Monday 20 July 2015

Buhari akutana na Obama


Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari anafanya mazungumzo mjini Washington na rais wa Marekani Barack Obama.
Mazungumzo baina ya viongozi hao wawili yanalenga ushirikiano katika vita dhidi ya wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
null
Awali Marekani ilikubali kuisaidia Nigeria katika vita dhidi ya makundi ya uasi hasa baada ya kutekwa nyara kwa wasichana zaidi ya 200 wa shule kutoka Chibok mwaka jana.
null
Hata hivyo uhusiano baina ya Marekani na utawala ulioondoka madarakani wa Goodluck Jonathan ulidhoofika , baada ya shutuma za makundi ya kutetea haki za kibinadamu kuhusu ukiukaji wa haki za kibinadamu unaotekelezwa na jeshi la Nigeria.
Bwana Buhari pia ameahidi kushughulikia ufisadi na amesema atarejesha mabilioni ya dola yaliyofichwa kwenye benki za Marekani Uswiss na kwingineko.
Share:

Ziara ya mfalme wa Saudia Ufaransa yazua Ubishi


Ubishi umeibuka nchini Ufaransa, baada ya ufukwe maarufu wa bahari wa Riviera kufungwa ilikumruhusu mfalme wa Saudi Arabia na familia yake kujivinjari kwa amani faraghani.
Viongozi wa mji wa Vallauriswametangaza kuwa watafunga sehemu kubwa ya ufukwe huo ilikuhakikisha usalama wa mfalme huyo familia yake na takriban ujumbe wa watu 400.
Familia hiyo ya kifalme, inatarajiwa kuishi katika jumba la kifahari lililoko huko.
Jumba hilo lililowahi wakati mmoja kuwa jumba la mapumziko la Sir Winston Churchill linatarajiwa kuzingirwa na maafisa wa usalama.
Maafisa wa Vallauris iliyoko kwenye mwambao wa Cote d'Azur, kilomita 10 kutoka kwenye ufukwe huo wanasema wamethibitisha kuwa shughuli kwenye ufukwe wa Milandore zitafungwa kwa muda wote wa majira ya kiangazi.
null
Hatua hiyo imewagadhabisha wakazi wa maeneo hayo ya mwambao , ambao wametishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mpango wa kuziba barabara ya ardhini kuelekea kwenye ufukwe huo.
Familia hiyo ya kifalme ya Saudi Arabia , ikiongozwa na Mfalme Salman, inamiliki jumba la kifahari ambalo Rita Hayworth alitumia kama mahala pa mapokezi ya wageni wakati wa harusi yake .
Sir Winston Churchill na Elizabeth Taylor walikua miongoni mwa wale waliolitumia kama makazi ya mapumziko.
null
Wakazi wa eneo hilo wamekasirishwa na shughuli za ukarabati katika eneo hilo, hasa baada ya kuwekwa kwa sakafu kubwa ya saruji kwenye mchanga ulioko ufukweni, zimeleza ripoti za wakazi wa eneo hilo.
Blandine Ackermann, rais wa shirika la wanaharakati wanaolinda mazingira katika maeneo ya Golfe-Juan na Vallauris amesema anapanga kuchukua hatua za kisheria kama ufukwe huo hautaendelea kuwa wazi na kurejeshwa katika hali yake
Maafisa wa kulinda bahari wamesema tayari kuwa chombo chochote hakitaruhusiwa kukaribia eneo hilo kwa takriban mita 300 ndani ya bahari.
Share:

Burundi:AU huenda isishiriki uchaguzi.


Yaelekea Muungano wa Afrika hautaweza kupeleka wanajeshi na waangalizi wa haki za kibinadamu nchini Burundi kabla ya uchaguzi wa urais unaotarajiwa kufanyika kesho Jumanne.
Katika taarifa kwa waandishi wa habari, Muungano huo wa Afrika wanasema kupelekwa kwa maafisa hao kumesababishwa na masharti mapya ya Burundi kwamba waangalizi sharti wawe na vibali vya kuingia Burundi mbali na vyeti vyao vya kusafiria vya kibalozi.
null
Mazungumzo baina ya serikali na upinzani yalivunjika mwishoni mwa juma baada ya pande hizo mbili mbili kushindwa kufikia makubaliano.
Upinzani unadai kuwa rais Nkurunziza anakiuka katiba ya taifa na mapatano ya Arusha yaliyokomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe.
null
Burundi imezama katika mgogoro wa kisiasa uliokumbwa na ghasia tangu rais wa nchi hiyo kutangaza kugombea nia ya kuwania muhula wa tatu .
Zaidi ya raia laki moja wa Burundi wamekimbia nchi hiyo tangu mwezi Aprili kulipozuka ghasia kupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Share:

Hatimaye mabenki yafunguliwa Ugiriki.


