Thursday 11 February 2016

Roboti inayoiga Mende ..BBC


Wanasayansi nchini Marekani wametengeneza roboti inayofanana na mende ambayo inaweza kutumiwa kuwaokoa watu kunapotokea tetemeko la ardhi.
Watafiti wanasema roboti hiyo inatumia mbinu zinazotumiwa na mende kutembea kwenye nyufa kupenya vifusi na kuwaokoa walionaswa katika maporomoko.
Wanasayansi hao wanasema kuwa endapo roboti hiyo inawezavishwa kamera kisha ikatumwa kwenye vifusi vya jengo lililoporomoka inaweza kurahisisha uchunguzi wa usalama wa vifusi kabla ya makundi waokoaji kuingia.
Ukubwa wa roboti hiyo ni sawa na kiganja cha mwanadamu.

Roboti hiyo inaweza kupenyeza katika mianya midogo maradufu ama nusu wa ukubwa wake.
Miguu yake inapanuka kama vile mende.
Utafiti huo umechapishwa katika jarida la kisayansi lijulikanalo kama ''Proceedings of the National Academy of Sciences''.
Share:

Ashtakiwa kwa kumrusha burukenge mgahawani....BBC


Mtu mmoja mjini Florida anakabiliwa na mashtaka ya unyanyasaji baada ya kumtupa burukenge katika mgahawa mmoja wa chakula.
Joshua James mwenye umri wa miaka 23,ametuhumiwa kwa kumtupa mnyama huyo aliye hai kupitia dirisha la mgahawa huo wa Wendy.
Mamaake amesema kuwa alikuwa akitaka kumtania rafikiye aliyekuwa akifanya kazi katika mgahawa huo.
Mnyama huyo alikamatwa na kurudishwa msituni.
Bwana James kutoka eneo la Jupiter mjini Florida alimpata burukenge huyo katika upande mmoja wa barabara na kumbeba katika lori lake,kulingana na ripoti ya tume ya kuwahifadhi wanyama mjini Florida.
Baadaye alienda katika mgahawa huo huko Royal Palm Beach,ambapo aliagiza kinywaji katika dirisha la mgahawa huo kabla ya kumrusha nyama huyo mwenye urefu wa futi tatu kupitia dirisha hilo.
Kisa hicho kilitokea mnamo mwezi Octoba lakini mshukiwa amekamatwa na anazuiliwa kwa sasa.
Pia anakabiliwa na mashtaka ya umiliki wa mnyama huyo pamoja na usafirishaji wake kinyume cha sheria.
Share:

Ndege yenye shimo: Maswali 5 bila majibu...BBC


Ndege moja ya abiria ililazimika kutua kwa dharura baada ya bomu kulipuka ilipokuwa angani muda mchache tu kutoka uwanja wa ndege wa Mogadishu.
Rubani wa ndege hiyo alilazimika kurejea ardhini baada shimo kubwa kutokea karibu na hifadhi ya mafuta katika sehemu ya kulia ya ubavu wa ndege hiyo ya Daallo Airlines.
Licha ya serikali ya Somalia kukiri kuwa bomu lililotegwa ndani ya ndege hiyo ndiyo iliyosababisha shimo hilo maswali mengi yamebakia bila majibu.

Nani aliweka bomu hiyo ndani ya ndege? 
Ripoti moja ya uchunguzi ilidai kuwa mshukiwa mkuu aliyetega bomu hiyo ndiye aliyetupwa nje kutokana na kishindo cha mlipuko huo ndege ikiwa angani.
Afisa mmoja wa serikali ya Somali alisema kuwa mshukiwa huyo Abdulahi Abdisalam Borle, raia wa Somalia alikuwa na umri wa 55 .
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Daallo, ilikuwa ikielekea Djibouti, na ilikuwa imebeba abiria 60.
Awalio duru zilisema kuwa abiria hao walikuwa wamenunua tiketi ya shirika la ndege la uturuki ila walilazimika kuabiri ndege hiyo ya daalo baada ya ile ya Uturuki kukosa kufika kwa wakati siku hiyo.
Kuna dukuduku kuwa abiria huyo alikuwa amebebwa kwenye kiti chenye magurudumu ila kauli hiyo imepingwa na mkurugenzi wa Daallo Airlines bwana Mohamed Yaseen.
Olad told BBC's Newsday that this was not recorded when he was checked in.
Wachunguzi walisema kuwa mwili wa mtu mmoja ulipatikana katika kitongoji cha Balad, takriban kilomita 30 kaskazini mwa Mogadishu.
Utafiti wa kina haujafanyika kufikia sasa kujua iwapo kweli ndiye anayeshukiwa ndiye.

