Monday 8 June 2015

Jack Warner azidi kuchunguzwa.


Makamu wa Rais wa zamani wa Shirikisho la Kandanda duniani FIFA Jack Warner amekumbwa na kashfa ingine na uchunguzi dhidi yake kuhusiana na kupotea kwa fedha ambazo zililengwa kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi lililoikumba Haiti mwaka 2010.
Warner aliitembelea nchi hiyo miezi kadhaa baada ya tetemeko hilo a kuchangisha kiasi cha dola dola mia saba na elfu 50 kutoka FIFA na shirika la mpira wa miguu la Korea kusini kwa ajili ya kuijenga upya nchi hiyo.
Lakini hata hivyo, Wachunguzi wa kashfa hiyo rushwa inayoikabili FIFA wanasema fedha hizo zilihamishwa katika Akaunti inayodhibitiwa na Bwana Warner kwa ajili ya matumizi yake binafsi. Miaka minne baadaye fedha hizo bado hazijatolewa maelezo.Warner mwenyewe amekana tuhuma zote zilizotolewa dhidi yake.
Share:

Lewis Hamilton afurahia ushindi


Dereva wa mbio za magari ya Langalanga Lewis Hamilton, amekiri kuwa alihitaji ushindi kwenye mashindano ya Canadian Grand Prix baada ya kuibuka kidedea mara nne katika mashindano saba ya msimu huu.
Lewis hakufanikiwa kushinda katika mashindano yaliyopita yaliyofanyika Monaco kutokana na matatizo ya kiufundi yaliyoikumba gari lake. ''Sikuhitaji ushindi? Nafikiri nilihitaji" alisema Hamilton.
''Hakika tulipata tatizo ambalo lilimwezesha Nico kushinda mbio zile, lakini kwa ujumla nilikuwa na kasi nzuri kwa mashindano mawili ya mwisho kwahiyo hairidhishi, ni vizuri kuendelea na nguvu nzuri na inapendeza kuona timu ikiendelea kuwa na nguvu huku ikisonga mbele.

Hilo ndilo jambo la kuvutia zaidi" aliongeza mchezaji huyo.
Meneja mkuu wa Mercedes Toto Wolff, amesema timu yao imepitia katika wiki mbili ngumu kutokana na ukosoaji mkubwa walioupokea kutokana na makosa ya Monaco ambayo yamepelekea kufanya tathmini kuhusiana na maamuzi ya kiufundi ya mbio.
Share:

Google yamuorodhesha Modi kama muhalifu


Kampuni ya mtandao wa Google imeomba radhi baada ya picha za waziri mkuu wa India Narendra Modi kuonekana katika picha za watu kumi wahalifu.
''Tunaomba radhi kwa kuchanganyikiwa na kutoelewana ambako kumesababishwa na picha hizo'',taarifa iliotoka kwa kampuni hiyo ilisema.
Picha za Modi zinaonekana unapowatafuta watu 10 wahalifu pamoja na magaidi,wauaji na madikteta.

Viongozi wengine duniani waliomo katika orodha hiyo ni aliyekuwa rais wa Marekani George Bush na Libya Muammar Gaddafi.
Viongozi wengine wakuu wanaopatikana ni waziri mkuu wa Delhi Arvind Kejriwal,wakili Ram Jethmalani na mtoro Dawood Ibrahim pamoja na mwigizaji wa Bollywood Sanjay Dutt ambaye kwa sasa anahudumia kifungo kutokana na mlipuko mkubwa uliotokea mjini Mumbai mwaka 1993.
''Haya matokeo yanatushangaza na hayawakilishi maoni ya Google'',kampuni hiyo ilisema katika taarifa yake iliotolewa jumatano usiku.

Kampuni hiyo imesema kuwa matokeo hayo yanatokana na gazeti moja la Uingereza ambalo lilichapisha picha ya Modi kimakosa.
Msamaha huo unajiri baada ya wanasiasa wengi wa India kuonyesha wasiwasi wao katika mitandao ya kijamii.
Share:

Polisi asimamishwa kazi Marekani..


Polisi mmoja mzungu katika jimbo la Texas nchini Marekani amesimishwa kazi baada ya video moja kuwekwa kwenye mitandao ikionyesha akihangaisha kundi moja la vijana wengi wao wakiwa ni weusi.
Afisa hiyo anaonekana akiwalenga vijana wawili wa kiume kwa bunduki yake huku pia akimuangusha chini na kumkamata msichana wa umri wa miaka 14.
Polisi hao walikuwa wameitwa na wenyeji waliokuwa wakilalamikia kuwepo usumbufu kwenye kidimbwi kimoja cha kuogelea.