Mabenki Nchini Ugiriki yanafunguliwa leo kwa mara ya kwanza katika mkipndi cha majuma matatu.
Kuna milolongo mirefu kwa sasa nje ya mabenki hayo, pale bunge la taifa hilo lilipopitishia masharti magumu juma lililopita kama sehemu ya kutatua matatizo yake ya kifedha.
null
Baadhi ya masharti yangali pale pale, ikiwemo viwango vya fedha ya mtaji kutoka mataifa ya ulaya.
Badala ya kutoa fedha kila siku kulingana na kiwango kilichowekwa sasa raia wanaweza kutoa kiwango cha Euro 420 mara moja kwa juma.
null
Ushuru wa mauzo umeongezwa hasa kwa bidhaa na huduma ukiwemo nauli ya usafiri na bei ya chakula mikahawani.
Jana Jumapili, Rais wa Ufaransa Francois Hollande, alisema kuwa shida nchini Ugiriki inafaa kutoa fursa kwa mataifa ya bara Ulaya kubuni serikali moja ya muungano.
Share:

Buhari akutana na Obama.


Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari anafanya mazungumzo mjini Washington na rais wa Marekani Barack Obama.
Mazungumzo baina ya viongozi hao wawili yanalenga ushirikiano katika vita dhidi ya wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
null
Awali Marekani ilikubali kuisaidia Nigeria katika vita dhidi ya makundi ya uasi hasa baada ya kutekwa nyara kwa wasichana zaidi ya 200 wa shule kutoka Chibok mwaka jana.
null
Hata hivyo uhusiano baina ya Marekani na utawala ulioondoka madarakani wa Goodluck Jonathan ulidhoofika , baada ya shutuma za makundi ya kutetea haki za kibinadamu kuhusu ukiukaji wa haki za kibinadamu unaotekelezwa na jeshi la Nigeria.
Bwana Buhari pia ameahidi kushughulikia ufisadi na amesema atarejesha mabilioni ya dola yaliyofichwa kwenye benki za Marekani Uswiss na kwingineko.
Share:

Rais wa zamani Chad,ashtakiwa Senegal.


Rais wa zamani wa Chad Hissene Habre atafikishwa mahakamani nchini Senegal kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu, ukatili dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita .
Kesi hiyo mjini Dakar ni ya kwanza ya aina yake ambapo nchi moja ya Afrika imemshitaki kiongozi wa zamani wa taifa jingine.
Bwana Habre anashutumiwa kwa kuhusika na vitedo vya ukatili na mauaji ya maelfu ya watu wakati wa enzi ya utawala wake kuanzia 1982 hadi 1990, shutuma anazozikanusha..
Kesi hiyo inafuatia miaka 25 ya kampeni za kumfikisha mbele ya sheria.
null
Wengi miongoni mwa watu wanaodaiwa kuwa waathirika wa uhalifu uliotekelezwa na Bwana Habre' wamekua wakitoa wito wa kufunguliwa mashtaka dhidi yake tangu alipopinduliwa mamlakani na kukimbilia uhamisho nchini Senegal 1990.
Mnamo mwaka 2005 mahakama ya Ubelgiji iliytoa kibali cha kumkamata, ikidai kuwa na haki ya kimataifa ya kufanya hivyo , lakini baada ya mazungumzo na Umoja wa Afrika , AU iliiomba Senegal kuendesha kesi dhidi Bwana Habre " kwa niaba ya Afrika ".
Share:

Wednesday 15 July 2015

NASA wapata taarifa za Sayari ya Pluto


Wana sayansi wa NASA kutoka Marekani wanasema kuwa majaribio yao ya kurusha chombo kwenda katika sayari ya Pluto yamekuwa na mafanikio makubwa.
Chombo hicho kimefanikiwa kutuma taarifa katika kituo cha utafiti huo cha Maryland zilizochukua takribani saa nne na nusu hadi kufika duniani na kupokelewa na antenna NASA.
Saa chache zijazo wanasayansi hawa wa NASA wameeleza kuwa wanatarajia kupata mfululizo wa taariza zaidi na picha kutoka sayari hiyo ya Pluto ambazo zitatoa uhalisia wa undani wa sayari hiyo ya Pluto.
Share:

