Saturday 29 August 2015

Waandishi wa Al Jazeera miaka 3 Jela


Mahakama nchini Misri imewahukumu waandishi watatu wa kituo cha runinga cha Al jazeera miaka mitatu jela.
Wakati wa kutolewa kwa hukumu hiyo, Mohamed Fahmy, Peter Greste na Baher Mohamed walipatikana na hatia ya kutangaza habari za uongo na kulisaidia kundi la Muslim Brotherhood ambalo kwa sasa linatambuliwa kuwa kundi la kigaidi.
Baher Mohamed pia alihukumiwa kifungo kingine cha miezi sita.
Hata hivyo Peter Greste, yuko nje ya nchi baada ya kutimuliwa kutoka nchini humo mwezi Ferbruari.
Share:

Mkutano wa usalama kufanyika Ufaransa


Mawaziri wa masuala ya ndani wa nchi za ulaya wakutana mmji Paris hii leo kujadili njia za kuboresha usalama kwenye usafiri wa reli baada ya shambulizi lililotibuka wiki iliyopita kwenye treni iliyokuwa safarini kutoka Amsterdam kwenda Paris.
Ufaransa inataka kutangaza hatua kali za usalama ikiwemo vifaa vya kutambua chuma kwenye treni za kimataifa, kuweka wahudumu waliojihami na mifumo ya mawasiliano iliyoboreka kufuatilia mienendo ya wanamgambo walioshukiwa.

Raia wa Morocco ambaye alikuwa amejihami vikali (Ayub al-Khazani) ambaye alishindwa nguvu na abiria baada kupanda treni mjini Brussels alikuwa akifanya safari kote barani Ulaya hata baada uhispania kutoa onyo kuwa huenda mtu huyo alikuwa ni gaidi.
Share:

Ban aitaka ulaya kuwasaidia wahamiaji


Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki Moon ametoa wito kwa serikali zote zinazolishughulikia suala la wakimbizi barani ulaya kutenga maeneo salama kwa wahamiaji na kuonyesha utu.
Ban amesema kuwa idadi kubwa ya wakimbizi na wahamiaji ni ishara ya matatizo makubwa kama ya vita vilivyo nchini Syria ambapo ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuonyesha moyo wa kutatua mizozo kama hiyo.

Ban amesema kuwa masuala hayo yatapewa kipaumbele wakati viongozi wa dunia watapokusanyika kwenye mkutano wa umoja wa mataifa mwezi ujao.
Mapema umoja wa mataifa uliwataka viongozi wa nchi za ulaya kuzuia vifo vya wahamiaji baada ya mamia kuaga dunia siku tatu zilizopita.
Share:

Mafuriko yaua 20 Dominica


Waziri mkuu nchini Dominica anasema kuwa watu 20 wanariporitiwa kuaga dunia kwenye mafuriko yaliyosababishwa na kimbunga Erika.
Kwa njia ya televisheni Roosevelt Skerrit alisema kuwa mamia ya nyumba, madaraja na barabara vimeharibiwa na kisiwa hicho kumerudishwa nyuma miaka ishirini.
Kimbunga kwa sasa kinazikumba Haiti na Jamhuri ya Dominica kikiwa na upepo unaovuma kwa kasi ya karibu kilomita 85 kwa saa.
Watabiti wa hali hewa wanaseme kuwa hata hivyo kinaonyesha dalili za kupoteza nguvu zake.
Share:

Yaliomo kwenye makubaliano ya S.kusini


Hivi ndio vipengee vikuu kwenye makubaliano ya amani ambayo rais wa Sudan kusini Salva Kiir anatarajiwa kusiani Juba:
Mapigano yasite mara moja. Wanajeshi wasalie kweny kambi zao kwa siku 30, vikosi vya nje viondoke katika siku 45 na watoto wanaotumiwa jeshini na wafungwa wa vita waachiliwe huru.
Vikosi vyote vya usalama vitoke umbali wa kilomita 25 kutoka Juba, nabadala yake vikosi maalum na polisi ya pomoja vichukuwe nafasi hiyo.
Waasi wapewe cheo cha "makamu wa kwanza wa rais"
Serikali ya mpito ya muungano wa kitaifa iidhinishwe katika muda wa siku 90 na iongoze nchi kwa miezi 30.
Uchaguzi ufanyike siku 60 kablaya ya kumalizika kipindi cha mpito.
Serikali ipate uwingiwa nyadhifa serikalini katika kiwango cha kitaifa na katika majimbo 7 kati ya 10 yaliopo.
Katika majimbo yanayokumbwa na vita - Jonglei, Unity, na Upper Nile - waasi wanapata uwakilishi ulio sawana serikali.
Tume ya ukweli na mapatano ichunguze ukiukaji wa haki za binaadamu.
Share:

Kidimbwi kinachounganisha majumba 2 UK


Kidimbwi cha kuogelea chenye urefu wa mita 25 kinachounganisha kilele cha majumba mawili marefu yenye ghorofa 10 kitajengwa mjini London.
Kidimbwi hicho kinachoitwa ''Sky Pool'' ni cha kwanza duniani na kitakuwa na eneo la chini lililo wazi.Uwazi huo utawasaidia waogoleaji kuwaona raia wanaotembea chini ya majumba hayo kwa urefu wa mita 35.
Kampuni ya Eckersley O'Callaghan ambayo imeshirikiana na ile ya Apple kuhusu mtindo wa kidimbwi hicho cha kuogelea itatengeza mradi huo.
Kidimbwi hicho ni miongoni mwa miradi ya ujenzi ya maeneo ya kujivinjari kwa jina Embassy Gardens at Nine Elms,karibu na kituo cha umeme cha Battersea

Inatarajiwa kuwa mradi huo utakamilika ifikiapo mwaka 2019,lakini mtindo huo una changamoto zake hususan kutokana na hatua kwamba kidimbwi hicho kitazuiliwa na misukumo itakayotoka kutoka kuta za majumba hayo mawili ambayo yamejengwa na misingi tofauti.
''Upepo unapovuma majumba hayo huyumba tofauti na hivyobasi kuwa changamoto kwa watengezaji wa kidimbwi hicho'' kulingana na Brian Eckersley
Share:

Treni iliyosheheni dhahabu yapatikana


Afisa mmoja wa serikali ya Poland, amesema kuwa ana imani kuwa treni moja ya kijeshi ambayo imefichwa tangu vita vya pili vya dunia, zaidi ya miaka sababini iliyopita, na kusemekana kubeba vitu vya dhamani, imepatikana, chini ya ardhi Kusini Magharibi mwa nchi hiyo.
Naibu waziri wa utamaduni amesema shehena iliyoko kwenye treni hiyo bado haijulikani.
Kwa mujibu wa ripoti treni hiyo ilipotea ikiwa imejaa shehena ya dhahabu kutoka mji wa Breslau nchini Ujerumani, mji ambao kwa sasa unajulikana kama Wroclaw and sehemu zingine za Poland, wakati wanajeshi wa Ujerumani walipokaribi mji huo.
Afisa mkuu wa makavazi ya kitaifa, Piotr Zuchowski, amesema anaimani kuwa treni hiyo itapatikana chini ya ardi karibu na mji wa Walbrzych.
Amesema ameona picha zilizopigwa na kifaa maalum chini ya ardhi ikionyesga treni hiyo yenye urefu wa karibu mita mia moja ikiwa na bunduki juu yake.
Amesema hamna anayefahamu kile treni hiyo ilikuwa imebeba wakati huo na asema anatarajia iwe na vitu vya Sanaa vilivyoibiwa nchini Ujerumani wakati wa utawala wa Kinazi.
Raia wawili ambao hawajatambuliwa kutoka Ujerumani na Poland waliifahamisha utawala wa eneo hilo kuwa wanafahamu eneo lililofichwa treni hiyo, na wamedai wapewe asilimia kumi ya vitu vitakavyopatikana ndani yake.
Watu hao wanasema kuwa walipewa habari hizo na mtu mmoja ambaye alikuwa miongoni mwa walioficha treni hiyo, muda mfupi tu kabla ya mtu huyo kufariki.
Share:

Wednesday 5 August 2015

Wasifu wa Edward Lowassa


Umoja usio rasmi wa vyama vinne vya upinzani nchini Tanzania unajulikana kwa jina la Katiba ya Wananchi (UKAWA), baada ya kusubiri kwa muda hatimaye umemtangaza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.
Lowassa anagombea kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), huku vyama vingine vitatu vikimuunga mkono. Hii inatokana na sheria za Tanzania ambayo haitambui umoja wa vyama.
Kabla ya kujiengua chama Tawala chama cha Mapinduzi CCM, Edward Lowassa amekuwa mwanachama wa CCM kwa muda wa miaka 38, ambapo alijiunga na chama hicho mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka 1977.
Hatua ya mwanasiasa huyo mashuhuri nchini Tanzania kuamua kujiunga na chama cha upinzani Chadema, ikiwa imebaki miezi mitatu tu kuelekea uchaguzi mkuu, kumebadilisha kabisa upepo wa kisiasa nchini Tanzania, na hasa uchaguzi mkuu ujao.

Lowassa alikuwa Maziri Mkuu kati ya mwaka 2005 na 2008 kabla ya kujiuzuLu wadhifa huo kufuatia sakata la kashfa ya rushwa iliyohusisha kampuni ya kuzalisha umeme ya ki-Marekani Richmond Development Company LLC ya Houston Texas.
Hata hivyo wakati anatangaza kuhamia kwake Chadema, Lowassa alikanusha katu katu kuhusika kwa namna yoyote na kashfa hiyo na kudai kuwa yeye alifuata tu amri kutoka kwa ‘wakubwa’ walio juu yake.
“Kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi basi na aende mahakamani ama sivyo anyamaze” alisema Lowassa

Kuhama kwake kunamfanya Lowassa kuwa ndie kiongozi wa kwanza wa ngazi ya juu kabisa wa CCM kukihama chama hicho tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania mnamo mwaka 1992.
Mwanajeshi wa zamani na aliyewahi kupigana wa vita kati ya Uganda na Tanzania mwaka 1978/79, Lowassa aliiambia hadhara kwamba akiwa kama mtu mwenye uchungu na nchi yake isingekuwa rahisi kubaki ndani ya CCM huku akiona chama hicho kimepoteza mwelekeo na sifa ya kuongoza nchi.
Lowassa amekimbilia upinzani baada jina lake kukatwa wakati alipoomba kuwa mgombea urais kupitia chama tawala CCM katika uchaguzi mkuu ujao utakafanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Wakati mchakato wa CCM wa kumtafuta mgombea wao wa urais ulipoanza, Lowassa ndiye aliyekuwa kinara wa wagombea wote 42. Kila kona aliyozunguka, mikutano yake ya hadhara ilivutia maelfu ya watu waliomuunga mkono.
Wakati chama cha CCM kilimtaka kila mgombea apate sahihi za wadhamini 450 lakini Lowassa alipata sahihi za wadhamini zaidi ya 700,000.

Hata hivyo mchujo wa chama ulipofanyika jina lake lilikatwa mapema kabla hata ya kupelekwa kwenye vikao vya vya juu vya chama hicho. Ambapo baadae Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli ndiye aliyeibuka kidedea na kuwa mgombea kupitia chama tawala CCM.
Lowassa ameushutumu mchakato CCM wa kutafuta mgombea urais akiuita kuwa ulijaa chuki na mizengwe dhidi yake, hali ambayo aliifananisha na ‘ubakaji wa demokrasia’
“Nitakuwa mnafki nikisema bado nina imani na CCM. CCM niliyoiona Dodoma si CCM niliyokulia”, alisema, na kuongeza “kama Watanzania hawapati maendeleo kupitia CCM basi wakayatafute nje ya CCM”
Wakati sakala la Richmond lilipoibuka miaka michache tu iliyopita, Chadema ilimfanya limsakama Lowassa kuwa ni mmoja wa mafisadi wakubwa nchini. Lakini wakati chama hicho kinamkaribisha kuwa mwanachama wao, kiligeuka na kusema hakuna mtu msafi nchini na kwamba hawawezi kuacha kumpokea mwanasiasa mwenye mtaji mkubwa wa wafuasi kama Lowassa.
Wakati akiwa Waziri Mkuu, Lowassa alisifika kama mchapakazi hodari na msimamiaji wa moja kwa moja wa shughuli za serikali. Bado anaendelea kufahamika kwa jina la utani la ‘mzee wa maamuzi magumu’.

