Sunday 31 May 2015

Mhudumu wa baa taabani kwa kifo cha mteja


Muhudumu mmoja wa baa amepatikana na hatia ya mauaji baada ya kumpa mteja wake jumla ya vipimo 56 vya pombe na kisha akafa.
Raia huyo wa Ufaransa alimpa Renaud Prudhomme, mwenye umri wa miaka 56, ''shoti'' 56 za mvinyo katika baa yake kwa nia ya kuvunja rekodi ya mywaji pombe nambari moja.
Marehemu Prudhomme, aliyekuwa ameandamana na binti yake kujiburudisha, alipelekwa nyumbani akiwa mlevi chakari.
Inaarifiwa kuwa alikimbizwa hospitalini ambapo alipatikana ameaga dunia siku iliyofuatia.
Hata hivyo mahakama ilimpata na hatia mhudumu huyo Gilles Crepin, mwenye umri wa miaka 47, kwa kumchochea marehemu Prudhomme aendelee kubugia mvinyo ilihali alikuwa mlevi kupindukia.
Mahakama ilisema kuwa Crepin aliendelea kuandika nani anayeshikilia rekodi hiyo kwenye ubao uliotundikwa hadharani kwa wateja wake.
Sasa Crepin amehukumiwa kifungo cha nyumbani cha miezi minne na kupigwa marufuku ya kufanya kazi katika baa yeyote kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Wakili wake Renaud Portejoie tayari amesema kuwa atakata rufaa dhidi ya kauli hiyo ya mahakama.

"kauli hii haina hata chembe ya haki bali ni hisia tu zilizotumika hapa ,ninavyoona mimi hizi ni jitihada za amahakama kutoa hukumu ili iwe funzo''
Awali alikuwa ameiambia mahakama kuwa kifo cha Prudhomme hakikutokea kimsingi na kufuatia matukio ya mteja wake kwani marehemu alikuwa na maradhi ya kupumua mbali na kuwa mraibu wa tembo.
''kwa hakika hatuwezi kuwalazimisha wateja wote wa pombe kutoa ithibati kuwa wako katika hali nzuri ya afya''
Wakili wa mwanawe marehemu Antoine Portal, alisema kuwa familia yao imetulizwa na marufuku hiyo ya Crepin ya mwaka mmoja.
''Nilikuwa nataka tu kuwakumbusha wahudumu wa baa kuwa ni kinyume cha sheria kuendelea kumpa pombe mlevi''
Share:

Ujerumani ina idadi ndogo zaidi ya watoto duniani


Idadi ya watoto wanaozaliwa nchini Ujerumani imepungua zaidi ya mataifa yote duniani.
Utafiti umeonesha kuwa idadi ya watoto wanaozaliwa nchini Ujerumani ndiyo ya chini zaidi duniani na sasa kunahofu kuwa kupungua kwa uzazi kutaathiri pakubwa uwezo wa vijana kuendeleza kasi ya ukuaji wa uchumi wa taifa hilo tajiri zaidi barani Ulaya.
Watafiti wanaonya kuwa endapo jitihada mahsusi hazitafanywa ilikuimarisha idadi ya watoto nchini humo basi uchumi wa taifa hilo utaathirika vibaya.
Kulingana na utafiti huo,watoto 8.2 pekee walizaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.
Awali idadi ya chini zaidi ilikuwa ya Japan ambayo huandikisha idadi ya watoto 8.4 wanaozaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.

Kampuni ya uhasibu ya Ujerumani BDO ikishirikiana na chuo cha utafiti wa kiuchumi cha Hamburg Institute of International Economics (HWWI) ndiyo iliyoendesha utafiti huo kwa lengo la kutathmini uwezo wa uchumi wa taifa hilo kujiendesha mbali na viwango vya uzazi vinavyoripotiwa nchini humo.
Barani Ulaya, Ureno na Italia ziliorodheshwa katika nafasi ya tatu na nne zikiwa na jumla ya watoto 9.0 na 9.3 mtawalia.
Ufaransa na Uingereza zinasajili watoto 12.7 wanaozaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.
Niger iliyoko Afrika ndiyo inayoandikisha idadi kubwa zaidi ya watoto wanaozaliwa duniani.
Nchini humo watoto 50 huzaliwa miongoni mwa watu wazima 1000.

Kulingana na utafiti huo wa BDO iwapo hali itaruhusiwa kuendelea hivyo basi idadi ya watu wenye umri wa kati ya miaka 20 na 65 wenye uwezo wa kufanya kazi na uwezo wa kuendesha uchumi wa taifa hilo itapungua kwa asilimia 61% hadi 54% ifikapo mwaka wa 2030.
Aidha afisa wa BDO Arno Probst, aliwatahadharisha wajerumani kuwa kiwango cha malipo na mishahara ya wafanyikazi kitaongezeka maradufu kadri ya upungufu wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi .
Probst alisema Ujerumani italazimika kuwaruhusu wahamiaji kuingia nchini humo na kufanya kazi ilikuepuka kuzorota kwa uchumi wake.
Share:

China yatetea miradi yake baharini


Mmoja wa makamanda wa ngazi za juu katika jeshi la China ametetea sera za China za kujenga miradi katika maeneo yanayozozaniwa baharini katika bahari ya kusini mwa china siku moja baada ya marekani kutaka miradi hiyo kusitishwa mara moja.
Su Jianguo ambaye ni naibu wa mkuu wa majeshi aliuambia mkutano mkuu nchini singapore kuwa miradi hiyo ina lengo la kuboresha uwezo wa China wa kutekeleza majukumu yake ya kimataifa na kusaidia eneo hilo.
Alisema kuwa kati ya majukumu hayo ni pamoja na jitihada za uokoaji, utunzi wa mazingira na uhuru wa safari za baharini. China inasema kuwa karibu eneo lote la kusini mwa bahari ya china ni lake.
Share:

Majeshi yazima shambulizi la Boko Haram.


