakazi wa eneo hilo.

Kazi hiyo ilifanyika majira ya saa tisa alasiri katika eneo la Yombo, Kisiwani Kata ya Sandari jijini Dar es chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi na wakishirikiana na Mwanyekiti wa Mtaa huo, Yahya Bwanga.

Akizungumza na wandishi wa habari jijini wakati wa zoezi hilo, Ofisa Afya wa Manispaa ya Temeke, Floyd Tembo alisema tukio hilo walilipata juzi juzi jioni, baada ya kulipata waliwatuma Watendaji wa Afya wa Kata hiyo wafanye utafiti wakujua tatizo hilo lilikuwa na ukubwa gani.

“Baada ya kufanya utafiti wao pia walimpata mhusika, ambapo tulischukua jukumu la kwenda kumhoji Mkuu wa washule hiyo ili kujua kama mwalimu Gaudensia alikuwa na akili timamu au la, hata hivyo, Mkuu wa shule atueleza kuwa alikuwa na akili timamu,”alisema Tembo.

Alisema pamoja na kuutekeza mlundikano huo wa kinyesi pamoja mikojo na matapishi bado wanaendelea na utaratibu wa kumfikisha mwalimu huyo kwenye vyombo vya sheria ili haki iweze kutendeka.

“Hili tukio halihusiani na ugonjwa wa akili inawezekana kuna tatizo lingine ingawa hatuwezi kuamini mambo ya ushirikina lakini haiwezekani mwalimu kama yule ajisaidie na kuhifadhi uchafu kama ule ndani,”alisema.

Aidha, alisema mwalimu huyo hakuweza kufika kwenye eneo la tukio hali iliyofanya mlango wa chumba chake uvunjwe chini ya uwaangalizi wa polisi.

Tembo, alisema mwalimu huyo alishindwa kutokea kwenye eneo la tukio kwa vile alipelekwa Hospitali ya Temeke kisha kuhamishiwa Haspitali ya Taifa muhimbili kwa ajili ya kupimwa afaya baada ya kupata mshituko ambao umesababishwa na taarifa hizo.

Afisa Afya wa Usafi wa Mazingira, Jumamne Muhogo, alisema uchafu walioubaini ulikuwa ni uchafu wa kinyesi, mikojo na matapishi inasemekana kuna kipindi alikuwa anatapika.

Pia alisema kipo kifungu cha sheria, walifika pale maofisa kutoka idara mbalimbali kupima uzito wa tukio, ambapo kama wangemkuta wangemkamata kwa hatua za kimfikisha mahakamani.

Mhogo, alisema hata kama alikuwa mtaalamu wa sayansi, alikuwa amehifadhi uchafu ule kwa ajili ya utafiti basi hayo yote angekwenda kuyaeleza mahakamani.

“Tukio hili kwa manispa ya Temeke ni la kwanza kutokea yani inaekekea huyu mtu hana akili ya kawaida kama angekuwa na akili za kawaida asingeweza kufanya na mna hii,”alisema.

Umati mkubwa wa wakazi wa eneo hilo walikusanyika kwa wingi tangu saa tatu asubuhi wakisubiri kazi hiyo hadi ilipofnyika saa tisa jioni na wataalamu wa manispaa hiyo.

Wataalamu hao walimwagia dawa uchafu huo kisha kuanza ubeba na kutumbukiza chooni kwa uangalifu mkubwa.

Walipomaliza walvisafisha vyombo hivyo kwa kutumia dawa ambazo zimeweza kusaidia kuondoa harufu mbaya iliyokuwa imezagaa hewani.

Awali, Sajenti wa Jeshi la Polisi  Ramadhan Kagolo, alisema aliwajibika kusimamia kuvujwa kufuli la chumba hicho kwa vile Kazi iliyokua ikifanyika ni kwa ajili ya kulinda afya ya jamii.
Share:

Mtandao wa 5G hadi mwaka wa 2020...



Wanasayansi wamefaulu kuzindua mtandao wa 5G......>>>>>INGIA HAPA<<<<<
Share:

BBC yawateua Vijana wabunifu Kenya..


Makundi mawili ya ubunifu wa kiteknoligia wameteuliwa kuisaidia shirika la utangazaji la BBC kuafikia ruwaza yake ya kupanua upeo wa usikilizaji wa vijana kupitia kwa mfumo mpya wa kidijitali.
Vijana hao wataalamu wa digitali kutoka muungano wa Go Sheng na Ongair walichaguliwa kutoka timu 13,zilizoshiriki mashindano hayo kutoka Afrika na Marekani.
Mashindano ya ubunifu "hackathon" ya BBC yalilofanyika mjini Nairobi Kenya mapema mwezi huu.
Watafadhiliwa kufanikisha majaribio ya miundo msingi waliozindua kwa kipindi cha miezi sita ijayo.
‘’Nimefurahia kwamba studio ya kwanza iliyoshikanishwa ya BBC Afrika inalengo la kuchochea vipaji vya ubunifu hapa hapa barani'' alisema
Dmitry Shishkin mhariri wa BBC wa maswala ya kiteknolojia ya dijitali.
Bwana Shishkin alikuwa miongini mwa wakaguzi katika mashindano hayo ya ubunifu.
Timu mbili zilizochaguliwa zilikuwa zimepeana natharia mahsusi ya jinsi ya kuwafikia vijana kupitia mfumo huu wa kidijitali.
Kundi la Go Sheng lilipendekeza kuwafikia wasilikizaji na watazamaji wa BBC kupitia lugha ya mtaani iitwayo ''Sheng''
Nahodha wa kundi hilo Euticus Mola alisema kuwa wanatazamia kuwafikia vijana kupitia kwa lugha ya sheng.
Aidha wapinzani wao Ongair nao walipendekeza kufungua njia za mawasiliano na vijana kwa nia ya kuwakutanisha vijana na kuelewa matakwa yao.
Kiongozi wa kundi hilo Trevor Kimenye 30 aliiambia BBC kuwa mbinu hiyo anahakika itawezesha vijana kujieleza.
Share:

Vikombe vya kahawa vinavyoliwa..


Maduka ya kuuza vyakula kote duniani KFC yamezindua kikombe cha kwanza duniani cha kahawa ambacho kinaliwa.
KFC imezindua kikombe hicho ambacho kimeundwa kutokana na Chokoleti iliyochanganywa na Biskuti.
Vikombe hivyo pia vimewekwa harufu ya kupendeza ya mnazi.
Vikombe hivyo vinavyoitwa ‘’Scoff-ee-cup’’ vinautamu uliyotengenezwa kutoka biskuti ya kipekee iliyofungwa na karatasi ya sukari safi ya chokleti ,inayoweka kahawa kuwa moto.
Lakini baada ya muda chokleti hiyo inaanza kuyeyuka kwa hivyo inakupasa ule ‘’kikombe ‘’chako kwa haraka.
Ikitengenezwa kwa ushirikiano wa wanasayansi maarafu wa vyakula ’’The Robbin Collective’’,vikombe hivyo vya kahawa ambavyo ni asilimia mia

mmoja vinaweza liwa zimetengenezwa na harufu nzuri inayoweza kusisimua .
Aidha upishi na viungo vya Robbin collective ‘’siyo tu kuwa vikombe hivyo bali pia vina ladha nzuri mbali na harufu ya kupendeza’’alisema Jocelyn
Bynoe ambaye ndiye meneja wa mauzo wa kampuni hiyo.
Vikombe hivyo vya kahawa vimebuniwa kuadhimisha kahawa nzuri ya ‘’Seattle’’iliyotengenezwa kutokana na kahawa aina ya Arabica .
'Scoff-ee Cups' haziko katika maduka yao kwani bado zinafanyiwa majaribio ya ubora wa bidhaa.
Share:

Upandikishaji wa kichwa sasa unawezekana..


Unaposikia habari hii utadhani ni maudhui ya filamu ya kutisha ,lakini wanasayansi wanaamini upasuaji wa upandikishaji wa kichwa cha mwanadamu katika mwili mwengine huenda ukafanikiwa.
Madaktari watazindua mradi huo katika kongamano wakati wa msimu wa joto ,kwa lengo la kuanzisha utaratibu huo mnamo mwaka 2017.
Mtu atakayeongoza mpango huo ni daktari raia wa Italy Sergio Canavero kutoka kundi moja la wanasayansi mjini Turin.
Anaamini kwamba upandikishaji wa vichwa vya watu utawasaidia wanaosumbuliwa na magonjwa ya misuli na saratani.
Baada ya kutoa wazo hilo mnamo mwaka 2013,daktari Canavero anaamini vikwazo vikuu vya upasuaji huo vimekabiliwa ,kulingana na ripoti mpya ya wanasayansi.
Vikwazo hivyo ni pamoja na usimamizi wa uti wa mgongo kuingiliana na kichwa kipya pamoja na kuhakikisha kuwa kinga ya mwili haikikatai kiungo hicho kipya.
Daktari Canevaro alichapisha taarifa iliokuwa na nadharia kuhusu vile anavyoamini upasuaji huo unaweza kufanyika.
Share:

Wapiganaji wa IS wavunja sanamu Iraq...


Wapiganaji wa Islamic State wametoa kanda ya video inayowaonyesha wakivunja sanamu ndani ya makavazi katika mji wa Mosul nchini Iraq.
Video hiyo inaonyesha wanaume kadhaa wakiwa katika chumba kimoja cha makavazi ya kitaifa wakiangusha na kuharibu sanamu ziliko ndani,
Moja baada ya nyingine sanamu hizo zilizoundwa kwa njia maalum, zilirushwa na kutapakaa kila mahala.
Kisha wanaharibu sakafu na kisha sanamu za watu walioshika visu zikigongwa na kuharibiwa kabisa.
Miongoni mwa sanamu zilizoharibiwa ni pamoja na sanamu ya fahali iliyotengenezwa karne ya tisa kabla ya kuja kwa yesu kristu.
Mmoja wa wanamgambo hao anasikika akisema kuwa sanamu hizo ni miungu bandia na kusema kuwa mtume Mohammad, aliamuru kuwa vitu kama hivyo viharibiwe kabisa.
Share:

Bomu lazua taharuki uwanjani Dortmund.....