Moja ya mafanikio makubwa ya uwaziri mkuu wake ni jitihada kubwa na mafanikio ya upatikanaji wa fedha za kujenga chuo kikuu cha Dodoma. Chuo hiki kikuu cha umma kilichopo katikati ya Tanzania kilianzishwa mwaka 2007.
Lowassa ni mashuhuri pia kwa kusimamia mpango wa serikali uliofanikiwa wa ujenzi wa shule za kata ambazo uliiletea Tanzania sifa kubwa kwa kutoa fursa ya watoto wengi kupata nafasi shuleni.
Mtoto wa Mzee Ngoyai Lowassa, ambaye aliwahi kuwa mtumishi wa serikali ya kikoloni, Lowassa ameanza harakati zake za kuwania urais tangu mwaka 1995 lakini inaarifiwa kwamba rais wa kwanza wa Tanzania Mwl Julius Nyerere alimkatalia kushika nafasi hiyo. Wafuasi wa Lowassa wamekuwa wakiyatupilia mbali madai hayo
Ulipofika uchaguzi wa mwaka 2005, Lowassa hakutaka kuwania urais, lakini badala yake alimnadi rafiki yake wa siku nyingi Rais wa sasa Jakaya Kikwete ambaye alipata ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 80.
Share:

China ni haramu kuhifadhi mayai ukiwa hujaolewa


Mjadala mkali umeibuka nchini China baada ya serikali kupiga marufuku kwa uhifadhi wa mayai kwa wanawake ambao hawajaolewa.
Aidha mayai ya wanawake walioolewa wanaweza kuhifadhi mayai iwapo tu wanapata matibabu ya saratani ama matibabu ambayo yatadhuru kizazi chao.
Marufuku ya aina hii si jambo geni kwa raia wa China ambao tayari wanastahimili sheria kali ya kupanga uzazi.
Hata hivyo,ripoti zilipoibuka kuwa muigizaji Xu Jinglei alikwenda Marekani kuhifadhi mayai yake ya uzazi ndipo wachina wakang'amua kuwa huenda sheria hiyo inawalemga maskini.

Maelfu ya wachina wameikashifu sheria hiyo wakisema kuwa ni ya kibaguzi kwa misingi ya jinsia.
Aidha wengine wanahoji kwanini serikali inaingilia kati maswala ya kibinafsi na mambo ya kijamii.
Mjadala huu ulitibuka mwezi Julai baada ya Xu Jinglei alipokiri kuwa ni kweli amehifadhi mayai yake huko Marekani tangu mwaka wa 2013.

Muigizaji huyo mwenye umri wa miaka 41 alisema alichukua uamuzi huo kwani hajui ni lini hamu ya kupata mtoto itamwandama.
Siku ya jumapili televisheni ya kitaifa ya CCTV ilitoa ripoti kuhusiana na swala hilo na kuonyesha athari zake na kusema marufuku hiyo haina uhusiano na upangaji uzazi.
Ripoti hii ilisisimua watu katika mitandao ya kijamii ambao wengi wamekuwa wakiitupia dongo serikali.
Share:

Boti la abiria lazama ziwa Victoria Kenya


Boti moja iliyokuwa imebeba abiria 23 imegongana na mtumbwi wa wavuvi na kuzama katika ziwa Victoria Magharibi mwa Kenya.
Taarifa za awali zilikuwa zimetoa idadi hiyo kuwa 200 lakini maafisa wa usalama nchini Kenya wamethibitisha kuwa idadi ya abiria kwenye boti hiyo ilikuwa 23.
Watu 21 wameokolewa.
Miili ya watoto wawili imepatikana ikielea kwenye ziwa hilo.
Afisa huyo ameiambia BBC kuwa waliwaokoa watu 14 walipowasili katika eneo la tukio kabla ya kuwanusuru wengine saba waliporejea mara ya pili.
Wavuvi wanne waliokuwa kwenye mtumbwi wa pili pia waliokolewa.
Kwa mujibu wa walionusurika, boti hilo lililokuwa limewabeba abiria liligonga mtumbwi wa wavuvi kisha zote mbili zikazama majini.
Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi hii leo.

