Wednesday 10 December 2014

Matatani kwa kumvua nguo mwanamke Kenya.......


Wafanyakazi wa basi moja waliotuhumiwa kwa kumnyanyasa kimapenzi mwanamke wanakabiliwa na hukumu ya kifo baada ya kushitakiwa kwa kosa la wizi wa mabavu.
Watu watatu wakiwemo wafanyakazi wanaofanya kazi katika basi hilo walikamatwa mwezi jana baada ya mwanamke huyo kujitoza na kusidia polisi kwuatambua watu waliomvamia.
Kanda ya video iliosambaa kwenye mitandao ya kijamii nchini Kenya na kusababisha maandamano ya wanawake nchini Kenya akiwasihi kutombaka na kuingiza chupa katika sehemu zake za siri.
Hata aliwasihi awape pesa wakati walipokuwa wanamtisha lakini wakakataa.
Mamia ya waandamanaji waliandamana mjini Nairobi baada ya tukio hilo na kulaani kitendo cha wanaume kuwavua wanawake nguo kwa kisingizio kuwa wamevalia nguo fupi sana au vimini hasa katika vituo vya basi.

Maandamano hayo yalipangwa kupitia kwa mtandao wa kijamii. Kauli mbiu ya maandamano hayo ilikuwa #MyDressMychoice yaani nitavalia kama nipendavyo.
Polisi walilazimika kubuni kikosi cha kuchunguza wale wanaowavua wanawake nguo zao kwa madai kuwa wamevalia nguo fupi sana.
Takriban wanawake watano wamevuliwa nguo zao mjini Nairobi na katika mji wa Mombasa pwani ya Kenya.

Polisi mmoja wa utawala alikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la kumvua nguo mwanamke mjini Nairobi.
Serikali ya Kenya imesema itafuta leseni za kampuni za basi ambazo wafanyakazi wake wanapatikana na hatia ya kuwavua nguo wanawake.
Share:

Ashindwa kujizuia kula 'Tissue'.....

 Mama mwenye watoto watano, ameelezea kuwa yeye hula roli moja ya karatasi ya msalani au Tissue kila siku.
Jade Sylvester,mwenye umri wa miaka 25, alianza kutamani kula karatasi hio alipokuwa mjamzito lakini hata baada ya kujifungua yeye hujipata akila roli moja ya tissue kila siku.
Kwa mujibu wa jarida la Mirror, Uingereza, kwa mara ya kwanza alipata hamu ya kula karatasi hio ni pale alipokua na mimba ya mtoto wake mdogo Jaxon.

Jade, anayetoka mtaa wa Gainsborough, Lincolnshire, alinukuliwa akisema, "miezi mwili tangu kushika mimba hio, nilianza kutamani kula karatasi ya chooni. Hadi sasa sijui kwa nini mimi bado huila. ''
"ninapenda tu ninavyojisikia nikiiweka mdomoni mwangu, lakini sipendi ladha yake. Familia yangu huniambia sio visuri kwangu kuila , lakini siwezi kujizuia. ''

Licha yakujifungua mwanawe miezi 15 iliyopita, Jade hawezi kabisa kujizuia kutokula karatasi hio.
Mama huyo ambaye hafanyi kazi, anasema yeye husubiri anapopata haja kwenda chooni na hapo ndipo haunza kuila karatasi ile. Yeye huitafuna na kuimeza yote kila siku.
Amepata wakati mgumu kujaribu kukomesha uraibu wake tangu alipojifungua lakini anasema ameshindwa kabisa.

''Najua kwamba sio vyema kwa afya yangu, lakini hadi sasa sijapata matatizo yoyote ya kiafya kama wanavyohofia watu wengi.''
Jade ana watoto watano , wavulana wanne na msichana mmoja.
Anasema yeye hujaribu kujificha kutoka kwa wanawe kwa sababu anahofia wakimpata akila karatasi hio watamkanya sana.
Share:

Soko la Nguo lashambuliwa Nigeria....

Bomu limelipuka karibu na soko katika mji wa Kaskazini mjini mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa maafisa wakuu wanasema bomu hilo lilipuka katika eneo ambako mizigo hupakiwa, katika soko la nguo la Kantini Kwari.