Jeshi la Nigeria limezima mashambulizi ya wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram katika mji wa Maiduguri ulioko Kaskazini Mashariki mwa taifa hilo.
Wapiganaji hao wa Kiislamu walikuwa wanafyatua makombora mazito mazito kuelekea mji huo usiku wa kuamkia leo lakini wanajeshi wakahimili mashambulizi na kuwakabili.
Watu 13 wameripotiwa kupoteza maisha yao katika mashambulizi hayo ya Boko Haram.

Shambulizi limetokea saa chache baada ya kuapishwa kwa rais mpya wa Nigeria Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari ambaaye ameahidi kukabiliana na tishio la mashambulizi ya kigaidi ya Boko Haram bila huruma.
Mwandishi wa BBC aliyeko Nigeria anasema kuwa huenda hii ni njia ya kundi hilo la wapiganaji kumuonesha Rais mpya kuwa wangali wapo licha ya mashambulizi makali dhidi yao na majeshi ya muungano wa mataifa ya Magharibi mwa Afrika.

Rais Buhari akihutubia taifa punde baada ya kuapishwa alisema kuwa jeshi la taifa hilo litakita kambi yake katika mji huo wa Maiduguri ilikuitokomeza kabisa kundi hilo la waislamu la Boko Haram.
Awali Katika mahojiano maalumu na BBC, kiongozi huyo mstaafu wa jeshi amesema anatarajia kulishinda kundi hilo baada ya dhamira mpya kutoka jeshini na msaada wa nchi jirani.
"Kwa ushirikiano na majirani zetu Cameroon, Chad, Niger na jumuia ya kimataifa na dhamira ambayo tutapata kutoka katika jeshi, Nafikiri itachukua muda mfupi zaidi kukabiliana nao."

Jenerali Buhari amesema tayari ameainisha msingi wa tatizo linalokabili nchi ya Nigeria, lakini amewataka raia wa nchi hiyo kuwa wavumilivu.
"Tumebaini matatizo makubwa matatu.
Ambayo ni kukosekana kwa usalama nchini, tatizo ambalo kila mmoja analifahamu na lingine ni ukosefu wa ajira, hii ina maana uharibifu wa uchumi ikiwa ni kutokana na vitendo vya rushwa na rushwa yenyewe.

Matatizo haya matatu makuu, Wanigeria wote wanafahamu na tunaomba ushirikiano wa wananchi wa Nigeria,
wasitarajie miujiza kutokea katika kuyapatia ufumbuzi matatizo haya katika kipindi cha miezi michache baada ya kutwaa madaraka kwa sababu uharibifu umechukua miaka mingi,
miaka kumi na sita ya utawala wa chama tawala cha nchi hii." Anasema rais huyo mpya wa Nigeria.
Share:

Maandamano yafanyika Venezuela


Maelfu ya watu wamefanya maandamano ya amani nchini Venezuela wakipitia barabara za mji mkuu Caracas wakitaka kuachiliwa kwa viongozi wa upinzani ambao wamekuwa gerezani kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Wanasiasa hao ni pamoja na mameya wawili wa zamani Leopoldo Lopez na Daniel Ceballos ambao wanazuiliwa kwa mashtaka ya kuchochea maandamano ya kuipinga serikali.
Rais wa Venezuela Nicholas Maduro amewalaumu kwa vifo 43 vilivyotokea wakati huo. Wiki hii wawili hao walitangaza kuanza mgomo wa kutokula wakiwa gerezani.
Share:

Nkurunziza:Sitahudhuria mkutano Tanzania


Msemaji wa rais wa Burundi amesema kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza hatahudhuria mkutano wa viongozi wa kikanda ambao utaangazia mzozo ulio nchini mwake.
Msemaji huyo aliliambia shirika moja la habari la Ufaransa kuwa rais Pierre Nkurunziza atakuwa akifanya kampeni ya uchaguzi wa urais na kwamba waziri wa mashauri ya kigeni ndiye atahudhuria mkutano ambao utawajumuisha marais wa Rwanda, Uganda , Tanzania na Kenya mjini Dar es Salaam.
Wakati Nkurunziza alihudhuria mkutano kama huo mpema mwezi huu baadhi ya maafisa wa kijeshi walijaribu kumpindua.
Burundi imekumbwa na ghasia tangu Nkurunziza atangaze kuwa atawania urais kwa muhula wa tatu.
Hapo jana Nia ya rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu ilipata pigo baada Afisa mmoja tume hiyo ya uchaguzi kuiambia redio moja ya Ufaransa kuwa Spes Caritas Ndironkeye aliabiri ndege ijumaa na haijulikani kama alijiuzulu au la.

