Saturday 13 December 2014

Maelfu waandamana Washington na New York........
















Maelfu ya watu wanatarajiwa kuandamana katika bara-bara za miji ya Washington na New York kupinga mauaji ya wanaume weusi wasiokuwa na silaha yaliyofanywa na polisi wa Marekani, ili kulitaka bunge lilinde wananchi.

Taarifa iliyotolewa na kiongozi wa kutetea haki za raia, Al Sharpton, ilieleza kuwa bunge linahitaji kuchukua hatua kubadilisha sheria na hali bara-barani.
Kati ya wataohudhuria maandamano hayo ni familia za Michael Brown, kijana aliyeuwawa katika jimbo la Missouri, na Eric Garner, ambaye alikufa wakati anakamatwa mjini New York.
Kesi za askari polisi waliohusika na vifo hivyo zilifutwa na kuzusha maandamano kote Marekani.
Share:

Al-Bashir asema ameishinda ICC........















Rais Omar al-Bashir wa Sudan amedai ushindi katika mvutano wake na Mahakama ya Jinai ya Kimataifa, ICC, baada ya mkuu wa mashtaka wa ICC, Fatou Bensouda, kusimamisha uchunguzi kuhusu madai ya uhalifu wa vitani katika jimbo la Darfur.
Rais Bashir, ambaye alishtakiwa kwa mauaji ya kikabila mwaka wa 2009, alisema ICC imeshindwa katika kile alichoeleza kuwa juhudi za ICC za kuiaibisha Sudan.
Alisema wananchi wameamua kuwa afisa yoyote wa Sudan asisallim amri kwa mahakama ya kikoloni.
Fatou Bensouda alisema Ijumaa kwamba kwa vile Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa halikuchukua hatua basi wanaofanya uhalifu wa vitani Darfur wamepata nguvu kuendelea na ukatili wao hasa dhidi ya wanawake na wasichana.
Share:

Watu 3 wauawa katika vita Somalia......


Mapigano kati ya vikosi vya serikali na wanamgambo katikati ya Somali yamesababisha vifo vya watu watatu.
Pande hizo mbili zinapigania udhibiti wa jimbo la Galgadud ambalo linatarajiwa kuwa miongoni mwa majimbo ya serikali ya Somali.
Pande zote zinadai kudhibiti mji mkuu wa jimbo hilo Dusa Mareb na kuna mapigano mengine kusini magharibi kutoka kwa kundi la Ahlu Sunna,ambalo ndio kundi la kwanza lililowafukuza wapiganaji wa Alshabaab katika eneo hilo mwaka 2011 wakisaidiwa na wanajeshi wa Ethiopia.
Kundi la Ahlu Sunna limekuwa likiunga mkono Serikali ya Mogadishu lakini sasa viongozi wake wanasema kuwa wametengwa katika mpangilio mpya wa utawala.
Share:

Mahujaji milioni 17 wakusanyika Karbala...........















Mamilioni ya mahujaji wa Kishia wamemiminika katika mji wa Karbala, Iraq, kwa ibada ya kila mwaka ya Arbaeen ingawa kuna tishio la mashambulio ya wapiganaji wa madhehebu ya Sunni wa Islamic State.
Wakuu wa Iraq wanasema mahujaji zaidi ya milioni 17 wamekusanyika Karbala kuhudhuria Arbaeen.
Picha zilizopigwa kutoka angani zinaonesha barabara zinazoelekea Karbala kama mito ya watu waliovaa nguo nyeusi, hadi upeo wa macho.
Na kuna wasiwasi kuwa mji wa Karbala hautaweza kuwapatia malazi waumini wote.
Ulinzi mkubwa umewekwa kuzuwia mashambulio ya wapiganaji wa Islamic State.
Arbaeen ni siku ya mwisho ya maombolezi baada ya kifo cha Imam Hussain cha karne ya 7 katika Vita vya Karbala - tukio muhimu ambapo Wasunni waligawanyika na Washia.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.