Bomu la vita vya pili vya dunia ambalo halijalipuka limepatikana katika uwanja wa Borussia Dotmund.
Bomu hilo lililoripotiwa na mwandishi wa DW nchini Ujerumani linadaiwa kuwa na chimbuko la Uingereza na sasa kuna mpango wa kulivunja makali.
Ugunduzi huo unajiri saa kadhaa kabla ya mkufunzi wa kilabu hiyo Jurgen Klopp kuzungumza na vyombo vya habari kabla ya mechi ya siku ya jumamosi na kilabu ya Shalke.
Watu waliokuwa karibu na uwanja huo unaobeba takriban watu 80,720 waliondolewa.
Haijulikani ni kwa mda gani eneo hilo la uwanja litakuwa haliendeki walisema wamiliki wa kilabu hiyo waliofunga eneo la mashabiki pamoja na makavazi ya kilabu hiyo.
Share:

Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC (Bensouda) awasili Uganda....


Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC Fatou Bensouda amewasili nchini Uganda ili kutafuta ushahidi kuhusu kesi ya aliyekuwa kamanda mkuu wa wapiganaji wa LRA nchini Uganda .
Dominic Ongwen ambaye alisema alitekwanyara na LRA akiwa mtoto alifikishwa mbele ya mahakama ya ICC mjini Hague mnamo mwezi Januari akikabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita.
Mwandishi wa BBC mjini Kamapala anasema kuwa Bensouda atazuru kazkazini mwa Uganda katika ziara ya siku tano ili kuzungumza na mashahidi mbali na kutembelea maeneo yaliotekelezewa uhalifu huo.
Pia anatarajiwa kukutana na rais Yoweri Museveni wa Uganda ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa mahakama hiyo ya ICC akiishtumu kwa kuwabagua viongozi wa Afrika.
Share:

Mchinjaji wa IS 'Jihadi John' atambuliwa..



Mwanaume ambaye amekuwa akitekeleza mauaji ya mateka wa kundi la wapiganaji wa Islamic State ajulikanaye kwa jina la utani "Jihadi John",ametambuliwa.
Bwana huyo ambaye taswira yake akiwachinja mateka kwa kisu bila huruma ndiyo nembo ya wapiganaji hao sasa ametambuliwa kuwa anatokea Uingereza.
Shirika la Habari la BBC limetambua kuwa jina lake kamili ni Mohammed Emwazi.
Emnuazi ameonekana kwenye video kadhaa ya mauwaji ya mateka wa mataifa wa magharibi, akiwemo Mmarekani James Foley, Raia wa Uingereza, Alan Henning na mwaandishi habari wa Japan, Kenji Goto.
Inaaminika kuwa Emwazi ni raia wa Uingereza na hasa anatokea magharibi mwa London.
Yamkini Emnuazi aliyezaliwa Kuwaiti na mwenye umri wa kati ya miaka 20 -29 alikuwa amefahamika sana na vyombo vya usalama lakini kwa sababu za kiusalama haikuwezekana kumtambua.
Anaaminika amewahi kuishi Somalia mnamo mwaka 2006 na anauhusiano mkubwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabab nchini humo.
Polisi nchini Uingereza imeziomba vyombo vya habari kutosambaza habari ambazo hawajazithibitisha kumhusu jamaa huyo kwani uchunguzi unaendelea.
Hata hivyo bado habari za kina kumhusu Jihadi John hazijatolewa.
Mwandishi wa maswala ya Usalama wa BBC Tomi Oladipo anasema kuwa vyombo vya usalama vya serikali za mataifa yanayokaribia Somalia sasa yana kila sababu ya kutahamaki.

Kwa sababu Kuhusika kwake na kundi la Al Shaabab kisha akajiunga na kundi la Islamic State ambalo kwa wakati mmoja lilikuwa linashindana na wanamgambo wa Al Qaeda kuhusu yupi kati yao anayeushawishi
mkubwa
Ishara kuwa Al Shabab inazingatia msimamo mkali wa kidni hata zaidi ya Al Qaeda.
Kwa sababu itakumbukwa kuwa Al Qaeda ilipinga hatua kali ya kuwachinja mateka nchini Iraq na Syria.
Emnuazi ambaye amekuwa akiwabeza mataifa ya Magharibi kabla ya kuwakata shingo naaminika kuwa mtaalamu wa maswala ya kompyuta alisomea chuo kikuu cha Westminster.
Kwa mujibu wa mwandishi wa BBC bwana huyo anaaminika kuwa alikwenda Syria mwaka wa 2012, lakini kabla ya wakati huo majasusi wa Uingereza na Marekani walikuwa hawajajua tishio lake.
Share:

Monday 23 February 2015

Bwana harusi aanguka kifafa kabla ya harusi..