Tume hiyo ya uchaguzi ina maafisa wakuu watano na inaweza kuendelea kuhudumu hata baada ya kuondoka kwa mmoja wao.
Hata hivyo duru zinaelezea kuwa huenda afisa wa pili wa tume hiyo akajiondoa na hivyo kulemaza shughuli za tume hiyo.
Juma lililopita kanisa katoliki nchini Burundi lilijiondoa kutoka kwa harakati zozote za uchaguzi mkuu uliokumbwa na utata siku moja tu kabla ya umoja wa Ulaya kuondoa maafisa wake katika shughuli hizo za uchaguzi.
Umoja wa ulaya ulikuwa umetuma maafisa wa kucimamia na kuhakikisha kuwa uchaguzi huo ni wa huru na haki.
Taarifa hiyo imetokea wakati ikisalia wiki moja tu uchaguzi wa wabunge na madiwani ufanyike nchini humo.

Kanisa katoliki ni kiungo muhimu katika suala la amani na demokrasia nchini Burundi tokea kuanzishwa mazungumzo ya amani ya Arusha mnamo miaka ya tisini.
Haya yamearifiwa wakati maandamano dhidi muhula wa tatu wa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza yanaendelea kufanyika katika mitaa kadhaa ya mji mkuu Bujumbura kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
Makundi ya kutetea haki za binadamu, yanasema kuwa zaidi ya watu 20 wamefariki wakati wa ghasia za maandamano,
Tangu rais Pierre Nkurunziza alipotangaza mwezi uliopita kuwa anapania kuwania tena kiti cha urais kwa muhula wa tatu, kinyume na katiba ya Burundi.
Uchaguzi wa urais umepangiwa kufanyika Juni tarehe tano, huku ule wa urais ukiwa mwishoni mwa mwezi huo wa Juni.
Share:

Wednesday 27 May 2015

Bolt ashinda mita 200


Mwanariadha raia wa Jamaica Usain Bolt ameshinda kwa urahis katika shindano lake la kwanza mwaka huu huko barani Ulaya japokuwa ameshindwa kuvunja rekodi yake ya sekunde 20, kwenye mbio za mita 200 za Golden Spike huko Ostrava Jamhuri ya Czech.
Katika shindano hilo lililofanyika jana Bolt alitumia sekunde 20.13 ikiwa ya rekodi yake ya dunia ya sekunde 19.19 akimbwaga mmarekani Isiah Young "huwezi ridhika kama sivunji sekunde 20" alisema Bolt ambaye anajiandaa kwa mashindano ya dunia yatakayofanyika Beijing mwezi August. Naye Asafa Powell ameshinda katika mbio za mita 100 akitumia sekunde 10.04.
Share:

Wakili nchini Kenya kuwa mkwe wa Obama?


Taarifa kuwa wakili mmoja wa kenya amesema yuko tayari kutoa mahari kwa mtoto wa raisi wa Marekani,Barrack Obama zimeenea duniani kote Felix Kiprono amesema yuko tayari kutoa ng'ombe 50,kondoo 70 na mbuzi 30 kwa ajili ya mahari ya mtoto wa Obama,Malia Obama.Hivyo anajiandaa kuzungumzia swala hilo na baba wa mtoto huyo atakapo tembelea Kenya ,mwezi Julai.
Share:

Rushwa:Maafisa wa Soka wakamatwa Zurich.


Waandishi wa Habari wakishuhudia kukamatwa kwa maafisa wa Soka nje ya hoteli mjini Zurich

Maafisa sita wa shirikisho la soka duniani Fifa wamekamatwa katika hoteli moja mjini Zurich,Switzerland. kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa.
Watuhuhumiwa hao ambao wanasemekana kuwa ni pamoja na makamu wa rais wa Fifa,wanashikiliwa wakisubiri kusafirishwa kwenda Marekani.
Shutma hizo zinahusisha rushwa ya takriban kiasi cha dola za Marekani milioni 100 kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20
Wanachama wa Fifa wanakutana mjini Zurich kwa ajili ya mkutano wao wa mwaka siku ya ijumaa, ambapo rais wa Shirikisho hilo Sepp Blatter anawania muhula wa tano.
Mwana mfalme Ali Bin Al-Hussein wa Jordan,ambaye ndiye mpinzani pekee wa Blatter amesema tukio hilo ni "baya kwa maendeleo ya soka".

Rais wa Fifa ambaye anawania muhula wa tano ndani ya shirikisho hilo, Sepp Baltter

Gazeti la New York Times limesema askari kanzu walichukua funguo za chumba cha hoteli kutoka eneo la mapokezi ya hoteli ya Baur au Lac hotel ambayo maafisa hao walikuwa wakiishi na kuingia vyumbani mwao.Gazeti hilo limesema Operesheni hiyo ilifanyika kwa utulivu.
Jeffrey Webb, Mkuu wa shirikisho la Amerika ya Kaskazini na Kati na Visiwa vya Caribbean ametajwa kuwa mmoja kati ya maafisa waliokamatwa.
Maafisa wengine wa Fifa walishuhudiwa na BBC wakisindikizwa na Polisi kutoka kwenye hoteli hiyo ni:
Mkuu wa Shirikisho la soka la Costa Rica, Erduado Li, ambaye alikuwa akitarajia kuwepo kwenye mkutano wa kamati ya Fifa siku ya ijumaa.Wengine ni rais wa shirikisho la Uruguay Eugenio Figueredo,rais wa shirikisho la soka Amerika kusini Conmebol na wa Brazil,Jose Maria Marin,mwanakamati ndani ya Fifa,Polisi walionekana wamebeba mikoba yake kwenye mifuko ya Plastiki.
Watu wengi wamekuwa wakijiuliza ni kwa vipi Blatter amekuwa Kiongozi wa Fifa kwa muda mrefu, pamoja na kuwepo kwa ripoti nyingi za vitendo vya rushwa lakini ameendelea kushikilia wadhifa huo.
Wizara ya sheria ya Uswiss imesema katika tamko lake siku ya jumatano kuwa maafisa wa serikali ya Marekani waliwashuku maafisa hao kupokea rushwa ya dola milioni 100, tangu mwanzoni mwa miaka ya 1990 kwa ajili ya michuano ya Amerika ya kati.
Serikali ya Uswiss imesema itaidhinisha haraka kusafirishwa kwao.
Mwanzoni mwa mwezi huu, Blatter alisema anafahamu baadhi ya wafanyakazi wenzake wa zamani walikuwa wakichunguzwa lakini amekanusha kuwa uchunguzi huo ulimhusu pia.
Share:

AfDB kupata rais mpya kumrithi Kaberuka.


Rais wa Benki ya maendeleo Afrika, Donald Kaberuka

Benki ya Maendeleo ya Afrika inaendesha shughuli zake chini ya uongozi wa rais, ambaye anafanya kazi kama mwakilishi halali wa Benki, mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi na mnadhimu wa Benki hiyo. Rais anaendesha shughuli za sasa za Benki, chini ya maelekezo ya Bodi ya Wakurugenzi. Rais huchaguliwa na Bodi ya Magavana na anahudumu kwa miaka mitano. Pia anaweza kurudia kipindi kimoja tu cha miaka mitano mingine.
Rais wa sasa wa AfDB, Dr. Donald Kaberuka, raia wa Rwanda, alichaguliwa mwezi Julai 2005,na alianza awamu yake ya kwanza Septemba Mosi 2005. Kufuatia kuchaguliwa kwake tena mwezi Mei 2010, alianza kipindi chake cha pili cha miaka mitano mingine Septemba Mosi 2010. Kwa mujibu wa taratibu za uongozi katika Benki hiyo, Bodi ya Magavana inalazimika kumchagua mtu mwingine kuchukua nafasi hiyo
Wanaowania kushika nafasi hiyo ni:

Birima Sidibe, Mali Birama Sidibe ni mhandisi ambaye amejikita katika utaalam kilimo umwagiliaji. Kwa zaidi ya miaka thelathini, alikuwa akifanya kazi katika sekta ya maendeleo. Alifanya kazi na Benki ya Maendeleo ya Afrika tangu mwaka 1983-2006. Birama Sidibé pia alifanya kazi katika benki ya Maendeleo ya kiislamu, mjini Nairobi na kwa ajili ya shirika la River Senegal.

Benki ya Maendeleo ya Afrika

Jalloul Ayed, Tunisia Jelloul Ayed ni mfanyakazi wa benki mwenye mafanikio nchini mwake na ana umri wa miaka 64. Yeye pia anajulikana kwa kuendesha harambee ya kuchangisha fedha zilizotolewa katika soko la Ulaya kwa ajili ya kampuni za Tunisia na Morocco. Mwaka 2011, akiwa waziri wa fedha wa mpito wa serikali baada ya kuanguka kwa Serikali ya aliyekuwa rais wa Tunisia Ben Ali, aliwahi kuwasilisha programu ya maendeleo ya kijami na kiuchumi katika mkutano mkuu wa G8. Bedourma Kordje, Chad, Ni waziri wa fedha nchini Chad sasa ivi, huyu mhandisi wa mawasiliano ya simu kwa miaka 29 ameitumikia benki ya maendeleo Afrika kabla ya kurudi nchini kwake na kuwa waziri wa fedha mwaka 2012. Rais Idriss Deby ameahidi kushawishi wanachama wa jumuiya ya afrika ya kati kwa ajili ya uchaguzi wa benki ya maendeleo ya Afrika AfDB.

Cristina Duarte, Sura Verde Ni mgombea mwanamke pekee kwa nafasi hii, lakini si kwa sababu yeye ni mwanamke, bali Anataka aangaliwe kwa uwezo wake wa kazi pia na si jinsia yake. Amelirudia mara kadhaa hilo na pengine ni sahihi. Amekuwa waziri wa fedha wa nchi yake tangu mwaka 2006. Anasifa kubwa ya kufanya mageuzi na kunyanyua uchumi wa nchi yake. Amefanya kazi pia na mashirika tofauti ya kimataifa ya kuleta maendeleo. Adesina Akinwumi, Nigeria Ni waziri wa sasa wa Kilimo na Maendeleo ya vijijini, Nigeria. Ana miaka 55 na amewahi kuwa Makamu wa Rais wa Muungano wa Mapinduzi ya Kijani Afrika (AGRA). Elimu yake ni shahada ya juu ya uzamivu katika uchumi wa Kilimo.Jarida liitwalo Forbes lilimtunuku jina la mwafrika wa mwaka 2013 kutokana na mageuzi yake katika sekta ya Kilimo.

