Wednesday 3 December 2014

Msafara wa UN waponea shambulizi Somalia.....


Mlipuko mkubwa umetokea katika mji wa Mogadishu nchini Somalia karibu na uwanja wa ndege.
Takriban watu wanne wameuawa katika mlipuko wa bomu lililokuwa limetegwa ndani ya gari karibu na msafara wa magari ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishu.
Polisi wanasema kuwa bomu hilo lililipuka wakati msafara huo ulipokuwa unaelekea karibu na barabara iliyoko karibu na uwanja wa ndege mjin humo.

Mlipuko wa pili iliripotiwa kulenga vikosi vya muungano wa Afrika umbali wa kililomita 25 kutoka mjini humo ingawa taarifa bado ni finyu.
Duru zimearifu kuwa mlipuko huo huenda umesababishwa na mtu aliyejitolea muhanga aliyejilipua ndani ya gari.
Kundi la wapiganaji wa kiislamu la Al- Shaabab mara kwa mara hutumia milipuko ya magari, lakini kufikia sasa halijakiri kuhusika na mlipuko huo.

Kundi la Al-Shabab, ambalo limehusishwa na wapiganaji wa al-Qaeda, limekuwa likifanya mashambulizi ya mara kwa mara nchini Somalia na katika nchi jirani ya Kenya.
Mnamo siku ya Jumanne liliwaua watu 36 mjini Mandera karibu na mpaka na Somalia.
Hata hivyo bado halijatoa yamko lolote kuhusu shambulizi lililofanywa mjini Mogadishu.

Share:

Kibarua kinachomkabili Rais Uhuru Kenyatta.......BBC


Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuhutubia taifa kwa mara nyingine baada ya wapiganaji wa Al Shabaab kufanya shambulizi lengine la kinyama katika mji wa Mandera Kaskazini mwa Kenya.
Shambulizi lililolfanywa Jumanne asubuhi dhidi ya wafanyakazi wa mgodini mjini Madera Kaskazini mwa Kenya, limetokea siku kumi baada ya shambulizi lengine kama hilo dhidi ya basi lililokuwa limewabeba wasafriki wengi wakiwemo walimu kutoka Mandera.
Watu 28 waliuawa katika shambulizi la kwanza wiki jana.
Mji huu wa Mandera unapakana na Somalia na Ethiopia. Mandera ni mji wenye idadi kubwa ya wakenya wenye asili ya kisomali wengi ambao ni waisilamu.

Mashambulizi ya leo bila shaka yataathiri uchumi na mfumo wa kijamii wa eneo hilo, kwani wengi wa wafanyakazi walio mjini humo ni vibarua tu na vibaria wenyewe pia sio waisilamu na pia wanatoka katika maeneo mengine ya nchi.
Wengi wa wafnyakazi hao ni walimu na wauguzi na wachimba migodi lakini kwa sasa wameanza kuutoroka mji huo baada ya shambulizi la wiki jana.
Tetesi zinasema hali hii ya watu kutoroka na kurejea makwao huenda ikaendelea.
Punde baada ya mashambulizi ya wiki jana , mshauri wa Rais anayetoka Mandera, Abdikadir Mohamed alionya kuwa kundi la Al Shabaab linajaribu kuanzisha vita kwa msingi wa dini.

Baadhi ya wakristo, pia wamewakosoa viongozi wa kiisilamu kwa kukosa kufanya juhudi za kutosha kukabiliana na kuenea kwa itikadi kali za kidini miongoni mwa waumini wa kiisilamu na hata miongoni mwa viongozi wenyewe.
Serikali ya Kenya nayo imelaumiwa kwa kukosa kuchukua hatua za kutosha kudhibiti usalama na shambulizi la hivi karibuni bila shaka litamuongeza shinikizo Rais Kenyatta za kukabiliana na mashambulizi hayo.
Upinzani umekuwa ukitoa wito kwa Rais Uhuru Kenyatta kujizulu hasa kwa kuwa ameshindwa kukabiliana na hali ya utovu wa usalama nchini humo. Hata hivyo Rais Kenyatta emekuwa akisisitiza kwamba kila mwananchi ana wajibu wa kuhakikisha usalama