Bi harusi mmoja kaskazini mwa nchi ya India alifanya maamuzi ya papo kwa hapo kuolewa na mmoja wa wageni waliofika kushereheka naye katika harusi yake baada ya mumewe kuugua ghafla.
Mwanamke huyo ajulikanaye kama Indra anayetokea Rampur jimbo la Uttar Pradesh, inaelezwa kuwa sekunde chache kabla ya ndoa ya wawili hao mume akaanguka kifafa, na hivyo kumlazimu kuondoka harusini na kwenda kumwona daktari.
Bi harusi Indra, alishikwa na hasira ya hali ya juu, kwakuwa mume alimficha juu ya hali yake, naye hakuwahi kujua hata siku moja kuwa , jamaa ana tatizo la kuanguka kifafa.
Indra akatoa ombi lake kuwa anahitaji kuolewa na mmoja wa wana familia ya bwana harusi , ambaye alikuja harusini kusherehekea harusi ya nduguye,na Indra akamtaka achukue nafasi ya nduguye badala yake, jamaa akaona nyota ya jaha imemuangukia, si akakubali !
Ndoa ikafungwa, hali ya bwana harusi wa kwanza mwenye kuanguka kifafa, haijajulikana mpaka harusi ya pili ilipokwisha.
Share:

Al Shabaab yatishia kushambulia Ulaya

Westgate Nairobi baada ya shambulio la Al Shabaab  2013

Waziri wa Usalama wa Marekani anasema analitia maanani sana tishio la kundi la Waislamu wa Somalia, Al Shabaab, kwamba litashambulia maeneo ya maduka huko Marekani, Canada na Uingereza.
Katika mahojiano kwenye televisheni, Jeh Johnson alisema pametokea mabadiliko katika vitisho vya makundi ya wapiganaji Waislamu ambayo sasa yanatoa wito kwa washabiki wao katika nchi maalumu kufanya mashambulio.
Ulinzi umezidishwa kwenye eneo moja la maduka la Marekani katika jimbo la Minnesota, ambalo lina wakaazi wengi Wasomali
Mwaka wa 2013, shambulio lilofanywa na Al Shabaab dhidi ya eneo la maduka la Westgate mjini Nairobi, Kenya, liliuwa watu zaidi ya 60.
Share:

Al-Sisi,aomba msaada dhidi ya IS.



Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi amesema kuna haja majeshi ya muungano wa jumuiya ya kiarabu ya Pan-Arab kutoa majeshi yao ili kukabiliana na ugaidi.
Amesema kuwa mataifa kadhaa yametoa majeshi yao kukabiliana na kundi la wapiganaji wa Kiislam wa Islamic State tangu kuuawa kwa Wakristuhuko nchini Libya. Mataifa yaliyotoa misaada ya kifedha na kijeshi ni Jordan,Falme za Kiarabu na Marekani kwa lengo la kuangamiza kundi hilo Syria na Iraq. Akizungumza kupitia Televishen Sisi amesisitiza misaada ya kifedha kutoka mataifa ya Saud Arabia ambao walisaidia wakati wa kuuangusha utawala wa aliyekuwa Rais wa Kiislam wa Mohammed Morsi.
Share:

500 waokolewa machimboni Afrika Kusini



Inakadiriwa kuwa wachimbaji wapatao mia tano wameokolewa na magari ya zima moto kutoka machimboni baada ya kuwa wamebanwa chini ya mashimo yenye kina kirefu katika machimbo ya madini nchini Afrika Kusini.
Moto mkubwa uliripuka mapema mwanzoni mwa wiki hii umbali wa zaidi ya kilomita mbili katika machimbo ya mgodi wa Kusasalethu Magharibi mwa mji wa Johannesburg.
Mmiliki wa mgodi huo ni kampuni ya Harmony Gold wameeleza kuwa waliwaokowa wanaume zaidi ya mia nne na themanini na sita waliokuwa zamu siku hiyo .
Moto huo unasadikiwa ulianza wakati wa kazi ya matengenezo ilipokuwa ikiendelea.
Mwaka wa jana mgodi huo ulifungwa kwa muda wa wiki mbili ili kuwaondoa wachimbaji haramu ambao waliuvamia mgodi huo ambao wanshukiwa kuwa wao ndio walioanzisha moto huo.
Share:

Monday 16 February 2015

Waliowajeruhi polisi TZ wasakwa........


Polisi nchini Tanzania wamesema wanawasaka watuhumiwa waliowajeruhi askari sita kwa risasi mkoani Tanga.
Askari hao walijeruhiwa wakati wakifanya kazi ya kuwatafuta watuhumiwa wa uhalifu wa kutumia silaha wanaodaiwa kuwa walijificha eneo moja nje ya mji wa Tanga wakiwa na silaha.
Awali kulizagaa taarifa na hofu kuwa wahusika walikuwa na itikadi za kigaidi, lakini taarifa ya maandishi iliyotolewa na polisi imewaita watu hao kuwa ni majambazi na kwamba msako wa kuwatafuta unaendelea.
Hata hivyo taarifa haikuleleza wanaotafutwa ni watu wangapi, ingawa imetaja kuhusika kwa jeshi lenye silaha jambo linaloashiria mapambano yalikuwa makali.
Share:

Oscar Pistorius apandishwa hadhi jela....