Wanaowania Urais wa Benki ya maendeleo Afrika

Sufian Ahmed, Ethiopia Waziri huyu wa fedha na maendeleo ya kiuchumi mwenye umri wa miaka 57 anataka kutumia matokeo mazuri ya kiuchumi ya nchi yake kama mtaji kwa ajili ya kazi anayo iomba. Anasifika kwa kiasi kikubwa sana kwa kuwa na mchango mkubwa wa kiuchumi nchini mwake. Kamishna huyu wa zamani wa Mamlaka ya Forodha Ethiopia anajichukulia kama mwanamatumaini wa kiafrika. Pia elimu yake yote ameipatia nchini mwake.

Samura Kamara, Sierra Leone Ni mfanyakazi wa zamani wa shirika la fedha duniani, IMF na sasa ni waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa kimataifa pia ni mwanamchumi mzoefu. Hiyo ni sababu kuu ya Rais Ernest Bay Koroma ametaka awe mjumbe wa serikali yake. Yeye awali alikuwa waziri wa Fedha. Ushirikiano wa Afrika ni kati ya mada kuu ya kampeni zake.

Thomas Sakala, Zimbabwe SADC imemchagua Raia wa Zimbabwe huyu kuwa mgombea wa kanda ya kusini mwa Afrika. Alistaafu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika mwaka jana tu na hadhi yake hiyo inaweza kuwa msaada mkubwa kwenye kinyang'anyiro hicho. Alifanya kazi na serikali nyingi za Afrika katika programu mbalimbali. Yeye anapigia upatu maendeleo ya miundombinu miongoni mwa masuala mengine.
Share:

Tuesday 26 May 2015

Papa Francis: Sijatazama Tv kwa miaka 25.


Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis, amesema kuwa hajawahi kutazama runinga kwa miaka 25 sasa.
Papa Prancis ambaye amewatamausha wachanganuzi wa kanisa hilo kwa kususia maisha ya kifahari katika makao makuu ya kanisa Vatican alisema alitizama runinga mara ya mwisho tarehe 15 mwezi julai mwaka wa 1990.
Alikoma kutizama runinga baada ya kumuahidi maria mtakatifu kuwa angekoma kushiriki uraibu huo.

Isitoshe raia huyo wa Argentina amesema kuwa hatumii mtandao wa intaneti.
Na akitaka kupata habari za kimataifa , Papa anasema kuwa huwa anatenga dakika 10 tu ya muda wake kusoma gazeti la kiitaliano.

Papa Francis vilevile anafuatilia habari za klabu yake maarufu huko Argentina kupitia kwa wahudumu wake ambao humsimulia yanayojiri.
Je unaweza kukaa mbali na Runinga yako Simu yako ama mtandao wa Intanet japo kwa siku moja ?
Share:

Jela siku 1 iwe ilani ya Ufisadi China.


Maafisa wa serikali Mashariki mwa China wamelazimika kuzuru gereza moja nchini humo kama ilani ya kutoshiriki ufisadi.
Maafisa hao 70 wakiwa wameambatana na wachumba wao walilazimishwa kushinda mchana kutwa katika gereza moja lililoko mjini Shiyan katika mkoa wa Hubei tarehe 15 mwezi Mei.
Serikali kuu ya China ilianzisha harakati za kukabiliana na ufisadi miongoni mwa wafanyikazi wa uma tangu rais aliyeko madarakani Xi Jinping alipochukua mamlaka mwaka wa 2012.

Tangu mwaka huo 2012, maelfu ya wafanyikazi wa uma wamechunguzwa na asilimia kubwa yao kuhukumiwa jela baada ya kupatikana na hatia ya kutumia madaraka yao vibaya.
Ziara hiyo ya lazima iligundulika baada ya shirika la kupambana na ufisadi kuchapisha ripoti hiyo katika jarida lake la hivi punde siku ya jumamosi.
Kulingana na ripoti hiyo ya tume ''ziara hiyo ilipaswa kuwaonya na kuwapa fursa ya kuonja maisha ndani ya jela nyuma ya vyuma vikubwa na madirisha yaliyoweka juu zaidi''
Picha zilizochapishwa zinaonesha maafisa hao wakuu wa umma wakiambatana na wachumba wao.

Maafisa hao walipata fursa ya kuzungumza na maafisa wanaotumikia vifungu tofauti kwa makosa ya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka yao.
Aidha walitembelea maonyesho ya picha na maandishi ya wafanyikazi wenza waliofungwa.
Tume hiyo ya kupambana na ufisadi CCDI ilisema katika ripoti hiyo kuwa wengi wa maafisa hao walipigwa na butwaa walipowaona maafisa waliowahi kufanya kazi pamoja na wengine wakawachwa vinywa wazi baada ya kuwatambua vigogo waliotamba katika enzi zao lakini sasa wakiwa ni wafungwa.

Maafisa hao walilazimishwa kusikiza sauti za maafisa waliowatangulia wakikiri makosa yao.
China imekuwa ikiendesha kampeini kubwa ya kupambana na ufisadi na ubadhirifu wa mal ya uma huku maafisa wa uma wakitakiwa kuishi maisha yao kadri ya mishahara yao.
Aisha wafanyikazi wa umma wametakiwa kukoma kupokea zawadi ghali kutoka kwa wanakandarasi na watu wenye nia ya kufanya biadhara na serikali.
Vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti visa ambayo maelfu ya wafanyikazi wadogo serikalini wanakamatwa na kilele cha kampeini hiyo dhidi ya ufisadi ilikuwa kukamatwa kwa aliyekuwa mkuu wa usalama wa ndani Zhou Yongkang.

Share:

Wimbi la Joto lawaua watu 430 India.


