Saturday 18 April 2015

Balotelli ndiye aliyebaguliwa zaidi EPL


Mario Balotelli ndiye mchezaji aliyebaguliwa sana katika ligi ya Uingereza ,huku mchezaji huyo akipokea zaidi ya ujumbe 8000 ,asilimia 50 zikiwa ni za kibaguzi.
Takwimu hizo za kushtua zimeripotiwa na Kick it Out ,ambao walibaini kwamba raia huyo wa Itali alilengwa sana katika mitandao ya Twitter huku mshambuliaji wa Arsenal Danny Welbeck akipokea ujumbe 1700 asilimia hamsini zikiwa za kibaguzi.
Mshambuliaji mwenza wa Balotelli katika kilabu ya Liverpool Daniel Sturridge pia alionekana kulengwa katika mitandao ya kijamii baada ya kupokea ujumbe wa 1600 asilimia 60 ikiwa ni ujumbe wenye mwelekeo wa kijinsia.
Utafiti huo pia umebaini kwamba kilabu ya Chelsea ndio kilabu iliobaguliwa zaidi kwa ujumbe 20,000 huku liverpool ikiwa ya pili na ujumbe 19,000 Arsenal ikiwa ya tatu kwa ujumbe 12,000 huku Manchester City na Manchester United zikipokea ujumbe 11,000.
Share:

Obama: mabadiliko ya hewa hayakanushiki

Mwanamme mbele ya moto Colorado, Marekani,  Juni 2013,
Rais Obama ameonya kuwa mabadiliko ya hali ya hewa hayawezi tena kukanushwa au kudharauliwa, na amesema ndio tishio kubwa kabisa linalokabili dunia.
Katika hotuba yake ya kila juma, Rais Obama alisema anataka aweze kuwatazama watoto na wajuukuu wake machoni na kusema kuwa kila liwezalo limefanywa kupambana na msukosuko huo.
Bwana Obama hivi karibuni aliahidi kupunguza sana kiwango cha gesi inayozidisha joto inayotolewa na Marekani - kiwango cha pili kikubwa kabisa duniani - kabla ya mkutano wa viongozi wa dunia mwezi wa Disemba.
Mipango yake inapingwa vikali na wanasiasa wengi wa chama cha Republican ambao wanadai kuwa itaumiza makampuni ya Marekani.
Share:

Saudia kutoa msaada unaohitajika Yemen


Saudi Arabia, inayoongoza mashambulio ya ndege dhidi ya wapiganaji nchini Yemen, imeahidi kutoa idadi ya fedha ambayo Umoja wa Mataifa imesema inahitajika nchini Yemen.
Umoja wa Mataifa uliomba msaada huo wa kimataifa hapo jana, kwa shughuli za dharura za usaidizi nchini Yemen.
Shirika la habari la taifa la Saudi Arabia, linasema kuwa nchi hiyo itatoa dola laki mbili na 74 milioni, kama msaada wa kiutu kwa Wayemeni walioathirika na vita.

Taarifa rasmi ilisema Saudi Arabia inasimama pamoja na ndugu zake wa Yemen.
Oparesheni inayoongozwa na Saudi Arabia, dhidi ya wapiganaji wa Houthi (na askari wanaopigana kwa niaba ya rais wa zamani, Ali Abdullah Saleh, ilianza wiki tatu zilizopita.
(Umoja wa Mataifa unasema mamia ya watu wamekufa, na maelfu ya familia zimekimbia makwao wakati vita vikizidi.)
Share:

Ghasia zasababisha mauaji ya watu Libya


Zaid ya watu kumi wameuawa katika msururu wa ghasia viungani mwa mji mkuu wa Libya Tripoli.
Ghasia hizo kutoka maeneo mawili zilikuwa kati ya wanamgambo walio watiifu kwa serikali ya tripoli na wale walio watiifu kwa serikali inayatombuliwa na jamii ya kimataifa iliopo mashariki mwa taifa hilo.
Milipuko ya mabomu ya mara kwa mara pamoja na milio ya risasi imesika katika eneo la Fashloum ambapo baadhi ya watu wamekamatwa na wapiganaji walio watiifu kwa serikali ya Tripoli.
Share:

Jacob Zuma aahirisha ziara ya Indonesia


Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ameahirisha ziara yake ya ughaibuni kutokana na hali ya ghasia za kibaguzi dhidi ya wageni katika taifa lake.
Alitarajiwa kuhudhuria mkutano nchini Indonesia. Rais Zuma ambaye amekosolewa kwa kushindwa kuonyesha uongozi anatarajiwa kuitembelea kambi ya wakimbizi ya Chatsworth mjini Durban.
Polisi nchini Afrika Kusini wamewaagiza raia kutotuma ujumbe usiothibitishwa kuhusu mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni kwa sababu hatua hiyo inazua hofu.
Polisi wanesema kuwa kuna wasiwasi kuwa uvumi huo unachochea ghasia dhdi ya wahamiaji.Rais wa Afrika kusini Jacob Zuma ameahirisha ziara yake ya ughaibuni kutokana na hali ya ghasia za kibaguzi dhidi ya wageni katika taifa lake.
Alitarajiwa kuhudhuria mkutano nchini Indonesia. Rais Zuma ambaye amekosolewa kwa kushindwa kuonyesha uongozi anatarajiwa kuitembelea kambi ya wakimbizi ya Chatsworth mjini Durban.
Polisi nchini Afrika Kusini wamewaagiza raia kutotuma ujumbe usiothibitishwa kuhusu mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni kwa sababu hatua hiyo inazua hofu.
Polisi wanesema kuwa kuna wasiwasi kuwa uvumi huo unachochea ghasia dhdi ya wahamiaji.

Watu 30 waliakamatwa wakati wa ghasia za usiku kucha mjini Johannesburg.
Biashara kadha zinazomilikiwa na raia wa kigeni ziliharibiwa.
Takriban watu watano wameuawa kwenye mashambulizi yaliyaonza baada mfalme wa kizulu Goodwill Zwelethini kusema kuwa wageni wanahitajka kuondoka Afrika Kusini.
Share:

Watu zaidi ya 30 wauawa Afghanistan


Shambulizi la kujitoa mhanga kwenye mji ulio mashariki mwa Afghanistan wa Jalalabad limewaua watu 33 na kuwajeruhiwa karibu wengine 100.
Ripoti zinasema kuwa shambulizi hilo lilitokea karibu na benki ambapo wafanyikazi wa serikali wanalipwa misharaha yao.
Maafisa wanasema kuwa mtu aliyeendesha shambulizi hilo alikuwa na pikipiki.
Kulitokea shambulizi la pili karibu na madhabahu mjini Jalalabad lakini haijulikani kama kulikuwa na madhara yoyote.
Hakuna kundi lililokiri kuhusika, lakini mji wa Jalalabad umekuwa ukilengwa kila mara na kundi la Taliban.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.