Taarifa za majeruhi bado hazijatolewa. Takriban watu 2,000 wameuawa katika mashambulizi yaliyofanywa na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram mwaka huu.
Mwezi jana zaidi ya watu 100 walifariki katika shambulizi lengine lililofanywa na kundi hilo wakati wa maombi katika msikiti mkubwa mjini Kano.

Mwandishi wa BBC Habiba Adamu anasema Kantin Kwari ni soko kubwa zaidi la nguo mjini Kano ambako watu kutoka nchi jirani na maeneo mengine ya nchi kuendeshea biashara zao.
Soko hilo daima huwa limejaa watu.
Share:

Ukatili wa majasusi Marekani wafichuliwa......

Ripoti ya Seneti Marekani imekosoa vikali zinazotumiwa na CIA, kuwahoji washukiwa wa uhalifu, kwamba ni za kikatili na zisizofaa.
Ripoti ya kamati ya bunge la Seneti nchini Marekani imekosoa vikali mbinu zinazotumiwa na Shirika la Ujasusi la nchi hiyo za kuwahoji washukiwa wa uhalifu na kuelezea kwamba ni za kikatili na zisizofaa.
Mwenyekiti wa kamati ya usalama ya bunge la seneti Dianne Feinstein amesema katika baadhi ya matukio wanavyotendewa washukiwa hao ni sawa na mateso.
''Watu waliowekwa kizuizini walipaswa kutii mbinu zilizokuwa zikitumiwa, kuvuliwa nguo na kuachwa watupu, walikuwa wakiwekwa katika hali ya mateso ya muda mrefu.


Walikuwa wakizuiwa kulala kwa siku kadhaa, hadi saa 180- ikiwa ni sawa na siku saba na nusu, zaidi ya wiki bila ya kulala, kawaida wakiwa wamwesimama au katika hali ya kuwachosha na wakati huohuo mikono yao ikiwa imefungwa pamoja juuya vichwa.
Mbonu hizo za utesaji zilianzishwa baada ya shambulio la kigaidi la Septemba 11, mwaka 2001
nchini Marekani...''
Mbinu hizo zinazotumiwa na shirika hilo la ujasusi zimeelezwa na wabunge hao wa seneti kuwa zinamapungufu na kwamba CIA imekuwa ikitoa taarifa zisizo sahihi kwa umma.
Share:

Kilio cha Albino Tanzania...


