Monday 20 July 2015

Buhari akutana na Obama


Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari anafanya mazungumzo mjini Washington na rais wa Marekani Barack Obama.
Mazungumzo baina ya viongozi hao wawili yanalenga ushirikiano katika vita dhidi ya wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
null
Awali Marekani ilikubali kuisaidia Nigeria katika vita dhidi ya makundi ya uasi hasa baada ya kutekwa nyara kwa wasichana zaidi ya 200 wa shule kutoka Chibok mwaka jana.
null
Hata hivyo uhusiano baina ya Marekani na utawala ulioondoka madarakani wa Goodluck Jonathan ulidhoofika , baada ya shutuma za makundi ya kutetea haki za kibinadamu kuhusu ukiukaji wa haki za kibinadamu unaotekelezwa na jeshi la Nigeria.
Bwana Buhari pia ameahidi kushughulikia ufisadi na amesema atarejesha mabilioni ya dola yaliyofichwa kwenye benki za Marekani Uswiss na kwingineko.
Share:

Ziara ya mfalme wa Saudia Ufaransa yazua Ubishi


Ubishi umeibuka nchini Ufaransa, baada ya ufukwe maarufu wa bahari wa Riviera kufungwa ilikumruhusu mfalme wa Saudi Arabia na familia yake kujivinjari kwa amani faraghani.
Viongozi wa mji wa Vallauriswametangaza kuwa watafunga sehemu kubwa ya ufukwe huo ilikuhakikisha usalama wa mfalme huyo familia yake na takriban ujumbe wa watu 400.
Familia hiyo ya kifalme, inatarajiwa kuishi katika jumba la kifahari lililoko huko.
Jumba hilo lililowahi wakati mmoja kuwa jumba la mapumziko la Sir Winston Churchill linatarajiwa kuzingirwa na maafisa wa usalama.
Maafisa wa Vallauris iliyoko kwenye mwambao wa Cote d'Azur, kilomita 10 kutoka kwenye ufukwe huo wanasema wamethibitisha kuwa shughuli kwenye ufukwe wa Milandore zitafungwa kwa muda wote wa majira ya kiangazi.
null
Hatua hiyo imewagadhabisha wakazi wa maeneo hayo ya mwambao , ambao wametishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mpango wa kuziba barabara ya ardhini kuelekea kwenye ufukwe huo.
Familia hiyo ya kifalme ya Saudi Arabia , ikiongozwa na Mfalme Salman, inamiliki jumba la kifahari ambalo Rita Hayworth alitumia kama mahala pa mapokezi ya wageni wakati wa harusi yake .
Sir Winston Churchill na Elizabeth Taylor walikua miongoni mwa wale waliolitumia kama makazi ya mapumziko.
null
Wakazi wa eneo hilo wamekasirishwa na shughuli za ukarabati katika eneo hilo, hasa baada ya kuwekwa kwa sakafu kubwa ya saruji kwenye mchanga ulioko ufukweni, zimeleza ripoti za wakazi wa eneo hilo.
Blandine Ackermann, rais wa shirika la wanaharakati wanaolinda mazingira katika maeneo ya Golfe-Juan na Vallauris amesema anapanga kuchukua hatua za kisheria kama ufukwe huo hautaendelea kuwa wazi na kurejeshwa katika hali yake
Maafisa wa kulinda bahari wamesema tayari kuwa chombo chochote hakitaruhusiwa kukaribia eneo hilo kwa takriban mita 300 ndani ya bahari.
Share:

Burundi:AU huenda isishiriki uchaguzi.