Je bomu hilo lilitegwa vipi? 
Utawala nchini Somalia ulitoa Video inayoonesha watu wawiliwakimkabidhi abiria mmoja anayeshukiwa kuwa mlipuaji wa kujitolea mhanga kitu kinachoonekana kama Laptop kabla ya mlipuaji huyo kuabiri ndege hiyo ya Daallo iliyokumbwa na mkosi huo.
Msemaji wa serikali anasema kuwa watu hao ndio washukiwa wakuu katika ulipuaji uliotokea juma lililopita kwa ndege ya abiria ilipolazimika kutua kwa dharura baada ya bomu kulipuka ikiwa angani.
Inasadikika kuwa mmoja kati ya watu walioleta kipakatilishi hicho alikuwa ni mfanyikazi wa shirika linalohudumu katika uwanja huo wa ndege wa Mogadishu.
Bwana Abdisalam Aato anasema kuwa kifaa hicho kinachofanana na kipakatilishi ndicho kinachoshukiwa kuwa ni kilipuzi kilichosababisha ndege ya Daallo kurejea ardhini mara moja muda mchache baada ya kupaa ikiwa na abiria.
Takriban watu 20 wamekamatwa wakiwemo wale wawili walionaswa kwenye video hiyo .
Mtaalamu wa maswala ya usalama wa ndege bwana David Learmont, anashuku iwapo hilo linaweza kubainika kupitia kwa video hiyo moja iliyotolewa na serikali ya Somalia.
Hata hivyo anakiri kuwa wafanyikazi katika viwanja vya ndege kote duniani ndio watepetevu na ndio wanaoruhusu mashambulizi kuendelea kutokea katika ndege za abiria.
''Njia rahisi kabisa ya kuingiza na kutega bomu katika ndege za abiria ni kuwasajili wahudumu wenye vibali vya kuingia katika maeneo ya kuegesha ndege'' alisema Learmont
Rubani a ndege hiyo hata hivyo hakuficha lolote ''hakuna usalama wa aina yeyote katika uwanja wa ndege wa Mogadishu'' alisema Vlatko Vodopivec

Kwanini bomu hilo halikusababisha madhara makubwa? 
Rubani wa ndege hiyo alikiri kuwa walikuwa na bahati sana kwa sababu ndege hiyo ndio ilikuwa imepaa tu na haikuwa mbali ndio sababi=u ilitua kwa haraka na ghafla.
''kama ndege hii ingekuwa katika anga ya mbali ,,,bila shaka ndege ingeanguka'' aliiambia shirika la habari la AFP.
Mtaalamu wa usalama wa ndege David Denman anasema laiti shimo hilo lingetokea ndege hiyo ikiwa imepanda hadi zaidi ya futi elfu 20,000 juu ya usawa wa bahari hata shimo dogo kabisa lingesababisha hewa kusaki watu nje ya ndege hiyo na hivyo ndege ingepasuka mara mbili au zaidi.
''Msidharau mlipuko huo mdogo eti haukusababisha madhara makubwa ,ilikuwa bahati hawakuwa wamefyonza hewa kutoka ndani ya ndege ilikuiruhusu kupaa kwa urahisi zaidi''

Wangelikuwa wamefanya hivyo bila shaka ndege ingepasuka msamba na hakuna aliyekuwemo angepatikana akiwa hai'' alisema bwana Denman
''Bahati ilikuwa yakwamba bomu hilo lililipuka dakika 15 tu baada ya ndege hiyo kupaa na wakati huo ndege ikiwa takriban futi elfu 11,000'' alielezea mtaalamu huyo wa mabomu.
 Je kwanini bomu hilo lililipuka wakati huo ?
Ni vigumu kubaini bila ya kuwahoji waliopanga njama hiyo.
Kwanini hakuna kundi lililodai kutekeleza shambulizi hilo ?
Mwandishi wa idhaa ya kisomali ya BBC Abdirahman Koronto kuna kundi la wapiganaji waliodai kutekeleza shambulizi hilo.
Kwa kawaida kundi la wapiganaji wa al-Shabab, hutuma taarifa wakidai kutekeleza mashambulizi muda mchache tu baada ya tukio lenyewe.
Kundi hilo lilmewahi kutumia bomu iliyofichwa ndani ya Laptop yapata miaka mitatu iliyopita.
Hata hivyo katika tukio hilo la mwaka wa 2013 walichanganya bomu iliyotegwa ndani ya kipakatilishi na ile iliyotegwa ndani ya gari.
Wakati huo walifanikiwa kuua watu 6 katika shambulizi hilo.
Sio mara ya kwanza shambulizi limetekelezwa na likaenda bila kundi lolote kudai kupanga.
Kwa mfano kunashambulizi lililotekelezwa dhidi ya kundi la madaktari kutoka Syria lililosababisha 3 kati yao na mwenyeji wa kuuawa hakuna aliyedai kutekeleza shambulizi hilo.
Hata kundi la wanamgambo wa al-Shabab walipinga kutekeleza mauaji hayo.
Share:

Ndovu aingia mjini na kuhangaisha watu India...BBC

Ndovu mwitu aliingia katika mji mmoja katika jimbo la Bengal Magharibi nchini India na kuhangaisha wakazi kwa saa kadha.
Maafisa walitumia vishale vyenye dawa ya kutuliza wanyama kumtuliza.
Ndovu
Lakini tayari alikuwa ameharibu nyumba, magari na pikipiki kabla ya kudhibitiwa.
Hata hivyo, maafisa wa mji huo wa Siliguri wanasema hakuna mtu aliyeumizwa wakati wa kisa hicho.
Ndovu
Ndovu huyo baadaye alipelekwa kwenye hifadhi moja ya wanyama ambayo hutumiwa kuwafuga ndovu na wanasema wanapanga kumrejesha porini baadaye.
Watu walioshuhudia wanasema ndovu huyo aliingia mjini kutoka msitu ulio karibu na alionekana kuwa na wasiwasi na kukanganyikiwa.
Kisa hicho kimetokea siku chache tu baada ya chui kuingia shuleni na kujeruhi watu sita katika eneo la Bengaluru.

Vishale              
Ndovu              
Ndovu
Share:

Magufuli akerwa na hali wodi ya wazazi Muhimbili...BBC

Magufuli
Rais wa Tanzania John Magufuli ameahidi kuchukua hatua baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika wodi ya wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Kiongozi huyo alifika huko jana baada ya msafara wake kusimamishwa na wazazi waliomtaka kwenda akajionee jinsi wazazi wanavyokabiliwa na kero mbalimbali ikiwemo ya kulala chini kutokana na kukosa vitanda.

Alifika mwenyewe na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo.
"Nimeiona hali halisi mimi mwenyewe, watu wanapata shida, watu wana mateso, na ndio maana nimeamua kuja kwa makusudi, sikuomba ruhusa ili nijionee hali ilivyo, nimejifunza mengi, ninayabeba na nitajua namna ya kuyatatua," alisema Rais Magufuli.
Rais Magufuli alisimamishwa na kina mama hao alipokuwa akitoka katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alikokwenda kumuona na kumjulia hali Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubery Bin Ally.
Mwezi Novemba, siku chache baada ya kuchukua hatamu, Dkt Magufuli alifanya ziara ya kushtukiza katika sehemu kuu ya ya hospitali hiyo ya Muhimbili na kuhuzunishwa na hali ya huduma kwa wagonjwa hususan baadhi waliolala chini.
Alifanyia mabadiliko usimamizi wa hospitali hiyo na kumteua Prof Lawrence Mseru kuwa mkurugenzi mkuu.

Share:

Nestle yavunja mkataba na IAAF...BBC


Kampuni kubwa ya chakula pamoja na vinywaji Nestle imevunja ufadhili wake katika shirika la riadha duniani IAAF ,ikihofia kwamba kashfa ya utumizi wa dawa za kusisimua misuli inyokumba shirika hilo huenda ikaharibu sifa zake.
Kampuni hiyo kutoka Uswizi imesema kuwa imechukua uamuzi huo mara moja.
Hatahivyo ,rais wa shirikisho hilo Lord Coe amesema kuwa amekasirishwa na uamuzi huo na hataukubali.
Mwezi uliopita,kampuni ya nguo za michezo Adidas ilivunja mkataba wake na shirikisho hilo.
Tumeamua kuvunja uhusiano wetu na mpango wa riadha miongoni mwa jina katika IAAF mara moja.

