Friday 12 February 2016

Riek Machar makamu wa rais Sudan Kusini...BBC


Katika kutafuta amani ya Sudan Kusini, Rais Salva Kiir amemteua mpinzani wake Riek Machar kuwa makamu wa rais.Majeshi yanayowatii watu hawa wawili , walipigana vita vya wenyewe kwa wenyewe na kusababisha watu zaidi ya milioni moja na nusu kukimbia makazi yao.
Machar ambaye alikuwa amehaidiwa wadhifa huo wa makamu wa raisi kama atakubali kuweka sahihi katika makubalino ya kuleta amani ulifanyika mwezi Agosti mwaka jana .lakini bado baadhi ya majeshi yamejigawa na kuendeleza mapigano katika baadhi ya maeneo ya Sudan Kusini.
Mtangazaji akisoma kwa sauti ya juu amri ya raisi kumteua Machar kuwa msaidizi wake,amri hiyo ilisomwa kama ifuatavyo;katika zoezi la mgawanyiko wa utawala chini ya kifungu namba 524 cha sheria cha kwanza cha makubaliano ya kufikia hatima ya mgogoro unaoendelea jamuhuri ya sudan ya kusini.
Salva Kiir,raisi wa Jamuhuri ya Sudan ya kusini amemteu Dr,Riek Machar kuwa makamu wa kwanza wa raisi ya jamuhuri ya Sudan ya Kusini kuanzia tarehe 11 Februari 2016
Share:

Wanasayansi wagundua mvutano wa mawimbi...BBC


Wanasayansi nchini Marekani wamefanikiwa kubaini Mvutano wa asili wa mawimbi na kusema uvumbuzi huo unawapa mwanya mpya wa kuuelewa ulimwengu zaidi.
Albert Einstein alitabiri kuwa uwepo wa mvutano huo wa mawimbi karne iliyopita,Nadharia yake ilikuwa kwa ujumla ikihusisha jimbo ambalo linasafiri kwa kasi na kumulika mwanga ikiwa inajaribu kujikunja na kutaka kutosha katika muda unaotumika.
Mpaka sasa wamedhibitisha kuwa ni ndoto,ingawa watafiti wa LIGO na mashuhuda wa suala hili nchini Marekani,wanasema kadri wanavyoyaona mawimbi yanayotoka katika mashimo mawili meusi wanaamini kuwa hiyo ni ishara iliyo wazi kabisa.

Msemaji wa wanasayansi hao Gabby Gonzalez anaeleza;"tunasikia mvutano wa asili wa mawimbi hayo,tunaona mzunguko wake ni jambo zuri kwa kweli kwa kuwa hatuoni tu maajabu ya ulimwengu bali tunasikia,lakini kiufupi hilo ni jambo ambalo halikubaliki,na sisi tulichokifanya ni kupata ishara ya sauti tu,''umesikia hiyo sauti nzuri?Ni sauti tu inayounguruma,oops hiyo ndiyo sauti tuliyokuwa tunaipima"
wakati katika mkutano wa habari mjini washington,mkurugenzi mtendaji wa Interferometer Gravitational wave Obsever Dave Rietze - akitoa tangazo hili:"mabibi na mabwana ,tumeweza kuchunguza mvutano huo wa asili wa mawimbi,na tumeweza,nina furaha kubwa kuwaambia kuwa mivutano wa asili wa mawimbi haya yaliandaliwa na katika mashimo mawili meusi ambayo yanakuja kwa pamoja na kutengeneza shimo moja,ni kama kitu cha miongo kadhaa iliyopita"
Share:

ICC kuamua juu ya William Ruto...BBC


Mahakama ya jinai ya kimataifa -ICC leo inatarajiwa kutoa uamuzi ambao huenda ukakuwa na athari kwa kesi inayomkabili naibu rais wa Kenya William Ruto. Bwana Ruto na mushtakiwa mwenzake, mwana habari Joshua arap sang wameshatkiwa kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu kuhusiana na ghasia zilizotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa 2007.
Mashtaka kama hayo yaliyomkabili rais Uhuru Kenyatta yalifutiliwa mbali na mwendesha mkuu wa mashataka ya ICC, Fatou Bensouda kwa ukosefu wa ushahidi.
Share:

Bunge lachafuka A.Kusini, Malema nje...BBC


Kumetokea malumbano makali bungeni nchini Afrika Kusini ambapo wanasiasa wa upinzani wamechelewesha hotuba ya rais Jacob Zuma aliyekuwa akilihutubia taifa na kuzua maswali kuhusu utaratibu.
Baadhi ya wanasiasa wanasema rais huyo hakupaswa kuhutubia bunge kutokana na kashfa mbali mbali alizonazo
Ni mvutano huo baada ya spika wa bunge la Afrika Kusini mama Baleka Mbete na wafuasi wa upinzani wengi wao kutoka chama cha Ecoomic Freedom Fighters EFF wakiongozwa na Juliasi Malema ambao walikuwa wanadai kutaka utaratibu na kuvuruga hotuba ya Rais Jacob Zuma..
Hatimaye uvumilivu ukamshsinda spika wa bunge Baleka Mbete na kumuru kiongozi wa EFF Julias Malema kutolewa nje ya ukumbi wa bunge.
Baada ya fujo hizo Rais Jacob Zuma alijaribu kuendelea kuhutubia lakini wabunge wa upinzani walibaki wakarudia tena kumkatiza

Baada fujo hizo baadae angalau kidogo pakawa na utulivu ambapo Rais Zuma aliweza kumalizia hotuba yake na Katika hotuba hiyo Rais Zuma mbali na mambo mengine alisema serikali yake imekuwa akibana matumizi lakini anaona bado hatua zaidi zinahitajika.
"Tumekuwa tukichukua hatua za kubana matumizi ya fedha za umma kwa hekima ikiwa ni pamoja na kubana matumizi yasiyo ya lazima. Lakini bila kuathiri wajibu muhimu wa serikali na kutoa huduma kwa raia. Mwaka 2013 waziri wa fedha alitangaza hatua za kubana matumizi. Matumizi ya ziada na yale yasiyo ya lazima yamepunguzwa lakini bado hatua zaidi zinapaswa kuchukuliwa kubana upotevu wa fedha za umma."
Rais Zuma anakabiliwa na kashfa kadhaa lakini kubwa la hivi karibuni ni hatua ya kutumia fedha za umma kufanya ukarabati wa kasri lake la kifahari la Nkandla.
Share:

Clinton na Sanders wajibizana kuhusu Obama...BBC

Sanders Clinton
Wagombea urais wa chama cha Democratic Marekani Hillary Clinton na Bernie Sanders wamejibizana kuhusu Rais Barack Obama kwenye madahalo wa kwanza tangu kumalizika kwa mchujo wa New Hampshire.
Bi Clinton alijionesha kama mlinzi wa sifa za utawala wa Barack Obama, na kumshambulia Bw Sanders kwa kumkosoa rais huyo.
“Ukosoaji ambao nimekuwa nikisikia kutoka kwa Seneta Sanders, ningetarajia hilo kutoka kwa wafuasi wa Republican pekee,” Bi Clinton alisema.
Bi Clinton tena na tena alirejelea uhusiano wake mwema na Bw Obama ambaye anapendwa sana na makundi ya wachache Marekani, hasa Wamarekani weusi.
Bw Sanders kwa upande wake alijaribu sana kuweka ujumbe wake kuonesha kwamba anataka kutetea usawa wa kiuchumi na kuwasaidia Waamerika weusi.
Bi Clinton alisisitiza kwamba ujumbe wake unaambatana na vitendo, na akatilia shaka ahadi ya Bw Sanders ya kutoa huduma ya afya kwa wote na kuondoa karo katika taasisi za elimu ya juu.
“Tunawajibika kueleza kwa uwazi yale ambayo tunayoahidi na ndiyo maana hatuwezi kutoa ahadi ambazo hatuwezi kutimiza,” Bi Clinton alisema.

