Thursday 18 December 2014

Gari linaloweza kujiegesha kwa kutumia saa.
























>>>> SOMA ZAIDI HAPA<<<<
Share:

Purukushani bungeni nchini Kenya.


Wabunge wa Kenya wametofautiana vikali bungeni na kuvuana mashati huku wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswada tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.
Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani walipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.

Mwenyekiti wa kamati ya usalama wa bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyaja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo wakisema 'bado mapambano.'
Spika wa bunge Justin Muturi wakati mmoja aliamuru walinzi wa bunge kuwaondoa baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.
Mswada huo ambao umewasilishwa bunge kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.


Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.
Pia ikiwa mswada huo utapistihwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa faini ya hadili shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.
Mswada huu umetolewa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab wakilalamika na kutaka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia
Rais Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikzo kuimarisha usalama wa tangui mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Share:

JK:Akatiza ziara ya Mizengo Pinda.... Source BBC


Waziri Mizengo Pinda amekatiza kwa muda, ziara yake katika Falme za Kiarabu kwa maelezo kwamba ameitwa nyumbani na Rais Jakaya Kikwete kwa shughuli maalumu.
Waziri Mkuu ambaye yuko katika ziara ya kutembelea nchi za Falme za Kiarabu, ikiwa ni sehemu ya kudumisha ushirikiano na kutafuta wawekezaji, amekatisha ziara hiyo siku mbili baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema kujiuzulu kutokana na kashfa ya Escrow.
Werema alijiuzulu juzi na Rais Kikwete akaridhia hatua hiyo, huku umma ukisubiri hatua zaidi dhidi ya mawaziri na watendaji wa Serikali waliotajwa katika sakata hilo.
Katika barua yake ya kujiuzulu, Jaji Werema alisema ushauri wake wa kisheria kuhusu Akaunti ya Tegeta Escrow haukueleweka na hivyo kuchafua hali ya hewa.

Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, leo Waziri Mkuu alitarajiwa kufanya mazungumzo na washiriki wa maonyesho ya B2B pamoja na kutembelea maeneo mengine lakini ziara hiyo imefutwa na badala yake anaondoka asubuhi kurudi nyumbani.
Baadaye leo Pinda alitakiwa kwenda Doha, Qatar kwa ziara kama hiyo hadi Desemba 23.
Baada ya kukamilisha jukumu aliloitiwa, Waziri Mkuu anatarajiwa kurejea Falme za Kiarabu Jumamosi kuendelea na ziara yake.
Share:

M'marekani ahusishwa na fedha bandia UG.


Mamlaka ya Marekani imemkamata raia mmoja wa taifa hilo kwa kuongoza kashfa ya kimataifa ya fedha bandia,BBC imebaini.
Ryan Gustafson mwenye umri wa miaka 27 alishtakiwa kwa njama ya kuwa na fedha bandia nje ya Marekani baada ya fedha hizo kutumika katika biashara tofauti za Marekani.
Shirika la kijasusi la Marekani lilifuatilia fedha hizo hadi Kampala ,ambapo walibaini kuna njama ya fedha hizo bandia inayotengeza yuro,rupee pamoja na fedha tofauti za nchi za Afrika.
Mshukiwa huyo anakabiliwa na kifungo cha miaka 25 gerezani.

Maajenti wa FBI waligundua fedha hizo zinatumwa kutoka Uganda.
Alama ya kidole kutoka kwa kifurushi cha fedha hizo ilitoa maelezo ya fedha hizo kutoka kwa bwana Gustafson,raia wa Marekani.
Shirika hilo la maafisa wa ujasusi lilishirikiana na mamlaka ya Uganda ili kuanzisha uchunguzi wa siri kwa lengo la kununua fedha hizo kutoka kwa mshukiwa huyo.
Alikamatwa ,na msako kufanywa katika nyumba yake ambapo fedha bandia za Uganda,Francs za Congo,Cedis za Ghana,Rupees za India na Yuros pamoja na vifaa vya kutengeza fedha bandia.
Mamlaka ya Marekani inakisia kwamba washukiwa hao waliingiza takriban dola millioni 2 fedha bandia katika soko.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.