Mahujaji 27 waaga dunia India


Zaidi ya mahujaji 27 wameuawa kufuatia mkurupuko uliotokea katika warsha moja ya kidini katika jimbo la Andhra Pradesh nchini India.
Mkanyagano huo ulitokea wakati wa kuanza kwa sherehe za Maha Pushkaralu ambapo maelfu ya watu waliokuwa wamekusanyika kuoga kwenye maji ya mto Godavari walianza kusukumana.
Mkurupuko huo ulitokea mwendo wa saa nane u nusu katika mji wa Rajahmundry
Polisi wanasema kuwa umati ulikimbia kwenda kwa lango la kuinga mtoni.
Mikurupuko kama hii hutokea kwa wingi wakati wa warsha za kidini nchini India ambapo watu wengi hung'ang'ania nafasi katika maeneo madogo.
null
Waandalizi wanasema kuwa takriban watu milioni 24 wanatarajia kushiriki katika hafla hiyo inayotarajiwa kudumu kwa siku 12.
Mahujaji hao wa dini hiyo wanaamini kuwa kuoga na maji ya mto huo huosha mtu madhambi yake.
Waziri mkuu wa jimbo hilo Andhra Pradesh bwana Chandrababu Naidu, alisema kuwa inahuzunisha mno kuwa mahujaji waliokuwa wakitarajia kuosha madhambi yao wanaangamia.
Mwaka wa 2013 watu 115 walipoteza maisha yao katika mkurupuko uliotokea katika hafla ya kidini ya wahindu katika jimbo la Madhya Pradesh
Share:

ATM ya Maji yazinduliwa Kenya.


Wakazi wa kitongoji duni cha Mathare katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, sasa wanaweza kupata maji safi ya kunywa na kwa matumizi mengine.
Mpango unaoungwa mkono na serikali umezinduliwa kwenye mji mkuu wa Kenya Nairobi unaowawezesha watu wanaoishi kwenye mitaa ya mabanda kununua maji kwa kutumia kadi.
Vituo vya kuuza maji vimebuniwa kote katika sehemu za mabanda ambapo wenyeji hutumia kadi zilizo na pesa kununua maji safi na kwa bei nafuu.
null
Wenyeji wa mitaa ya mabanda nchini Kenya wamekuwa na tatizo la kupata maji safi ambapo hulazimika kununua maji kwa bei ghali kutoka kwa wauzaji au kutoka kwa magenge ambayo hudhibiti na kuuza maji hayo kwa kuyachuuza.
Mradi kama huo umefaulu katika baadhi ya maeneo ya vijijini nchini Kenya, lakini hii ni mara ya kwanza kuzinduliwa katika mji huo mkuu.
null
Vituo hivyo vya kutoa huduma hiyo ya maji vimefanikiwa kutokana na ushirikiano kati ya serikali ya mitaa nchini Kenya na kampuni ya maji ya Grundfos ya Denmark.
Kampuni ya kusimamia huduma ya usambazaji maji, ina mikakati ya kuhakikisha kuwa huduma hii walioianzisha itasambazwa kote katika mji mkuu wa Nairobi na kwengineko nchini humo.
null
Huku hilo likianzishwa wakaazi wa mitaa kadhaa mjini Nairobi bado wanalalamikia ukosefu wa maji.
Share:

Sketi fupi zawaponza wanawake Morocco.


Wanawake wawili raia wa Morocco waliofikishwa mahakama baada ya kushtakiwa kwa utovu wa nidhamu, kwa kosa la kuvaa sketi fupi,hatimaye wameachiliwa huru.
Wanawake hao wawili walikamatwa mapema mwezi uliopita katika maeneo ya soko la Inezgane karibu na Agadir,baada ya kuzuiliwa na wafanya biashara wa soko hilo.

Kesi ya wanawake hao ilikuwa na mvuto wa kipekee katika nchi nzima ya Morocco na hata katika mitandao ya kijamii nchini humo ,na pia kulikuwa na harakati za kutaka kusainiwe hati ya kutaka kutenguliwa kukamtwa na kushambuliwa kwa wanawake hao na kuita jaribio hilo kama kuingilia uhuru binafsi ;ikawavutia maelfu ya watu waliotia saini hati hiyo.