Uamuzi huu unatokana sifa mbaya kutoka kwa umma kutokana na madai ya ufisadi na utumizi wa dawa za kutumia nguvu dhidi ya IAAF.
Tunaamini kwamba hili huenda likaathiri vibaya sifa na sura yetu na hivyobasi tumevunja mkataba wetu na IAAF,ulioanzishwa 2012.
Tumeelezea IAAF kuhusu uamuzi wetu na sasa tunasubiri jibu lao kwamba ushirikiano wetu umekwisha.
Share:

Utafiti:Farasi hubaini hisia za mwanadamu...BBC


Farasi huweza kubaini kati ya mtu aliye na furaha na aliye kasirika kwa kuangalia uso wa mwanadumu,utafiti umesema.
Katika jaribio, kwa kutumia picha za mwanamume wanasayansi kutoka chuo kikuu cha Sussex walionyesha kwamba farasi wanaofugwa nyumbani huchukizwa na sura zilizokasirika.
Wanasayansi hao wanasema kuwa ufugaji huo huenda umewawezesha farasi kuelewa tabia za binaadamu.
Matokeo hayo yamechapishwa katika jarida la Biology Letters.
Kundi hilo lilifanya vipimo vyake kwa kuwasilisha picha nyingi mbele ya farasi 28.
''Mtu mmoja anashikilia farasi huku mwengine akishikilia picha,''alielezea mtafiti Amy Smith.
Matokeo yake ,alielezea ni kwamba waliangalia picha za watu waliokasirika na jicho lao la kushoto.
Akili za wanyama zimeumbwa kana kwamba hisia zinazotolewa na jicho la kushoto huangaziwa na eneo la kulia la ubongo ambalo hutumiwa kuangazia hisia mbaya.
Watafiti hao pia waliweka vipimo vya moyo katika moyo wa farasi hao ,ambavyo vilibaini kwamba nyuso zilizokasirika hufanya myoyo ya wanyama hao kudunda kwa haraka.
Matokeo kama hayo yameripotiwa miongoni mwa mbwa na kuzua maswali kuhusu ni vipi kuishi na binaadamu kuna badili tabia za wanyama hao.
Share:

Al-Shabab ''lashambulia uwanja wa ndege Somalia''..BBC


Wanamgambo wa kiislamu wamefanya mashambulio ya makombora katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.
Walioshuhudia wanasema wanamgambo hao walirusha makombora hayo usiku kucha na kuwa milipuko kadhaa ilisikika karibu na uwanja mkuu wa ndege.
Hata hivyo hakuna ripoti yoyote kuhusu majeruhi, lakini ripoti zinasema kuwa safari kadhaa za ndege kuelekea Mogadishu zimefutiliwa mbali.
Uwanja wa ndege wa Mogadishu unalindwa vikali na unakaribiana na kambi ya wanajeshi wa kulinda amani wa muungano wa Afrika nchini Somalia.
Kikosi hicho cha wanajeshi elfu ishirini na mbili wa muungano huo wanaunga mkono serikali ya nchi hiyo katika harakati zake za kupambana na wanamgambo wa kiislamu.
Ofisi za umoja wa mataifa pia ziko katika kambi hiyo sawa na ubalozi wa mataifa ya kigeni.
Kufikia sasa hakuna kundi lolote ambalo limedai kuhusika na shambulio hilo, lakini wapiganaji wa Al shabaab walio na uhusiano na kundi la kigaidi la Al Qaeda, wamefanya mashambulio kadhaa ya mabomu mjini humo.
Wakati huo huo uchunguzi unaendelea kufuatia mlipuko wa bomu katika ndege moja ya abiria iliyotokea tarehe mbili mwezi huu.
Mlipuko huo ulitokea katika ndege inayomilikiwa na shirika la Daalo muda mfupi tu baada ya kuruka kutoka uwanja huo wa ndege wa Mogadishu na kusababisha kifo cha mlipuaji huyo wa kujitolea, hali iliyoilazimisha ndege hiyo kutua kwa dharura.
Watu kum na watano wamekamatwa kuhusiana na shambulizi hilo la Ndege.
Share:

Shule zafungwa Bangalore kwa sababu ya chui... BBC

chui
Shule zaidi ya 100 zimefungwa nchini India baada ya chui mwingine kuripotiwa kuonekana viungani mwa mji wa Bangalore.
Wakazi wametakiwa kutotoka nje kwa sababu ya usalama wao. Polisi na maafisa wa misitu wanamsaka mnyama huyo.
Chui dume aliingia katika shule moja Jumapili na kuwajeruhi watu sita waliojaribu kumkamata.
Mwanasayansi na mfanyakazi wa idara ya misitu ni miongoni mwa waliojeruhiwa kwenye operesheni ya kumdhibiti mnyama  huyo iliyodumu saa 10.

