Monday 26 January 2015

Unywele wa Lincoln wauzwa dola 25,000.


Vitu vya kumbukumbu vya aliyekuwa rais wa 16 wa Marekani Abraham Lincoln vimeuzwa katika mnada mjini Dallas nchini Marekani na kupata dola 800,000.
Msokoto mmoja wa nywele za rais huyo aliyeuawa umeuzwa kwa dola 25,000 lakini barua iliokiri kwamba vita vya wenyewe kwa wenyewe havikuwa vizuri haikuuzwa.
Barua iliotiwa sahihi na naibu wake John Wlkes Booth iliuzwa kwa dola 30,000 huku agizo lake la kijeshi likitia kibindoni dola 21,250.





















Vitu vya Lincoln vilipigwa mnada mjini Dallas marekani.

ukusanyaji wa vitu hivyo 300 ulianzishwa mwaka 1963 na mmiliki wa jumba la sanaa Donald Dow aliyefariki miaka mitano iliopita.
Mwanawe Greg amesema kuwa ni wakati wakusanyaji wengine wapate fursa ya kuifurahia.
Amesema kuwa babaake alikuwa ameanza ukusanyaji huo kutokana na maslahi yake katika vita vya wenyewe kwa wenyewe pamoja na historia ya kijeshi,lakini baadaye alikuwa na hamu na Lincoln na mauaji yake.
Share:

0 comments:

Blog Owner

Blog Owner
FESTO MDEMU

Blog Archive

Flag


Total Pageviews

Translate

Powered by Blogger.