Mkuu wa polisi McKinney anasema kuwa, anachunguza tukio hilo ambalo linafanyika wakati kuna misukosuko baina ya jamii za watu weusi nchini Marekani wanaodai kunyanyaswa na polisi.
Share:

Nyuki avuruga safari ya ndege Uingereza


Abiria wa ndege moja ya shirika la ndege la Flybe linalohudumu nchini Uingereza walicheleweshwa kwa zaidi ya saa mbili baada ya wahandisi wa ndege hiyo kubaini kuwa nyuki alikuwa amepenyeza na kuingia ndani ya mitambo ya ndege hiyo na hivyo safari haingewezekana.
Ndege hiyo ya Flybe yenye namba ya usajili BE384 ilikuwa ikitoka Southampton kuelekea Dublin.
Wahandisi walilazimika kutafuta mbinu ya kumwdoa mdudu huyo.
Abiria mmoja aliyekuwa ndani ya ndege hiyo Noel Rooney, anasema hakuamini tukio hilo hasa kwani ndge hiyo imeitwa jina la nyuki!
Taarifa kutoka kwa shirika hilo lilisema kuwa nyuki huyo alikuwa ndani ya mitambo muhimu ambayo ingehatarisha maisha ya abiria wake.
''rubani wetu alitahadharishwa na kuwepo kwa nyuki na akalazimika kurejea maramoja katika uwanja wa ndege wa Southampton'.'

Nyuki huyo alikuwa ndani ya mitambo muhimu ambayo ingehatarisha maisha ya abiria wake.

Shirika hilo limewaomba radhi abiria wote waliokerwa na hatua ya kurejea kwa ndege hiyo.
Watu wengi waliitania ndege hiyo kufuatia ripoti hiyo kuenea kwenye mitandao ya kijamii.
Rooney aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter kuwa ''nimebeba jaa ilikuhakikisha kuwa safari yangu ikamilike''
Share:

Burundi;Watoto Wakimbizi wanadhulumiwa


Shirika la kutoa misaada la Save the Children limesema kuwa zaidi ya watoto elfu mbili mia tatu 2,300 ambao hawana wazazi, wamekimbia machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini Burundi.
Shirika hilo limesema kuwa baadhi ya watoto hao walitembea kwa miguu kwa muda wa wiki moja hadi mataifa jirani ya Rwanda, Tanzania na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Msemaji wa shirika hilo la Save the Children, Edwin Kuria,amesema idadi kubwa ya watoto hao walifika katika kambi za wakimbizi wakiwa hawana hata viatu na mali waliyokuwa nao ni mavazi tu waliokuwa nayo mwilini.

Tangu aprili mwaka huu watoto wengi kutoka Burundi wamekuwa wakitembea hadi kambi hizo za muda nchini Rwanda,Tanzania Uganda na DRC.
Shirika hilo limeonya kuwa idadi hiyo huenda ikaongezeka huku wengi wakitoroka Burundi wakihofia kuzuka kwa mapigano.
Taifa hilo linajianda kwa uchaguzi mkuu ambao awali ulipangiwa kuandaliwa mwezi huu.
Aidha shirika hilo limesema watoto hao wanakabiliwa na matatizo mengi njiani na wanapofika katika kambi hizo ambazo kwa sasa zimefurika usalama wao bado sio shwari.
Baadhi ya watoto hao wameripotiwa kunyanyaswa na kudhulumiwa na wakaazi wa maeneo hayo.

Watoto hao hawaendi shuleni na sasa jukumu lao kuu ni kukusanya kuni au kuchimba vyoo majukumu ambayo sio salama kwa watoto amesema bwana Kuria.
Katika kambi ya Mahama nchini Rwanda watoto hao wanakabiliwa na matatizo ya kupata maakazi ya kuishi na pia maji safi ya kutumia.
Nchini Tanzania katika kambi ya Nyarugusa, idadi ya watoto wanaogonjeka imeongezeka hasa kufuatia kufungwa kwa vituo viwili ya muda kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
Share:

Jeshi la Nigeria lahamia Maiduguri


Makao makuu ya jeshi la kulinda usalama la Nigeria limehamisha kitovu cha operesheni ya kukabiliana na wapiganaji wa kundi la kiislamu la Boko Haram hadi mji wa Maiduguri.
Hatua hii inafuatia ahadi ya rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari alipokuwa akiapishwa kuwa moja ya kauli mbiu ya utawala wake ni kukabiliana na Boko Haram.
Msemaji wa jeshi kanali Sani Usman amesema kuwa wanajeshi wakuu wote wamehamia huko ilikuendesha operesheni dhidi ya kundi hilo.
Mji huo ulioko kaskazini mwa taifa hilo tajiri zaidi barani Afrika kiuchumi umekuwa kitovu cha mapigano makali baina ya wapiganaji wa Boko haram na majeshi ya serikali.
Katika siku za hivi punde Maiduguri Imeshuhudia visa vingi mno vya mashambulizi ya kujitolea mhanga ambayo yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 80.
Rais mpya aliyechaguliwa majuzi, Muhammadu Buhari, aliamuru kuhamishwa kwa kituo hicho hadi Maiduguri kutoka mji mkuu wa Abuja - mahala ambapo aliapishiwa mwishoni mwa mwezi uliopita.