Mtobi Namigambo, ni mvuvi anayeuza samaki, amekaa kwa utulivi nje ya nyumba yake ya matope katika kisiwa cha ukerewa mahali ambapo zamani palikuwa makao ya albino lakini kwa sasa si hivyo. Mtoto wake wa miaka nne May Mosi ameketi kwenye paja lake akionyesha umarufu wake wa hisabati kwa kuhesabau moja hadi kumi kwa ujasiri.
Mara kwa mara Mtobi anamtazama mke wake, Sabina, ambaye ameketi kwa mkeka kando yake akitayarisha chakula cha jioni. Watoto wake wengine wawili wanachezea hapa karibu na pia wamejaliwa na mtoto mchanga amabye yuko chumbani analala.
May alipokuwa na umri wa miezi mitatu, aliponea jaribio la kutekwa nyara.
" nilikuwa nimeenda ziwani kuvua samaki. walikuwa pekee yao nyumbani wavamizi walipokuja, mke wangu alitorokea kwa dirisha na kukimbillia usalama akiwa na May, na akawawacha watoto hawa wawili nyumabani ambao hawakuwadhuru kabisa", Mtobi ananiarifu.
"Wavamazi hao walikuwa wakimtaka May," Sabina anaongezea, "mume wangu alikuwa ameenda safari ya uvuvi na wavamizi hao walijua na hio ndio sababu walikujia mtoto wangu, baada ya kutorokea kwa dirisha, bado waliniandama huku nikipiga mayoye ya usaidizi, waliwacha kuniandama wakati tu niliwaamsha majirani"
May ni mojawapo wa Albino sabini wanaoishi katika kisiwa hiki cha Ukerewa ambacho ni masaa matatu tu kutoka mwanza, mji wa pili mkubwa zaidi Tanzania.
Elimu kwa jamii
Mtobi anasema "tunaiomba serikali kufanya juhudu zaidi za kuelimisha jamii hapa, serikali ishawahi kuandaa majadiliano kuhusu Albino na kulikuwa na mabadiliko makuwa, akini si hivyo tena"
Shirika lisilo la kiserekali chini ya mrengo wa 'The Same Sun' linalowashughulikia jamii ya Albino hapa Ukerewa, linasema kuwa kisiwa hiki hakina usalama kando na vile watu wangependa kuamini.
Mwenye kiti wa chama cha maalbino tawi la Mwanza, (TAS) Alfred Kapole, mzaliwa wa Ukerewe, alilazimika kutorokea mji wa Mwanza akiwa mmoja wa albino wa kwanza kufika kortini baada ya kiognozi mmoja wa kijiji akitaka kumuua kwa ajili ya nywele zake.
Mwaka uliopita boma lake lilivamiwa, kwa bahati nzuri alikuwa ameenda mwanza. Kulikuwa na jairibio lEngine la kumuua mwaka huu.
Kampeni kabambe
Serikali ya Tanzania imeanzisha kampeni ili kuchangisha fedha za kuelimisha jamii.
Kampeni nyingi za uhamasishaji hufanyika mijini kwani ni rahisi kufikia watu,lakini ni vijiji ndivyo vinahitaji msaada zaidi.
Ramadhan Khalfan, ambaye ni mwenyekiti wa chama cha albino Ukerewa,anasema kuwa wanataka kufikia maeneo ya vijiji na kuzungumza na watu,lakini ni vigumu kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha.''Hatuna uwezo ama njia za kufikia jamii zilizoko vijijini.Aliongezea kusema,''tunategemea pakubwa redio na televisheni,lakini hatuwezi kufika mashinani kwa sababu ya gharama.''
Sehemu ya Serengema inapatikana kilomita 60 (maili 33.5) kutoka Mwanza.Ili kusisitiza shida hii,umejengwa mnara katika mzunguko katikati ya mji.
Ni sanamu ya chuma kimo cha binadamu,inayoonyesha baba mwenye rangi akimbeba begani mto wake albino huku mama yake mwenye rangi akitundika kofia yenye ukingo mpana kwenye kichwa cha mwana huyo kumkinga kutokana na miale ya jua.Pia kuna majina ya watu 139 ya waathiriwa waliouawa,kuvamiwa ama miili yao kuibiwa kutoka kwenye makaburi.
Serengema ndio sehemu iliyoathirika vibaya zaidi.
Kuna mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi pamoja na chama cha Tanzania Albino katika kuhamasisha na pia kujenga makaazi.
Mashirika yasiyo ya kiserikali yanaamini kuwa uhamasisho na kuacha imani potovu zinaweza kusimamisha mauaji haya.
Mwakilishi wa chama cha Serengema Mashaka Benedict anasema kuwa watu bado wanaamini kuwa sehemu za mwili wa albino zinaweza kuleta utajiri.''Kama hiyo ndiyo hali,mbona sisi si matajiri?''anauliza.
Anadai kuwa watu mashuhuri wanahusika katika ''biashara ya mauaji'' na ndio maanake watu wachache sana wamekamatwa,kushitakiwa,kupatikana na hatia ama kufungwa.''Itakuwa vipi masikini kutoa dola 10,000 kwa kipande cha mwili?,ni wanabiashara na wanasiasa ndio wanaohusika.''
Hata hivyo polisi wanasema kuwa wanachungunza kila moja ya visa lakini wanakosa ushahidi wa kuthibitisha madai yanayotolewa.Kamanda wa polisi wa Mwanza,Valentino Mlolowa anasema,''Kesi hizi ni ngumu kwa kuwa visa hufanyika mashinani sana katika sehemu ambazo hazina stima kwa mfano,na hiyo inafanya kuwajua wahalifu usiku kuwa vigumu.Tunachunguza kila moja ya kesi na madai,lakini kama uonavyo,si rahisi.''
Yaweza onekana kama kuwa tumepoteza kila kitu lakini hii haiwazuilii watu wanaoishi na hali ya Uhalbino kama May Mosi,kutokuwa na tumaini kuwa fedha zinazochangishwa kutoka kwenye kampeni iliyoanzishwa na serikali zitasaidia kusikizwa zaidi kwa Albino nchini Tanzania.





Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.