Kuhusiana na mwanariadha Oscar Pistorius aliyeko kifungoni, imeelezwa kwamba sasa anaweza ama kuruhusiwa kukumbatiana na wageni wake na hata kuwabusu wanaomtembelea ,anaruhusiwa kusikiliza redio na hata kuvaa vitu vya thamani ikiwemo vito vya thamani akiwa ndani ya gereza.
Mtuhumiwa huyo wa mauaji,amepewa ruhusa ingine ya kuwa huru kupiga simu atakavyo,vile vile bajeti yake inayodaiwa kuwa kubwa, imekubaliwa aweze kununua vyoo atakavyo na hata akitaka chipsi ataletewa,na huu ni uamuzi wa bwana jela anaye angalia wafungwa na hadhi zao naye Pistorius yuko kundi B.
Ikumbukwe kwamba Oscar alimuua mpenzi wake mnamo mwezi kama huu na siku inayotajwa kuwa muhimu ulimwenguni tarehe ya kumi na nne Valentine's Day,mwaka wa jana akiwa nyumbani kwake.
Akiwa jela Pistorius anajaribu kuyazoea mazingira ya jela na inamuwia vigumu kukubali kuwa ameupoteza uhuru wake, na pia kuonekana kama tishio la usalama na hivyo yumo ndani
Msemaji wa familia ya Pistorius mwanamama,Annalise Burgess, amemzungumzia mwanariadha huyo aliyekuwa maarufu duniani kiasi cha kupachikwa jina la Blade Runner,sasa amepandishwa hadhi na kuwa daraja la A .
Familia ya Oscar ina Whatsapp la familia yao ambalo linafuatilia taarifa zote za mwanariadha huyo na pia hutumia akaunti hiyo kujadiliana masuala ya biashara za familia.
Inaelezwa kuwa watu wanaoongoza kumtembelea Oscar Pistorius Jela ni kaka na dadake Aimee Carl na wakiisha kuonana naye hutuma taarifa na picha katika kundi hilo na kinachoendelea kumhusu yeye gerezani.
Kupandishwa kwa Oscar kuna maanisha kuwa anaruhusiwa kutembelewa na wageni zaidi ikiwemo familia yake.Hapo mwanzo kila anayemtembelea huzungumza naye kwa njia ya simu akiwa ametengwa na mgeni wake na vioo, na hakuruhusiwi kuguswa,lakini mambo sasa yamebadilika.
Sasa Oscar mwenye umri wa miaka ishirini na nane, anaweza kuwakumbatia jamaa zake wamtembeleapo,na muda wa kumuona umeongezwa kutoka saa mbili hadi tatu kwa mwezi,na wageni wamtembeleao bado wanakabiliwa na sheria ya kupekuliwa kabla ya kuonana ma mfungwa huyo ambaye bado anatakiwa kuvaa sare za jela zenye rangi ya samawati ama ita orange
Suala la hadhi ya Oscar kupandishwa daraja limewakera wafungwa wenziwe walioko kwenye gereza la Death Island: lilotengwa,ambalo limezunguukwa nyaya za umeme wamelalama kuwa mwanariadha huyo mlemavu anapewa hadhi ya kifalme kwa muda mfupi sana ilhali wao wanataabika muda mrefu gerezani.

Share:

Runinga 3 Kenya zimezima matangazo yao..


Kampuni tatu kubwa za kibinafasi za utangazaji zimesitisha kupeperusha matangazo kwenye televisheni kwa muda wa siku tatu zilizopita,
baada ya serikali kudhibiti mitambo ya zamani ya kupeperusha matangazo kwa mfumo wa analojia.
Kampuni hizo za Standard Media, inayomiliki runinga ya kwanza ya kibinafsi nchini Kenya KTN Nation media Group inayomiliki NTV na QTV
na Royal Media Services inayomiliki Citizen TV zimekuwa katika malumbano makali na serikali kuhusu uhamiaji wa kupeperusha matangazo kwa kutumia mfumo wa digitali kutoka ule wa zamani analojia.
Runinga hizo tatu zimekuwa zikilumbana na halmashauri ya serikali ya mawasiliano kuhusu swala la kuhama kutoka mfumo wa zamani hadi digitali kwa zaidi ya miaka nne sasa.
Hatua ya mwsihoni mwa wiki ya kufunga mitambo ya zamani ya kurushia matangazo yaani analogue ya runinga hizo ilichukuliwa baada ya amri ya mahakam ya juu zaidi nchini Kenya kuidhinisha uhamiaji huo.
Wamiliki wa runinga hizo tatu wanasema hawajajiandaa vilivyo kwa uhamiaji huo.
Lakini, je, nini hasa chimbuko la vyombo hivyo tatu vya habari kusitasita katika uhamiaji huu wa digitali?
Mwenyekiti wa chama cha wamiliki wa vyombo vya habari vya Kenya anasema kuwa Serikali ilipendelea vyombo vya habari vinavyomilikiwa na wageni na hivyo kuwanyima fursa wakenya kumiliki na kuchangia katika ukuaji wa
sekta ya utangazaji nchini Kenya.