Mwana habari wa BBC wa maswala ya usalama barani Afrika, amesema kuwa kumekuweko na lawama dhidi ya makamanda wakuu wa kijeshi kujitenga na hali ilivyo katika kikosi cha kwanza kinachopambana na Boko Haram.
Hali hiyo imechangia pakubwa kutokuwa na uwezo wa kufanya maamuzi ya busara.
Amesema kuwa uamuzi huo wa kuhamishiwa kwa kituo hicho kikuu hadi Maiduguri, kutasaidia pakubwa katika vita dhidi ya Boko Haram, kundi ambalo limesababisha maafa makubwa na hasara Nchini Nigeria.
Share:

Mguu bandia wenye hisia wazinduliwa


Watafiti katika chuo kikuu nchini Ausralia wamevumbua mguu wa kwanza bandia duniani wenye uwezo wa kusisimua hisia halisi za binadamu.
Mguu huo wenye tofauti chache mno na ule halisi unahisi hata maumizi.
Katika uvumbuzi huo wa Profesa Hubert Egger wa chuo kikuu cha Upper Austria, mguu huo bandia unatumia neva za mwili wa mtu aliyekatwa mguu wake.

Aidha neva za ncha za mguu wa mgonjwa hushikanishwa na waya zinazowasiliana na ubongo kupitia kwa paja.
Professor Egger anaelezea kuwa bwana mmoja mlemavu amekuwa akiuvaa mguu huo bandia kwa miezi sita.

Bwana Wolfgang Rangger alisema kuwa katika muda huo wa miezi sita anauwezo wa kubaini iwapo anakanyaga mawe, simiti,na hata nyasi.
''ninapo kanyaga jiwe,nahisi kitu kigumu na pia nikikanyaga mbao,pia najua kuwa kile nilichokanyaga ni tofauti.''
''Nimepata maisha mapya baada ya kupokea mguu bandia'' alisema Wolfgang Rangger.
Share:

Mtandao wa kijeshi Marekani wadukuliwa


Jeshi la Marekani lilisimamisha kwa muda mtandao wake baada ya kisa cha kuingiliwa kimitandao. Jeshi la Syria la Electroniki - linalomuunga mkono Rais Bashar al-Assad - limesema katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter, kuwa ndilo lililotekeleza shambulizi hilo la kimitandao. Lakini habari za hivi punde zasema kuwa mtandao huo wa jeshi la Marekani umerejeshwa.
Share:

Mtandao wa kijeshi Marekani wadukuliwa


Jeshi la Marekani lilisimamisha kwa muda mtandao wake baada ya kisa cha kuingiliwa kimitandao. Jeshi la Syria la Electroniki - linalomuunga mkono Rais Bashar al-Assad - limesema katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter, kuwa ndilo lililotekeleza shambulizi hilo la kimitandao. Lakini habari za hivi punde zasema kuwa mtandao huo wa jeshi la Marekani umerejeshwa.
Share:

Hong Hong yatoa tahadhari ya MERS.


Serikali ya Hong Kong imetoa tahadhari dhidi ya kusafiri kwenda nchini Korea Kusini, kufuatia kuwepo mlipuko wa homa ya Middle East Respiratory Syndrome ambayo pia inafahamika kama MERS nchini humo.
Onyo hilo linatolewa kwa safari ambazo si za lazima, ishara kuwa Hong Kong inaamini kwamba usafiri kwenda Korea kusini ni jambo ambalo ni hatari.
Wizara ya afya nchini Korea Kusini inasema kuwa watu 7 kwa sasa wameaga dunia kutokana ugonjwa huo.
Kumeripotiwa visa 8 vipya vya homa ya MERS na kufikisha idadi ya watu walioambukizwa kuwa 95.
Share:

G7 yatishia kuiongezea Urusi vikwazo.


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema kuwa, viongozi wa mataifa saba yenye uwezo mkubwa wa kiuchumi Duniani-G7, wamekubaliana kuwa vikwazo dhidi ya Urusi vinafaa kuendelea.
Bi Merkel amesema hadi pale muafaka wa kukomesha mapigano nchini Ukraine utakapoheshimiwa vikwazo sharti ziendelee.

Akiongea katika siku ya mwisho ya mkutano wa siku mbili, Merkel amesema kuwa mataifa ya G7 yalikuwa tayari kuzidishia Urusi vikwazo zaidi, iwapo hali ingeruhusu.
Kuhusu mzozo wa kifedha unaokumba Ugiriki, Bi Merkel, alionya kuwa muda uliosalia kabla makubaliano hayajatiwa sahihi ni mchache mno.

Alishauri Ugiriki kuchukua hatua madhubuti ilikunusuru sarafu ya taifa hilo.
Viongozi hao wanafanya mazungumzo katika siku ya pili ya mkutano mkuu, wenye nia ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa, huku pia swala la kuongezeka kwa makundi yenye itikadi kali likijadiliwa.
Bi Merkel pia amewataka wanachama wa G7 kuchangia hazina ya kuyasaidia mataifa maskini ambayo yanaathirika na mabadiliko ya hali ya anga.

Viongozi kutoka Nigeria na Tunisia watahudhuria kikao maalum, kuhusiana na hatari iletwayo na makundi yenye itikadi kali hasa yale ya Afrika.
Kwa mara ya pili tangu mzozo huo na Ukrain utokee rais Putin wa Urusi hakualikwa kwenye kikao hicho licha ya Urusi kuwa mwanachama wa G7.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.