Ajali hiyo imetokea karibu na visiwa viwili vidogo ndani ya ziwa Victoria viitwavyo Kiwa na Remba Magharibi mwa Kenya.
Boti hiyo iliyokuwa na abiria ilikuwa inaelekea Sori kutoka kisiwa cha Remba.
Shughuli za uokoaji zinaendelea huku maafisa wa idara za serikali ya Kenya na wavuvi wakishirikiana kuwanusuru abiria hao.
Share:

Japan yakumbuka shambulio la Heroshima


Raia wa Japan leo wanaadhimisha kumbukumbu ya miaka 70 tangu shambulio la kwanza la bomu la Atomiki kutekelezwa mjini Heroshima.
Takriban watu laki moja na arobaini walikadiriwa kupoteza maisha baada ya Ndege ya Marekani kudondosha bomu ambalo liliuharibu mji huo tarehe 6 mwezi Agosti mwaka 1945.
Watu elfu sabini walipoteza maisha papo hapo, huku wengine wa idadi kama hiyo walipoteza maisha kutokana na athari za mionzi ya sumu.
Katika hotuba yake, Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe alisema kumbukumbu ya Heroshima inasisitiza uhitaji wa kufanya jitihada ya kupiga vita matumizi ya Nuklia.
Shambulio la Heroshima lilifuatiwa na shambulio jingine la bomu la Atomiki katika mji wa Nagasaki.
Japan ilijisalimisha siku kadhaa baadae, hatua iliyomaliza vita ya pili ya dunia.
Share:

Hofu baada ya boti iliyojaa wahamiaji kuzama Libya


Waokoaji wanaendelea na shughuli ya kuwasaka mamia ya wahamiaji waliotumbukia baharini baada ya boti walimokuwa wakisafiria kwenda Ulaya kuzama majini katika bahari ya Mediterrania karibu na ufuo wa Libya.
Ripoti ambazo hazijathibitishwa zinasema kuwa takriban watu 700 walikuwa kwenye mtumbwi huo uliozama baada ya kukumbana na mawimbi makali.
Wanajeshi wa majini kutoka Ireland wanakisia kuwa idadi kubwa ya watu wamekufa maji.
Aidha shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka Medecins Sans Frontieres (MSF) limeonya kuwa huenda kukazuka maafa makubwa kufuatia idadi kubwa ya abiria waliokuwa kwenye mtumbwi huo uliozama.
Inakisiwa kuwa takriban wahamiaji 2,000 walikufa maji kwanza mwanza wa mwaka huu wakijaribu kufika ulaya kupitia bahari hiyo ya Mediterranea
Meli nne za uokozi na ndege tatu zimetumwa huko kujaribu kunusuru maisha ya wahamiaji hao.

Walinzi wa Ufuo wa bahari ya Uitaliano wamesema boti hiyo ya uvuvi iliyokuwa imebeba mamia ya wahamiaji.
Inavyoelekea boti hiyo ilikumbwa na dharuba lakini pia ilipenduka pale watu walipokurupuka upande mmoja walipoona chombo kingine kilichokuwa kikienda kuwasaidia.
Zaidi ya watu 150 wameokolewa lakini wengine wengi wanahofiwa wamekufa maji.
Msemaji wa shirika linalohusika na maswala ya wahamiaji IOM, Leonard Doyle ameiambia BBC kuwa
''Lazima tukumbuke kuwa hawa ni watu ambao hawajazoea usafiri wa baharini kwahivyo waliogopa.''
''Na wakati walipoona chombo kingine kinakuja kuwaokoa wakataharuki na kukurupuka upande mmoja''.

Hilo ndilo tunalokariri kuwa hao walanguzi wa kusafirisha watu hawajali kabisa kuhusu maisha ya wahamiaji hao licha ya kuwa wamewalipa pesa nyingi kwa safari hizo hatari''.
Kwamba mkasa wa aina hii unaweza kutokea wakati ambao hata watu wamepelekewa chombo cha kuwaokoa karibu yao ni jambo la kusikitisha sana.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.