Kwa sasa, watazamji wanategemea sana vituo viwili vikubwa, kile cha K24 ambacho kinadaiwa kumilikiwa na familia ya rais wa Kenya na runinga ya kitaifa ya shirika la utangazaji la Kenya.
Kwa upande wake, serikali ya Kenya kupitia halmashauri ya mawasiliano CAK inasisistiza kwamba zaidi ya wakenya asilimia 60 wanavyovijisanduku vipya vya kuwawezesha kupokea matangazo kwa njia ya digitali.
Katika mitaa ya mji mkuu wa Nairobi, baadhi ya wakenya wanaelezea jinsi walivyokosa kutizama vipindi vyao wanavyovipenda.
Hata hivyo wengine wanakubaliana na serikali kuwa sharti mipango ya serikali ya kuhamishwa kwenye masafa ya kidijitali yaendelee mbele ilikufungua sekta nzima ya sanaa.
Kulingana na sera za serikali ya Kenya runinga zote zinahitajika kuandaa na kupeperusha asilimia 60% ya vipindi kutoka nchini Kenya huku asilimia 40 ikiwa vipindi kutoka ughaibuni.
Wakenya wengi wanahisi kuwa serikali iliharakisha uhamiaji huo ila wangependa sekta nzima ifuate sheria za nchi.
Mnano mwaka wa 2006, kongamano la kimataifa kuhusu mawasiliano lililoandaliwa mjini Geneva Switzerland liliazimia kwamba nchi wanachama ziwe zimehama kutoka mfumo wa zamani wa utangazaji wa analogue hadi digitali
ifikapo tarehe 17 mwezi juni mwaka wa 2015.
Ingawa tarehe hiyo bado haijawadia, mamilioni ya watazamji wanaotegemea runinga za KTN, NTV na Citizen tayari wanaonja athari za kukera za maendelezi ya teknologia.
Share:

Misri yaishambulia ISIS Libya..


uu wa kanisa la Coptic Taarifa kutoka Misri zasema kuwa, ndege za kijeshi zimewashambulia wapiganaji wa jihadi nchini Libya kwa mabomu, baada ya kutolewa kwa mkanda wa video ulioonyesha wakristo wa Misri wa madhehebu ya Coptic wakikatwa shingo.
Jeshi la Misri linasema kuwa limelenga kambi za Islamic State, kituo cha mafunzo na maghala ya silaha, katika shambulizi hilo la mapema leo alfajiri.
Walioshuhudia wanasema kuwa, mji wa Derna ulioko mashariki mwa Libya na ambao umetekwa na wapiganaji wa jihadi ndio ulioshambuliwa vibaya.
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, amesema kuwa mashambulio hayo ya angani ni jibu kwa wapiganaji hao ambao walitoa mikanda hiyo ya video hapo jana jumapili ilioOnyesha waumini kumi kati ya 21 waliotekwa nyara wakichinjwa.

Waumini hao wa madhehebu ya Coptic walikuwa wametekwa nyara majuma kadha yaliyopita.
Jeshi la Misri limetoa taarifa kwa vyombo vya habari inayosema kuwa raia wa taifa hilo walioko mbali ama karibu, wanafaa kuelewa kuwa wana jeshi la taifa linalowalinda kokote waliko. Taarifa kutoka Misri zasema kuwa, ndege za kijeshi zimewashambulia wapiganaji wa jihadi Nchini Libya kwa mabomu, baada ya kutolewa kwa mkanda wa video ulioonyesha wakristo wa Misri wa madhehebu ya Coptic wakikatwa shingo.
Jeshi la Misri linasema kuwa limelenga kambi za Islamic State, kituo cha mafunzo na maghala ya silaha, katika shambulizi hilo la mapema leo alfajiri.
Walioshuhudia wanasema kuwa, mji wa Derna ulioko mashariki mwa Libya na ambao umetekwa na wapiganaji wa jihadi ndio ulioshambuliwa vibaya.

Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, amesema kuwa mashambulio hayo ya angani ni jibu kwa wapiganaji hao ambao walitoa mikanda hiyo ya video hapo jana jumapili ilioOnyesha waumini kumi kati ya 21 waliotekwa nyara wakichinjwa.
Waumini hao wa madhehebu ya Coptic walikuwa wametekwa nyara majuma kadha yaliyopita.
Jeshi la Misri limetoa taarifa kwa vyombo vya habari inayosema kuwa raia wa taifa hilo walioko mbali ama karibu, wanafaa kuelewa kuwa wana jeshi la taifa linalowalinda kokote waliko.
Rais wa Misri alikuwa amesema nchi yake ina haki ya kujibu mashambulio kwa namna yoyote ile inayoona inafaa katika kulipiza kisasi cha mauaji ya kundi la Wakristo wa madhehebu ya Coptic yaliyofanywa na kikundi cha wapiganaji wa jihad nchini Libya wenye uhusiano na kikundi cha Islamic State.

