Friday 12 February 2016

Wanasayansi wagundua mvutano wa mawimbi...BBC


Wanasayansi nchini Marekani wamefanikiwa kubaini Mvutano wa asili wa mawimbi na kusema uvumbuzi huo unawapa mwanya mpya wa kuuelewa ulimwengu zaidi.
Albert Einstein alitabiri kuwa uwepo wa mvutano huo wa mawimbi karne iliyopita,Nadharia yake ilikuwa kwa ujumla ikihusisha jimbo ambalo linasafiri kwa kasi na kumulika mwanga ikiwa inajaribu kujikunja na kutaka kutosha katika muda unaotumika.
Mpaka sasa wamedhibitisha kuwa ni ndoto,ingawa watafiti wa LIGO na mashuhuda wa suala hili nchini Marekani,wanasema kadri wanavyoyaona mawimbi yanayotoka katika mashimo mawili meusi wanaamini kuwa hiyo ni ishara iliyo wazi kabisa.

Msemaji wa wanasayansi hao Gabby Gonzalez anaeleza;"tunasikia mvutano wa asili wa mawimbi hayo,tunaona mzunguko wake ni jambo zuri kwa kweli kwa kuwa hatuoni tu maajabu ya ulimwengu bali tunasikia,lakini kiufupi hilo ni jambo ambalo halikubaliki,na sisi tulichokifanya ni kupata ishara ya sauti tu,''umesikia hiyo sauti nzuri?Ni sauti tu inayounguruma,oops hiyo ndiyo sauti tuliyokuwa tunaipima"
wakati katika mkutano wa habari mjini washington,mkurugenzi mtendaji wa Interferometer Gravitational wave Obsever Dave Rietze - akitoa tangazo hili:"mabibi na mabwana ,tumeweza kuchunguza mvutano huo wa asili wa mawimbi,na tumeweza,nina furaha kubwa kuwaambia kuwa mivutano wa asili wa mawimbi haya yaliandaliwa na katika mashimo mawili meusi ambayo yanakuja kwa pamoja na kutengeneza shimo moja,ni kama kitu cha miongo kadhaa iliyopita"
Share:

0 comments:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.