Monday 8 December 2014

Maelfu wahitaji msaada Somalia......


Umoja wa Mataifa unasema kua zaidi ya watu milioni tatu wanahitaji msaada wa dhahura kwa sababu ya tatizo kubwa la utapia mlo na mgogoro.
Tahadhari hio imetolewa miaka mitatu baada ya zaidi ya robo ya watu milioni moja kufariki kutokana na ukosefu wa chakula.
Katika taarifa yake ofisi ya mratibu wa misaada ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa inasma kuwa wasomali wanaendelea kukabiliwa na hali ngumu ya kibindamau.

Maelfu ya watu wameathirika kutokana na vita vinavyosababishwa na wanamgambo wa Al Shabaab.
Kikosi cha wanjeshi wa Muungano wa Afrika kiko nchini humo kuoambana na wanamgambo hao.
Wadadisi wanasema hali hiyo imechocewa zaidi na ukame pamoja na mafuriko katika baadhi ya sehemu za nchi hio.
Share:

Amezwa na Nyoka aina ya Anaconda....















Watu nchini Marekani wameelezea ghadhabu na hasira zao kwenye mitandao ya kijamii kufuatia utafiti wa mtaalamu wa wanyamapori Paul Roslie kumezwa na Nyoka aina ya Anaconda ili ku chunguza maumbile ya ndani ya Nyoka huyo.
Lengo la utafiti huo ambao ulikuwa wa kwanza wa aina yake duniani, ilikuwa ni kuchunguza maumbulie ya ndani ya Nyoka huyo anayepatikana katika msitu wa Amazon.
Hata hivyo inaarifiwa bwana Paul alilazimika kusitisha utafiti wake ambao umezua utata muda mfupi tu baada ya kuuanzisha.
Watu nchini Marekani walijionea kwenye televisheni zao kipindi kilichokuwa kinapeperushwa cha mtaalamu huyo kuingia ndani ya tumbo la Anaconda akiwa amevalia vazi maalum ambalo yangesaidia kuchunguza kiwango cha joto mwilini mwake na pia kupima mipigo ya Moyo wake wakati akiwa ndani ya tumbo la Nyoka huyo.















Rosolie na kikundi cha wasaidizi wake walipata Nyoka ya Anaconda mwenye uzito wa kilo 180, walipokuwa katika msitu huo. Alipanga kuwa ataonyeshwa kwenye stesheni hio akiwa anamezwa mzima mzima na Nyoka huyo.
Rosolie alionekana akiingia ndani ya mdomo wa Anaconda kwa kichwa chake huku wenzake wakimtazama.
Alikuwa amevalia vazi maalum lenye Carbon na likiwa limepakwa damu ya Nguruwe, kabla ya kujielkeza kwa Nyoka huyo kama mlo wake.
"sikutana kumhangaisha mno mnyama na pia mimi mwenyewe sikutaka kujiumiza. ''
Share:

Watoto wauawa kikatili DRC......


Inaarifiwa kuwa watu kama 30 waliuwawa katika mashambulio kwenye vijiji mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Taarifa zinasema kuwa mashambulio hayo yalifanywa Jumamosi usiku kwenye vijiji karibu na mji wa Beni ambako watu zaidi ya 250 wameuawa tangu mwezi Oktoba.
Wakuu na mashirika ya raia yanawalaumu wapiganaji kutoka Uganda wa kundi la ADF, lakini baadhi ya wadadisi wanasema hakuna ushahidi wa kutosha wa kuhusisha kundi hilo.
Mwandishi mmoja wa habari katika eneo hilo aliambia BBC kuwa waliofariki ni pamoja na wanawake na watoto ambao walibururwa kutoka kwa nyumba zao na kukatwa katwa kwa mapanga.
Alisema haijulikani nani aliyefanmya mashambulizi hayo, ingawa maafisa wakuu wamelaumu kundi la waasi la Uganda la ADF.
Alisema maelfu ya watu wameachwa bila makao kutokana na vurugu zinazoendelea na kwamba wanahofia sana kurejea makwao.
Share:

Yaya aliyemtesa mtoto UG aomba msamaha..

Mfanyakazi wa nyumbani aliyenaswa kwenye kanda ya video akimchapa na kumkanyaga mtoto nchini Uganda, amefikishwa mahakamani leo.
Mfanyakazi huyo Jolly Tumuhirwe aliambia mahakama kuwa anajulia kile alichokifanya na hata kuomba msamaha. Ameshitakiwa kwa kosa la kumtesa mtoto Arnella.
Licha ya taarifa ya polisi kusema Jolly atashitakiwa kwa kosa la jaribio la ,mauaji, kiogozi wa mashitaka alimshitaki Jolly kwa kosa la kumtesa mtoto mdogo

Bi Tumuhirwe alikiri makosa yake na kuomba msamaha. Hakuna wakili yeyote aliyemwakilisha Jolly mahakamani licha ya mmoja wa mawakili mashuhuri kusema angemwakilisha Jolly bila malipo.
Kesi hio imeakhirishwa hadi Jumatano, wakati ambapo hakimu anatarajiwa kutoa hukumu yake dhidi ya Jolly.
Huenda akafungwa jela miaka 15 au kutozwa faini ya dola mianne au adhabu zote mbili.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.