Rais Abdel Fattah al-Sisi ametoa kauli yake kupitia televisheni ya taifa baada ya video moja kuonyesha mateka wapatao kumi wa kundi la waumini wa madhehebu ya Coptic kukatwa vichwa.
Waumini ishirini na mmoja wa madhehebu ya Coptic nchini Misri walitekwa nchini Libya wiki kadhaa zilizopita. Maandishi yaliyowekwa katika video hiyo yanaonyesha walilengwa kwa sababu ya dini yao. Misri imetangaza wiki moja ya maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo vya watu hao.
Mamlaka ya Kiislam inayoongoza nchini Misri,-- Al Azhar -- imeshutumu mauaji hayo na kuyaita ni ya "kinyama". Maelfu ya Wamisri wamekuwa wakivuka mpaka kwenda kutafuta kazi nchini Libya licha ya ushauri wa serikali yao ya Misri kuwakataza wasiende huko.

Share:

Watoto wanashiriki mzozo wa Sudan Kusini..


Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu, Human Rights Watch limezituhumu serikali ya sudan kusini pamoja na vikosi vya waasi nchini humo kwa kuwasajili watoto walio na umri wa miaka 13 kupigana katika vita vya kiraia nchini humo.
Katika ripoti hiyo ambayo serikali imekana, Human Rights Watch limesema serikali imekuwa kiwasajili watoto hao, mara nyingi kwa nguvu, huku waasi waliwatumia watoto katika mzozo wa nchi hiyo ambao umeendelea kwa miezi 14 sasa.
Mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za kibinadam la human rights watch daniel bekele, amesema kuwa licha ya kuwepo na ahadi kati ya serikali na upinzani ya kuacha kutumia watoto kama wanajeshi, pande zote mbili bado zinaendelea kuwasajili watoto jeshini.
Waziri wa habari wa Sudan Kusini Michael Makuei amepuuzilia mbali ripoti hiyo na kusisitiza kwamba kuna watu wengine wazima wenye uwezo wa kusajiliwa au kuajiriwa jeshini.

Lakini shirika hilo la Human Rights Watch limesema kuwa vikosi vya serikali vinachukua watoto , katika tukio moja shirika hilo limedai kuwa baadhi watoto huchukuliwa nje ya makao ya umoja wa mataifa iliyoko kaskazini mwa nchi hiyo mjini Malakal.
Malakal, ni mji wenye utajiri wa mafuta, umebadilisha mamlaka mara sita tangu kuanza kwa vita Desemba mwaka wa 2013, vita ambavyo vimesababisha raia takriban 21000 kutafuta makaazi katika kambi za muda za umoja wa mataifa.
Mji huo wa malakal kwa sasa uko chini ya udhibiti wa serikali.

Shirika la umoja wa mataifa la unicef limesema mwaka uliopita watoto 12,000, wengi wao wavulana, walisajiliwa kujiunga na jeshi, la serikali au kulazimishwa kuwa wapiganaji wa waasi na wanamgambo washirika wa serikali.
Kuanzia mwanzoni mwa mwaka, huu shirika la Unicef, limefaulu kuandaa mazungumzo na kundi la waasi linaloongozwa na David Yau Yau na kuezesha kuachiliwa huru kwa watoto 3000, lakini watoto wengi wangali wanatumiwa na pande hizo mbili.
Kufuatia shinikizo la kimataifa, serikali ya sudan kusini imepitisha sheria mpya inayopiga marufuku watoto kuajiriwa au kusajiliwa jeshini kabla ya umri wa miaka kumi na nane.
Vita vilianza desemba 2013 nchini humo baada ya rais wa nchi hiyo salva kirr kumtimua makamu wake riek machar kwa madai ya kujaribu kupindua serikali..
Share:

Ebola:Shule zafunguliwa Liberia..


Kuanzia leo shule nchini Liberia zinaendelea kutoa mafunzo baada ya kufungwa kwa miezi kadhaa kufuatia mlipuko wa Ebola.
Huku kukiwepo vifo vya karibu watu 4000, Liberia imekuwa nchi iliyoathirika zaidi katika nchi tatu zilizogubikwa na janga hilo,
lakini wiki kadhaa zilizopita maafisa wa serikali wameamua kwamba kupungua kwa visa vipya vya maambukizi kunatoa nafasi ya kufunguliwa upya shule hizo.
Lakini wakati watoto wengi wanaelekea madarasani, hatua za kiafya zilizochukuiwa kudhibiti ugonjwa huo zimesababisha baadhi ya wanafunzi kutojumuika na wenzao kwa mafunzo.
Shule zimefunguliwa tena nchini Liberia, baada ya kufungwa kwa miezi kadhaa kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa ebola.
Muhula mpya umeanza rasmi siku moja tu baada ya marais wa Liberia na Sierra Leone, kufanya ziara ya kwanza katika nchi za ngambo.

Wawili hao walihudhuria mkutano wa kimataifa nchini Guinea ambako waliapa kutokomeza ugonjwa huo kufikia aprili mwaka huu.
Afisa mmoja wa shirika la umoja wa mataifa la masuala ya watoto UNICEF amesema kuwa wanafunzi wengi wamerejea shuleni mapema hii leo na alishuhudia jinsi waalimu katika shule kadhaa wanavyochukua hatua za tahadhari.
Wanafunzi walilazimishwa kunawa mikono yao kabla ya kuingia darasani huku viwango vya joto vikichukuliwa kutoka kwa kila mwanafunzi.
Waalimu pia waliwaeleza wanafunzi jinsi ya kujikinga na ugonjwa huo wa ebola.
Shirika la UNICEF limekuwa mstari wa mbele kuhamasisha jamii kuhusiana na mbinu za kuzuia ugonjwa huo ambao umesababisha vifo vya zaidi ya watu elfu tisa katika mataifa ya Guinea, Sierra Leone na Liberia.
Rais wa Guinea Alpha Conde , Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia na Ernest Bai Koroma wa Sierra leone, wameungana pamoja na kutoa taarifa ya pamoja wakisema nia yao ni kutokomowza ugonjwa huo katika kipindi cha siku sitini.
Hata hivyo, kumekuwa na visa vipya vya maambukizi nchini Guinea katika siku za hivi karibuni.