Na kufuatia mvuto wa kesi hiyo na hali ya kuitishwa kwa hati hiyo kuliwavutia wanasheria kadhaa nchini humo,ambao walikuwa tayari kuwatetea wanawake hao kwa gharama zao.
mwanaharakati wa haki za wanawake na mwendesha kampeni dhidi ya jinsi hiyo, Fouzia Assouli ameliambia shirika la habari nchini Ufaransa AFP kwamba kuachiliwa kwa wanawake hao kumeonesha kuwa uvaaji wa sketi fupi nchini Morocco siyo kosa la jinai "

Nayo tovuti ya habari nchini humo ya Tel Quel,imemnukuu wakili wa wanawake hao , Houcine Bekkar Sbai,akisema kwamba baada ya kuachiliwa kwa wanawake hao,kinachofuata ni kuwafikisha mahakamani watu waliowafedhehesha wanawake hao sokoni.
Share:

Mtoto aliyekosha ulimwengu apewa msaada


Mtoto wa miaka 9 aliyepigwa picha nje ya mkahawa wa Mac Donalds huko Ufilipino anaendelea kupokea msaada utakaomsaidia atimize ndoto yake ya kupata elimu.
Daniel Cabrera alipigwa picha akiwa nje ya duka maarufu la Mac Donalds amejikunyata kwenye kibao anachokitumia kama meza ya kuwekea vitabu vyake akifanya mabaki ya kazi aliyopewa shuleni.
Cabrera alikuwa akitumia mwangaza wa bango la kutangaza duka la McDonald kama taa yake akidurusu !
null
null
Mtoto aliyekosha ulimwengu kwa ari yake
Mwanafunzi wa Uuguzi bi Joyce Torrefranca, ndiye aliyeipiga picha hiyo nje ya mkahawa huo McDonald ulioko katika mji wa Cebu nchini Ufilipino na akaichapisha kwenye mtandao wake wa kijamii wa Facebook na ujumbe
''mtoto huyo amenikumbusha niwekee bidii maishani''
''kwangu mimi kama mwanafunzi ,nilipigwa na mshangao kutokana na ari ya mwanafunzi huyu mdogo aliyekuwa amechutama akikamilisha kazi yake ya shuleni bi Torrefranca aliiambia runinga ya ABS-CBN katika mahojiano.
''kwa hakika ilinipatia changamoto kubwa niendeleee kufanya bidii katika kila jambo linalonikabili''
Muda mchache baada ya bi Torrefranca kuchapisha picha hiyo kwenye Facebook maelfu ya watu waliichapisha pia wakisema kuwa ilikuwa imewavutia sana.
Sasa wahisani wamejitokeza kwa wingi kufadhili elimu yake.
Mamake kijana huyo Christina Espinosa anasema kuwa Cabrera anapenda shule na masomo yake licha ya shida chungu nzima wanazokabiliana nazo hususan umaskini.
''ameniambia mara nyingi tu kuwa mama mimi sitaki kuwa maskani'' alisema Espinosa
null
Bi Joyce Torrefranca akihojiwa katika moja ya runinga ya taifa
Aidha Cabrera ambaye nyumba yao haina stima amepewa taa zenye mwangaza wa kutosha na wahisani mbali na dawati la kisawasawa ilikumwezesha kusoma bila bugdha.
Na kwa sababu angependa kuwa afisa wa polisi, maafisa wa polisi katika mji huo wa Cebu walimpeleka katika moja ya maduka maarufu ya wanasesere na kumnunulia moja mfano wa gari la polisi.
Hata hivyo misaada imekuwa mingi kupita matarajio yake na mamake bi Espinosa na sasa kanisa lililoko karibu na kwao limekubali kupokea bidhaa zaidi kwa niaba yao.
Vilevile afisa anayeshughulia maswala ya watoto ameingilia kati na kusema kuwa sasa wameanza kuweka mikakati ya kuhakikisha ufadhili wowote unaomkusudia kijana huyo unamnufaisha.
Share:

Wairan wafurahia makubaliano ya nyuklia.