Takriban watu 430 wamekufa kutokana na wimbi la joto linalovuma nchini India.
Watafiti wamesajili kiwango cha juu mno cha nyuzijoto 48'C katika maeneo mengi nchini humo.
Vifo vingi zaidi vimeripotiwa katika majimbo ya kusini ya Telangana na Andhra Pradesh, ambapo watu 140 wamepoteza maisha yao kuanzia jumamosi wimbi hilo la joto lilipotokea.
Mji wa Allahabad ulioko Uttar Pradesh ulisajili vipimo vya nyuzijoto 48C huku wakaazi wa mji mkuu wa India New Delhi ukistahimili kiwango cha nyuzijoto 44C .

Maafisa wa utawala nchini humo wameanza kampeini ya kuwahamasisha wanainchi kukaa majumbani mwao na kuwashauri wanye waji mengi.
Yamkini viwango vya joto vimekuwa juu zaidi katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita lakini vifo vimeanza kuripotiwa mwishoni mwa juma.
Jimbo la Andhra Pradesh ndilo lililopoteza watu wengi zaidi ikiwa na jumla ya watu 246 waliopoteza maisha yao kuanzia juma lililopita.

"asilimia kubwa ya wale waliopoteza maisha ni watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50 walioshinda nje ya majumba yao.'' alisema kamishna wa kupambana na majanga katika jimbo la Andhra Pradesh.
Wakfu wa waandishi wa habari wanasema kuwa watu 186 wameaga katika wilaya 10 za jimbo la Telangana.
Watu 58 wamekufa kuanzia siku ya jumamosi.
Idara ya utabiri wa hali ya hewa imesema kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa hali hiyo ya joto kuendelea kwa siku kadha zijazo.

Watu wengine kumi walpoteza maisha yao katika jimbo la Magharibi mwa Bengal.
Waendesha teksi ambazo hazina kiyoyozi hawataruhusiwa kuhudumu kwa saa tano katika mji mkuu wa Kolkata. Hii inafuatia vifo vya madereva wawili.
Idara ya utabiri wa hali ya hewa inasema kuwa hali hiyo ya juu ya joto inatokana na ukosefu wa mvua.
Share:

Mafuriko yaua 18,Texas Marekani.


Mafuriko yamesababisha vifo vya watu 18 Magharibi mwa Marekani na Kaskazini mwa Mexco.
Wengi wa waliothibitishwa kufariki dunia kutokana na mafuriko hayo ni kutoka mpakani mwa Mexco katika mji wa Acuna.
Hata hivyo katika mji wa Texas watu watatu wamearifiwa kufa pia na wengine 12 hawajulikani waliko baada ya makazi yao kusombwa na mafuriko.
Gavana wa Texas Greg Abbott anasema mafuriko hayo yameleta madhara makubwa katika jimbo lake.
Share:

Urusi yaanzisha mazoezi ya Kijeshi.


Urusi imeanza mazoezi makali ya kivita yanayojumuisha kikosi cha anga cha wanajeshi 150 pamoja nakikosi cha mashambulio ya mbali ya makombora.
Wizara ya mambo ya ndani ya Urusi inasema kuwa wanajeshi 12,000 wanatarajiwa kuhusishwa na mazoezi hayo makali ya siku nne yanayolenga kutaka kujua uimara wa jeshi hilo na utayari wake.
Mazoezi hayo makali yanakuja sawa nay ale yanayoendeshwa na vikosi vya NATO na majeshi ya Ulaya Nordic yanayojumuisha zaidi ya wapiganaji 100 wa jeshi la anga.
Hata hivyo tukio hili la mazoezi ya majeshi ya Urusi yanaleta kwa nchi za magharibi kufuatia machafuko yanayoendelea Ukraine ambapo Urusi imekuwa ikinyooshewa kidole kutokana na machafuko hayo.
Share:

Ufisadi:Mawaziri 4 kushtakiwa Kenya


Kutumia ujumbe kwa vyombo vya habari, mkuu wa mashtaka ya umma nchini Kenya Keriako Tobiko, hii leo amevumbua yaliyomo katika hati za kesi za mawaziri wanne.
Tume ya maadili na kupambana na ufisadi ya Kenya imependekeza waziri wa uchukuzi mMhandisi Michael Kamau na waziri wa leba Kazungu Kambi kushtakiwa na matumizi mabaya ya ofisi.
Mhandisi Michael Kamau anakumbwa na shutuma za kutumia fedha ubadhirifu wa fedha za umma na kufanya mabadiliko katika ubunifu wa barabara ambayo tiyari ilikuwa imetengenezwa na mashauri.
Kazungu Kambi naye anadaiwa keteuwa wanachama wawili katika bodi ya shirika la taifa la hazina ya uzeeni kinyume na sheria.
Akizungumza na waandishi wa habari jana alasiri jumapili, afisa mkuu wa tume ya maadili na kupambana na ufisadi Halakhe Waqo, alisema kwamba mawaziri wanne waliochunguzwa ni waziri wa Uchukuzi Mhandisi Michael Kamau, waziri wa ardhi, makao na ustawi wa miji bi Charity Ngilu, waziri wa kilimo Felix Kosgei, waziri wa leba Kazungu kambi, seneta wa Nairobi Mike Sonko na mbunge .
Tume hio imemwandikia rais Uhuru Kenyatta ombi la kuongeza muda wa uchunguzi wa kesi zilizobaki.
Siku sitini ambazo walikuwa wamepewa kukamilisha uchunguzi wa ripoti hiyo zimetimia leo.