Mwezi huu pekee watu sitini walipatikana na virusi vya ebola, na nchini Sierra Leone shirika la afya duniani limesema watu sabini na sita waliambukizwa.
Liberia ndio nchi iliyoshuhudia visa vingi vya ugonjwa huo na ndio nchi iliyoadhirika zaidi.
Shirika la UNICEF na mashirika mengine yametoa vifaa elfu saba mia mbili vitakavyotumika katika shule elfu nne nchini Liberia.
Zaidi ya waalimu elfu kumi na tano na wakuu wa shule mbali mbali nchini humo pia wamefunzwa mbinu
za kuzuia na kujikinga kutoka na virusi vya Ebola.
Katika nchi jiranai ya Guinea zaidi ya watoto milioni moja nukta tatu wamerejea shuleni hii leo.
Share:

Saturday 14 February 2015

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE.....


Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani nchini Dk.Charles Msonde akizungumza na wanahabari jijini dar leo.

Shule za sekondari za binafsi zinaongoza 10 bora matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana.

Akizungumza na waandish wa habari leo ofisini kwake jijini Dar es salaam, katibu mtendaji wa Baraza la mitihani nchini (NECTA)
, Dk. Charles Msonde amesema katika matokeo ya kidato cha nne ya mtihani wa mwaka jana ufaulu umeongezeka kwa 12.67% ikilinganishwa na mwaka 2013.

katika matokeo hayo msichana wa shule ya sekondari ya Baobab, Nyakaho I. Marungu ndio aliyeongoza mtihani huo na kufuatia wavulana.

Shule za sekondari za St.Fransis ya mkoani Mbeya wanafunzi sita na Feza wanafunzi nane na kufanya shule hizo kuingia katika 10 bora kwa kutoa idadi
wanafunzi wengi ikilinganishwa na shule zingine.

Msonde anasema matokeo hayo yanatokana na mfumo mpya wa GPA kwa kuangalia masomo saba hivyo ufaulu umetokana na mfumo huo.
Share:

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE..

Share:

Amkodishia mkewe mume wa 'kumhudumia'...


Mtu mmoja katika mahakama ya Kwale nchini Kenya ameshtakiwa kwa kumkata pua na mkono mkewe ambaye anamshuku kwa kufanya uasherati.
Kulingana na gazeti la the Nairobian nchini Kenya,Chirope Mwaruwa anadaiwa kumkodisha mwanamume ili kulala na mkewe mjamzito akidai kwamba ana matatizo.
Alishtakiwa kwa kumshambulia mkewe Sada Dzea katika kijiji cha Mukundi taarafa ya Mangawani ,kaunti ya Kwale.
Kulingana na upande wa mashtaka Dzea mara ya kwanza alimkataa mtu aliyekodishwa na mumewe wafanye naye tendo la ngono akiwa mjamzito.
Baada ya Dzea kukataa mumuwe alianza kumshtumu kwa kufanya uzinzi huku akitaka kumvua nguo kwa lengo la kutafuta ushahidi.
Na alipokasirishwa na shtuma hizo Dzea alidaiwa kumtembelea mtu huyo aliyekodishwa na mumewe ili afanye naye tendo la ngono kwa lengo la kumfurahisha mumewe.
lakini kabla ya yeye kufika kwa mawanmume huyo mumewe mwenye wivu mwingi alidaiwa kumvamia na kuanza kumshambulia.
Share:

Zuma: hakuna ruhusa mgeni kumiliki ardhi...

Sanamu ya Mandela, Afrika Kusini
Wageni hawatoruhusiwa kumiliki ardhi Afrika Kusini, kufuatana na sheria kali zinazopendekezwa na Rais Jacob Zuma.
Siku zijazo wageni wataruhusiwa tu kukodi kwa muda mrefu ardhi ya mashamba ya Afrika Kusini.
Mbali ya hayo, mtu yeyote anayemiliki zaidi ya hekta 12,000 atalazimishwa kuiuzia serikali ili ipate kugawiwa.
Ardhi bado ni swala linalozusha hamasa nchini humo - ambako karne tatu za ukoloni na ubaguzi wa rangi - zimeacha ardhi nyingi mikononi mwa wachache, hasa wazungu.
Tangu kumalizika ubaguzi wa rangi mwaka 1994, chama tawala cha ANC, kimeshindwa kufikia lengo lake la kugawa thuluthi ya ardhi ya kilimo kwa Waafrika, ulipofika mwaka 2014.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.