Thursday 11 February 2016

Shule zafungwa Bangalore kwa sababu ya chui... BBC

chui
Shule zaidi ya 100 zimefungwa nchini India baada ya chui mwingine kuripotiwa kuonekana viungani mwa mji wa Bangalore.
Wakazi wametakiwa kutotoka nje kwa sababu ya usalama wao. Polisi na maafisa wa misitu wanamsaka mnyama huyo.
Chui dume aliingia katika shule moja Jumapili na kuwajeruhi watu sita waliojaribu kumkamata.
Mwanasayansi na mfanyakazi wa idara ya misitu ni miongoni mwa waliojeruhiwa kwenye operesheni ya kumdhibiti mnyama  huyo iliyodumu saa 10.

Chui wa sasa anadaiwa kuonekana na mfanyakazi wa ujenzi Jumatano eneo la Nallurhalli, karibu na Whitefield, mwandishi wa idhaa ya Kihindi ya BBC Imran Qureshi aliyeko Bangalore anasema.
"Tumeunga makundi ya maafisa wa misitu na polisi ambao wanazunguka eneo hilo wakimtafuta. Lakini kufikia sasa hatujaona dalili za kuwepo kwake,” afisa mkuu wa huduma za wanyamapori jimbo la Karnataka Ravi Ralph amesema.
chui
Chui huyo alijeruhi watu sita shule ya Vibgyor Jumapili
Mnamo Alhamisi, serikali ya jimbo hilo iliagiza kufungwa kwa shule 129, zikiwemo 53 za serikali.
“Tutaamua baadaye jioni iwapo shule zitaendelea kufungwa Ijumaa au la. Tunasubiri uamuzi wa maafisa wa misitu na polisi,” afisa wa serikali KS Satyamurthy amesema.
Sensa ya karibuni zaidi ilionesha kuna karibu chui 14,000 nchini India.
Share:

0 comments:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.