Chui wa sasa anadaiwa kuonekana na mfanyakazi wa ujenzi Jumatano eneo la Nallurhalli, karibu na Whitefield, mwandishi wa idhaa ya Kihindi ya BBC Imran Qureshi aliyeko Bangalore anasema.
"Tumeunga makundi ya maafisa wa misitu na polisi ambao wanazunguka eneo hilo wakimtafuta. Lakini kufikia sasa hatujaona dalili za kuwepo kwake,” afisa mkuu wa huduma za wanyamapori jimbo la Karnataka Ravi Ralph amesema.
chui
Chui huyo alijeruhi watu sita shule ya Vibgyor Jumapili
Mnamo Alhamisi, serikali ya jimbo hilo iliagiza kufungwa kwa shule 129, zikiwemo 53 za serikali.
“Tutaamua baadaye jioni iwapo shule zitaendelea kufungwa Ijumaa au la. Tunasubiri uamuzi wa maafisa wa misitu na polisi,” afisa wa serikali KS Satyamurthy amesema.
Sensa ya karibuni zaidi ilionesha kuna karibu chui 14,000 nchini India.
Share:

Rwanda lawamani juu ya Burundi.


Maafisa wa Wizara ya mambo ya nje ya Marekani wamesema wameona ushahidi kuwa serikali ya Rwanda imekua ikichangia matukio ya machafuko katika nchi jirani ya Burundi.
Inaelezwa kuwa Rwanda imekuwa ikiwapa silaha na mafunzo wakimbizi waliokimbia machafuko nchini Burundi.
Burundi imetumbukia mgogoro wa wenyewe kwa wenyewe tangu Rais Pierre Nkurunziza alipoamua kugombea uraisi kwa muhula wa tatu.
Maafisa hao wa Marekani wanasema taarifa walizo nazo kutoka kwa maafisa wenzano waliopo kwenye kambi za wakimbizi nchini Rwanda, zinasema Rwanda imekuwa ikihusika na vurugu katika nchi jirani ya Burundi.

Akihojiwa na Bunge la Congress mmoja wa wanadiplomasia amesema kuna taarifa za kuaminika kwamba wakimbizi wa Burundi ikiwa ni pamoja na watoto wamekuwa wakipewa mafunzo katika makambi nchini Rwanda, na kufunzwa kupambana kwa silaha na serikali.

Ghasia zilizuka nchini Burundi mwaka jana baada ya rais wa nchi hiyo kusema atagombea kwa muhula wa tatu.
Serikali za nchi hizi mbili zina makabila ambayo ni mahasimu, na kuna ongezeko la wasiwasi wa kimataifa kuwa mgogoro mwingine wa kikabila inaweza kuota mizizi katika eneo hilo.
Tayari Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda amekanusha tuhuma hizo ambapo amesema Umoja wa Mataifa unapaswa kutafuta mikakati ya kutatua mgogoro ya kisiasa badala ya kutafuta nani wa kumtupia lawama.
Share:

Aliyeishi muda mrefu na moyo wa kupandikizwa afariki... BBC

John McCafferty
Mwanamume aliyeishi muda mrefu duniani na moyo wa kupandikizwa amefariki, baada ya kuishi miaka 33 na moyo huo.
John McCafferty aliambiwa alikuwa amesalia na miaka mitano pekee ya kuishi alipofanyiwa upasuaji katika hospitali ya Harefield, Middlesex Uingereza mnamo tarehe 20 Oktoba 1982.
Mjane wake Ann amesema: "Miaka 30 iliyopita ilikuwa ya furaha sana. Tulitembea na kujionea ulimwengu.”
Bw McCafferty, kutoka Newport Pagnell eneo la Buckinghamshire, alifariki Jumanne akiwa na umri wa miaka 73 akitibiwa hospitali ya Milton Keynes.
Alitambuliwa na Guiness World Records mwaka 2013 kuwa mtu aliyeishi muda mrefu zaidi na moyo wa kupandikizwa.
Wakati huo alisema: “Ninataka rekodi hii ya dunia iwapo moyo wote wanaosubiri kufanyia upasuaji wa kupandikiza moyo na kwa wale, ambao kama mimi, wamebahatika kupandikizwa moyo mwingine kama mimi.”

Bw McCafferty alipatikana na maradhi ya moyo akiwa na umri wa miaka 39.
Alifanyiwa upasuaji na Sir Magdi Yacoub.
Upasuaji wa kwanza wa kupandikiza moyo uliofanikiwa ulifanyiwa nchini Afrika Kusini mwaka 1967 na Prof Christiaan Neethling Barnard na kundi la matabibu 30 katika hospitali ya Groote Schuur, Cape Town.
Mgonjwa wao, Louis Washkansky, alifariki siku 18 baada ya kupokea moyo mpya.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.