Yaelekea Muungano wa Afrika hautaweza kupeleka wanajeshi na waangalizi wa haki za kibinadamu nchini Burundi kabla ya uchaguzi wa urais unaotarajiwa kufanyika kesho Jumanne.
Katika taarifa kwa waandishi wa habari, Muungano huo wa Afrika wanasema kupelekwa kwa maafisa hao kumesababishwa na masharti mapya ya Burundi kwamba waangalizi sharti wawe na vibali vya kuingia Burundi mbali na vyeti vyao vya kusafiria vya kibalozi.
null
Mazungumzo baina ya serikali na upinzani yalivunjika mwishoni mwa juma baada ya pande hizo mbili mbili kushindwa kufikia makubaliano.
Upinzani unadai kuwa rais Nkurunziza anakiuka katiba ya taifa na mapatano ya Arusha yaliyokomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe.
null
Burundi imezama katika mgogoro wa kisiasa uliokumbwa na ghasia tangu rais wa nchi hiyo kutangaza kugombea nia ya kuwania muhula wa tatu .
Zaidi ya raia laki moja wa Burundi wamekimbia nchi hiyo tangu mwezi Aprili kulipozuka ghasia kupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Share:

Hatimaye mabenki yafunguliwa Ugiriki.


Mabenki Nchini Ugiriki yanafunguliwa leo kwa mara ya kwanza katika mkipndi cha majuma matatu.
Kuna milolongo mirefu kwa sasa nje ya mabenki hayo, pale bunge la taifa hilo lilipopitishia masharti magumu juma lililopita kama sehemu ya kutatua matatizo yake ya kifedha.
null
Baadhi ya masharti yangali pale pale, ikiwemo viwango vya fedha ya mtaji kutoka mataifa ya ulaya.
Badala ya kutoa fedha kila siku kulingana na kiwango kilichowekwa sasa raia wanaweza kutoa kiwango cha Euro 420 mara moja kwa juma.
null
Ushuru wa mauzo umeongezwa hasa kwa bidhaa na huduma ukiwemo nauli ya usafiri na bei ya chakula mikahawani.
Jana Jumapili, Rais wa Ufaransa Francois Hollande, alisema kuwa shida nchini Ugiriki inafaa kutoa fursa kwa mataifa ya bara Ulaya kubuni serikali moja ya muungano.
Share:

Buhari akutana na Obama.


Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari anafanya mazungumzo mjini Washington na rais wa Marekani Barack Obama.
Mazungumzo baina ya viongozi hao wawili yanalenga ushirikiano katika vita dhidi ya wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
null
Awali Marekani ilikubali kuisaidia Nigeria katika vita dhidi ya makundi ya uasi hasa baada ya kutekwa nyara kwa wasichana zaidi ya 200 wa shule kutoka Chibok mwaka jana.
null
Hata hivyo uhusiano baina ya Marekani na utawala ulioondoka madarakani wa Goodluck Jonathan ulidhoofika , baada ya shutuma za makundi ya kutetea haki za kibinadamu kuhusu ukiukaji wa haki za kibinadamu unaotekelezwa na jeshi la Nigeria.
Bwana Buhari pia ameahidi kushughulikia ufisadi na amesema atarejesha mabilioni ya dola yaliyofichwa kwenye benki za Marekani Uswiss na kwingineko.
Share:

Rais wa zamani Chad,ashtakiwa Senegal.


Rais wa zamani wa Chad Hissene Habre atafikishwa mahakamani nchini Senegal kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu, ukatili dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita .
Kesi hiyo mjini Dakar ni ya kwanza ya aina yake ambapo nchi moja ya Afrika imemshitaki kiongozi wa zamani wa taifa jingine.
Bwana Habre anashutumiwa kwa kuhusika na vitedo vya ukatili na mauaji ya maelfu ya watu wakati wa enzi ya utawala wake kuanzia 1982 hadi 1990, shutuma anazozikanusha..
Kesi hiyo inafuatia miaka 25 ya kampeni za kumfikisha mbele ya sheria.
null
Wengi miongoni mwa watu wanaodaiwa kuwa waathirika wa uhalifu uliotekelezwa na Bwana Habre' wamekua wakitoa wito wa kufunguliwa mashtaka dhidi yake tangu alipopinduliwa mamlakani na kukimbilia uhamisho nchini Senegal 1990.
Mnamo mwaka 2005 mahakama ya Ubelgiji iliytoa kibali cha kumkamata, ikidai kuwa na haki ya kimataifa ya kufanya hivyo , lakini baada ya mazungumzo na Umoja wa Afrika , AU iliiomba Senegal kuendesha kesi dhidi Bwana Habre " kwa niaba ya Afrika ".
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.