Maelfu ya raia wa Iran wamekuwa wakishangilia mitaani kufutia makubaliano mapya ya mpango wa nyuklia kati ya Iran na mataifa makubwa yenye nguvu dunian ambapo sasa Iran itapunguziwa vikwazo vya kiuchumi.
Hata hivyo katika makubaliano hayo Iran imepewa masharti katika harakati zake za kutengeza nuklia.
Huenda hatua ya kupunguziwa vikwazo vya kiuchumi vikawa vimechangia furaha ya wa Iran wengi katika makubaliano hayo ambapo Kiongozi mkuu wa Kidini Ayatollah Ali Khamenei alipongeza juhudi za wapatanishi kutoka Iran.
Hata hivyo kumekuwa na hisia tofauti kwa mataifa ya kiarabu na yale ya mashariki ya kati kufuatia makubaliano hayo ya nyuklia ya Irani.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamini Netanyahu amepinga kwa nguvu zote mapendekezo ya makubaliano hayo yaliyofikiwa. Ambapo katika makubaliano hayo Iran itaondolewa vikwazo vya kiuchumi vya kimataifa, kwa Iran kuacha kutengeneza silaha za nyuklia.
"Bila kugawanya mpango huu wa nyuklia wa Iran, katika miongo, mpango huu hautabadili chochote, hautawafanya Iran wajutie makosa yao, na unajenga utawala wa kigaidi kwa kuwa na uwezo wa kutengeneza mabomu ya nyuklia, ki ukweli silaha zote za nyuklia na namna ya kuziendeleza. Kosa hili kubwa ni la kushtua na kushangaza. Israel haitahusika na makubaliano hayo na Iran, kwa sababu Iran imekuwa ikifanya mipango ya kutuharibu. Tutaendelea kujihami wenyewe." Amesema Netanyahu.
Kwa upande wake waziri wa mambo ya nje wa Iran ameiambia BBC makubaliano hayo ya nyuklia ni hatua mojawapo ya kuimarisha uhusiano kati ya Iran na mataifa ya magharibi. Amesema ushirikiano mkubwa unahitajia kupambana na vitisho vya Islamic State.
Share:

Kampuni za mbao zadaiwa kufadhili vita CAR


Kundi la kutetea haki la Global Witness limayalaumu baadhi ya makumpuni ya mbao barani Ulaya kwa kusaidia kufadhili vita nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, kupitia kusaidia kusaini mikataba ya fedha nyingi na makundi ya wapiganaji.
Kundi hilo la Global Witness pia linasema kuwa muungano wa Ulaya umeshindwa kuzuia mbao haramu ambazo zinauzwa barani Ulaya.
Maelfu ya watu wameuawa miaka ya hivi majuzi nchini Jamhuri ya Afrika ya kati kwenye mzozo ambao ulisababisha kuwepo kwa mauaji ya waislamu ambao ni wachache nchini humo.
Share:

IMF laishtumu EU kuhusu Ugiriki


Shirika la fedha duniani IMF limelaumu vikali masharti ya msaada wa kifedha ambao linasema mataifa yanayotumia sarafu ya euro yaliipa Ugiriki.
Afisa mmoja wa IMF amesema kuwa mabadiliko hayo ya Ugikiri ni vigumu kutekeleza na malengo katika ukuaji wake yatakuwa magumu kutimizwa.
IMF inasema kuwa Ugiriki inaweza kustahimili deni lake kwa kuchukuliwa hatua ambazo Ulaya haijakuwa na nia kuzitekeleza.
null
Waziri mkuu wa ugiriki Alexis Tsipras amekuwa akijaribu kuwashawishi wabunge kuyaunga mkono mabadiliki yaliyotolewa na mkutano wa Brussels huku yeye mwenyewe akisema kuwa hana imani nayo.
Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha televisheni bwana Tsipras alisema kuwa Ugiriki ingetimiliwa kutoka kwa muungano wa Ulaya ikiwa haingekubali makubaliano hayo.
Share:

Desmond Tutu alazwa hospitalini


Askofu mstaafu Desmond Tutu amelazwa katika hospitali moja mjini Cape Town Afrika Kusini.
Familia yake inasema kuwa amekuwa akiugua maambukizi yasioisha na kwamba huenda akatoka hospitalini hivi karibuni.
Bwana Tutu alijiuzulu katika maisha ya umma miaka minne iliopita lakini anaendelea kusafiri maeneo mengi.
Amelazwa hosptalini mara kadhaa katika miaka ya hivi karibuni na kutibiwa saratani ya tezi dume kwa mara kadhaa.
Mapema mwezi huu yeye na mkewe waliimarisha ndoa yao baada ya kula kiapo kwa mara ya pili miaka sitini baada ya kuoana.
Share:

Historia ya John Magufuli wa CCM.