Share:

Uganda:Spika asema waliokeketwa hawafai..........source BBC

 Spika wa Bunge la Uganda Bi Rebecca Kadaga amewashauri wanaume kutowaoa wanawake waliokeketwa akiwataja kuwa mzigo ambao hauwezi kuijenga jamii.
Kulingana na gazeti la daily Monitor,Spika Kadaga alitoa wito huo wakati wa sherehe ya kitamaduni ambayo inapinga ukeketaji ilioandaliwa na mfuko wa umoja wa mataifa unaosimamia idadi ya watu na wahisani wengine.
''Mwanamke ambaye amekeketwa hana thamani yoyote. Achaneni na wanawake waliokwenda kukeketwa na badala yake chagueni wanawake ambao hawakukeketwa na ambao wanaweza kuimarisha jamii'',alisema Bi Kadaga.
Utamaduni huo unaojulikana kama upashaji tohara wanawake umekithiri miongoni mwa tamaduni nyingi na bara la Afrika kwa jumla na hutumiwa kumuandaa mwanamke anayeolewa ama hata kuonyesha kwamba ,mwanamke amebalehe.
Nchini Uganda ,utamaduni huo hufanyika mashariki mwa Uganda katika makabila matatu ikiwemo lile la Pokot,Sabiny na Tepeth hususan katika wilaya za Kampchorwa,Kween na Bukwo.
Bi Kadaga ambaye aliyeandamana na waziri wa maswala ya kijinsia Rukia Nakadama wote walitia sahihi ya kumaliza ukeketaji nchini Uganda.
Pia aliwaonya wazazi katika eneo hilo kukoma kuwalazimisha wanao katika ndoa za mapema na badala yake kuwataka kuwapeleka shule.
Baadhi ya wanawake waliokuwa wakitekeleza tendo hilo waliiomba serikali kulisaidia kundi la watu ambao wamewacha kuwapasha tohara wanawake
Share:

Hali bado tete mjini Mandera...........source BBC


Hali ya taharuki imetanda mjini Mandera mpakani mwa Kenya na Somalia baada ya mashambulizi mapya yaliyotokea Jumanne na kusababisha mauaji ya watu 36 wengi wao wakiwa sio waislamu.
Hatua hiyo imemfanya Rais wa Nchi hiyo Uhuru Kenyatta kumuachisha kazi waziri wa usalama wa ndani na mkuu wa polisi.
Inaarifiwa kuwa idadi kubwa ya wafanyakazi wa serikali wanaoishi katika eneo hilo wameanza kulihama kwa hofu ya usalama wao.
Wakati huohuo, msemaji wa Rais Uhuru Kenyatta ameonya kuwa kushinda vita dhidi ya wapiganaji wa Al Shabaab huenda ikachukua muda mrefu sana.
Bwana Manoah Esipisu aliyasema hayo baada ya wapiganaji hao kuwaua watu 36 waliokuwa kwenye machimbo ya kokoto mjini Mandera karibu na mpaka na Somalia.
Esipisu, aliambaia BBC kwamba, serikali inafanya kila iwezalo kuzuia mashambulizi lakini haiwezi kuahidi kwamba hapatatokea shambulizi lengine.
Alisema wanajeshi wa Kenya wataendelea na operesheni yao nchini Somalia dhidi ya Al Shabaab hadi wakenya watakapohakikishiwa usalama wao
Share:

Mlipuko mkubwa wakumba Mogadishu.......


Mlipuko mkubwa umetokea katika mji wa Mogadishu nchini Somalia karibu na uwanja wa ndege.
Duru zimearifu kuwa mlipuko huo huenda umesababishwa na mtu aliyejitolea muhanga aliyejilipua ndani ya gari.
Kundi la wapiganaji wa kiislamu la Al- Shaabab mara kwa mara hutumia milipuko ya magari, lakini kufikia sasa halijakiri kuhusika na mlipuko huo.
Haijajulikana ni watu wangapi wameuwawa
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.