Wagombea wanajiandaa kwa uchaguzi wa mchujo katika majimbo ya Nevada na South Carolina, ambayo yana raia wengi wa makundi ya wachache.
Bi Clinton anajaribu kujenga upya kampeni yake baada ya kushindwa pakubwa na Bw Sanders kwenye mchujo wa New Hampshire.
Alipokea uungwaji mkono muhimu kutoka kwa kundi la wabunge weusi katika chama cha Democratic mnamo Alhamisi.
Sanders, seneta wa Vermont, alishinda New Hampshire kwa zaidi ya asilimia 22 na alishindwa mchujo wa Iowa kwa kura chache mno.
Sanders
Lakini majimbo hayo yote yana Wazungu wengi.
Sasa anakabiliwa na changamoto ya kutafuta kura miongoni mwa watu wa asili ya Amerika Kusini na Mexico pamoja na Wamarekani weusi katika majimbo ya Nevada na South Carolina.
Bi Clinton anaungwa mkono sana na makundi hayo na anatarajiwa kufanya vyema Nevada na South Carolina.
Kura ya maoni ya karibuni iliyofanywa na NBC News/Wall Street Journal/Marist jimbo la South Carolina ilisema Bi Clinton anaongoza akiwa na asilimia 74 ya kura dhidi ya Bw Sanders mwenye asilimia 17 miongoni mwa wapiga kura weusi.
Share:

Syria: Mataifa yaafikiana vita visitishwe...BBC

Lavrov
Mataifa yenye ushawishi duniani yameafikiana kuhusu mkataba wa kusitisha mapigano nchini Syria ambao utaanza kutekelezwa katika kipindi cha wiki moja ijayo.
Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya mazungumzo nchini Ujerumani.
Mwafaka huo hata hivyo hautahusisha makundi ya kijiihadi ya Islamic State (IS) na al-Nusra Front.
Mawaziri wa mataifa wanachama wa Kundi la Kimataifa la Kusaidia Syria pia wamekubaliana kuharakisha na kuongeza juhudi za kutoa misaada.
Tangazo hilo limetokea huku jeshi la Syria, likisaidiwa na Urusi kwa mashambulio ya kutoka angani, likiendelea kupiga hatua eneo la Aleppo.
Hatua hiyo ya kijeshi inatishia kuzingira maelfu ya raia katika maeneo mengi ya mji wa Aleppo yanayodhibitiwa na waasi.
Waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani John Kerry amekiri kwamba mpango wa kusitisha mapigano unaazimia kutimiza makuu lakini akasema changamoto kubwa itakuwa kuona iwapo pande zote zitaheshimu mkataba huo.
Syria
“Kile tulicho nacho kwa sasa ni ahadi kwenye karatasi, siku chache zijazo tunafaa kusubiri tuone iwapo hayo yatatekelezwa,” amesema.
Jopo kazi linaloongozwa na Marekani na Urusi litasaidia kutekeleza mkataba huo kupitia mashauriano na makundi yanayopigana nchini Syria.
Misaada inatarajiwa kuanza kufikishwa kwa raia waliozingirwa na majeshi katika baadhi ya maeneo Ijumaa.
Bw Kerry ametoa tangazo la kupatikana kwa mwafaka huo akiandamana na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov na mjumbe maalim wa Umoja wa Mataifa Syria, Staffan de Mistura.
Bw Lavrov amesema kuna sababu za kuwa na matumaini kwamba “tumefanya kazi kubwa na nzuri leo”. Pendekezo la awali kutoka Urusi lilikusudia mapigano yasitishwe kuanzia tarehe 1 Machi.
Share:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.