Chama tawala nchini Tanzania Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemtangaza daktari John Magufuli kuwa mgombea wake wa kiti cha Urais katika uchaguzi mkuu wa ujao.
Daktari John Magufuli, alisajili asilimia 87 % ya kura za wajumbe, hiyo ikiwa ni kura 2104.
Daktari John Magufuli, aliwashinda wapinzani wake Bi Amina Salulm Ali na dakta Asha-Rose Migir.
Magufuli ni Nani?
Lakini je Daktari John Magufuli ni Nani?
null
Mgombea wa urais wa chama cha CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2015 Daktari John Pombe Joseph Magufuli ni mbunge wa jimbo la Chato lililoko mkoa wa Geita na ni waziri wa ujenzi wa Tanzania.
Alizaliwa tarehe 29 Oktoba 1959 wilayani Chato Mkoani Kagera.
Kielimu, daktari Magufuli ana Stashahada ya elimu ya sayansi akibobea kwenye masomo ya Kemia, Hisabati.
Mgombea huyo wa urais ana shahada ya umahiri wa Sayansi na shahada ya uzamivu ya kemia.
Aidha daktari Magufuli amewahi kufundisha katika shule ya sekondari Sengerema miaka ya themanini kisha akajiunga na mafunzo ya JKT .
Alizaliwa Oktoba 1959
null
Alipohitimu, daktari Magufuli na aliaanza kufanya kazi katika kiwanda cha ‘Nyanza Cooperative Union akiwa Mkemia kabla ya kuondoka hapo na kuwania ubunge.
Magufuli alianza mbio za ubunge mwaka 1995 katika jimbo la Chato na kushinda kisha akateuliwa na Rais Benjamin Mkapa kuwa naibu waziri wa Miundombinu.
Katika uchaguzi wa Mwaka wa 2000 pia aligombea ubunge na kushinda na Rais Mkapa akamteua kuwa Waziri wa miundombinu.
Alianza siasa mwaka 1995
Katika uchaguzi wa mwaka 2005 daktari Magufuli aligombea ubunge kwa mara ya tatu na kupita bila kupingwa.
Rais Kikwete alimteua kuongoza wizara ya Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi na baadaye akamhamishia hadi wizara ya Mifugo na uvuvi.
null
Mwaka 2010 alichaguliwa kuwa mbunge kwa mara ya nne na Rais Kikwete alimrudisha katika Wizara ya Miundombinu na ujenzi.
Daktari Magufuli anachukuliwa kuwa ni mwanasiasa mwenye msimamo thabiti, mchapa kazi na asiye yumbishwa au hata kufuata upepo wa kisaisa.
Anatambulika kuwa Mchapa kazi
Watanzaniania wanamkumbuka kwa usimamizi na ujenzi wa barabara na majengo thabiti.
Anakumbukwa kwa kuchukua hatua za kutoa amri za kubomolewa kwa majengo ya kifahari ambayo alihisi yalikiuka sheria za ujenzi.
null
Na alipokuwa waziri wa Maendeleo ya Mifugo, Bwana John Magufuli alikwenda hadi bandari ya Dar-es-Salaam na kuizuia meli ya wachina iliyokuwa inashukiwa kufanya uvuvi haramu katika sehemu ya bahari ya Tanzania.

Share:

Rais Mseveni na usuluhishi wa Burundi


Rais wa Uganda Yoweri Museveni leo ameingia siku yake ya pili ya mazungumzo ya amani nchini Burundi.
Ikiwa imebaki siku chache tu kufanyika kwa uchaguzi wa Rais, inaonekana kuna nafasi ndogo ya Rais Museveni kuweza kushawishi lolote kuhusiana na msimamo wa Serikali ya Burundi kuhusiana na uchaguzi wa Burundi.
Mara baada ya kuwasili nchini Burundi kwa njia ya barabara akitokea Uganda, Rais Museven amewaambia wanasiasa wa Burundi, makundi ya kijamii na kidini kwamba Burundi kama ilivyo mataifa mengine ina matatizo ambayo yanatafsiriwa kama matokeo ya fikra tofauti ndani ya vichwa vya watu
Museveni amewakumbusha raia wa Burundi moja ya jambo baya lililowahi kutokea nchini humo na ambalo halipaswi kuwepo kwa sasa ambalo ni mgawanyiko wa kikabila kati ya Wahutu na Watusi, na jambo la pili ni kudhani kuwa madarakani ndilo jambo la mhimu kuliko mambo mengine yote yanayoweza kuleta ustawi wa taifa zima
Katibu wa jumuiya ya Afrika Mashariki Richard Sezibera amesema kuwa uchaguzi mkuu wa Burundi,haupaswi kusababisha raia kuikimbia nchi yao na kwenda kutafuta hifadhi nchi jirani
Jana Usiku Rais Mseveni amekuwa na majadiliano ya pamoja na viongozi wa kambi ya upinzani wa Burundi,mashirika ya kiraia na uwakilishi wa viongozi wa Kidini.
Rais Museveni leo atakutana na kundi jingine la wawakilishi wa serikali na viongozi wengine wastaafu katika mazungumzo
Share:

Friday 3 July 2015

WHO:Cuba haina Kaswende, ukimwi kwa watoto.