''Tumekuwa na shinikizo la kukamilisha kesi kwa wakati uliotolewa ila wajibu wetu wa kufanya uchunguzi wa kina ambao unaweza kustahimili uchunguzi mahakamani umetulazimu kuomba muda zaidi''alisema Halakhe Waqo
Kwa sasa tume hio imekamilisha kesi 56 kati ya 124 zilizowasilishwa kwa uchunguzi zaidi baada ya ripoti yao ya awali iliyokabidhiwa rais Kenyatta kuwasilishwa bungeni .
Kesi 21 tayari zimefikishwa kwa mkuu wa mashtaka ya umma Keriako Tobiko.
Kufikia sasa maafisa 19 wamefikishwa mahakamani na wengine 29, kulingana na afisa mkuu wa EACC, watafikishwa mahakamani siku chache zijazo katika maeneo kadhaa nchini yakiwemo Turkana, Machakos, Nyamira, Nairobi na Trans nzoia
Hata hivyo tume hii nayo pia imekumbwa na malumbano ya ndani kwa ndani ya shtuma za ufisadi, zilizosababisha kuchunguzwa kwa kiongozi wa tume hiyo na baadhi ya wanatume wake ambao hatimae walijiuzulu.
Share:

Basi lachomwa Burundi.


Basi moja la uchukuzi limechomwa moto mjini Bujumbura Burundi na waandamanaji waliorejea mabarabarani kupinga uamuzi wa rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Waandamanaji wanachoma moto magurudumu haswa katika eneo la Kanyosha.
Kitongoji hicho kimekuwa kitovu cha maandamano haya dhidi ya awamu ya tatu ya rais Nkurunziza.

Mwandishi wa BBC mjini Bujumbura Ismael Misigaro amesema milio ya risasi inasikika mjini humo.
Maandamano haya yanarejea baada ya kuuawa kwa kiongozi wa chama cha upinzani Zedi Feruzi nje ya nyumba yake katika mji mkuu Bujumbura.
Aidha wanaharakati wa upinzani nchini humo wamesitisha mazungumzo na serikali rais Pierre Nkurunziza ya kutaka kutanzua mzozo ulioko wa kisiasa.

Mzozo huo unafuatia hatua ya Nkurunziza kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi ambao wengi wanasema kuwa unaenda kinyume na sheria na ndio iliyosababisha kuwepo kwa jaribio la kumpindua, na maandamano ya wiki kadhaa.
Tayari zaidi ya raia 100,000 wa taifa hilo wametorokea mataifa jirani.
Share:

Wednesday 20 May 2015

Somalia:Majeshi ya Burundi kuondolewa?


Mjumbe wa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa nchini Somalia, Nicholas Kay amesema ikiwa hatua ya kuondoa majeshi ya Burundi itafanyika nchini Somalia itaathiri mapambano dhidi ya wanamgambo wa Al Shabab.

Mwanzoni mwa juma hili Marekani ilitangaza kupunguza kiasi cha pesa inachotoa kwa majeshi ya Burundi baada ya shutuma kuwa jeshi hilo limejihusisha katika vitendo vya ukiukwaji wa haki za binaadamu wakati wakizima vurugu zilizojitokeza katika jaribio la mapinduzi dhidi ya Serikali ya Rais Pierre Nkurunziza liliposhindwa.
Umoja wa mataifa ya Afrika AU, nayo imesita kupeleka kundi jingine la wanajeshi wa Burundi nchini Somalia.

Lakini Kay, ameiambia BBC kuwa majeshi ya Umoja wa Afrika yanahitaji msaada kuweza kupambana na Al Shabaab.
Aidha Kay ametahadharisha kuongezeka kwa mahitaji ya kibinaadamu nchini Somalia na kutoa wito wa jumuia ya kimataifa kuendelea kupeleka misaada nchini humo.
Share:

Burundi:Nkurunziza ahairisha uchaguzi..


Rais wa Burundia Pierre Nkurunziza amehairisha uchaguzi wa ubunge kwa siku kumi .
Msemaji wa rais Willy Nyamitwe ameiambia shirika la habari la AFP kuwa kufuatia jaribio la mapinduzi juma lililopita na vurugu zilizofuatia ni bora kuahirisha uchaguzi huo kwa muda.
''Uchaguzi huo wa ubunge ulikuwa umeratibiwa kufanyika tarehe 26 mwezi Mei lakini sasa inatubidi kuihairisha ili kuwasikiza washirika wetu wa kimataifa pamoja na tume ya uchaguzi ambayo pia inatumia muda huo kutatua maswali yaliyoulizwa na vyama vya upinzani.'' alisema Nyamitwe.
Hadi kufikia sasa tarehe rasmi ya uchaguzi wa urais uliopangwa kufanywa Juni tarehe 26 haijabadilika.
''Subiri tu'' Nyamitwe aliwaambia waandishi wa habari.

