Thursday 11 February 2016

Rwanda lawamani juu ya Burundi.


Maafisa wa Wizara ya mambo ya nje ya Marekani wamesema wameona ushahidi kuwa serikali ya Rwanda imekua ikichangia matukio ya machafuko katika nchi jirani ya Burundi.
Inaelezwa kuwa Rwanda imekuwa ikiwapa silaha na mafunzo wakimbizi waliokimbia machafuko nchini Burundi.
Burundi imetumbukia mgogoro wa wenyewe kwa wenyewe tangu Rais Pierre Nkurunziza alipoamua kugombea uraisi kwa muhula wa tatu.
Maafisa hao wa Marekani wanasema taarifa walizo nazo kutoka kwa maafisa wenzano waliopo kwenye kambi za wakimbizi nchini Rwanda, zinasema Rwanda imekuwa ikihusika na vurugu katika nchi jirani ya Burundi.

Akihojiwa na Bunge la Congress mmoja wa wanadiplomasia amesema kuna taarifa za kuaminika kwamba wakimbizi wa Burundi ikiwa ni pamoja na watoto wamekuwa wakipewa mafunzo katika makambi nchini Rwanda, na kufunzwa kupambana kwa silaha na serikali.

Ghasia zilizuka nchini Burundi mwaka jana baada ya rais wa nchi hiyo kusema atagombea kwa muhula wa tatu.
Serikali za nchi hizi mbili zina makabila ambayo ni mahasimu, na kuna ongezeko la wasiwasi wa kimataifa kuwa mgogoro mwingine wa kikabila inaweza kuota mizizi katika eneo hilo.
Tayari Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda amekanusha tuhuma hizo ambapo amesema Umoja wa Mataifa unapaswa kutafuta mikakati ya kutatua mgogoro ya kisiasa badala ya kutafuta nani wa kumtupia lawama.
Share:

0 comments:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.