Shirika la afya duniani WHO, limethibitisha kuwa Cuba imemaliza kabisa maambukizi ya ukimwi kutoka kwa mama mzazi na Kaswende.
Mkuu wa shirika hilo WHO, Daktari Margaret Chan, ametaja ufanisi huo kuwa ''ni mkubwa zaidi kuwahi kutokea kwa afya ya umma.''
Mafanikio hayo ya kutajika yanafuatia kampeini ya muda mrefu miongoni mwa wanawake waja wazito ambao wamekuwa wakishauriwa kuanza kupokea matibabu mapema na kufanyiwa vipimo mahsusi ilikujua hali ya afya ya mama na mwanaye .
WHO inatumai kuwa mafanikio hayo ya Cuba yataigwa na mataifa mengine.
Kwa mujibu wa takwimu za WHO, Kila mwaka takriban wanawake milioni moja nukta nne (1.4) i walioambukizwa virusi vya ukimwi duniani, hupata uja uzito.
Iwapo hawapokei matibabu mapema asilimia 15-45% ya wanawake hao huwaambukiza watoto wanaojifungua wakati wa kujifungua na pia kupitia kwa maziwa ya mama.
Hatari ya maambukizi hupungua kwa kiasi kikubwa na kufikia asilimia moja pekee 1% baada ya kupokea madawa ya kupunguza makali ya ugonjwa wa Ukimwi.
Aidha wanawake wengine milioni moja huambukizwa kaswende wakiwa wajawazito kila mwaka.
Iwapo wanawake hao watapokea matibabu mapema wanaweza kuzuia kuwaambukiza watoto wao.
null
Kote duniani wanawake waja wazito 7 kati ya 10 ambao wameambukizwa ukimwi hupokea,madawa ya kupunguza makali ya ukimwi
Nchini Cuba, chini ya asilimia 2% ya watoto huzaliwa na maambukizi ya maradhi hayo.
Hii ikiwa ni kiwango cha chini mno kinachoweza kufikiwa kufuatia matibabu.
Kote duniani wanawake 7 kati ya 10 ambao wameambukizwa ukimwi hupokea,madawa ya kupunguza makali ya ukimwi ilikuzuia maambukizi kwa watoto watakaojifungua.
Dr Carissa Etienne, ambaye amekuwa akishirikiana na WHO amesema kuwa mafanikio ya Cuba yanapaswa kuigwa kote duniani ilikupunguza au hata kumaliza kabisa maambukizi ya Ukimwi na kaswende kutoka kwa mama mja mzito kwa mwanawe.
Share:

Lazima ruhusa ya kushika mimba Uchina

Mwakamke mja mzito China
Kampuni moja ya Uchina inapanga kutoa masharti ambapo wafanyikazi wake watatakiwa kupata ruhusa kabla ya kuanza familia.
Sheria hizo zimechapishwa na kuzua malalamiko mengi katika mitandao.
Sheria kuu inaelezea kwamba wanawake wote walio kwenye ndoa lazima wawe wamehudumu kwa mwaka mmoja kwenye kampuni hiyo kabla ya kutuma kibali cha kukubaliwa kushika mimba.
null
Yeyote atakayeshika mimba kinyume cha sheria hiyo atatozwa faini na kunyimwa madaraka yoyote, hata kama amefuzu.
Shirika la utangazaji nchini China limekosoa vikali kampuni hiyo iliyoko mkoa wa Henan na kusema haina ubinadamu kwa wafanyikazi wake.
Muingilio wa masuala binafsi China ni jambo rasmi, hasa sheria ya mtoto mmoja iliyowekwa na serikali miaka ya sabini. Hii iliwalazimisha wazazi kupata mtoto mmoja pakee.
Share:

Roboti yamuua mfanyikazi wa Volkswagen.