Mwandishi wa BBC aliyeko huko Ruth Nesoba amesema kuwa tayari rais Nkurunziza ametia sahihi amri hiyo ya kuhairishwa kwa uchaguzi.
Umoja wa mataifa ya bara Ulaya EU, na Umoja wa mataifa ya Afrika AU, yametoa wito kwa uchaguzi huo uliokumbwa na utata mkubwa uhairishwe ilikutoa fursa kwa mazungumzo ya upatanishi kuendelea .
Hapo jana Rais wa Afrika Kusini alitilia pondo hoja hiyo ya kuahirisha uchaguzi akisema ni bora uchaguzi huo uliopangwa ''uhairishwe''.
Takriban watu 20 wameuawa kufuatia makabiliano baina ya polisi na waandamani katika mji mkuu wa Bujumbura kilele ikiwa ni juma lililopita makamanda waasi walipotangaza jaribio la mapinduzi rais
Nkurunziza akiwa mjini Dar es Salaam kuhudhuria mkutano wa viongozi wa kanda uliolenga kutatua mzozo wa kisiasa nchini mwake.

Wapinzani wa rais Nkurunziza wanasema kuwa kutangazwa kwake nia ya kuwania muhula wa tatu unakiuka sheria na makubaliano ya amani ya mwaka wa 2006 yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka 13.
Nkurunzizakwa upande wake anashikilia kukutu kuwa ana haki ya kuwania muhula mwengine kwani muhula wa kwanza hakuchaguliwa na wanainchi bali wabunge.
Takriban watu laki moja wamekimbilia mataifa jirani wakihofia kutibuka upya kwa mapigano ya wenyewe kwa wenyewe.
Share:

Obama ajiunga na Twitter.


Rais wa Marekani Barack Obama amejiunga na mtandao wa twitter, ikulu ya White House imethibitisha.
Akitumia anuani @POTUS (President Of The United States) Obama tayari amewavutia wafuasi 1.7 milioni moja nukta saba.
"Hamjambo, Twitter!Ni Barack.
Kwa hakika baada ya miaka 6 hatimaye wameniruhusu kujiunga na mtandao wa Twitter''Obama alisema kwenye ujumbe wake wa kwanza.
Obama alikuwa na anuani tofauti inayomilikiwa na wahudumu wa ikulu yake .Anuani hiyo inawafuasi Milioni 59.3m.
Anuani hiyo @BarackObama ilizinduliwa mwaka wa 2007, na kila akituma ujumbe anaanza na BO.
" Anuani ya @POTUS itamruhusu Obama kuwasiliana moja kwa moja na mamilioni ya wafuasi wake'' ilisema taarifa ya White House .

"Rais Obama angependa serikali yake iwe ya wazi @POTUS na hii ndio jukwaa mwafaka ya mazungumzo."
Kwa sasa rais Obama amewafuata watu 65 wakiwemo rais wa zamani wa Marekani ,Bill Clinton, George Bush na mkewe mwenye anuani ya kipekee @FLOTUS.
Hata hivyo hajamfuata Hillary Clinton wala waziri mkuu wa Uingereza David Cameron.
Tayari mawasiliano yake na Bill Clinton yamezua mjadala Clinton akimtania kwa kumuuliza iwapo ataondoka na anuani hiyo atakapo achia ngazi naye akam
Share:

Kinyesi cha panya na mkojo ndani ya vipodozi..


Je wewe ni mnunuzi wa bidhaa za urembo ?
Tahadhari .
Kinyesi cha panya na mkojo wa binadamu ni baadhi ya viungo vinavyotumika kutengeza bidhaa ghushi za urembo.
Utafiti wa bidhaa za urembo zinazouzwa kwa njia ya mtandao nchini Uingereza umebaini kuwa bidhaa hizo zina tengezwa kwa njia isiyofata maadili na kulinda afya ya binadamu.
Utafitri huo uliochunguza bidhaa za urembo kama vile vipodozi marashi na mafuta ya kujipaka iligundua kuwa zinaongezwa madini ya sumu kama vile arsenic.
Kwa mujibu wa Polisi waliotekeleza uchunguzi huo, mfumuko wa bei ya bidhaa kwa njia za kielektroniki kumechangia pakubwa ongezeko la mauzo ya bidhaa gushi.
''ni vigumu sana kubaini uhalali wa bidhaa haswa unaponunua kwa njia ya kielektroniki kwa sababu unachokiona hapo mtandaoni ni picha tu ya bidhaa halali''
''sasa bidhaa hiyo inapokufikia huwa tayari umekwisha lipia na ni vigumu sana kwako kurejesha bidhaa hizo pindi unapokuwa hujaridhia ubora wake'' alisema afisa aliyesimamia uchunguzi huo.

Bidhaa za kielektroniki zinazopendelewa na wafanyibiashara walaghai ni kama zile zile zinazosokota nywele na pia zingine zinazotumika kwa ususi.
Hata hivyo bidhaa hizo haziwezi kuhimili matumizi ya muda mrefu na hivyo zinahatarisha maisha ya watumizi kutokana na hatari kulipuka.
Isitoshe Polisi wanasema kuwa uchunguzi wao umegundua kuwa marashi ghushi yanayouzwa London yanajumuisha sumu aina ya Cyanide na mkojo wa binadamu.
Vipodozi vimepatikana na sumu aina ya arsenic madini yenye sumu ya zebaki na risasi .
Vipodozi hivyo vinaweza kusababisha kujikuna,vipele visivyokwisha na maradhi mengine ya ngozi.
Bi Maria Woodall, anayeongoza kitengo cha uchunguzi wa hati miliki ya bidhaa alionya kuwa watu wengi hawafahamu madhara ya kutumia bidhaa ghushi.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.