Mfanyikazi mmoja katika kiwanda cha kutengeza magari aina ya Volkswagen nchini Ujerumani amefariki baada ya roboti kum'beba na kumuangusha katika chuma
Marehemu mwenye umri wa miaka 22 alifariki hospitalini kufuatia ajali hiyo iliofanyika katika kiwanda kimoja kilichopo Baunatal yapata kilomita 100 kazkazini mwa Mji wa Frankfurt.
null
Alikuwa akifanya kazi miongoni mwa wafanyikazi wa kandarasi wa kuiweka roboti hiyo wakati ilipomkamata kulingana na na kampuni hiyo ya Kutengeza gari ya ujerumani.
Hatahivyo Heiko Helwig amelaumu makosa ya binadaamu kama sababu ya tukio hilo badala ya roboti hiyo.
null
Roboti hiyo hutumiwa kubeba vipuri katika kampuni hiyo.
Share:

Puff Daddy aepuka jela.


Msanii wa muziki aina ya rap Sean P Diddy Combs amesema kuwa hatakabiliwa na mashtaka ya shambulio kufuatia kisa kimoja mwezi uliopita kilichohusisha uzani wa 'kettlebell'.
P Diddy aliye na umri wa miaka 45 alikamatwa mnamo Juni 22 kwa tuhuma za kushambulia kwa kutumia silaha hatari katika chuo kikuu cha California.
Alizuiliwa katika jela kabla ya kuachiliwa kwa dhamana ya dola 160,000.
Hakimu wa wilaya hiyo ameipeleka kesi hiyo katika mji wa Los Angeles kuamua iwapo Combs atakabiliwa na mashtaka hafifu.
''Tunafurahia kwamba hakimu alikataa mashtaka ya kutumia nguvu kupitia kiasi dhidi ya Combs'',alisema wakili wake.
null
P Diddy na mwanawe Justin Combs
Vyombo vya habari vilisema kuwa P Diddy alihusika katika mgogoro kati yake na kocha wa timu ya soka ya Marekani chuoni humo.
Hatahivyo Combs amesema kuwa alikuwa akimtetea mwanawe Justin Combs ambaye ni mchezaji wa timu ya chuo hicho na kwamba alikuwa akifanya mazoezi wakati wa tukio hilo.
Share:

Bidhaa zauzwa bila nembo ya ubora TZ.


Soko la Tanzania limekuwa likipokea bidhaa kutoka ndani na nje ya nchi lakini baadhi ya bidhaa zinaarifiwa kuuzwa madukani huku zikikosa nembo za ubora.
Baadhi ya bidhaa hizo pia zimeonekana kuuzwa katika maonyesho ya kimataifa ya biashara yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Katika maonyesho kama hayo ya biashara ya saba saba nchini Tanzania huwa ni fursa ya wafanyibiashara na wajasiriamali kuonyesha bidhaa zao mbali mbali lakini kwa wengine huwa wanatumia fursa hiyo kusambaza na kuuza bidhaa duni kwa bei ya kutupa.
katika maonyesho hayo bidhaa hizo na nyingine zinaendelea kuuzwa huku kukiwa na sheria na utaratibu kamili .
Bi Roida Andusamile ni msemaji wa shirika la viwango Tanzania na anasema hali halisi ni kwamba kuna baadhi ya wajasiriamali ambao wanaonyesha biashara zao wakati bidhaa zao hazijathibitishwa na shirika la viwango kuwa zina ubora.
Hata hivyo viongozi wa maonyesho hayo wanasisitiza kuwa wameweka uthibiti wa kutosha ili kukinzana na tatizo hili la bidhaa feki katika maonyesho hayo ya biashara.
null
Ingawa baadhi ya wafanya bishara wanakiri kukosa kiambishi cha kuonyesha ubora wa bidhaa zao zinawanyima soko , sio nyumbani tu lakini hata kimataifa kwa kuwa uwezo wao bado ni mdogo ingawa bidhaa zao zina ubora.
Wakati maonyesho hayo yakiendelea, maafisa wa serikali wanachukua fursa ya kuwepo kwenye maonyesho na kutoa mafunzo kuhusu ubora wa bidhaa .
Mamlaka ya chakula na dawa inasema iko makini katika hilo kwani maafisa wao bado hutembelea mabanda ili kubaini bidhaa feki zilizoingia.
Afisa wa uelimishaji jamii;James Ndege anasema sio vyema kuwalaumu wafanyabiashara pekee yao kutokana na tatizo hili kwani tatizo la bidhaa feki linamgusa kila mmoja.
Hata hivyo bidhaa hizi zisizo na viwango zimekuwa ni changamoto kwa kuwa na athari nyingi kiafya na usimamizi wake kuwa mgumu.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.